Pinda ataka Rais apunguziwe Madaraka

Pinda ataka Rais apunguziwe Madaraka

Dickson Ng'hily

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2010
Posts
473
Reaction score
508
Wakati Balozi Semfue akitaka rais asipunguziwe madaraka katika katiba mpya, mtoto wa mkulima Mh. Pinda amesema rais ana madaraka makubwa sana na ni vema akapunguziwa madaraka hayo.

Pia ameshauri katiba mpya isiruhusu Waziri mkuu pamoja na mawaziri wengine kutokana na Bunge (wasiwe wabunge) ili kuwe na checks and balance...

Wakati huo huo Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi yeye ataka katiba mpya ieonyeshe kutambuliwa kwa uwepo wa MUNGU katika shughuli za mahakama na ilitaje jina lake (MUNGU) wazi wazi...


My Take:
Hili la Pinda najua ni maoni yake na ana haki ya kusema hivyo na ninamuunga mkono kwa kutambua hilo...La Lubuva lina ukakasi kidogo coz ile dhana ya serikali kutokuwa na dini sijui itakuwa implemented vipi lakini vile vile ni Mungu yupi! Maana wengine mungu wao ni wanyama, miti, vinyago nk. Sasa ni Mungu yupi na aandikwe kwa jina lipi coz kama ni Mungu muumba mbingu na nchi, wengine humwita Allah, Mungu, God, Jah nk.....
 
Mbona hata JK angependa madaraka ya Rais yapunguzwe kuanzia 2015, ni Malecela na mtoto wake labda ili ndugu yao ze utamu aachiliwe au kusamehewa na Raisi na makuwadi wengine ndio fikra zao ni tofauti.
 
Mhh? hii mpya. Malecela na Sefue wanapingana na Pinda na Samata. Je wapi wapo sahihi kwa maoni ya wananchi?
 
Mbona hata JK angependa
madaraka ya Rais yapunguzwe kuanzia 2015, ni Malecela na mtoto wake
labda ili ndugu yao ze utamu aachiliwe au kusamehewa na Raisi na
makuwadi wengine ndio fikra zao ni tofauti.

Mkuu kumbe ze utamu lilikuwa na connection na le mutuz... ndio maana tabia ya ukuwadi anaiendeleza....
 
Wakati Balozi Semfue akitaka rais asipunguziwe madaraka katika katiba mpya, mtoto wa mkulima Mh. Pinda amesema rais ana madaraka makubwa sana na ni vema akapunguziwa madaraka hayo.

Pia ameshauri katiba mpya isiruhusu Waziri mkuu pamoja na mawaziri wengine kutokana na Bunge (wasiwe wabunge) ili kuwe na checks and balance...

Wakati huo huo Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi yeye ataka katiba mpya ieonyeshe kutambuliwa kwa uwepo wa MUNGU katika shughuli za mahakama na ilitaje jina lake (MUNGU) wazi wazi...


My Take:
Hili la Pinda najua ni maoni yake na ana haki ya kusema hivyo na ninamuunga mkono kwa kutambua hilo...La Lubuva lina ukakasi kidogo coz ile dhana ya serikali kutokuwa na dini sijui itakuwa implemented vipi lakini vile vile ni Mungu yupi! Maana wengine mungu wao ni wanyama, miti, vinyago nk.
Sasa ni Mungu yupi na aandikwe kwa jina lipi coz kama ni Mungu muumba mbingu na nchi, wengine humwita Allah, Mungu, God, Jah nk.....

Hiyo itakuwa shida kubwa sana. Tutaanza kufarakania hapo tu. Bora tuachanane na mambo ya mungu kutajwa kwenye katiba. Wacheni atajwe makanisani, misikitini, masinagogini, kwenye miti, kwenye mibuyu, kwenye majabali, nk.
 
Mnaota nyie pelekeni usinga wenu FB....we need evidence sio porojo
 
Kwa hili namuunga mkono Pinda kama nilivyomuunga mkono Sumaye. Ingawa kila mtu ana haki ya kueleza mawazo yake, mawazo yaliyotolewa na Sefue na Malecela ni ya kujigonga kwa rais na kuturudisha kwenye awamu za ujima. Rais wa Tanzania kwa sasa ni sawa na sultani au mfalme wa Uarabuni. Anatumia pesa na madaraka yetu atakavyo akiwazawadia marafiki zake vyeo na kuwalinda pale wanapotenda makosa ya jinai mfano Benjamin Mkapa na mkewe na familia yake, Edward Lowassa, Andrew Chenge, Peter Noni, Mwanaidi Majaar, Rostam Aziz na wengine wengi ambao ufisadi wao unachefu ana kujulikana kwa watanzania wengi. Anyways, kama rais asingekuwa sultani nadhani kashfa za EPA na Richmonduli zingemtupa nje Jakaya Kikwete. Lakini nani anamgusa iwapo katiba imempa madaraka ya usultani kiasi cha kuamua kuyatumia vibaya yeye na familia yake na waramba viatu wake? Hapa Pinda umenena mwanangu.
Wakati Balozi Semfue akitaka rais asipunguziwe madaraka katika katiba mpya, mtoto wa mkulima Mh. Pinda amesema rais ana madaraka makubwa sana na ni vema akapunguziwa madaraka hayo.

Pia ameshauri katiba mpya isiruhusu Waziri mkuu pamoja na mawaziri wengine kutokana na Bunge (wasiwe wabunge) ili kuwe na checks and balance...

Wakati huo huo Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi yeye ataka katiba mpya ieonyeshe kutambuliwa kwa uwepo wa MUNGU katika shughuli za mahakama na ilitaje jina lake (MUNGU) wazi wazi...


My Take:
Hili la Pinda najua ni maoni yake na ana haki ya kusema hivyo na ninamuunga mkono kwa kutambua hilo...La Lubuva lina ukakasi kidogo coz ile dhana ya serikali kutokuwa na dini sijui itakuwa implemented vipi lakini vile vile ni Mungu yupi! Maana wengine mungu wao ni wanyama, miti, vinyago nk. Sasa ni Mungu yupi na aandikwe kwa jina lipi coz kama ni Mungu muumba mbingu na nchi, wengine humwita Allah, Mungu, God, Jah nk.....
 

Wakati huo huo Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi yeye ataka katiba mpya ieonyeshe kutambuliwa kwa uwepo wa MUNGU katika shughuli za mahakama na ilitaje jina lake (MUNGU) wazi wazi...

We are a secular democracy and definitely don't need that!

If somebody wants to pray before court proceedings let them pray on their own.
 
Wakati Balozi Semfue akitaka rais asipunguziwe madaraka katika katiba mpya, mtoto wa mkulima Mh. Pinda amesema rais ana madaraka makubwa sana na ni vema akapunguziwa madaraka hayo.

Pia ameshauri katiba mpya isiruhusu Waziri mkuu pamoja na mawaziri wengine kutokana na Bunge (wasiwe wabunge) ili kuwe na checks and balance...

Wakati huo huo Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi yeye ataka katiba mpya ieonyeshe kutambuliwa kwa uwepo wa MUNGU katika shughuli za mahakama na ilitaje jina lake (MUNGU) wazi wazi...


My Take:
Hili la Pinda najua ni maoni yake na ana haki ya kusema hivyo na ninamuunga mkono kwa kutambua hilo...La Lubuva lina ukakasi kidogo coz ile dhana ya serikali kutokuwa na dini sijui itakuwa implemented vipi lakini vile vile ni Mungu yupi! Maana wengine mungu wao ni wanyama, miti, vinyago nk. Sasa ni Mungu yupi na aandikwe kwa jina lipi coz kama ni Mungu muumba mbingu na nchi, wengine humwita Allah, Mungu, God, Jah nk.....

Safi sn mtt wa mkulima kwa maoni mazuri wanakatavi wenzako 2po nyuma yako japo ulinilimisha sana shambani kwako kibaoni wakati wa ziara yako ya kuzungukia jimboni mwako mwezi desemba mwaka jana
 
Pinda ametoa maoni yake vizuri. Jaji Lubuva amepepesa macho! Nchi yetu haina dini!
 
Yaani ccm wanajua wanachosema. Wanataka madaraka ya Rais yapunguzwe ili cdm wakija kushika Dola ile kwao. Hata sisi cdm tunasema madaraka ya Rais ni makubwa sana
 
Aache unafiki mbona hasemi waziri mkuu nae apigiwe kura uswahilini huku na raisi wake anataka raisi apunguziwe madaraka halafu tuwe na waziri mkuu kilaza kama yeye mbona itakuwa balaa na anataka asiwe mbunge ndo maana alihonga apite bila kupingwa katavi nadhani anaogopa sana wananchi ndo maana hata krisimasi alitembelea hata buchani kuuliza bei ya nyama yaani tusipokuwa na raisi mwenye nguvu kikatiba halafu mkapata waziri mkuu style ya mfalme wa nyuki tumekwisha .
 
Ukishaanza kuingiza habari za mungu katika serikali utaanza kufungua a Pandora's box, kwa sababu inevitably utajikuta na swali "mungu gani?".

Hapoooooo, ndo mgogoro utakapoanzia.

Isitoshe, kuna Watanzania wengine hatuamini katika uwepo wa mungu na kumuweka mungu katika katiba ni kutunyima uhuru wetu wa kutoabudu ambao umejumuishwa kama sehemu ya uhuru wa kuabudu.

This move is unconstitutional.
 
wote wanaotaka Rais apunguziwe madaraka wana nia njema na Rais ajaye.

Hivi sasa Rais analaumiwa sana katika jamii kwa sababu katiba imetoa madaraka mengi.

kila jambo lawama kwa Rais kwa sababu tuna vyombo vichache ambavyo katiba ingeweza kukasimu madaraka kwa niaba ya Rais,
 
Back
Top Bottom