PICHA: Ndege mpya za Fastjet hizi

PICHA: Ndege mpya za Fastjet hizi

Mambo ambayo Magufuli ameyafanya muhimbili nayo hamyaoni? Angalia kwenye huduma za afya nchini angalia nidhamu kazini kwa watumishi. Najua strategy ya upinzani ni kupindisha mafanikio ya Magufuli ili aonekane mmbaya kwa wananchi na matokeo yake Lowassa ndio aonekane mwema.
Muhimbili kimefanyika nini kigeni? Nidhamu gani unayoongelea iliyoko Serikalini...wee kariri siku ukiamua kuutafuta ukweli utakuwa umechelewa
 
Chanjo za watoto VIP?haya Passport zimeisha huko uhamiaji lakini Land Cruiser V 8 zipo Kibaoo mtaani daah
1474780183591.jpg
 
Muhimbili kimefanyika nini kigeni? Nidhamu gani unayoongelea iliyoko Serikalini...wee kariri siku ukiamua kuutafuta ukweli utakuwa umechelewa
Muhimbili nilikuwa huko kwa siku tatu tena fast track lakini sikuweza kupatiwa huduma niliyohitaji. Ni kuzungushwa tu. Mara mtandao hamna, mara daktari hayupo. Huduma ni mbovu hamna mabadiliko yoyote. Na mbaya zaidi vifaa na dawa vimepungua manesi wanalalamika kweli.

Huko MOI ndio majanga ni ghali na huduma zenywewe ni full kuzungushwa
 
Muhimbili nilikuwa huko kwa siku tena fast track lakini sikuweza kupatiwa huduma niliyohitaji. Ni kuzungushwa tu. Mara mtandao hamna, mara daktari hayupo. Huduma ni mbovu hamna mabadiliko yoyote. Na mbaya zaidi vifaa na dawa vimepungua manesi wanalalamika kweli.

Huko MOI ndio majanga ni ghali na huduma zenywewe ni full kuzungushwa
Kuna majitu akili zao zimepondwapondwa hayawezi kutumia akili zao kufatilia mambo wanasubiri kukaririshwa waje kutapika humu....watu walikuwa na Imani na Rais wakati naanza tuliamini atatenda tofauti na watangulizi wake kwamaana yakuwatosa CCM ambao wamefilisi hili Taifa kumbe imani yetu ilikuwa Potofu...siku zinavyokwenda Mh...anaitukuza ccm tena kwa mikwara ya Askari ukiangalia hata teuzi zake zinafifisha matumaini yaliyotegemewa Leo kuna mijitu inamwaga povu eti...kuna mabadiliko yapi...kama kununua Ndege sawa lkn sio zaidi ya hapo!
 
Sidhani hata kama hata anajua hizo ndege. Atakuwa amesikia watu wanaponda na yeye amejiunga nao as long ni wa chama kimoja. Watanzania sijui lini tutaanza kuthamini vitu vyetu.
Tunathamini. Bali hatushabikii upuuzi.

Unanunua ndege ilhali huna madawati? Huna tofauti na anaenunua gari na hana godoro la kulalia yuko kwa wazazi.
 
Profesa Mbarawa ameitaka Bodi hiyo kuipa ATCL mifumo imara, makini na mahiri ili kuweza kutatua changamoto zinazoikabili Shirika hilo ikwemo wizi wa mafuta ya ndege na upotevu wa mapato.

Ili kupima ufanisi wa utendaji wa Shirika hilo Profesa Mbarawa ameitaka Bodi hiyo kuandaa mkataba kwa kila mfanyakazi kuanzia ngazi ya juu hadi chini.

Katika hatua nyingine Waziri Mbarawa amesema kuwa Serikali ina mpango wa kununua ndege mbili mpya aina ya Jet ifikapo mwaka 2017 kwa lengo la kuboresha sekta ya usafirishaji wa anga nchini.
Mbona hawazungumzii lini chanjo zaja? Tangu lini ndege imekua tatizo kwetu katika usafiri?

Kuna mazao ya wakulima hayafiki sokoni na pembejeo haziki kwa wakati kisa madaraja hakuna. Leo hii bilioni 120/= zinatumika kununua ndege 2 pesa taslimu.

Ikiwa daraja la mto mdogo la barabara ya vumbi inagharimu milioni 120/=, basi hizo pesa za ndege 2 zingejenga hayo madaraja au makalavati 1000!!
 
Kuna mtu aliniambia nyie watanzania wa ajabu sana, hata siku moja hamuwez kujivunia chochote cha kwenu, mna tatizo gan, mnaweza hata kataa mlima kilimanjaro wenyewe mkasema uko kenya nyie wenyewe, there is nothing good for tanzanians instead they like being beggers only ther u will have many of them
Of being beggers, would give alms to one who packs a Prado besides him and begs for food rations? Common sense says you'd quickly reprise the unwise Matonya to sell the Prado then invest in his welfare.

Such is the scenario to us clear headed chaps.

On the contrary, your 'caliber' would go on to praise Matonya for the new model Prado that he owns while still begging on the roadside. PATHETIC to the CORE!!
 
...

Tunavyoanza kujenga nchi, kujenga uchumi tujielekeze kwenye viopaumbele halisi..na sio chuki kwa serikali pekee.

Vipaumbele kwa sasa si ndege regardless ya utakavyoichagua vizuri. Even worse, hao fastjet walivyoona mmevuta mapangashaa wakakamata jet kuwakata ngebe.

Vipaumbele kwa sasa ni elimu, afya, miundombinu rafiki kwa uchumi shirikishi, huduma zingine za jamii km makazi bora n.k.

Ukiwekeza hiyo bilioni 120/= popote kati ya hivyo hapo juu, uhakika ni mkubwa kuleta matokeo chanya kuliko ndege inayobeba watu 70 kwa gharama za ajabu.

Halafu hizo ndege hazina multiplier ya maana. Hadi mafundi wanatoka Canada. Upuuzi mtupu. Bora tuwekeze kwenye reli maana walau hata tuna karakana kubwa morogoro.

Biashara zifanywe na sekta binafsi. Hakuna ufahari wowote kuwa na ndege wakati hakuna madawa hospitali.
 
Wee wawapi? CV ndio kitu gani...unayo habari walioua hii NCHI nihao mlioamini CV zao!
Kwahiyo wawekwe wasio na CV za maana? Yaani msababishe ufisadi wenyewe na kupeana kazi bila kuangalia weledi kisha leo mnadharau elimu na uwezo?
 
Perception kitu kibaya.... Mimi nasema kwa dhati, ATC wakianza, na price zikawa up to 120% ya other operators, nitapanda ATC.
Mi sipandi ndege ambayo imenunuliwa kwa kuacha kununua dawa hospitali au kutengeneza madawati.
 
Nyinyi siku zote ndio mlikuwa mnalalamika watu wanalipwa mishahara mkubwa, Mh. Raisi ameliona analifanyia kazi mnaanza kutunga mengine. Watu wa ajabu ajabu sana.
Hamna ambae alishateuliwa mkaacha kisema ni mzuri. Matokeo tunayo hata hivyo
 
Mashetani tutaendelea kuhangaika na mabasi yetu. Hongereni nyie malaika kwa kuongezewa vitu vikali mtakuwa mnakata mapanga shaa huko angani sisi tukiwa tunakula vumbi tu na tochi kibao. wenzetu huko angani hakuna tochi ni mapanga shaa tu.
 
Matatizo ya ATC hayana uhusiano wowote ule na siasa za ccm. ukiangalia lilipoanzishwa lilitumia wataalam wale wale waliotoka EAA ambako nako waliheshimiwa sana. Na waliporudi serikali ikawa inawategemea wao waliendeshe.
Adui yao namba moja ilikuwa kuwekeana vitina wao kwa wao. Mzee Rwebangira alipigwa vita na wenzake kwa sababu ya vyeo. Baada ya hapo wakaanza kuingizana kazini kirafiki/ndugu na mwishowe hao hao wafanyakazi ndiyo walikuwa abiria wakuu wa kwenda nje kununua bidhaa [hasa kina mama]. Kuna wengine walikuwa wanatumia muda mwingi kusafiri kwa shughuli binafsi kuliko kazini.
Ninakumbuka kisa kimoja -Nilisafiri na ATC kwenda J'burg na wakati nataka kurudi staff wa ATC Jburg wakaniarifu kuwa ndege yao imejaa ila ninaweza safiri na ndge ya SA. Mimi nilikataa na nikasisitiza kuwa nilikuwa na cfmd booking ya ATC lakini dada yangu huyo alishikilia kuwa ndege imejaa. ili kufupisha kisa hiki, mwishowe nilifanikiwa kurudi na ndege
ya ATC lakini cha kushangaza iliondoka na abiria karibu nusu tu na sehemu kubwa ilikuwa haina abiria.
Vitu kama hivi ndivyo na vinginevyo viliendelea kama cancer na mwishowe shirika limefika lilipofikia.
Kupeana kazi kwa kujuana kunaanza na ukada. Wa juu wakishawekwa makada na chini kunafata. Ingelikua sio wanasiasa wanahusika wangeshakemea mapema sana
 
Tunathamini. Bali hatushabikii upuuzi.

Unanunua ndege ilhali huna madawati? Huna tofauti na anaenunua gari na hana godoro la kulalia yuko kwa wazazi.
Ndio maana ndani ya kila serikali Kuna baraza la mawaziri. Kila wizara huwa inafanya thamini ya nini cha kufanya ndio wanafanya. Kwa raisi huyu na baraza lake la mawaziri watatufikisha pazuri sana. Suala la madawati ni wizara nyingine kabisa ambayo nayo so far imeshafanya vizuri sana kutatua tatizo la madawati na bado wanaendelea.
 
Lipo daraja lajengwa kuanzia mwakani coco beach kuunganisha Aghakani kupitia sarenda
 
Mimi siyo ccm na wala sijawahi kuwa ccm ila upinzani kwa raisi huyu inabidi mjipange. Kwasababu yupo makini na anafanya mambo kwa maslahi ya taifa.
Kununua ndege 2 kwa bilioni 120/= siyo maslahi ya taifa kamwe. Kununua madawati zaidi ya 200,000/= ndio maslahi ya taifa.
 
Back
Top Bottom