Polisi wachemka, CCM waandamana Mwanza

Polisi wachemka, CCM waandamana Mwanza

Suala no maandamano kuzuiliwa haijalishi ya amani au ya nini jamani CCM mwogopeni mungu


Hivi yale yalikuwa ni maandamano kweli au ni propaganda tu...watu wamekuja na daladala tatu walizokodisha na wakaingia ofisini mwao na mabango, sasa hayo ndiyo yanaitwa maandamano???!!!
 
Mbona mnashangaa! Hivi ukiambiwa ukamate bajaji daladala zinakuhusu nini? halafu unaambiwa kuna basi limepita barabara ya mwendokasi unasema hiyo sijui ah! mambo ni hivi, Tii amri kwanza maelezo baadaye!
 
Nimeangali taarifa ya habari ya ITV saa 2 usiku pamoja na ile ya Star tv kuhusu kile kinachodaiwa ni wafuasi wa CCM kuandamana huko mkoani Mwanza.

Star tv hawajasema kama wafuasi hao wa CCM wameandamana badala yake wameonyesha picha za wafuasi hao wakiwa wamekusanyika katika ofisi za CCM huko Mwanza.

ITV,kwa upande wao wameripoti kuwa wafuasi hao wa CCM wameandamana kwa aina yake kwa kukodi magari (magari 3 kama sikosei) mpaka katika ofisi hizo za CCM.

Maswali:
1.ITV,kusafiri kwa magari ya kukodi ndio kuandamana?

2.Je,inawezekana ITV mkawa mmeripoti tukio hili pasipo ukamilifu wake?

3.Star tv,nanyi hamjasema kama waliandamana au laa,je ukweli ni upi?

4.ITV,nimewasikia mkiripoti kumuhoji RPC wa Mwanza kuhusu maandamano hayo.Sasa ITV, mnaweza kweli kumuhoji RPC kuhusu maandamano kama kweli walisafiri kwa magari na si kuandamaa barabarani?

Bahati mbaya hata maelezo ya RPC mliyoyatoa nilishindwa kuyaelewa kama ndio yalikuwa mahususi yanajibu swali hilo au ndio alikuwa anatoa tu maelezo ya jumla kuhusu tukio zima maana sikumsikia akitamka neno maandamano.

Kwa taarifa,katika moja ya kituo cha tv kati ya hivi viwili nilivyovitaja hapa (sikumbuji ni kipi) wafuasi hawa wa CCM wameonekana kukusanyika huku wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali.

Ninachojouliza,mabango bila kuandamana inawezekana?

Je,ndio tuseme mabango yale yalikusudiwa kuonyeshwa katika ofisi za CCM tu na si huko walikopita?

Naona tusubiri magazeti ya kesho labda ndio yataweka wazi ni nini hasa kilitokea huko Mwanza.
Soma Tanzania Daima la kesho.
 
Wananchi wamevurugika baada ya kuvurugwa na Maamuzi ya kukurupuka ya Mwendokasi. That's why unapata Taarifa ziluzovurugika Mwanzo mwisho. Kila mtu kavurugika, hata wewe mkuu umevurugika hata hauelewi kipi ni kipi.
 
Kumbe ulinielewa kiasi cha kutokuwa na hoja za kupinga nilichoandika!! Haya ukipata ushahidi wa maandamano utatuonesha. Kilichoonekana ni mkusanyiko wa wanaccm wakiwa na mabango kwenye ofisi yao.
Wanachadema huwa hamjui kuteua maneno ya kuwasilisha taarifa zenu kwa makusudi au kwa kutokujua. Mlichokiandika maandamano si maandamano.

Maandamano na mikusanyiko ya vyama vilipigwa marufuku.
 
Kuna kitu kinaitwa body language,kwani hukuona sura ya muulizwa swali haikua na amani na badala yake kajibu kitu tofauti
 
Hizi Taarifa za Kiintelijensia za Jeshi la Polisi huwa ni kwa vyama vya Upinzani pekee yake? Mbona maandamano ya Chama Cha Majipu/Magamba (CCM) hizo intelijensia hupoteza dira?!?

Katika Serikali inayojinasibu "Hapa Kazi Tu" RPC kushindwa kujua yamefanyika maandamano au la, ni Uzembe wa hali ya juu!

Na kama kweli alikuwa hajui, basi Chama Cha Majipu (CCM) kishtakiwe kwa kuendesha maandamano bila kibali cha Polisi.

Haya yanawezekana tu, katika nchi isiyofuata Misingi ya Utawala wa Sheria, Haki na Usawa.
Hahahahah! Eti Chama Cha Majipu.. Nimeipenda hii mkuu
 
ITV wapo kwenya payroll ya mzee wa mamvi so lazima wajitutumue ili kulipa fadhila
Wale watu wangekuwa ukawa hata kama wangekodi magari bado wangekutana na kipigo na maji ya kuwasha kuwasha kwa kisingizio maandamano yamekatazwa. Kwani inteligensia ya polisi ilikuwa wapi mpaka watu wajipange wasafiri tena wakiwa kwenye unifomu hadi kwenye ofisi?
 
Wangekuwa wametembea kwa miguu picha lazima zingefurika mitandaoni wala usingesubiri magazeti ya kesho.

Kwanza ITV inajulikana habari za aina hii haiwezi kumumunya maanake ndo wanazipenda ingekuwa Startv sawa.
 
Nimeona. Ila wale walikuwa wameandamana kwenda ofisi za CCM kudai ulinzi wa Meya wao. Hawa wanaCCM wametokea kata ya Meya.

Kisichowazi ni kuwa wamehojiwa wakiwa ofisini pale tu.
 
Yule mkuu wa polisi alikuwa anajibu maswali huku anajishitukia
 
Back
Top Bottom