Pillow talk

Ndio wameharibu dhana nzima ya pillow talk kama walivyochafua hii post mpaka ukakereka

Mkuu;
Pillow talk haitakufa ila itapungua na tatizo ni kuwa mapenzi ya kweli ni nadra saana sku hizi. Zama zile, hata ka mume ni mpiga tungi, alikuwa akiingia ndani, mamaa anampokea, anamvutia chumbani, anamvua zote halafu anamlaza kitandani. Saa nyingine zinapanda na anachafua chumba, mamaa anafuta usiku ule ule. Jamaa akiamka asubuhi mamaa kakaa kimya kama vile hakuna baya lilitokea. Jamaa anaona aibuuu na hakika akirudia sio mbaya kama hiyo. Kidogo kdogo anajirudi.
Mama wa leo, utaamka na kupiga deki weye mwenyewe na mitusi mikuubwa juu. Hiyo pillow talk itokee wapi?? Ulio waonesha hapo wamevumiliana. Mapenzi kuvumiliana ndo dawa.
Huhitaji viagra, unahitaji Pillow talk. Kitu inasimama ka mlingoti wa bendera
 
Naona kuna umuhimu mkubwa wa kutoa darasa kwa wadogo zetu hapa jamvini wa kike na wa kiume kwa pamoja, kwamba nini dhima ya ndoa! Nini maana ya mapenzi, privacy tuo na mipaka
Nini maana ya kuwa mwili mmoja! Nini maana ya bedroom kuitwa sehemu ya faragha, kwamba kwa jinsi unavyojisitiri na nguo hata bedroom yako iwe na limitations ya watu wanaoingia humo
Kuna mengi Tunahitaji kuyaongea kwa uwazi lakini kwa hekima na busara na heshima
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…