Polepole amefanya nimwelewe Magufuli

Polepole amefanya nimwelewe Magufuli

Wabongo wengi ni kama walianza kumjua Magu akiwa Rais...

Lakini ka utakuwa ulimfuatilia tangu akiwa waziri, jamaa alikuwa mwamba sana...

Kuminya siasa mbadala na CCM hii ndio kasoro pekee katika uongozi wake iliyoweka doa jeusi...
Siyo kuminya Siasa mbadala tu, Ongeza na hizi:-

1. Kuitisha Mahakama na kuifanya kibaraka wa Mhimili wa Serikali. Mahakama imebakia kupokea maelekezo ya Serikali, hii kitu inasumbua sana haki za watu. Angalia hata kesi ya TAL inavyopigwa danadana

2. Kuminya uhuru wa maoni na vyombo vya habari

3. Kuliendesha bunge kwa remote control. Kumbuka maelezo aliyokuwa anampa Ndugai, anamuambia awabane wabunge ndani ya bunge na yeye atawabana nje

4. Kuiba uchaguzi wote wa 2019 na wa 2020. Michezo ya kuharibu uchaguzi kwa kuwa disqualify wagombea wa upinzani ilianzishwa na Magufuli

5. Kuanzisha kikundi cha utekaji na mauaji (rogue unit within the security system) maarufu kama wasiojulikana chini ya Daudi Bashite

Hitimisho:-
Yaani kama mtu ameharibu hiyo misingi 5 hapo juu sielewi mnaomtetea mnatumia mantiki gani. Maana haya machafu ya Samia kipindi hiki cha 2021-25 ni muendelezo wa uchafu wa Magufuli ambao zamani haukuwapo. Hata hivyo Samia amejitahidi kwa kiasi kikubwa kupunguza uchafu huo japo hajamaliza.

Watanzania too wepesi wa kusahau. Hebu kumbukeni historia ya nchi yetu hadi November 2015, haikuwa na haya mambo tunalalamika. Ni Magufuli ndiyo katufikisha hapa
 
Jamaa ni bilionea... Si ajabu ndiyo maana kule kigamboni alikatwa😄😆
Allen Kilewella unejivunjia heshima yako kwa kiasi kikubwa kwa kuanzisha uzi huu. Yaani elimu yako yote, exposure yako yote na contacts zako za vyombo vya habari vya nje, wewe kweli ndiyo wa kuanza kumuabudu Humphrey Polepole??

Tutake radhi please
 
Mkuu wangu Allen Kilewella naungana na fikira zako Concrete, na mimi nakiri nilikua kwenye mkondo huo huo wa kwako, lakini toka majuzi nimekua napitia picha za maombolezo ya JPM natiririkwa na machozi ya kiume.

Perverse 😞
Kama unatiririkwa machozi kwa picha za msiba wa Magufuli basi wewe machozi yako hayana thamani. Wewe ni bwege tu
 
Unaongelea matibabu ya TAL? Kwanini usiongelee tukio la kutaka kumuua Lissu? Magufuli alikuwa ni shetani kwenye umbo la binadamu (Satan trapped in human body)

Alipanga kabisa timu ya wachimba kaburi Ikungi, yaani maiti ikitoka Dodoma isije Dar iende moja kwa moja Ikungi.

Alizuia Lissu asifanyiwe maombi na watu walio print Tshirt za Getwell TAL walikamatwa.

Akamnyang'anya ubunge wake kwa kushirikiana na Ndugai na akamnyima mafao ya ubunge
Hili tukio halikuwa la kibinadamu kabisa.
 
Kwenye hotuba zake alikuwa anapenda sana kusema maneno haya;
1. Ndugu zangu watanzania mniombee
2. Ndugu zangu watanzania hakuna vita ngumu kama vita ya uchumi.
 
Kwanini unawalaumu vyombo vya ulinzi ilihali unawajua wanaowateua???

Wewe ni boss ukiniteua niwe RPC unadhani nitatenda kinyume na matakwa yako?
Japo Polepole kaonyesha hata kama umeniteua lakini natakiwa kufuata maadili ya kazi na viapo vya hiyo kazi na si kuwa upande wako hata kama unatindiganya mambo.

Amekili JK alimtuma kwenda somewhere kujifunza mambo na kuijua nchi yake kisawasawa na yale mafunzo yalimwingia barabara na ndo maana yuko tayari kuacha maslahi manono na privilege kibao za kibalozi na kupigania nchi yake.

Majeshi yetu na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ni kama wamekosa kabisa au hawana kabisa uzalendo kwa taifa lao. Haiwezekani nchi ichezeshwe mchakamchaka na kakikundi kadogo namna hiyo halafu wao wanafurahia kupewa viposho vya uongo na kweli huku taifa likineemesha majizi na walafi wa mali za nchi. Wanatakiwa wajitafakari sana na ikiwezekana wachukue hatua madhubuti za kukomesha udalali wa mali zetu. HHP ameonyesha uzalendo mkubwa na mnene sana kwa taifa lake. Mungu amlinde na ampe moyo wa dhati na pia atujalie taifa letu lijitoe kwenye makucha ya JK na genge lake.
Amina!!
 
Hakurudishwa tena bungeni....Juma Nkamia na yule ponjolo WA Rukwa Au umesahau?
Kwa hiyo Magufuli ndiyo alikuwa anawachagulia wananchi mbunge badala ya wananchi kumchagua mwakilishi wao?
 
Wakati akiwa hai nilikuwa namuona John Pombe Magufuli pamoja na kutaka aonekane mzalendo, niliona kuwa ni mtu asiye na nia njema Kwa Taifa letu na mtaka sifa.

Lakini baada ya Polepole kuelezea mambo mengi yaliyokuwa yanafanyika nyuma ya pazia, sasa nimeanza kuelewa kuwa Magufuli alikuwa na dhamira njema kwa Tanzania.

Kumbe Magufuli baada ya kugundua fedha zinachotwa serikalini, yeye akaamua kuziwekeza kwenye miradi ili kama ni madeni ni bora watanzania walipe lakini wakiwa wana miundombinu inayowasaidia kuendesha maisha yao.

Zile hotuba zake kama anapambana na mara majeshi au watumishi wa Serikali, Leo zinaleta mantiki zaidi kuliko wakati akizitoa.

Magufuli alikuwa anajua yupo peke yake kwenye harakati za kuijenga Tanzania maana hata watu kama Makonda kumbe nao Wana vimelea vya CCM mtandao.

Ukweli utajulikana siku moja.
Natamani Polepole amguse Makonda
 
Kwa ujinga wako huwa unachagua tukio la Lissu peke yake ili kutimiza lengo lako. Samia anaua vijana wasio na hatia kama nzi lakini wewe ndiye chawa wake mkubwa.
Amewaua akina nani? Au badala ya kuwa macho mdiliko umekuwa macho malyenge!!
 
Ili umhukumu lazima ujue aliambiwa Nini kuhusu huyo...Je kama alimwona kama adui wa Taifa wewe unge react vipi?
Ni nani anayepima mtu kuwa ni adui wa Taifa au Rafiki wa Taifa? Je kama ni adui wa Taifa kwa nini hakumpeleka Mahakamani? Hakuna mtu mwenye haki ya kutoa uhai wa mtu?? Hebu shirikisha ubongo kwenye kabla ya kuandika
 
Ni ujinga kumfananisha mwehu na Xi

Wewe bado ni mdogo sana kwenye siasa kama kirahisi tu unaendeshwa na propaganda za polepole.

Kwa kweli hili saga la polepole limefanya nijue kuwa Watanzania wengi bado ni wajinga sana katika mambo ya siasa inasikitisha hawa ndio wanataka kupata uhuru kamili wa kuchagua kiongozi makini so sad.
Watanzania wajinga sana mkuu. Yaani Polepole ambaye alikuwa ni architect wa kuharibu Tanzania yetu, leo kakosa nafasi nyeti kwenye Serikali na kuanza kuropoka, eti watu wanamuona mzalendo
 
Kosa lake ni kuua demokrasia na kuamini kuwa maadui zake walikuwa Chadema kumbe maadui alikuwa anakula nao meza moja.
Kwa nchi ilipofikia hakuwa na namna nyingine..... and of course kuna viongozi wa CDM pia kwao maendeleo ya nchi si kitu kikubwa chama chao kichukue dola....Hawa ungewezaje kudeal nao
 
Back
Top Bottom