Polisi wachemka, CCM waandamana Mwanza

Polisi wachemka, CCM waandamana Mwanza

Habari hii imethibitishwa? Watu wanajua kulaumu bila kuwa na facts hivi ikiwa RPC amejibu kwamba hana taarifa unawezaje kumlaumu bila Ushahidi?
 
SIKU chache baada ya Jeshi la Polisi nchini kupiga marufu maandamano na mikutano ya vyama vya siasa nchini, wafuasi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo wameandamana.

Maandamano ya CCM yamefanyika jijini Mwanza. Yameanzia katika Kata ya Mahina na kwenda kwenye ofisi za chama hicho zilizopo Barabara ya Nyerere kisha kupokelewa na Idd Mkowa, Katibu wa CCM Wilaya.

Hivi karibuni Jeshi la Polisi nchini lilipiga marufuku maandamano na mikutano ya vyama vya siasa kwa kile ilichodai kutokuwepo kwa hali nzuri ya usalama jambo ambalo limeibua mjadala kitaifa.

Hatua ya polisi kuzuia mikutano hiyo ilitokana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutangaza kufanya mikutano ya hadhara ya kuishtaki serikali kwa wananchi kutokana na kuendesha nchi bila kufuata kanuni na sheria pamoja na kuzuia kuoneshwa matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya Bunge.

Hata hivyo, baada ya Chadema kutangaza kufanya oparesheni hiyo iliopewa jina la ‘Okoa Demokrasia Nchini’ Polisi kupitia kwa Kamishna wa Mafunzo wa Polisi, ilizuia kufanyika kwa mikutano hiyo kwa kile ilichodai, hali ya usalama kuwa tete nchini.

Kutokana na zuio hilo, Chadema chini ya Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, kimekwenda mahakamani kuwashitaki Wakuu wa Polisi wa Wilaya za Geita na Kahama, Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Polisi Makao Makuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

Pamoja na kuwepo kwa katazo hilo, leo wafuasi wa chama tawala (CCM) wameandamana kwa madai kuwa James Bwire, Diwani wa Kata ya Mahina ambaye pia ni Meya wa Jiji la Mwanza ananyanyaswa pia kutishiwa kuuawa na baadhi ya madiwani na watumishi wa jiji hilo ambao hawakutajwa majina.

Wanachama na wafuasi hao waliandamana wakiwa na mabango huku wakiimba nyimbo za chama hicho. Kwenye maandamano hayo polisi hawakuingilia kati.

Maandamano hayo yaliongozwa na Felician Balukali, Mwenyekiti wa Wazazi Kata ya Mahina na Teleza Chacha, Katibu wa CCM wa kata hiyo.

“Tunataka diwani wetu (James Bwire) awaachie umeya wao abaki kuwa diwani wa kushughulikia matatizo yetu, kwa nini anyanyaswe kama shida ni uongozi wao wabaki nao waendeleo nao,” amesema Chacha.

Ahmed Msangi, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza akizungumza na waandishi wa wanahabari leo amedai kuwa, hana taarifa za tukio hilo na kwamba, polisi hawapo kwa ajili ya kukibeba chama chochote cha siasa licha ya kushindwa kuyazuia maandamano hayo.

Msangi ambaye pia ni Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi (SACP) amesema, ” kwanza hilo tukio silifahamu ndio nasikia kutoka kwenu, nitalifuatilia kwa ukaribu na polisi hatupo kwa ajili ya kukilinda chama chochote kile cha siasa,” amesema.
Badilisha Heading, kusema Polisi wachemka umewadhalilisha!
 
Sina porojo ukweli utatuweka huru
Mkuu ni kweli <UKWELI SIKU ZOTE UTATUWEKA HURU> Lakini si hiki ulichokileta hapa ambacho hakina kithibitisho chochote zaidi ya maneno uliyoaandika ukiwa CHUMBANI.....TUPIA PICHA ZA HAYO MAANDAMANO unayoita ni ya CCM hapa MWANZA...
 
Habari hii imethibitishwa? Watu wanajua kulaumu bila kuwa na facts hivi ikiwa RPC amejibu kwamba hana taarifa unawezaje kumlaumu bila Ushahidi?
Uko sahihi mkuu! Coz CCM huwa hawahitaji kupata kibari kuandamana!
 
Mkuu ni kweli <UKWELI SIKU ZOTE UTATUWEKA HURU> Lakini si hiki ulichokileta hapa ambacho hakina kithibitisho chochote zaidi ya maneno uliyoaandika ukiwa CHUMBANI.....TUPIA PICHA ZA HAYO MAANDAMANO unayoita ni ya CCM hapa MWANZA...
Umeangalia chanel Ten Tarifa ya Habari?
 
Umeangalia chanel Ten Tarifa ya Habari?
Mkuu uzi wako umeleta saa kumi na mbili jioni na taarifa ya HABARI chanel ten ni saa moja hivyo moja kwa moja wewe ndio primary source kuu ya information humu JF sasa tunategemea uje na full evidance na si kuniuliza nimeangalia taarifa chanel ten
 
Ahmed Msangi, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza akizungumza na waandishi wa wanahabari leo amedai kuwa, hana taarifa za tukio hilo....
Naona hapa taarifa za kiintelijensia hakupata....huyu kamanda ni [emoji90] [emoji90] [emoji90]
 
Msangi anajulikana alikotoka hadi hapo alipo....nini accelerator yake kufika hapo inajulikana! Hana lolote awezalo kufanya! Aibu imemjaa hata week bado double standard imemuumbua! Mchumia tumbo number 1 ndani ya jeshi la Polisi!.....Siku si nyingi watagombana na RC wake maana wote wajuaji! Tuone........sham on you RPC
Huyo RPC arejeshwe wizarani aende akasome magazeti maana huu unafiki wake umepitliza
 
Mfumo wa Serikali wa Chama cha Mapinduzi bado utaendelea kutukandamiza mpaka pale tutakapo weka unafiki pembeni ,wanaweza kuyafanya haya kwa sababu mefanikiwa kutugawa kwa dini zetu /itikadi zetu na mambo kibao.Katiba ya Nchi imempa Raisi mamlaka makubwa sana ,anaweza kuitumia vibaya kwa manufaa ya Chama anachotoka au kwa namna yeyote ile ...
 
What can you say. about this?

CHADEMA wanapigwa mabomu kahama, mikutano yote na maandamano yote kuzuiwa.

Sasa swali linakuja, iweje CCM washiriki siasa na hadi kufanya maandamano huko Mwanza?

Kama ikithibitika kuwa waliruhusiwa itakuwa double standards. Na kama hawakuruhusiwa kwanini hawakupigwa mabomu kama CHADEMA kule Kahama?

je hii itakuwa sawa?

Kama ingekuwa Ulaya mambo kama haya yanapotekea you take responsibility kwa kujiuzulu.

Tunamuomba IGP ajitafakari.
 
Ccm wanajua kuandamana kwa amani,

Hapo ingekuwa machadema watu wangefanyiwa fujo na kulazimishwa kuandamana
Leo maji yamewafika shingoni,
Nyie CCM kila siku huwa mnasema kuandamana ni upumbavu watu wakafanye Kazi, Leo hii mnasifia maandamano kwa kuwa ni wanywa viroba wa CCM ndiyo wameandamana?
 
Back
Top Bottom