Interesting.....
tuone 'mapanga shaa' na hizi nani zaidi
Tunasahau kuwa Fastjet wameamua kuleta ndege ndogo baada ya "kulost".
Huu ni ushahidi kuwa ndege kubwa hazifai kwa safari fupi za ndani.
Na huu ni ushahidi dhidi ya wale waliokuwa wanalilia "tungenunua airbus kama za fastjet".
Ni lazima sasa kundi hilo likiri kua walipotoka. Na kuwa ndege ndogo na za kati ndo mpango mzima kwa safaei za ndani na sio zile kubwa.
Hata precission walichemsha na ile jet yao mapema sana.
Na vile vile kuna mashirika mengi sana ya ndege yanarusha hayo "mapanga shaa" na wabongo wanapanda...lakini kwa kuwa ni cha serikali ishakuwa nongwa...watu hao hao wanapanda panga shaa la ethiopiana kwa tabasam na raha tele na wanashuka JKNIA kwa swagger....lakini ya serikali matusi..
Na precission kila walivyokuwa wanaongeza "mapanga" mapya tuliwasifu sana.....na nyuzi ziko hapa jukwaani. Watu hao hao leo matusi yake hayasemeki kama vile kununua "mapanga" ni dhambi kubwa.
Tuache unafiki na tubadilike.
Maswala yangu yanayonipa wasiwasi ni ishu za menejiment ya ile kampuni...kampuni iliyooza, je kampuni ile itaweza?
The Boss nakupa changamoto, Emirates ni kampuni ya ndege maarufu sana....je unajua ilianza na ndege ngapi miaka ya 80?
Menejiment na weledi wa biashara. Hili jambo sisikii likiongelewa. Tunatukana ndege weeee...hata ukipewa airbus mpya 100 kama huna menejiment nzuri utachemsha ndani ya miaka 5.
Tunavyoanza kujenga nchi, kujenga uchumi tujielekeze kwenye viopaumbele halisi..na sio chuki kwa serikali pekee.