Polepole amefanya nimwelewe Magufuli

Polepole amefanya nimwelewe Magufuli

Mawazo ya kijinga kama haya ndiyo yalimwangusha Magufuli na yakatufikisha hapa. Haya nikubaliane na huu ujinga kuwa hakuna upinzani wa kweli... kwa nini wasiweke mazingira mazuri kwa upinzani kuwepo kwa sababu ni jambo muhimu sana kwa nchi?
Hakuna kitu kigumu kujadili na mtu ambaye anajiona anajua wakati anaona upepo🤣🤣🤣

Haya Mkuu mm mjinga we mwerevu yaweke hayo mazingira mazuri tinayoyataka Mimi na wewe
 
Sema tena na tena. Alikuwa anatumia approach ya ajabu kabisa kwenye kuongoza. Nikupe mfano mwingine: Polepole anasema yule mbunge mjinga aliyependekeza eti Magufuli aongozewe muda wa urais, alitumwa na wana mtandao ili kumfanya Magufuli aonekane kuwa ni mroho wa madaraka. Well, inaweza kuwa ni kweli. Lakini hatua alizochokuwa ku deal na huyo mbunge zilikuwaje? Alimwita Polepole na kumlalamikia kuwa anahujumiwa na mtangulizi wake na kumwambia aseme kuwa Magufuli hataki kuongezewa muda. Je, alifanya nini kwa huyo mbunge mjinga ambaye alikuwa anamhujumu? Mbona hatukusikia anapewa onyo au adhabu nyingine yoyote?
Hakurudishwa tena bungeni....Juma Nkamia na yule ponjolo WA Rukwa Au umesahau?
 
Vipi kuhusu;-
1. Tsh 1.5 Trillion zilizoibuliwa na CAG 2016/17 na kisha kumfukuza CAG kazi

2. Fedha za Plea bargain feki alizokuwa anakusanya na DPP Biswalo Mganga na kuzificha China

3. Ununuzi wa ndege kupitia Boeing bila kufuata sheria ya manunuzi ya umma??

4. Mikataba ya akina Mayanga construction kujenga Chato International Airport

Nimesema machche lakini nataka nikuhakiishie hata Magufuli hakuwa na uchungu na mali za umma, bali alikuwa ni fisadi sawa na mafisadi wengine wa CCM.

Sina huruma naye kwa kuwa hata yeye Magufuli alikuwa anapanga kuwauwa wenzie, ni kwamba tu walimtaimu akaondoka yeye.

Polepole hana jipya
Wewe jamaa mjinga sana huyo CAG alitumika pia na wanamtandao
 
Vipi kuhusu;-
1. Tsh 1.5 Trillion zilizoibuliwa na CAG 2016/17 na kisha kumfukuza CAG kazi

2. Fedha za Plea bargain feki alizokuwa anakusanya na DPP Biswalo Mganga na kuzificha China

3. Ununuzi wa ndege kupitia Boeing bila kufuata sheria ya manunuzi ya umma??

4. Mikataba ya akina Mayanga construction kujenga Chato International Airport

Nimesema machche lakini nataka nikuhakiishie hata Magufuli hakuwa na uchungu na mali za umma, bali alikuwa ni fisadi sawa na mafisadi wengine wa CCM.

Sina huruma naye kwa kuwa hata yeye Magufuli alikuwa anapanga kuwauwa wenzie, ni kwamba tu walimtaimu akaondoka yeye.

Polepole hana jipya
Nilidhani utamzungumzia Jesca 😂😂
 
Yes, ila suala la matibabu ya TAL lilimchafua.
Unaongelea matibabu ya TAL? Kwanini usiongelee tukio la kutaka kumuua Lissu? Magufuli alikuwa ni shetani kwenye umbo la binadamu (Satan trapped in human body)

Alipanga kabisa timu ya wachimba kaburi Ikungi, yaani maiti ikitoka Dodoma isije Dar iende moja kwa moja Ikungi.

Alizuia Lissu asifanyiwe maombi na watu walio print Tshirt za Getwell TAL walikamatwa.

Akamnyang'anya ubunge wake kwa kushirikiana na Ndugai na akamnyima mafao ya ubunge
 
Mkuu wangu Allen Kilewella naungana na fikira zako Concrete, na mimi nakiri nilikua kwenye mkondo huo huo wa kwako, lakini toka majuzi nimekua napitia picha za maombolezo ya JPM natiririkwa na machozi ya kiume.

Perverse 😞
ni wakati wa Maungamo ni wakati wa kusema ukweli
 
Kauli zake kama mtanikumbuka,nimesacrifice maisha yangu na kadharika
Basi huko siyo kujiandaa bali ni kulalamika. Rais mwenye maono halalamiki bali anachukuwa hatua ili kama hayupo, mambo yasiharibike. Angekuwa ameandika katiba nzuri inayopunguza madaraka ya rais basi tusingefika hapa. Au angewachukulia hatua za kisheria wale CCM wenzake wote waliofanya ufisadi. Huyu mama Angela Kiziga, ni fisadi wa siku nyingi mno. Ni mtu wa Kikwete na kuna uzi uko hapa unamzungumzia tangu 2012. Hawa wote na hata Kikwete angewachukulia hatua sasa hivi wasingekuwa na nguvu. Hivi mtu kama Rostam unamfanyaje awe karibu na rais?
 
Unaongelea matibabu ya TAL? Kwanini usiongelee tukio la kutaka kumuua Lissu? Magufuli alikuwa ni shetani kwenye umbo la binadamu (Satan trapped in human body)

Alipanga kabisa timu ya wachimba kaburi Ikungi, yaani maiti ikitoka Dodoma isije Dar iende moja kwa moja Ikungi.

Alizuia Lissu asifanyiwe maombi na watu walio print Tshirt za Getwell TAL walikamatwa.

Akamnyang'anya ubunge wake kwa kushirikiana na Ndugai na akamnyima mafao ya ubunge
Kwa ujinga wako huwa unachagua tukio la Lissu peke yake ili kutimiza lengo lako. Samia anaua vijana wasio na hatia kama nzi lakini wewe ndiye chawa wake mkubwa.
 
Naona tuna mitazamo na uelewa tofauti wa siasa za Tanzania zilivyo na zinavyopaswa kuwa, hatuwezi fika muafaka...

Naona bado umekazana kutazama "ilivyo" na sio "inavyopaswa kuwa"...

Na kwa mtazamo wako huo maana yake hata hakuna haja ya kuwa na vyama including CCM kwa sababu watu wote kwenye siasa ni corrupt...
Umesema kweli...Kwanza hata uelewa wa mambo umetofautiana saaana Mimi na wewe...Usijali lakini hii ni kawaida kwenye maisha kwasababu experience na trainings zetu zinaweza kuwa ndiyo kisababishi
 
Basi huko siyo kujiandaa bali ni kulalamika. Rais mwenye maono halalamiki bali anachukuwa hatua ili kama hayupo, mambo yasiharibike. Angekuwa ameandika katiba nzuri inayopunguza madaraka ya rais basi tusingefika hapa. Au angewachukulia hatua za kisheria wale CCM wenzake wote waliofanya ufisadi. Huyu mama Angela Kiziga, ni fisadi wa siku nyingi mno. Ni mtu wa Kikwete na kuna uzi uko hapa unamzungumzia tangu 2012. Hawa wote na hata Kikwete angewachukulia hatua sasa hivi wasingekuwa na nguvu. Hivi mtu kama Rostam unamfanyaje awe karibu na rais?
Kulalamikia kifo ???
JPM ana mapungufu yake mengi,kwa upande wangu sitaki kuyaona hayo mapungufu maana siwezi kubadili chochote na hawezi badili chochote

Ninachokifanya nasheherekea ya mazuri niliyoyaona ndani ya uongozi wake

JPM🕊️
 
Unaongelea matibabu ya TAL? Kwanini usiongelee tukio la kutaka kumuua Lissu? Magufuli alikuwa ni shetani kwenye umbo la binadamu (Satan trapped in human body)

Alipanga kabisa timu ya wachimba kaburi Ikungi, yaani maiti ikitoka Dodoma isije Dar iende moja kwa moja Ikungi.

Alizuia Lissu asifanyiwe maombi na watu walio print Tshirt za Getwell TAL walikamatwa.

Akamnyang'anya ubunge wake kwa kushirikiana na Ndugai na akamnyima mafao ya ubunge
Ili umhukumu lazima ujue aliambiwa Nini kuhusu huyo...Je kama alimwona kama adui wa Taifa wewe unge react vipi?
 
Magufuli aliukataa mfumo mzima wa upinzani wakati alipaswa apambane na hao "wasaliti" na sio kutaka kufuta kabisa mfumo wa vyama mbadala...

Tazama sasa madhara ya alichokifanya sasa, hakuna mbadala na wenye CCM 'wamemuondoa' na wala hakuna wanaoweza pambana na jinamizi CCM...
Apumzike Kwa amani mwamba: Alisema Tanzania kuna hela nyingi....
 
Wakati akiwa hai nilikuwa namuona John Pombe Magufuli pamoja na kutaka aonekane mzalendo, niliona kuwa ni mtu asiye na nia njema Kwa Taifa letu na mtaka sifa.

Lakini baada ya Polepole kuelezea mambo mengi yaliyokuwa yanafanyika nyuma ya pazia, sasa nimeanza kuelewa kuwa Magufuli alikuwa na dhamira njema kwa Tanzania.

Kumbe Magufuli baada ya kugundua fedha zinachotwa serikalini, yeye akaamua kuziwekeza kwenye miradi ili kama ni madeni ni bora watanzania walipe lakini wakiwa wana miundombinu inayowasaidia kuendesha maisha yao.

Zile hotuba zake kama anapambana na mara majeshi au watumishi wa Serikali, Leo zinaleta mantiki zaidi kuliko wakati akizitoa.

Magufuli alikuwa anajua yupo peke yake kwenye harakati za kuijenga Tanzania maana hata watu kama Makonda kumbe nao Wana vimelea vya CCM mtandao.

Ukweli utajulikana siku moja.
Ndio maana Makonda aliachwa, acha upepo uendelee kuvuma nyeti za kuku zibaki wazi
 
Kulalamikia kifo ???
JPM ana mapungufu yake mengi,kwa upande wangu sitaki kuyaona hayo mapungufu maana siwezi kubadili chochote na hawezi badili chochote

Ninachokifanya nasheherekea ya mazuri niliyoyaona ndani ya uongozi wake

JPM🕊️
Unadhani ukifumbia macho upungufu wa rais kwa sababu ameshafariki na huwezi kurekebisha ndiyo dawa? Hapana. Dunia yetu imepata maendeleo kwa sababu ya kujifunza kutokana na makosa ya nyuma.
 
"SAFARI ya Maendeleo siyo lelemama" msemo huu ulitumiwa sana na aliyekuwa rais wa Tanzania,Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, kwa lengo la kuihamasisha jamii katika kuyapambania matamanio ya ndoto zao za maendeleo kwa manufaa ya sasa na baadaye.

Hatua hiyo ilikuwa ni chachu ya watu kufanya kazi kwa bidii baada ya serikali kuwatengenezea mazingira mazuri ya kuhakikisha kila mmoja anawajibika kwa kiwango chake ili kujiletea maendeleo yake,familia na taifa Kwa ujumla.

Hata hivyo kuna wakati alitumia maneno ya kitabu kitakatifu cha Biblia kwa nukuu ya "Asiye fanya kazi na asile" yote hayo ilikuwa ni kuwajengea watu uzalendo wa kufanya kazi kwa bidii na maarifa.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
YES... The guy was purely a scientist some sort of technocrats like China President Xi Jinping!
Ni ujinga kumfananisha mwehu na Xi

Wewe bado ni mdogo sana kwenye siasa kama kirahisi tu unaendeshwa na propaganda za polepole.

Kwa kweli hili saga la polepole limefanya nijue kuwa Watanzania wengi bado ni wajinga sana katika mambo ya siasa inasikitisha hawa ndio wanataka kupata uhuru kamili wa kuchagua kiongozi makini so sad.
 
Unadhani ukifumbia macho upungufu wa rais kwa sababu ameshafariki na huwezi kurekebisha ndiyo dawa? Hapana. Dunia yetu imepata maendeleo kwa sababu ya kujifunza kutokana na makosa ya nyuma.
Nimekuelewa ina maana vipi kuhusu yale mazuri ambayo alifanya marehemu.

Hastaili kupongezwa???
 
Back
Top Bottom