FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 100,506
- 123,802
Mtorela!
Kwanza pole maana najua ulikuwa huamini kuwa swahiba wako angeweza kuchukuliwa hatua hasa kupitia maandiko yako kule mtaa wa pili.
Pili, acha kufanya propaganda za kijinga kupitia maandiko yako! Swahiba wako hajazuiwa kukutana na wapiga kura wake na wala hakuna siku baada ya yeye kuvuliwa nyadhifa zake chadema waliyotamka kuwa haruhusiwi kwenda jimboni kuongea na wapiga kura wake. kama una ushahidi wa yeye kuzuia kwenda kigoma uweke hapa. Acha kupotosha!
Yeye akiamua anaweza kufanya mikutano mpaka Lumumba akisubiria stahili yake inayomfaa kwa namna kamati kuu itakavyo amua.
Usema kuwa tuhuma 11 zilisemwa kwenye jimbo lake?! zilisemwa na nani na lini?! tumia usomi wako na exposure uliyoipata kwa kuongea kwa facts usiwe unazomoka tu kama mtu ambaye hajui mlango wa darasa. Hayo mashtaka unayosema yasemwa jimboni kwake niyapi?!
Pole sana, ungekuwa unampenda sana rafiki unge mshauri asi betray coarse. Sikio likesha kufa halisikii tena dawa.
Nakushangaa sana unapojisahau na kufikiri kuwa majungu huwa yanashinda sehemu moja tu. Hao hao unaowaona wewe kuwa leo wema kwako, kesho na kesho kutwa watakugeuka vibaya sana.
Kijana chunga sana kauli zako. Hii dunia hujaijuwa bado.
Usifikiri kuwa siasa ni kazi ya muhimu sana kwako, naona bado hujajuwa kuwa siasa ni ufataani mtupu. Leo Mawaziri wanabwagwa na wanageukwa na watu wao wa karibu, itakuwa wewe?
Usimuone Zitto kuwa ni mjinga na ukadhani wewe na hao unaowatetea ni wajanja sana, mambo huwageukia hata Wafalme kwenye siasa. Shah wa Iran yuko wapi? Marcos wa Ufilipino yuko wapi? Fikiri kabla hujaandika utumbo.