Polepole amefanya nimwelewe Magufuli

Polepole amefanya nimwelewe Magufuli

Wabongo wengi ni kama walianza kumjua Magu akiwa Rais...

Lakini ka utakuwa ulimfuatilia tangu akiwa waziri, jamaa alikuwa mwamba sana...

Kuminya siasa mbadala na CCM hii ndio kasoro pekee katika uongozi wake iliyoweka doa jeusi...
 
Nikiona mtu anakuja na ngonjera za kumsifia katili magufuli namuona kama mpuuzi tu, kipindi cha magufuli watu wameiba pesa za umma. Kina makondo, sabaya ni mabillionear kupitia magufuli, magufuli amaea watu kwa maslah yake binafs.
 
Shida yake kubwa ilikuwa ni ukabila na ukanda, pamoja na kushindwa kukubali kukosolewa
Hata wewe utakubali kukosolewa sakata la makinikia mkuu, unaweza kukubali kukosolewa ujenzi wa bwawa la nyerere, unaweza kubali kukosolewa pesa kuziingiza kwenye miundombinu kama madaraja, barabara flyover, n.k.

unaweza kubali kukosolewa kwenye kuwachukulia hatua kali mafusadi ambao wanakula pesa za nchi kama zao.

Sasa mwamba amekosolewa vyote nilivyotajwa na tukawa tunaaminishwa hataki ushauri wala hakubali kukosolewa. Hili nalo lilikuwa tatizo la kimfumo ambalo baadhi ya watu waliingia kwenye mtego huo.

In short he was a man of vission. Hata huu uchumi tunaouona umekua kwa sasa ni initiatives alizozianzisha, kutoa tu umeme wa uhakika unakuza uchumi pakubwa, kupunguza foleni unaongeza uchumi pakubwa, kuweka sheria za madini unaongeza uchumi pakubwa n.k
 
Nikiona mtu anakuja na ngonjera za kumsifia katili magufuli namuona kama mpuuzi tu, kipindi cha magufuli watu wameiba pesa za umma. Kina makondo, sabaya ni mabillionear kupitia magufuli, magufuli amaea watu kwa maslah yake binafs.
Nilichojifunza watu hawawi wema kwa kuwa aliyeko madarakani ni mwema, bali ni kutokana na mfumo unaowalazimisha wawe wema.

Makonda alifikishwa kwenye Tume ya maadili ya umma, nini kilitokea... Sabaya alifikishwa mahakamani, mahakama iliamua nini?
 
Mambo mengi hujengwa kwa kufuata taswira ya mitazamo yetu. Leo unajiuliza imekuwaje waliokuwa wapinzani wake ndani ya CCM Leo hii ndiyo wameshika hatamu za kiuongozi ndani ya CCM na serikali?

Halafu kama ni yeye binafsi ndiye aliyekuwa hataki kukosolewa... Mbona hawa wa sasa ndiyo wamezidisha mbinyo kwa wakosoaji wao?
Mkuu una akili kubwa sana
 
Magufuli alikuwa na mabaya yake pamoja na mazuri yake,lakini ukipima kwenye mizani mazuri aliyoyafanya katik nchi hii ni mengi mno.

Na ninaamini hata mauji mengi yalifanywa na wanamtandao ili kuichafua hadhi yake na urasi wake

Kama yeye tu ndio alikuwa muuaji basi inamaana baada ya kifo chake haya mambo yangekoma,lkn mbona yanaendelea tena kwa kiwango cha juu?

Think big
 
Wabongo wengi ni kama walianza kumjua Magu akiwa Rais...

Lakini ka utakuwa ulimfuatilia tangu akiwa waziri, jamaa alikuwa mwamba sana...

Kuminya siasa mbadala na CCM hii ndio kasoro pekee katika uongozi wake iliyoweka doa jeusi...
Aliminya kwakua alijua hao pia wanatumiwa na siyo demokrasia kama inavyodaiwa...Mbona mnaelezwa hizo proxies zilizoundwa Kwa sababu maalumu? Au hata kumwelewa Slow slow bado?

Wewe unajua unacheza na midoli ambayo inakupiga makwenzi hatari utaendelea kuwapa good time tu Ili wakukwamishe?
 
Dar ana majumba ya kifahari, Arusha ana majumba na mashamba ya kahawa, hapa Mwanza ana mahekalu na Musoma pia.
TAKUKURU wanahangaika na Maafisa misitu ( sisemi siyo sawa) wanaochukua rushwa za wachoma mkaa.

Hata Mwendesha mashtaka wa Serikali ana mamlaka ya kuanzisha uchunguzi...
 
nikiwakumbuka keyboard warriors, nyie Netizens wa humu etc
nacheka... u GT wa humu sio wa kila mtu...

Napita kimya hapa kwasababu wengine na mie tusio hata wanachama wa chama chochote...
kama mie sina la kusema siku hizi. Aliyefurahiwa ndio atashine 2025 ni Mwanamke.

Wanawake oyeeeee...
Kazi iendelee....
 
Nikiona mtu anakuja na ngonjera za kumsifia katili magufuli namuona kama mpuuzi tu, kipindi cha magufuli watu wameiba pesa za umma. Kina makondo, sabaya ni mabillionear kupitia magufuli, magufuli amaea watu kwa maslah yake binafs.
Na sisi tukikusikia unasema ukatili wake tunajua wewe ni kizazi kile kile cha nyoka
 
Wakati akiwa hai nilikuwa namuona John Pombe Magufuli pamoja na kutaka aonekane mzalendo, niliona kuwa ni mtu asiye na nia njema Kwa Taifa letu na mtaka sifa.

Lakini baada ya Polepole kuelezea mambo mengi yaliyokuwa yanafanyika nyuma ya pazia, sasa nimeanza kuelewa kuwa Magufuli alikuwa na dhamira njema kwa Tanzania.

Kumbe Magufuli baada ya kugundua fedha zinachotwa serikalini, yeye akaamua kuziwekeza kwenye miradi ili kama ni madeni ni bora watanzania walipe lakini wakiwa wana miundombinu inayowasaidia kuendesha maisha yao.

Zile hotuba zake kama anapambana na mara majeshi au watumishi wa Serikali, Leo zinaleta mantiki zaidi kuliko wakati akizitoa.

Magufuli alikuwa anajua yupo peke yake kwenye harakati za kuijenga Tanzania maana hata watu kama Makonda kumbe nao Wana vimelea vya CCM mtandao.

Ukweli utajulikana siku moja.
naomba unisamehe ndugu yangu,najua ukipitia comment zangu tulipishana sana hasa la kumuhusu MAGUFULI, sikujua kama haukua unajua aliyokua anayapitia, nikadhani ulikua unafanya vile tu kwa sababu tu umpendi ,KARIBU SASA UJIUNGE NASI Hata yule aliepigwa risasi ilikua ni connection ya maneno ya lisu na Magu , Wanamtandao wakamaliza kazi, kuna mengi tu subiri kuyasikia
 
Wakati akiwa hai nilikuwa namuona John Pombe Magufuli pamoja na kutaka aonekane mzalendo, niliona kuwa ni mtu asiye na nia njema Kwa Taifa letu na mtaka sifa.

Lakini baada ya Polepole kuelezea mambo mengi yaliyokuwa yanafanyika nyuma ya pazia, sasa nimeanza kuelewa kuwa Magufuli alikuwa na dhamira njema kwa Tanzania.

Kumbe Magufuli baada ya kugundua fedha zinachotwa serikalini, yeye akaamua kuziwekeza kwenye miradi ili kama ni madeni ni bora watanzania walipe lakini wakiwa wana miundombinu inayowasaidia kuendesha maisha yao.

Zile hotuba zake kama anapambana na mara majeshi au watumishi wa Serikali, Leo zinaleta mantiki zaidi kuliko wakati akizitoa.

Magufuli alikuwa anajua yupo peke yake kwenye harakati za kuijenga Tanzania maana hata watu kama Makonda kumbe nao Wana vimelea vya CCM mtandao.

Ukweli utajulikana siku moja.
One sided story is always like that
 
Nilichojifunza watu hawawi wema kwa kuwa aliyeko madarakani ni mwema, bali ni kutokana na mfumo unaowalazimisha wawe wema.

Makonda alifikishwa kwenye Tume ya maadili ya umma, nini kilitokea... Sabaya alifikishwa mahakamani, mahakama iliamua nini?
Na hili ndilo kosa la JPM na Mwl JKN kutegemea self integrity zao badala ya kujenga mifumo ambayo haina conflict of interests.

Lakini kwenye hili sijui nimpongeze JPM au Pole Pole maana ndani ya CCM walitengeneza mfumo wa kuzuia conflict of interests na kama upo makini Utagundua soon alipofariki ulivirugwa na kurudisha the statusquo
 
Back
Top Bottom