PROFESA MUTHARIKA ATANGAZWA KUWA RAIS WA MALAWI
Joyce Banda amebana, ameachia! Hatimaye mshindi wa kiti cha urais nchini Malawi, Prof Bingu wa Mutharika, aliyesimama kwa tiketi ya chama cha Democratic Progressive Party (DPP), ametangazwa rasmi na tume ya uchanguzi ya Malawi (MEC) kuwa Rais wa Malawi. Katika uchaguzi huo Prof Mutharika aliyepata 34.6% ya kura zote, akifuatiwa na mgombea wa chama cha Malawi Congress Party (MCP), Bw Lazarus Chakwera (27.8%) aliyeshika nafasi ya pili. Nafasi ya tatu ilienda kwa mgombea wa chama cha People's Party (PP), Bi Joyce Banda (20.2%), aliyeangukia pua kwa kushika nafasi ya tatu.
MAONI YANGU
Bi Joyce Banda anastahili kushtakiwa kwa uchochezi wa kukataa matokeo na kusababisha vurugu zilizopelekea polisi kuwaua wanachi kadhaa wa Malawi ktk mji wa Lilongwe na Mzuzu. Lazima nchi za kiafrika zitunge sheria za kuwafikisha mahakamani viongozi ving'ang'anizi kama Joyce Banda wanaosababisha mauaji kwa raia wasiokuwa na hatia kwa sababu tu ya kupenda kuning'inia madarakani.
Aidha Bi Banda anastahili kuchukuliwa hatua kwa kuifukarisha Malawi na kupelekea uchumi wake kushuka kwa kasi ya kutisha, kitendo ambacho kimesababisha wananchi wa Malawi waamue kumpiga chini ili kumpisha Prof wa Mutharika aimarishe uchumi wan chi na kuboresha maisha ya wananchi wa Malawi wanaotopea kwenye umasikini wa kutisha.
FUNDISHO KWA TANZANIA
Uchaguzi huu uwe fundisho kwa wananchi wa Tanzania wanaotopea kwenye ufukara kwa sababu ya utawala dhalimu tulio nao, ili wafanye maamuzi sahihi mwaka 2015 na kuitosa CCM na serikali yake ambao ndio waliotufikisha hapa tulipo. Tusikae tu kulalamikia vitendo vya kifisadi (IPTL, ESCROW, EPA, RICHMOND, DEEP GREEN, KAGODA, UDA, etc) vinavyoisumbua nchi huku tukiwa hatuchuki hatua ya kuutupilia mbali utawala huu dhalimu na dhaifu unaonuka ufisadi.
Nawasilisha.
====================================================================================
OMBI
Mods tafadhali unganisha hii comment na uzi mkuu ili twenda kwa pamoja. Niliandaa uzi kabla ya kugundaua kama tayari uzi mwingine ulishaanzishwa.