POTOSHI Polisi auwawa kwa kuchomwa Moto na baadhi ya wananchi baada ya kubainika kushiriki kwenye mauaji ya October 29

POTOSHI Polisi auwawa kwa kuchomwa Moto na baadhi ya wananchi baada ya kubainika kushiriki kwenye mauaji ya October 29

Uhalisia wa taarifa hii umepindishwa ili kupotosha
Source #1
View Source #1
Auwawa kwa kuchomwa Moto na baadhi ya wananchi baada ya kubainika kushiriki kwenye mauaji ya October 29

1769672405039.png

 
Tunachokijua
Januari 28, 2026 kumekuwapo na video inayosambaa katika mitandao ya kijamii ikielezwa kuwa ni ya tukio la Polisi kuchomwa moto na kupokonywa silaha mkoani Njombe baada ya wananchi kubaini kuwa alishiriki katika matukio ya Oktoba 29, 2025.

Uhalisia wa video hiyo

JamiiCheck imefanya ufuatiliaji kwa kina na kubaini kuwa video hiyo si ya mwaka 2026 na haihusiani na tukio la polisi kuchomwa moto Arusha.

Ufuatiliaji kwa kutumia nyenzo za kidigitali ikiwemo Google lens umebaini kuwa video hiyo ilichapishwa mtandaoni kuanzia Agosti 3, 2025 ambapo ilielezwa kuwa mtu mmoja aliyedaiwa kuwa ni mwizi alichomwa moto.

Vyanzo mbalimbali viliripoti kutokea kwa tukio hilo tazama hapa na hapa. Vyanzo hivyo vinaibainisha kuwa tukio hilo lilitokea katika mtaa wa Kirika B, kata ya Osinyae mkoa wa Arusha.

Inaelezwa kuwa kijana huyo alitambulika kwa jina la alikutana na mashambulizi hayo baada ya kudaiwa kuiba vinywaji na spika katika bar mmoja katika eneo hilo.
Tetesi: kuna video inasambaa mtandaoni inayodaiwa ni tukio la polisi aliyedaiwa kuhusika kwenye mkumbo wa kuuwa raia oct 29 ameuwawa na wananchi.

Video hiyo inaonesha maelfu ya wananchi wakiwa wamekusanyika huku moshi ukivuka katikati yao inadaiwa polisi huyo ameuwawa kwa kuchomwa moto na kupokonywa silaha.
 
Kanisa katoliki nao wanasemaje??

Maana wao pia si walituma vijana wao ile siku??
 
Sisi kwetu m1 kapooza karudishwa kwao Musoma,

Mwingine toka tar 4/10 hajarudi pale kituoni, vijana wanamsubiri kwa hamu sana, siku akitokea basi wanamalizana nae.
 
Nilijua watakanusha ila ukweli utajulikana tutapoanza kusikia matukio ya mauaji kwa kutumia bunduki
 
Back
Top Bottom