Polisi wamsaka ...

Polisi wamsaka ...

Kabisa Mkuu wao ni baadhi ya Watanzania wanaopigika sana lakini bado wanakubali kutumika katika kubaka demokrasi nchini kunakofanywa na hii Serikali dhalimu.

Wao wanaona haiwahusu, lkn kumbe ndugu zao wana umia
 
Kamwe huwezi kutawala nchi hivi halafu utegemee mafanikio kwenye utawala wako.

Kitaani milio ya risasi, tunafukuzana na defenda utafikiri waasi, hawatulindi sisi hawana love hawako peace wanazidi kuichafua democracy
 
Baada ya kuishiwa majipu ya kutumbua, na baada ya utumbuaji huo kutokuonesha impact kwenye maisha ya kawaida (hali ya maisha imezidi kuwa ngumu kuliko hata kabla ya utumbuaji) na kwa sababu hawana majibu ya kero za watanzania ambazo nyingine wamezitengeneza wenyewe bila sababu ( refer la sukari), imewabidi na imewalazimu kuhakikisha wakosoaji wote wananyamazishwa wasije kuuanika uchi wa mfalme! Hii serikali imeonesha uoga uliopitiliza! Wanajihami hata kwa viyu vidogovidogo visivyokuwa na msingi!
 
Watu ambao wamejikita zaidi kwenye democracy wakati wanatakiwa wajikite zaidi kwenye shida za wananchi za kila siku watakua hawawazi vizuri.
 
Kabisa Mkuu juzi nimeona tena Mo Ibrahim karudisha bulungutu lake Bungeni kwa kukosa Kiongozi mstaafu wa Afrika akiwemo Kikwete kushindwa kutimiza vigezo vya utawala bora walipokuwa madarakani.

Inashangaza sana kuona mtu anachukua uongozi wa nchi na kuahidi mazuri mengi ikiwemo kulinda maslahi ya Tanzania na Watanzania lakini akishaingia tu Ikulu basi anageuka na kulinda maslahi ya wezi, mafisadi, watoa rushwa na wapokea rushwa na huyu wa sasa kaingia na jipya la kukandamiza haki zetu za kikatiba katika kujadili mambo mbali mbali nchini ikiwemo mustakabali wa nchi yetu. Anataka tuwe mazombie na maovu yote nchini tuyanyamazie. Inasikitisha sana kusema kweli. Na hivyo vyama vya upinzani watangaze rasmi kwamba vimefutwa.
Alirudishe tu,tutatengeneza mabulungutu ya kwetu wenyewe.
 
Kamwe huwezi kutatua shida za wananchi kwenye nchi ambayo haina demokrasi . Kumbuka issue ya v.ilaza wa UDOM huo ni mfano mmoja tu na ipo mifano mingi sana.

Watu ambao wamejikita zaidi kwenye democracy wakati wanatakiwa wajikite zaidi kwenye shida za wananchi za kila siku watakua hawawazi vizuri.
 
Ndugu watanzania, naomba mniombee. Nimejitoa mhanga kuwakomboa watu wa hali ya chini ambao naamini ndiyo walionipa kura nyingi. Mimi sikuchaguliwa na matajiri. Mnataka nimtumbue hapa hapa au? Namlipia huyu kijana akapate huduma huko regency. Hivi mlitarajia serikali iendelee kuwalipia na kuwakumbatia hawa va la za ? Haiwezekani kabisa hao wanaowatetea nao ni va li za. Hakuna siasa vyuoni. Nakumbuka hata JK hakuwa hata na kadi ya TANU alipokuwa chuo. MTAJIJU.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hajitambui kabisa huyu hata kauli zake ni za kukurupuka matokeo yake kauli zake zimekuwa za hovyo kupita kiasi.

Ndugu watanzania, naomba mniombee. Nimejitoa mhanga kuwakomboa watu wa hali ya chini ambao naamini ndiyo walionipa kura nyingi. Mimi sikuchaguliwa na matajiri. Mnataka nimtumbue hapa hapa au? Namlipia huyu kijana akapate huduma huko regency. Hivi mlitarajia serikali iendelee kuwalipia na kuwakumbatia hawa va la za ? Haiwezekani kabisa hao wanaowatetea nao ni va li za. Hakuna siasa vyuoni. Nakumbuka hata JK hakuwa hata na kadi ya TANU alipokuwa chuo. MTAJIJU.
 
Kuishi kama shetani haitawezekana.
Ndio sababu nimemshauri mtoa kauli hiyo aifute. Hatutaki mashetani wala hatutaki malaika. Tunataka watu waishi kama binadamu na sheria iwe ni msumeno.
 
Inawezekana kabisa akawa na lengo zuri,ila njia anayotumia ni mbaya Sana! Nafikiri tumpe ushauri wa njia za kufanya kazi vizuri kuliko kupo
nda mda wote
 
Polisi wamsaka Gwajima....Polisi wamuhoji Zitto, Polisi wazuia maandamano Pemba, Polisi watangaza kuzuia mikutano ya kisiasa nchi nzima, Polisi wazingira hoteli ambayo ACT wangelifanyia mkutano wa bajeti, Polisi wamkamata kijana aliyemuita rais "Bwege", Polisi wawatawanya wanafunzi wa UDOM waliohudhuria mahafali ya CHASO katika hoteli moja huko Dodoma, Polisi wazuia msafara wa Maalim Seif, Polisi.....Polisi....Polisi!!!!!!!????????

Ukiona kila taarifa ya habari inaanza na Polisi, jua tayari tumeingia kwenye...........

Kwa hisani ya Mtatiro
Bado kumzingira Mungu sasa na yeye akifanya Fyokofyoko anazingirwa. malaika jiandaeni!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Tatizo la huyu inaelekea hashauriki, yeye ndiye yeye.

Inawezekana kabisa akawa na lengo zuri,ila njia anayotumia ni mbaya Sana! Nafikiri tumpe ushauri wa njia za kufanya kazi vizuri kuliko kupo
nda mda wote
 
Uzi huu unaweza kabisa kuwa muafaka kuhusu unyanyaswaji mkubwa unaofanywa na Polisi nchini katika kubaka demokrasi ili kutimiza lengo la Dikteta la Watanzania kuishi kwenye nchi iliyojaa vitisho vya hali ya juu. Kufungua uzi mwingine pia wa manyanyaso ya Polisi nchini RUKHSA.
Tatizo mnalaumu idara ya polisi bila kufahamu kuwa polisi wanafanya kazi yao ya kila siku nayo ni kutekeleza maagizo kutoka kwa watawala, nashauri tusiwalaumu polisi wetu bali lawama zote zipelekwe kwa wanaotoa hizi ORDERS. Idara yetu ya Polisi ni nzuri sana sema aina ya wanasiasa tulionao ndio wanawaingiza matatizoni.
 
alafu cha kuchekesha polisi mshahara wao unalipwa na wananchi hao hao wanao wanyanyasa. Kama siyo dharau hiyo.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom