Matatizo ya ATC hayana uhusiano wowote ule na siasa za ccm. ukiangalia lilipoanzishwa lilitumia wataalam wale wale waliotoka EAA ambako nako waliheshimiwa sana. Na waliporudi serikali ikawa inawategemea wao waliendeshe.
Adui yao namba moja ilikuwa kuwekeana vitina wao kwa wao. Mzee Rwebangira alipigwa vita na wenzake kwa sababu ya vyeo. Baada ya hapo wakaanza kuingizana kazini kirafiki/ndugu na mwishowe hao hao wafanyakazi ndiyo walikuwa abiria wakuu wa kwenda nje kununua bidhaa [hasa kina mama]. Kuna wengine walikuwa wanatumia muda mwingi kusafiri kwa shughuli binafsi kuliko kazini.
Ninakumbuka kisa kimoja -Nilisafiri na ATC kwenda J'burg na wakati nataka kurudi staff wa ATC Jburg wakaniarifu kuwa ndege yao imejaa ila ninaweza safiri na ndge ya SA. Mimi nilikataa na nikasisitiza kuwa nilikuwa na cfmd booking ya ATC lakini dada yangu huyo alishikilia kuwa ndege imejaa. ili kufupisha kisa hiki, mwishowe nilifanikiwa kurudi na ndege
ya ATC lakini cha kushangaza iliondoka na abiria karibu nusu tu na sehemu kubwa ilikuwa haina abiria.
Vitu kama hivi ndivyo na vinginevyo viliendelea kama cancer na mwishowe shirika limefika lilipofikia.