Polisi wahaha kufuta ushahidi wa bomu na risasi

Polisi wahaha kufuta ushahidi wa bomu na risasi

Polisi mkoani Arusha wakishirikiana na kikosi kilichoundwa kufatilia swala la bomu na risasi walizofurumishiwa wana chadema tarehe 15.06.2013 zilizopelekea vifo vya watu wanne na majeruhi zaidi ya 70, leo wameanza msako wa kukamata wapiga picha wote ambao huonekana kwenye mikutano ya chadema na kila wanapo kukamata wana enda kwako kupekua na kuchukua memory card, flash, cd na kama una komputer wanabeba, mpka sasa wapiga picha wawili wamesha kamatwa.....

Polisi waache kutumia makamasi kufanya maamuzi. wanadhani waandishi ni wapumbavu kama akina Mwigulu kukaa na sensitive docs kama ile?
 
Waje kwangu niwape ili waone aibu...

Lakini wao nao ni wazembe kweli! Mbona siku ile walikuwepo kwenye gari lao pale uwanjani, ina maana hawana hata simu zenye kamera kurekodi matukio!:clap2:
 
muwaache, ni kwamba wanajaribu kutaka kufuta ushahidi na si kutafuta ushahidi. kama wangekuwa wanataka kutafuta ushahidi basi tangu day one wangekuwa wapole na kujaribu kuomba ushirikiano kwa raia wangefanikiwa. sasa chaajabu wanaleta mkuu wa kikosi maalumu kuja kufrastrate watu, tisha tisha, na wale waliosema wanaushahidi wakaanza kuwaita waoongo. sasa kama waongo leo wanatafuta nini? waache unafiki
 
Mi sishangai polisi wanachokifanya maana uwezo wa kufikiri sio kigezo cha mtu kuwa polisi.
 
Huwezi kufanya mawazo yako yakawa mawazo ya watanzania wote na huwezi kupotosha watu wote wewe.
 
Wanakumbuka shuka wakati kumekucha. Kwanini hawakuhangaika hivyo wakati wa Dr. Ulimboka, Kibanda na Kubenea? Utashaanga kesho kusikia wanapelekwa Igunga kufunguliwa kesi za ugaidi
 
Hawa wanadhani bado tuko mwaka 47!!!! Sijui wanaishi dunia ipi ya kudhani wanaweza kuharibu ushahidi wa bomu la magamba baada ya wiki mbili kupita!!!

Siku hizi habari hupepea kama upepo. Vilevile data huwekwa kwenye mawingu ambapo kuzipata ni shida. Ndio maana tunaona kuwa tukio likitokea linasambaa ulimwengu mzima baada ya sekunde chache, na ukitaka kuzifuta zipo mahali zimehifadhiwa huwezi kuzipata. Wamepitwa na wakati!
 
Hivi mtu akitaka kutukana polisi humu JF unaandikaje? Wakafute na ile damu iliyomwagika, halafu warudishe uhai wa waliowaua kabla hawajaponya majeraha ya mwili na roho ya wanaArusha na watanzania kwa ujumla.


...................................
 
Ama kweli ujinga ni zigo la kuni. Wanasahau kwamba hizi ni enzi za digitali, siyo zile enzi za black and white negative?
 
Tanzania nchi inayoendeshwa kidikteta. Hawa usalama wa tz hawajui kama kuna cloud computer siku hizi. Au hao wana Habari hawatumii cloud computers?
 
Huwezi kufanya mawazo yako yakawa mawazo ya watanzania wote na huwezi kupotosha watu wote wewe.

wewe Mwigulu ndio mpotoshaji,hamuwezi kuongoza nchi kwa mtindo wa zamani wa Zidumu fikra za Mwenyekiti..ngumu kuwashikia chini watanzania wa kizazi hiki.CCM imeshayeyushwa.
 
Huu ni ujinga kutaka kuwaaminisha watanzania kuwa sasa ukiwa chadomo hutakiwi kuhojiwa na vyombo vya usalama.lazima siasa zenu za kijambazi muweke kushoto hii nchi siyo yenu peke yenu na mjue kikinuka mtakuwa wa kwanza kukimbia,acheni polisi wafanye kazi yao kama hawqna hatia wataachiwa.
 
polisi acheni upambaf kwanini mtumie nguvu nyingi kiasi hicho kuliko akili agh
 
Mbwa nas mwenye mbwa wote vichaa. Nchi unamkabidhi mwigulu na nape, uchizi mtupu.
 
Back
Top Bottom