Nimeangali taarifa ya habari ya ITV saa 2 usiku pamoja na ile ya Star tv kuhusu kile kinachodaiwa ni wafuasi wa CCM kuandamana huko mkoani Mwanza.
Star tv hawajasema kama wafuasi hao wa CCM wameandamana badala yake wameonyesha picha za wafuasi hao wakiwa wamekusanyika katika ofisi za CCM huko Mwanza.
ITV,kwa upande wao wameripoti kuwa wafuasi hao wa CCM wameandamana kwa aina yake kwa kukodi magari (magari 3 kama sikosei) mpaka katika ofisi hizo za CCM.
Maswali:
1.ITV,kusafiri kwa magari ya kukodi ndio kuandamana?
2.Je,inawezekana ITV mkawa mmeripoti tukio hili pasipo ukamilifu wake?
3.Star tv,nanyi hamjasema kama waliandamana au laa,je ukweli ni upi?
4.ITV,nimewasikia mkiripoti kumuhoji RPC wa Mwanza kuhusu maandamano hayo.Sasa ITV, mnaweza kweli kumuhoji RPC kuhusu maandamano kama kweli walisafiri kwa magari na si kuandamaa barabarani?
Bahati mbaya hata maelezo ya RPC mliyoyatoa nilishindwa kuyaelewa kama ndio yalikuwa mahususi yanajibu swali hilo au ndio alikuwa anatoa tu maelezo ya jumla kuhusu tukio zima maana sikumsikia akitamka neno maandamano.
Kwa taarifa,katika moja ya kituo cha tv kati ya hivi viwili nilivyovitaja hapa (sikumbuji ni kipi) wafuasi hawa wa CCM wameonekana kukusanyika huku wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali.
Ninachojouliza,mabango bila kuandamana inawezekana?
Je,ndio tuseme mabango yale yalikusudiwa kuonyeshwa katika ofisi za CCM tu na si huko walikopita?
Naona tusubiri magazeti ya kesho labda ndio yataweka wazi ni nini hasa kilitokea huko Mwanza.