S.Liondo
JF-Expert Member
- Apr 20, 2011
- 3,408
- 1,712
Watu wa CCM wanajua kukuza mambo kweli. Habari kutoka katika chanzo changu cha kuaminika ni kwamba kulikuwa na vijana wapatao kama kumi na tano hivi ambao ndio waliofanya vurugu kwenye mkutano wa Dr. Slaa kwa kurusha mawe, hali iliyofanya polisi kuingilia kati kwa kupiga mabomu ya machozi ili kuwatawanya. Hali hii ilipelekea mkutano kuvunjika. Hii ni kumaanisha kwamba ni kikundi kidigo tu cha walevi walionunuliwa na wala isichukuliwe kwamba ni wananchi wote wa Kigoma kama Magamba wanavyotaka kutuaminisha.