PICHA: Mererani mwanajeshi ajitoa mhanga

PICHA: Mererani mwanajeshi ajitoa mhanga

KIBE naona umekomaa na thread hii acha kabisa! Labda nikukosoe kidogo kwenye hii dhana yako ya kusema jamaa wamemvalisha kombati,umekomaa nayo sana but kumbuka askari jeshi,polisi,magereza na wengineo nao ni watu wenye feelings zao pengine kinachowahold back ni mikwara/unafiki/sheria wanazoita za jeshi. Unamwambia mtu akapige kura kumchagua kioingozi anayetokea chama cha siasa ilhali yeye unmzuia kushiriki siasa ni uongo! lazima askari huyu ana chama chake. so hata huyu anaweza kwua askari kweli ila kashindwa tu kujizuia kama yule wa dodoma na nec
 
ameamua kuwa mkweli ameukataa unafiki
Mwanajeshi mmoja ameamua
kujitoa mhanga na yuko tayari kufukuzwa kwaajili ya CHADEMA maana
amechoshwa na maisha magumu ya kwake binafsi na ndugu zake...
View attachment 76434
Lema, Nassari na mwanajeshi aliyeamua kusema yupo tayari kufukuzwa kwa
ajili ya CDM LEO kwenye mkutano Mererani
 
Shimbo ndio amesababisha yote haya...hii ni hatari kama mwanajeshi anajitoa mhanga namna hii basi tumefika pabaya..serikali ianze kujali wananchi wake kuna hatari tukazalisha akina Joseph Koni na Lolaa Kunda wa Tanzania.!!
 
Haki ya nani huyu anajitakia kwenda Mabwepande!
 
Si afya sana kushuhudia mwanzo wa vijana wa jeshi kujihusisha na siasa. Kila kazi ina miiko yake, na ni vizuri ikafuata misingi chanya kwa mujibu wa viapo (for this matter kiapo cha utii kwa rais). hii ni muhimu sana na itazamwe vizuri kisiasa na kiusalama. Apewe adhabu kali ikithibitika. Nitakuwa wa mwisho kukubaliana/kushabikia uasi kama huu.

Sio inakijenga CDM wala Lema. Uasi wa jeshi si kitu cha kukifurahia.

Ila nafikiri Lema alipata munkari wa siasa, hakuua madhara yake kwa upana wake. Leo CDM tukichukua Dola ukaona vijana wanafanya hivyo sifikiri under any circumstance anaachwa. Cha kwanza atapimwa akili
 
Kama maofisini Siasa za CCM zinafanywa hadi vyuoni inakuwaje huko majeshini waanawabana kufanya wapendacho ? Najua walianza wenyewe but kwa hili kisasi huyu dogo kitampata
 
Narudia hii haijawahi tokea! vyovyote vile huyu ndio askari wa kwanza kwa majeshi yote kujilipua hivi!

Kuna wanajeshi wengi sana wanawaunga mkono CDM isipokuwa walie magamba tu ndiyo wanabana, Nakumbuka hata wakat wa uchaguzi na baada ya matokeo miongono mwa kilichomchanganya sana JK na Usalama ni kura nyingi sana alizopata Dr Slaa maoneo ya Kambi za Jeshi maana alifikiri wanajeshi wanamwuunga mkono, Just imagine mtu ni mwanajeshi anaishi Chumba kimoja na familia yake yote halafu mnasema CCM itatawa miaka 50 ijayo ili nini??

Wanaosema hivyo ujue wanawaandaa hadi watoto wao walioko chekechea kuja kuwa marais wa nchi hii.
 
jeshi lina sheria, kanuni na taratibu zake! lets wait...........

Ndio twajua kweli Jeshi lina sheria zake ila kumbuka kiukweli uchaguzi ulio Pita Maeno mengi amabako wanajeshi walikuwa wanaisha kura za kumchagua Rais kwa tiketi ya CCM ambae alikuwa Rais Jakaya Kikweti zilikuwa ni chache sana na Dr. Slaa alikuwa nazo nyingi sana hii ilionyesha kuwa watu wamechoshwa hili liko wazi serikali inayo ongozwa na CCM inatakiwa kuwa wazi na kukubali matokea na ianze kubadilika sasa


 
Ukada wako sisi hatuhusu,mbona mnatumia viongozi na watumishi wengi tu wasiostahili,Tuambie akina Tibaigana wakati wanagombea ubunge huko Muleba baada ya kustafu Polisi lini alikuwa mwana CCM,Je na James Kombe kamanda wa Polisi huyu kila cheo cha ccm anakitaka japo wanaflush,Je na huyu Jenerali Mboma?,na MADC,MARC ?.kafie mbali
Mimi sio kada kaka,mi ni mpiga kura tu wa kawaida na nafurahia kuwa hivyo, ningeshauri mmushauri huyo askari nae avue haya magwanda ndo aingie kwenye siasa kama hao uliowataja,sikumbuki tibaigana kufanya siasa wakati akiwa mtumishi wa umma,tunachoongelea hapa ni kama kuna sheria yoyote imevunjwa,nafikiri kama kichwa chako kinaweka kumbukumbu sahihi,mnajua alichofanywa yule askari polisi wa moro aliye taka kugombea NEC kupitia CCM.????na hicho ndicho atakachofanywa huyu askari,like or not.
 
Jeshini ukikosa kuna adhabu mpaka za kuchapwa njugu za moto...ila huyu bado mbichi kabisa sidhani kama ana medani zote zinazojulikana...ila ninachomuona nacho ni kama msoma ramani tu sidhani kama atakuwa na impact kubwa kwa sababu wapo mabosi wake tuko nao pamoja ila hawana mbwembwe kama zake maana hata alama ya vidole mbili anaonekana ameiweka kama learner flan hivi....
 
Kumbukeni wakuu wa Wilaya, Mikoa ni wanajeshia wapo wengi tu na ni Makada wa CCM
 
What if Angepiga picha na Nepi, Chichidodo, Jangili, Nyoka wa Mdimu, Vijicent, Prince...wangemtimua?
Mkuu ni muhimu sana kuwa na kumbukumbu ya matukio,kuna askari polisi morogoro alienda Dodoma kugombea NEC,uliza alichofanywa,na huyu naye atafanywa hivyohivyo
 
kwanza nasikitika kwa tukio hili, mimi nilikuwa kwenye huu mkutano jana huyu mwanajeshi huwa anafundisha mgambo mjini mererani, jana wakati chadema wakifanya mkutano wa hadhara mwanajeshi huyo aliwaamuru mgambo wote waende kwenye mkutano kuwasikiliza wabunge wa chadema, kabla mwanajeshi huyu haja fikia uwamuzi huo, kuna haice moja ilikuja na makamanda kadhaa wa Chadema, akiwepo mpambe mmoja wa Millya, Oleleshwa alikwenda kuongea na huyu mwanajeshi huyo na ndo migambo wakapewa amri ya kwenda kwenye mkutano, bado niko hapa Mererani nafanya uchunguzi wa kina na nimesha gundua kuwa, Lema, Nassari, Heche wakishirikiana na Millya wanatengeneza Jeshi na watatumia msitu wa Komolo wilayani simanjiro, mtu anayeratibu mafunzo ya wa wanajeshi hao wanafundishwa kwa mwamvuli wa mgambo ni mzee mmoja anaitwa Peter Peshut akishirikiana na Oleleshwa, kwa ufadhili wa kamanda Ndesamburo na Mbowe, naendelea na ufafiti na kuna taarifa kuwa gideon Sanago naye yuko hapa Mererani akiendelea kuwashawishi Apolo wajiunge na jeshi la kina Lema.

sio we ulikuja na taarifa za kuwapa kichapoo chadema wakikanyaga melerani au ndio umeshindwa kuzuia mvua kwa mkono
 
Wakitumia ccm siyo hatari,ila Lema hatari.! Uko vizuri kweli?
AkIli.
Wa askari wa morogoro aliyekwenda Dodoma kugombea Nec ya CCM mbona mmemsahau wakubwa,na alichofanywa yule askari ndo hichohicho atakachofanywa huyu askari.
 
Mbona uniform yenyewe haina "force number" kifuani na wala haina alama za Taifa letu juu ya bega? alizitoa au uniform feki?
 
ooh ooh,yule bwana visasi atakuwa amekasirishwa sana sana,2015 LAZIMA kuwe na revolution
 
binafsi katika hili siungi mkono ...hizi sio siasa na hukana na hakuna duniani kuwahi kutokea kituko cha wanasiasa kutafuta watu kuwavalisha kombati za jeshi kwa lengo la kufanikisha mambo yao ya kiasia..ndo naona hapa tz... Na ukweli uko wazi hasa hawa viongozi hawa vijana wa cdm ukweli ni hatari wanavuruga nchi wazi wazi... Tushabikie lakini tuangalie na ukweli wa swala hili ni hatari sana . Mbowe,slaa ,mzee mtei vyema mkaangalia upya njia ya kupata mafanikio katika siasa zenu kama ni sahihi au la...
Kwake lema,ni kwamba the end justifies the means,hii itatugharimu sana kama ambavyo saa hz mahakama ya kadhi ilivyotucost watz coz ya njaa za lyatonga mrema na mahakama yake ya kadhi.,mwanasiasa anapofilisika anaishia kutumia njia haramu kuingia ikulu,kwa faida ya nani sasa?
 
Sijaliona kosa lake bado labda angechukua kadi ya uanachama wa CHADEMA. Huo ndio ungekuwa uthibitisho ila sio vidole wala kupiga picha na wanasiasa.I stand to be corrected.
 
Back
Top Bottom