PICHA: Hali ya baridi mkoa wa Arusha inatisha

PICHA: Hali ya baridi mkoa wa Arusha inatisha

Hakuna sehem kuna baridi Tanzania hii Kama ngorongoro Arusha .... Acheni kabisa msiambiwe
 
wataalam wa jiografia nisaidieni,11°C inaweza kuleta barafu kweli?
 
Nilikuwa Makete wiki iliyopita Jioni kuanzia saa mojaTemperature ilikuwa inafika as low as 4 degrees....
 
Hiyo picha ya Theruji si ya arusha acha uongo na mimi niliipost jana kwanza kwa baridi ya nyuzi joto 11c haiwezi kusababisha theruji.
kaka kiiza hebu angalia vema hiyo picha. Hiyo gari namba zake na hayo mazingira. Naona kama ni Arusha
 
Sina uhakika hiyo picha imepigwa wap lakini arusha barabara ya kwenda namanga kuna sehemu inaitwa lengijave ni kawaida sana kutengeneza ice namna hiyo kipindi kama hiki cha baridi
kabisa "lengijave" ni neno la kimasai lenye maana ya "penye baridi" au ubaridini ni sawa tu na "Nairobi" yote yana maanisha kitu kimoja!
 
IPO shughuli wangeifanya wange zaana kinoma
 
Haahaa, chezeni kwa faida bana, sasa nyie mnaburudisha bure?! Halafu mnaendelea kushindia mihogo, kipaji hicho kitumieni vyema.
Tunashindia,mihogo,chips,maharage,ng'ombe,ndizi na vyakula vyote vinavyotoka mkoani kwako.We unafikiri tungekuwa tunalima wale wakulima wa mkoani kwako waliopauka kwa vumbi na ngozi iliyokomaa wangepata wapi soko la mazao yao?
 
Back
Top Bottom