Picha: Aibu jimboni kwa Ole Medeye

Picha: Aibu jimboni kwa Ole Medeye

Kila kitu ukikitafathiri kuwa ni uchochezi basi hata nyumbani kwako watoto wakilala mika kuwa umekuwa ukiwalisha dagaa ili hali wewe kila siku una lewa utaita uchochezi wa chadema..hahahah, nje ya mada; Badilisha jina mkuu siku hizi Okwi hayuko tena badala yake kuna dogo anaitwa Honongwa ni balaa...

Crashwise nimekusoma Kamanda wangu....hilo la User Name em tusaidiane, umaanisha iwe HONONGWA BOBAN SUNZU, unaweza pia kunipa nyingine. Kwa nini pia isiwe M4C IRAMBA
 
hapa haina kushangaa,watt wakipaya zero!mazingira yanaruhusu
 
Vipi na wewe ulisoma shule kama hii kama ndiyo mwaka gani? nakwanini hakuna mabadiliko ili hali deni la taifa lina zidi kuongezeka achilia mbali rasilimali tulizonazo....je kuna haja ya kuendelea na utwala huu..

Mkuu watakujibu eti Watu wameongezeka sana ndiyo maana serikali imeshindwa kuhudumia! Kwangu haya ni majibu ya kijinga! Hivi watu wanaongezeka ni vilema ambao hawana mchango katika kukuza uchumi? mbona Wachina wametumia wingi wao kukuza uchumi wao ila sisi watu wakiongezeka tunalalamika. Na ni kwanini watu wachache ndo wanakuwa matajiri wakati wengine wanakuwa masikini kwenye nchi hii moja? Uchumi wa Tanzania unakuwa kwa 6-7% ambacho ki kiwango kizuri sana na hata nchi za uraya na amerika husifia lakini cha ajabu ukuaji huu haulingani na hali ya maisha ya 99% ya watanzania. Hii inamaana kwamba uchumi ni kweli unakuwa kwa sababu ya lasilimali zinazovunwa na biashara za mafisadi. Hivyo basi Kanuni ya 20%/80% ndiyo inayotawala hapa yaani walalahoi 80% WANANYONYWA na uchumi kuonekana unakuwa lakini wanaofaidika ni mafisadi ambao ni only 20%!
 
ngoja ni mchane live huyu jamaa; nikiwa advance ilboru high school, mkuu wa shule hiyo ambaye kwa sasa amefukuzwa, alitulazimisha twende kwenye mkutano wa medey! kwenye mkutano alituahidi kununua coster ya shule na kuanzisha kilimo cha ndizi kwa gharama zake , akawaambia mabroo zetu waliokuwa cha sita muda huo, hwataondoka mpaka wamekula ndizi za shule na kupanda coster atakayo nunua! lakini hadi mm namaliza shuleni hapo, hakuna cha coster wala matunda ya olimedei! huwa nikimuona kwenye tv natamani ni msulubu kwa uongo wake...! tutategemea nn kwa kiongozi muongo kama huyu?
 
Tanzania mambo mengine kama tupo somalia,hivi JK anajisikiaje anapoona picha kama hizi?
 
ngoja ni mchane live huyu jamaa; nikiwa advance ilboru high school, mkuu wa shule hiyo ambaye kwa sasa amefukuzwa, alitulazimisha twende kwenye mkutano wa medey! kwenye mkutano alituahidi kununua coster ya shule na kuanzisha kilimo cha ndizi kwa gharama zake , akawaambia mabroo zetu waliokuwa cha sita muda huo, hwataondoka mpaka wamekula ndizi za shule na kupanda coster atakayo nunua! lakini hadi mm namaliza shuleni hapo, hakuna cha coster wala matunda ya olimedei! huwa nikimuona kwenye tv natamani ni msulubu kwa uongo wake...! tutategemea nn kwa kiongozi muongo kama huyu?
Pole sana mkuu ndiyo viongozi wa CCM na serikali yao uchwara...
 
Tanzania mambo mengine kama tupo somalia,hivi JK anajisikiaje anapoona picha kama hizi?
Huja wahi kusikia jibu lake aliulizwa kuhusu mvua akasema kwani yeye ni Mungu...hapa anaweza akasema kwani yeye ni fundi wa kujenga madarasa..chezea kikwete aka promota wa mchawi Diamond...
 
Duh!huku tunazid kuagiza ma-V8 tu nchi ya maabunuwasi hii kweli
Ikiwezekana mtakula hata nyasi lakini ndege ya raisi itanunuliwa kumbe walikuwa na 20% yao kwenye dili hilo...kudadadeki zao...
 
wewe Lema , acheni kumsumbua mwenzenu yupo usingizini!!!! unajua,,, mue na nidhamu. Mtu analala alafu mnamsumbua!
 
Picha za moja ya shule ya msingi jimbo la Ole Medeye (Enjoro) wanafunzi wa darasa la tano wanasomea chini ya mti huku walimu wakiishi kwenye mapango kama picha zinavyoonyesha, hakika CCM haina nia njeama na watanzania na kama watanzania nao wataendelea kulala basi tusishangaa watoto kuchora picha za ZOMBI na Messi.
View attachment 84059
View attachment 84060
View attachment 84061
Juu ni baadhi ya madarasa ya shule ya msingi Enjoro
View attachment 84062
View attachment 84063
Juu ni baadhi ya nyumba wanazoishi walimu..

Shule za hivi huwezi wakuta watoto wa akina Kawambwa wala Jeikei. Kwenye shule hizi utakuta watoto wa wapigakura, wale wanaowawezesha akina Kawambwa na Jeikei kupata kura za kutosha na kusomesha watoto wao nchi za nje kwenye world class academic institutions.

Mara nyingi wale wanaopiga kura kishabiki bila kufkiria wanampigia nani na ili awasaidie vp ndio huishia kuishi maisha ya kinyani na kuwaacha wapigiwa kura kusinzia bungeni na kushindwa kutekeleza majukumu waliyopewa na wananchi.

Mwaka 2015 umekaribia, tumia kura yako kuileta Tanzania tunayoitaka. Mabadiliko ya kweli yanaanza na wewe. Tumia kura yako.
 
Uko mbali sana kuna shule mwalimu haji kufundisha kisa hamna chaki
 
Lowasa si yupo karibu sana na hiyo shule aisee ! Kwa nini asipunguze kwenye lile fungu lake la makanisa ili kunusuru hiyo shule bhana !
 
Halafu utasikia,mheshimiwa Spika naunga mkono hoja,tumethubutu,tumeweza na tunasonga mbele.
 
Back
Top Bottom