Pinda ataka Rais apunguziwe Madaraka

Pinda ataka Rais apunguziwe Madaraka


Hili la Pinda najua ni maoni yake na ana haki ya kusema hivyo na ninamuunga mkono kwa kutambua hilo...La Lubuva lina ukakasi kidogo coz ile dhana ya serikali kutokuwa na dini sijui itakuwa implemented vipi lakini vile vile ni Mungu yupi! Maana wengine mungu wao ni wanyama, miti, vinyago nk. Sasa ni Mungu yupi na aandikwe kwa jina lipi coz kama ni Mungu muumba mbingu na nchi, wengine humwita Allah, Mungu, God, Jah nk.....

Kuna taifa moja kubwa hata kwenye pesa zao wameandika hivi: IN GOD WE TRUST! Je wewe hili unalionaje? Maana hata hao wenye kumtaja Muumba kwa majina tofauti hawako mbali na wahenga wetu wambao walikuwa na majina tofauti ya kumtaja Mungu kadiri ya lugha yao, lakini wote walimaanisha Mungu yule yule kwa sababu kila watu walimtambua Muumba kadiri na namna alivyojifunulia kwao.
 
uploadfromtaptalk1359005763331.jpg

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amependekeza katika Katiba mpya ijayo, madaraka ya Rais yapunguzwe hasa katika shughuli za uteuzi wa viongozi.

Akizungumza jana baada ya kutoa maoni mbele ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Pinda alisema muda aliokaa madarakani na Rais Jakaya Kikwete, ameona ana mambo mengi na ndiyo maana anapendekeza si lazima kila jambo liende kwake.

"Ni vema machache yabaki kwake. Kwa mfano uteuzi wa nafasi mbalimbali vipewe vyombo vya kufanya uteuzi huo," alisema bila kufafanua nafasi ambazo Rais anatakiwa kuacha kuteua. Kuhusu nafasi ya Waziri Mkuu, alisema hiyoni ya utendaji na kwa sasa
Waziri Mkuu lazima awe mbunge na kutokana na hali hiyo, anapendekeza itazamwe vizuri.

Alifafanua kuwa Waziri Mkuu atajikuta akilazimika kuangalia zaidi Serikali huku jimbo analowakilisha likilala kwa kukosa usimamizi mzuri.

Kutokana na hali hiyo, alipendekeza mawaziri wasitokane na wabunge, iliwafanye kazi vizuri yakusimamia majimbo yao wakisaidiana na wananchi. Uhuru wa Bunge, Mahakama Alisema Bunge na Mahakama ni vyombo muhimu vinavyostahili kupewa nafasi ya kutosha.

Alizungumzia mifuko iliyoundwa ya Bunge na Mahakama na kutaka itambuliwe kikatiba na Katiba ielekeze ni namna gani itumike. Kuhusu kinga ya mbunge, alisema ni vizuri itamkwe kwenye Katiba kuwa mbunge ana kinga, lakini ibaki bungeni tu si azungumze nje na kinga ya Bunge iendelee kumlinda.

Akizungumzia Muungano, Pinda alisema tangu azaliwe hadi anapata akili mwaka 1964, alikuta Muungano na ndicho kitu pekee anachoweza kukisemea vizuri kwa kuwa umejenga udugu, muungano na ukaribu.

"Hapakuwa na huyu ni mgeni,au huyu ametoka huku au kule," alisema akizungumzia Muungano wa Serikali mbiliulivyo. Alikiri kuwa kuna kero nyingi za Muungano na kupendekeza kuwa dawa ya kero hizo si kuua Muungano, bali kitafutwe chombo kitakachoshughulikia matatizo.

Alipendekeza Serikali zibaki mbili lakini iundwe tume ya kushughulikia matatizo yaliyopo. Pia akapendekeza kuundwe Serikali ya Umoja waKitaifa Tanzania Bara kama ilivyo Zanzibar na vyama vyote vipate ushiriki. Mafuta, gesi Akizungumzia rasilimali za
Taifa za mafuta na gesi, Pindaalisema haoni shida mafuta kuchimbwa Zanzibar na kusafirishwa Bara au kuchimbwa Bara na
kusafirishwa Zanzibar kwa kuwa atavuka tu kununua na kurudi.

Chanzo: Habari leo.

Ninakupongeza kwa kuwa na ujasiri wa kuzungumza maneno kama hayo ktk maoni yako. Wako ambao ama kwa kuogopa ama utashi wao wameonelea Rais abakiwe na madaraka aliyonayo ama kuongezewa ilihali waliowengi wanaona Rais hawezi kuubeba mzigo alionao.Mambo yameongezeka pamoja na vitengo mbalimbali hivyo ni lazima Rais apunguziwe mzigo.
 
Pinda kwa hili amejitahidi kutoa maoni yake kwa uhuru na sio unafiki, kama ule ulioneshwa na Jaji Mkuu Othman Chande, Katibu Kiongozi Ombeni Sefue na PM Mstaafu John Samuel Malecele. Hao viongozi hasa Jaji mkuu walitoa maoni ya hovyo hovyo sana. (No offense intended lakini wegine tumeanza hata ku question BUSARA zao).

Lakini sikubaliani na Pinda kuhusu Muungano wa serikali 2. Hata kiundwe chombo gani, hakiwezi kuondoa hizo kasoro za Muungano kwasababu zinatoka na muundo wa serikali mbili. Jawabu la Muungano wetu ni serikali moja, kama hili haliwezekani basi ni serikali tatu.
 
View attachment 80635

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda
amependekeza katika Katiba
mpya ijayo, madaraka ya Rais
yapunguzwe hasa katika
shughuli za uteuzi wa
viongozi.
Akizungumza jana baada ya
kutoa maoni mbele ya
wajumbe wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba, Pinda
alisema muda aliokaa
madarakani na Rais Jakaya
Kikwete, ameona ana mambo
mengi na ndiyo maana
anapendekeza si lazima kila
jambo liende kwake.
"Ni vema machache yabaki
kwake. Kwa mfano uteuzi wa
nafasi mbalimbali vipewe
vyombo vya kufanya uteuzi
huo," alisema bila kufafanua
nafasi ambazo Rais anatakiwa
kuacha kuteua. Kuhusu nafasi
ya Waziri Mkuu, alisema hiyo
ni ya utendaji na kwa sasa
Waziri Mkuu lazima awe
mbunge na kutokana na hali
hiyo, anapendekeza itazamwe
vizuri.
Alifafanua kuwa Waziri Mkuu
atajikuta akilazimika kuangalia
zaidi Serikali huku jimbo
analowakilisha likilala kwa
kukosa usimamizi mzuri.
Kutokana na hali hiyo,
alipendekeza mawaziri
wasitokane na wabunge, ili
wafanye kazi vizuri ya
kusimamia majimbo yao
wakisaidiana na wananchi.
Uhuru wa Bunge, Mahakama
Alisema Bunge na Mahakama
ni vyombo muhimu
vinavyostahili kupewa nafasi
ya kutosha.
Alizungumzia mifuko
iliyoundwa ya Bunge na
Mahakama na kutaka
itambuliwe kikatiba na Katiba
ielekeze ni namna gani
itumike. Kuhusu kinga ya
mbunge, alisema ni vizuri
itamkwe kwenye Katiba kuwa
mbunge ana kinga, lakini ibaki
bungeni tu si azungumze nje
na kinga ya Bunge iendelee
kumlinda.
Akizungumzia Muungano,
Pinda alisema tangu azaliwe
hadi anapata akili mwaka
1964, alikuta Muungano na
ndicho kitu pekee anachoweza
kukisemea vizuri kwa kuwa
umejenga udugu, muungano
na ukaribu.
"Hapakuwa na huyu ni mgeni,
au huyu ametoka huku au
kule," alisema akizungumzia
Muungano wa Serikali mbili
ulivyo. Alikiri kuwa kuna kero
nyingi za Muungano na
kupendekeza kuwa dawa ya
kero hizo si kuua Muungano,
bali kitafutwe chombo
kitakachoshughulikia
matatizo.
Alipendekeza Serikali zibaki
mbili lakini iundwe tume ya
kushughulikia matatizo
yaliyopo. Pia akapendekeza
kuundwe Serikali ya Umoja wa
Kitaifa Tanzania Bara kama
ilivyo Zanzibar na vyama
vyote vipate ushiriki. Mafuta,
gesi Akizungumzia rasilimali za
Taifa za mafuta na gesi, Pinda
alisema haoni shida mafuta
kuchimbwa Zanzibar na
kusafirishwa Bara au
kuchimbwa Bara na
kusafirishwa Zanzibar kwa
kuwa atavuka tu kununua na kurudi.
Chanzo: Habari leo.

Ninakupongeza kwa kuwa na ujasiri wa kuzungumza maneno kama hayo ktk maoni yako. Wako ambao ama kwa kuogopa ama utashi wao wameonelea Rais abakiwe na madaraka aliyonayo ama kuongezewa ilihali waliowengi wanaona Rais hawezi kuubeba mzigo alionao.
Mambo yameongezeka pamoja na vitengo mbalimbali hivyo ni lazima Rais apunguziwe mzigo.
ni sawa kabisa lakiniiiiiii.kama bodi mbalimbali nchini hushindwa kuchukua hatua dhiidi ya viongozi mbalimbali wa makampuni au mashirika ya uma wanayo yaongoza jee mamlaka hizi za uteuzi zinaweza kwajibika? hili nawasiwsi nalo hasa kwa silka ya sisi watanzania,
 
Kila mmoja wetu ana mawazo tofauti na mwingine ktk jambo fulani na ndiyo maana tupo tofauti kwa itikadi na vipaumbele kutoka mtu mmoja na mwingine.Sasa basi kwanini wahandishi wa habari wachukue mawazo ya mtu fulani kuwa ni majibu au mapigo kwa mawazo ya mwingine.
 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda,
ametofautiana na Waziri Mkuu
mwingine mstaafu ambaye aliwahi
kushika madaraka hayo juu ya
madaraka ya rais katika katiba
mpya ijayo na ameweka wazi kuwa
ni vyema ikampunguzia rais
madaraka.
Waziri Pinda alitoa mapendekezo
hayo wakati akizungumza na
waandishi wa habari katika ofisi za
Tume ya Mabadiliko ya Katiba, jijini
Dar es Salaam jana, mara baada ya
kuwasilisha maoni yake kwa tume
hiyo kuhusu uundwaji wa katiba
mpya.
“Nimejaribu kutazama majukumu ya
Rais, Makamu wa Rais, Waziri
Mkuu….Rais ana majukumu mengi
ya kufanya, lakini kwa uzoefu
wangu niliowahi kufanya kazi,
maeneo mengine ni lazima
tukasimu kwa wengine,” alisema
Pinda na kuongeza:
“Rais huyo huyo ashughulikie
mambo ya uteuzi, huyo huyo
ashugulikie masuala ya nidhamu…ni
lazima majukumu hayo pia vipewe
vyombo vingine vishughulikie.”
Pinda anatofautina na John
Malecela ambaye alikuwa waziri
mkuu kati ya mwaka 1990 hadi
1994, ambaye wiki iliyopita baada
ya kutoa maoni yake kwa Tume
aliwaambia waandishi wa habari
kuwa ni vyema madaraka ya Rais
yakaachwa yalivyo na kuhoji kuwa
ukipunguza madaraka hayo
yatapelekwa wapi kwani ni muhimili
unaojitegemea.
Malecela alisema nchi changa kama
Tanzania bado kuna haja ya rais
kuwa na madaraka makubwa ili
kumwezesha kusimamia vizuri nchi
anayoiongoza.
Pinda pia alizungumzia madaraka
ya Makamu wa Rais na Waziri
Mkuu, na kutaka nao katiba mpya
iwapunguzie madaraka kutokana na
kukabiliwa na majukumu mengi,
yakiwamo ya ubunge na serikali,
huku akitaka suala hilo liangaliwe
upya katika uundwaji wa katiba
hiyo.
“Waziri Mkuu humsaidia Rais katika
masuala yote ya utendaji wa
serikali. Pia huyo huyo mbunge…
nalo eneo hili lingetazamwa vizuri
kwenye katiba mpya ijayo,” alisema
Pinda.

ATAKA MAWAZIRI WASITOKANE na
UBUNGE

Kuhusu kushika nafasi mbalimbali,
Pinda alisema mawaziri wasitokane
na wabunge ili wawe na muda
mzuri wa kushughulikia majukumu
ya kiserikali na wabunge
washuhulikie majukumu ya
majimbo yao.

MIHIMILI YA DOLA ISIINGILIANE

Kuhusu mihimili mitatu ya dola,
ikiwamo Serikali, Mahakama na
Bunge, Pinda alipendekeza kuwa
katiba mpya iwe na kifungu
kinachoeleza kutoingiliana kwao
kwa madai ya kwamba kila chombo
kifanye kazi kwa uhuru bila
kuingiliwa na kingine.

MAHAKAMA

Kuhusu Mahakama, alipendekeza
katiba mpya ieleze jinsi chombo
hicho kinavyopaswa kutekeleza
wajibu wake kwa mujibu wa sheria.

BUNGE

Alisema kuwa Bunge ni muhimili
muhimu na kwamba lipewe nafasi
ya kutosha kwa kujijengea uwezo
ikiwa ni pamoja na kuwa na mifuko
ambayo inapaswa kuelezwa ndani
ya katiba mpya kwa ajili ya
kujiendesha vyema.

SERIKALI ZA MITAA

Pinda alisema badala ya kuwa na
ibara mbili tu zinazoelezea kuhusu
serikali za mitaa kama ilivyo ndani
ya katiba ya sasa, katiba mpya
iongeze vifungu vingine kwa ajili ya
kuzisaidia serikali hizo kujiendesha
zenyewe, ikiwamo vile vinavyohusu
mapato ndani ya vyombo hivyo.

MUUNGANO

Alipendekeza kuwa mfumo wa
serikali mbili uliopo uendelee, huku
akipendekeza kuundwa chombo
maalumu kwa ajili ya kusimamia
masuala yote yanayohusiana na
Muungano.
“Muungano ulianzishwa mwaka
1964, miaka 49 ni mingi kujenga
hisia. Mimi nilizaliwa mwaka 1948,
hivyo ninao uzoefu wa kutosha
kuhusu Muungano. Tangu
kuanzishwa kwake, Muungano
umeleta undugu kati ya pande hizi
mbili,” alisema Pinda na kuongeza:
“Kuna changamoto, lakini dawa si
kuuondoa bali kiundwe chombo
maalumu. Chombo hicho hicho
kiwe ni tume maalumu itakayokuwa
inashughulikia masuala yote
yahusuyo Muungano. Ndiyo maana
hata Zanzibar walipoona vyema,
waliamua kuwa na Serikali ya
Umoja wa Kitaifa. Muungano
ninaouafiki ni huu huu wa serikali
mbili, uendelee.”
Mbali na kutoa maoni, Pinda pia
alitumia muda huo kukagua kazi
inayofanywa na tume hiyo tangu
ianze kazi yake mwaka uliopita kwa
kuzunguka takriban mikoa yote ya
Tanzania Bara na Zanzibar
kukusanya maoni kwa ajili ya
uundwaji wa katiba mpya.
Alisema ameridhika na kazi ya Tume
kwamba inafanya vizuri.
Mawaziri wakuu wengine wastaafu
waliozungumzia madaraka ya Urais
kwa tume ni Federick Sumaye,
ambaye alitaka yapunguzwe.
Cleopa Msuya naye alitoa maoni
yake lakini vyombo vya habari
havikupata alichozungumza.
Mawaziri wakuu wastaafu wengine
ni Jaji Mstaafu Joseph Warioba na
Dk. Salm Ahmed Salim ambao ni
wajumbe wa Tume. Warioba ni
mwenyekiti na Salim ni makamu.

CHANZO: NIPASHE
 
Hivi pinda yupo???sijamsikia long time kitambo,tangia wasukuma wamzomee duh
 
Kwa kweli alichangia vizuri kwa ujumla alimaanisha kila muhimili uwekewe mipaka kwenye katiba mpya ili iweze kujitegemea.
 
Huyu mzee lubuva akili yake imechoka. Anafikiria kufa. Mwacheni mzee wa watu. Sio kosa lake. Ni umri ndio unaomsukuma kutoa maoni hayo.
 
Mimi naamini huyu Pinda ameamua kutema hizo nyongo, kutokana na kukerwa sana na lile sakata la Jairo! si mnakumbuka wakati ule alipowahakikishia wabunge kuwa kama masuala ya makatibu wakuu wa wizara yangekuwa chini ya mamlaka yake angekuwa ameshamfukuza kazi Jairo, kutokana na kitendo chake cha kuwahonga wabunge ili bajeti ya wizara yake ya Nishati na Madini ipite kiulaini! Lakini akawaeleza kuwa mamlaka ya uteuzi na kutengua ajira za makatibu wakuu, anayo Rais mwenyewe na akawahakikishia wabunge kuwa mara Rais atakaporejea toka kwenye ziara yake, Afrika kusini atamjulisha kila kitu kilichotokea, lakini kwa wakati huo anamsimamisha kazi. Aliporejea JK toka South, si kila mtu anajua kilichotokea, akaamuru swahiba wake Jairo arejeshwe kazini mara moja na akampa kiburi kuwa ikiwezekana awaburuze mahakamani, watu wote waliomchafulia jina lake, kuwa ni mtoa rushwa!! Na sote bado tunakumbuka jinsi Jairo alivyopokelewa kifalme, kwa mbwembwe nyingi pale wizarani kwa gari yake kusukumwa, na miongoni wa walioshiriki kulisukuma gari hilo, ni aliyekuwa waziri wakati huo William Ngeleja!!Kwa hiyo kwa usongo alionao Pinda ya jinsi alivyodharirishwa kiasi kikubwa, wakati ule, ameamua bora ateme nyongo na kuondoa unafiki na kuwadozoa wanafiki wengine akina Malecela, Sefue na Jaji mkuu Othman Chande, na kuwaunga mkono wapenda mabadiliko wengine, akina Jaji Lubuva, kuwa ni lazima haya madaraka makubwa sana ya ki-Mungu-mtu ya Rais wetu yaondolewe kwenye katiba mpya. Ni matumaini ya wananchi wengi kuwa, kwa kuwa maoni hayo ya kutaka madaraka ya Rais yapunguzwe yana nia ya kuitakia mustakabali mwema wa nchi, tunaamini Tume ya Warioba itayazingatia, na ya kuyaweka kwenye katiba mpya na kuyatupilia mbali maoni ya kinafiki ya kubembeleza kitumbua changu kisiingie mchanga ya akina Malecela na Sefue!!
 
Ukishaanza kuingiza habari za mungu katika serikali utaanza kufungua a Pandora's box, kwa sababu inevitably utajikuta na swali "mungu gani?".

Hapoooooo, ndo mgogoro utakapoanzia.

Isitoshe, kuna Watanzania wengine hatuamini katika uwepo wa mungu na kumuweka mungu katika katiba ni kutunyima uhuru wetu wa kutoabudu ambao umejumuishwa kama sehemu ya uhuru wa kuabudu.

This move is unconstitutional.

Mungu ni Mmoja , Mungu muumba mbingu na nchi , Bwana wa majeshi, Elisha Daya ,Mesiya , oooooooh shakalababaaabab la bosaya , kila goti litapigwa kwa mungu huyu , Mungu mwenye uweza Jina lipitalo majina yote ooooooh ni YESU KRISTU ndo tunayesema
 

.... ni Mungu yupi! Maana wengine mungu wao ni wanyama, miti, vinyago nk. Sasa ni Mungu yupi na aandikwe kwa jina lipi coz kama ni Mungu muumba mbingu na nchi, wengine humwita Allah, Mungu, God, Jah nk.....
Mkuu kwanza nakugongea like. Pili wakilazimisha katiba itaje Mungu, watazua tatizo kubwa kwani wengine Mungu wao hana utatu mtakatifu wakati wengine Mungu wao wa Israel ana utatu. Mungu wa Israel, Mungu wa Yakobo, Mungu wa Isaka ni tofauti sana na Allah. Kwa amani ya nchi, suala la dini liachwe kwenye vyombo vya imani za watu na serikali kamwe isijiingize. kinyume cha hayo, tunajitafutia matatizo.
 
Serikali hana dini wala mungu, kama mtu anataka kusali , asali kivyake na kwa muda wake. Pia hata kwenye ile nyimbo ya MUNGU ibariki, Nadhani tunawanyma haki wasio amini Mungu, wapagani, na wanao mwita mungu Mola, allah etc.....naona kama Tanzania*2 Nakupenda kwa moyo wote...Ndio ingekuwa ya Taifa.hii imetulia na haifungamani na dini yeyote...cha zaidi inatangaza hadi mali za asili zetu.


Wakati huo huo Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi yeye ataka katiba mpya ieonyeshe kutambuliwa kwa uwepo wa MUNGU katika shughuli za mahakama na ilitaje jina lake (MUNGU) wazi wazi...
 
Watanzania tujenge utamaduni wa kueshimu Maoni tofautitofauti ya Watusi Kwai kamwe hatuwezi sawa kwa kila kits
 
Aache unafiki mbona hasemi waziri mkuu nae apigiwe kura uswahilini huku na raisi wake anataka raisi apunguziwe madaraka halafu tuwe na waziri mkuu kilaza kama yeye mbona itakuwa balaa na anataka asiwe mbunge ndo maana alihonga apite bila kupingwa katavi nadhani anaogopa sana wananchi ndo maana hata krisimasi alitembelea hata buchani kuuliza bei ya nyama yaani tusipokuwa na raisi mwenye nguvu kikatiba halafu mkapata waziri mkuu style ya mfalme wa nyuki tumekwisha .

We dogo kuwa na busara na heshimu mawazo ya wenzako!

Nchi yetu ina Rais mtendaji hivyo hakuna sababu ya Waziri Mkuu kupigiwa kura na wananchi! Waziri Mkuu hupigiwa kura pale ambapo Rais au Mfalme/Malkia siyo mtendaji!
 
Kwa kweli hivi sasa inaelekea nchi yetu inaelekea kwenye mapambazuko ya mabadiliko makubwa kisiasa! maana viongozi wengi waandamizi wameamua kuuvua unafiki na kuamua kueleza yale yaliyo moyoni mwao. Mfano halisi ni maoni yaliyotolewa na Jaji Lubuva ya kutaka Tume ya uchaguzi iwe huru kikwelikweli kwa kupendekeza mambo mazito ambayo huwezi kuyatarajia yatolewe na mtu wa namna hiyo, kama vile, wajumbe wa Tume hiyo wasiteuliwe na Rais,badala yake wateuliwe na jopo la wataalam na majina hayo yakathibitishwe na bunge. Mambo mengine makubwa yaliyopendekezwa na Jaji Lubuva ni kukataa wajumbe wa Tume kuapishwa na Rais aliyeko madarakani na kumzuia Rais asiwe na mamlaka ya kuwafukuza kazi wajumbe wa Tume ya uchaguzi! Mapendekezo hayo ya Jaji Lubuva ni ushahidi wa kutosha kuwa malalamiko ya siku nyingi ya vyama vya siasa vya upinzani na wanaharakati wengine kuwa matokeo mengi ya uchaguzi huwa yanachakachuliwa kwa manufaa ya chama tawala kuwa ya kweli tupu na malalamiko hayo sasa yatakuwa yamepata nguvu sana!! Sasa ukichanganya na haya maoni ya waziri mkuu tuliye naye sasa,ya kupaza sauti bila woga kuwa madaraka ya bosi wake Rais, yamepitiliza, ni dhahiri sasa kunaanza kuonyesha dalili njema ya viongozi wetu kuuvua unafiki na kuamua kutoa maoni yenye maslahi kwa Taifa na wala sio kwa ajili ya maslahi ya chama tawala kilichopo madarakani!!Bravo Pinda na tunakupongeza sana jinsi ulivyojipambanua na wanafiki wengine,akina mzee Malecela na Sefue,ambao wao wandhani kumlamba miguu bosi wao ndiyo kujihakikishia kupata mkate wao wa kila siku!!
 
Hivi pinda yupo???sijamsikia long time kitambo,tangia wasukuma wamzomee duh

Punguza bangi! Pinda yuko live kila siku au umeuza luninga yako ili upate ugolo!
 
Nami natofautiana sana na Pinda, sikubaliani na serikali mbili kama Pinda anavyopendekeza, lazima au tuwe na serikali moja la sivyo, tuwe na serikali tatu.
Ni makosa kuendelea kuifuta Tanganyika katika ramani yetu kiutawala. Jambo ili la kutokubali utanganyika wetu ukubaliwe kikatiba litaendelea kuisumbua katiba ijayo na litaendelea kujenga muungano usio stable. Tanganyika ni muhimu, lakini kama hatutaki Tanganyika iwepo kiutawala, basi tuwe na nchi moja tu, Tanzania ikimaanisha nchi zote mbili zimekuwa tayari kuua utaifa wao na kuunda taifa moja. Tatizo ninaloliona kwa wanasiasa wetu ni kule kutotaka kutoa sababu kwa nini hawafikirii kurejeshwa kwa Tanganyika?
 
Back
Top Bottom