Pole Mhe. Lowassa Kufiwa na mkweo

Pole Mhe. Lowassa Kufiwa na mkweo

Wanabodi,
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Mhe. Edward Ngoyai Lowassa (Mb), amefiwa na mzazi mwenzake ambaye ni baba wa mtoto wa kiume aliyemuoa binti wa Mhe. Lowassa.

Kwa vile humu jf tuna kikundi chetu kiitwacho PROEL, nawaombeni tumpe pole zetu Mhe. Lowassa!.

Nawaombeni msiulize majina na wale mnaowajua naombeni msiwataje kwa hii sio thread ya RIP bali pole tuu kwa Mhe. Lowassa kupatwa msiba!.

Pole Mzee wetu Lowassa.

Na kwa vile yeye sio member humu, pole zenu mwageni hapa nami nitamfikishia kwa vile nitahudhuria msiba huu mkubwa kwa familia ya Lowassa!

dah! Hii mzazi mwenza ina utata sana. Nilidhani ni Regina
 

watu kwa kujipendekeza hamjambo

hata mimi nimefiwa na jirani wa jirani wa boss wangu naombeni pole

Huyu bwana aliyeanzisha uzi huu ni mtu wa kujipendekeza pendekeza sana kwa viongozi kwa kweli hastahili wala hana hadhi ya kuwa na wanaJF!! Mtu mzima lakini kila wakati ni wakujikomba komba ni mtu wa kuogopwa sana na kumuweka mbali I hope he is not one of the moderators ama sivyo identity za wanaJF zote atazipeleka TISS!!
 
Raisi wetu mtarajiwa anaandamwa na matatizo

alikuwa mdogo wake,sasa tena huyo du

tupo pamoja ktk wakati huu mgumu

R.I.P BABA
ila bado sina chama
naombe ugombea binafsi upite

Labda ndio kafara zenyewe za kuukwaa uprezidaa hizo...
 
Mkuu pasco, naamini unaweza kutupa ufaham mpana juu ya kichwa cha uzi huu. mimi nimeelewa kuwa aliyefariki ni mwanamke aliyepata kuzaa mtoto na lowasa, iweke sawa mkuu, naongelea heading.
Hivi kiswahili hakina neno/jina la uhusiano wa namna hii? Naona mods wamebadilisha, wameita "mkwewe" lakini still bado inapoteza. Inabidi tuazime majina ya 'kilugha' sasa....kule kwetu tunaitana "kivyele" (kwa hiyo Lowassa amefiwa na 'kivyele' wake/chake!)
 
Pole sana Waziri Mkuu mstaafu Mhe. Lowassa.
Aliyelazimishwa kujiuzuru kwa kashfa kubwa ya Richmond!! Hakujiuzuru hata kwa kujitolea... Alilazimishwa na kamati...
 

watu kwa kujipendekeza hamjambo

hata mimi nimefiwa na jirani wa jirani wa boss wangu naombeni pole

kumbuka kafiwa huyu el, kama bin adam, kama mtz mwenze2 anastahili kufarijiwa "pole mungu akupe moyo wa subira mzee lowassa kutokana na msiba"
 
Wanabodi,
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Mhe. Edward Ngoyai Lowassa (Mb), amefiwa na mzazi mwenzake ambaye ni baba wa mtoto wa kiume aliyemuoa binti wa Mhe. Lowassa.

Kwa vile humu jf tuna kikundi chetu kiitwacho PROEL, nawaombeni tumpe pole zetu Mhe. Lowassa!.

Nawaombeni msiulize majina na wale mnaowajua naombeni msiwataje kwa hii sio thread ya RIP bali pole tuu kwa Mhe. Lowassa kupatwa msiba!.

Pole Mzee wetu Lowassa.

Na kwa vile yeye sio member humu, pole zenu mwageni hapa nami nitamfikishia kwa vile nitahudhuria msiba huu mkubwa kwa familia ya Lowassa!
Hapo kwenye wekundu ndipo unapotosha,kwa mwandishi wa habari huo ni upotoshaji wa maksudi,anyway subiri panapo majaliwa utaupata ukuu wa kurugenzi ya mawasiliano pale magogoni
 
Huyu bwana aliyeanzisha uzi huu ni mtu wa kujipendekeza pendekeza sana kwa viongozi kwa kweli hastahili wala hana hadhi ya kuwa na wanaJF!! Mtu mzima lakini kila wakati ni wakujikomba komba ni mtu wa kuogopwa sana na kumuweka mbali I hope he is not one of the moderators ama sivyo identity za wanaJF zote atazipeleka TISS!!
Mkuu Bulesi asante kwa wasifu wako kwangu. Bahati nzuri sana mimi ni moderator wa kisiri siri na ni kweli true identity zote za wanajf nimeshazipeleka ofisini Tiss pale St. Peters hivyo kama ilifikiri haijulikani, kaa ukijua unajulikana vizuri tuu.

Na kwa vile majina yote nimesha yaripoti Tiss, what difference does it make or does it matter?.
 
Pole sana Lowassa, tumepata kwa masigitiko taarifa hizi kupitia kwa mfurukutwa wako Pasco
 
Back
Top Bottom