sungusungu
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 3,057
- 722
Hii nchi ina mengi
Hawaja chemka. Huo ndio muendelezo wa ukandamizaji wa upinzani. Yaani kama Chadema walusimama kusakimiana na wafuasi wao wakawekwa selo itakuwa watu kuandamana na mabango polisi hawajui?? Aibu jamani.SIKU chache baada ya Jeshi la Polisi nchini kupiga marufu maandamano na mikutano ya vyama vya siasa nchini, wafuasi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo wameandamana.
Maandamano ya CCM yamefanyika jijini Mwanza. Yameanzia katika Kata ya Mahina na kwenda kwenye ofisi za chama hicho zilizopo Barabara ya Nyerere kisha kupokelewa na Idd Mkowa, Katibu wa CCM Wilaya.
Hivi karibuni Jeshi la Polisi nchini lilipiga marufuku maandamano na mikutano ya vyama vya siasa kwa kile ilichodai kutokuwepo kwa hali nzuri ya usalama jambo ambalo limeibua mjadala kitaifa.
Hatua ya polisi kuzuia mikutano hiyo ilitokana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutangaza kufanya mikutano ya hadhara ya kuishtaki serikali kwa wananchi kutokana na kuendesha nchi bila kufuata kanuni na sheria pamoja na kuzuia kuoneshwa matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya Bunge.
Hata hivyo, baada ya Chadema kutangaza kufanya oparesheni hiyo iliopewa jina la ‘Okoa Demokrasia Nchini’ Polisi kupitia kwa Kamishna wa Mafunzo wa Polisi, ilizuia kufanyika kwa mikutano hiyo kwa kile ilichodai, hali ya usalama kuwa tete nchini.
Kutokana na zuio hilo, Chadema chini ya Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, kimekwenda mahakamani kuwashitaki Wakuu wa Polisi wa Wilaya za Geita na Kahama, Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Polisi Makao Makuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).
Pamoja na kuwepo kwa katazo hilo, leo wafuasi wa chama tawala (CCM) wameandamana kwa madai kuwa James Bwire, Diwani wa Kata ya Mahina ambaye pia ni Meya wa Jiji la Mwanza ananyanyaswa pia kutishiwa kuuawa na baadhi ya madiwani na watumishi wa jiji hilo ambao hawakutajwa majina.
Wanachama na wafuasi hao waliandamana wakiwa na mabango huku wakiimba nyimbo za chama hicho. Kwenye maandamano hayo polisi hawakuingilia kati.
Maandamano hayo yaliongozwa na Felician Balukali, Mwenyekiti wa Wazazi Kata ya Mahina na Teleza Chacha, Katibu wa CCM wa kata hiyo.
“Tunataka diwani wetu (James Bwire) awaachie umeya wao abaki kuwa diwani wa kushughulikia matatizo yetu, kwa nini anyanyaswe kama shida ni uongozi wao wabaki nao waendeleo nao,” amesema Chacha.
Ahmed Msangi, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza akizungumza na waandishi wa wanahabari leo amedai kuwa, hana taarifa za tukio hilo na kwamba, polisi hawapo kwa ajili ya kukibeba chama chochote cha siasa licha ya kushindwa kuyazuia maandamano hayo.
Msangi ambaye pia ni Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi (SACP) amesema, ” kwanza hilo tukio silifahamu ndio nasikia kutoka kwenu, nitalifuatilia kwa ukaribu na polisi hatupo kwa ajili ya kukilinda chama chochote kile cha siasa,” amesema.
Meza tu hata ufe tujue mojaMh..... Ngumu kumeza
Mkuu ni kweli <UKWELI SIKU ZOTE UTATUWEKA HURU> Lakini si hiki ulichokileta hapa ambacho hakina kithibitisho chochote zaidi ya maneno uliyoaandika ukiwa CHUMBANI.....TUPIA PICHA ZA HAYO MAANDAMANO unayoita ni ya CCM hapa MWANZA...
Cheki habari marudio saa tano usiku ITV au Channel 10....ha ha ha ha my lovely country TzHata chanel ten wameonyesha
Wasipokuwa na kazi watageuka kuwa majambazi huku mitaani.ukaguzi wa vyeti feki ukifanywa polisi kwa makini bila upendeleo karibu asilimia 60 (60%) ya polisi wote hawana kazi
Wewe umeangalia taarifa ya habari ya itv?Nipo mwanza sijaona maandamano mtoa post aweke picha tafadhali
Azam Tv,ITV na Channel 10 wameonesha...ushaidi tosha na mungu akipenda kesho front page ndio habari kuuMkuu uzi wako umeleta saa kumi na mbili jioni na taarifa ya HABARI chanel ten ni saa moja hivyo moja kwa moja wewe ndio primary source kuu ya information humu JF sasa tunategemea uje na full evidance na si kuniuliza nimeangalia taarifa chanel ten
Habari hii imethibitishwa? Watu wanajua kulaumu bila kuwa na facts hivi ikiwa RPC amejibu kwamba hana taarifa unawezaje kumlaumu bila Ushahidi?
Azam Tv mkuu wameonyesha tena wamepanda daladala 2 full kelele na walipokaribia wakashuka full mibango na wakapokewa....hiiITV wanaonyesha sasa
Wanahabari hawajui maandamano ni nini. Inasikitisha sana. Uchunguzi lazima ufanywe kujua lengo la huyu mwandishi kuita hili kusanyiko ni maandamano huku kashindwa kutuonesha hata mita ishirini ya watu wakitembea bali ni kutuonesha wakiinua mabango yao wakiwa ofisi za chama cha mapinduzi. Kama lengo lake ni kuuhabarisha umma kuwa polisi wanaupendeleo wakati si kweli hatua kali lazima zichukuliwe dhidi ya mwanahabari huyu.
Mikutano ya siasa na maandamano si yamepigwa marufuku...