Pesa mtaani zimepotelea wapi? Je, biashara yako inaendaje?

Jeep wrangler

JF-Expert Member
Jan 7, 2024
327
724
Wakuu habari zenu,

Wakati wa utawala wa Mkapa kuna hali ya ukata wa pesa ulijitokeza tukauita UKAPA.

Wakati wa JK kiasi flani mambo yakalainika japo ufisadi ulikuwa juu sana na mfumuko wa bei. Kila mtu aligeuka dalali. Pale Mnazi Mmoja wakazaliwa madali wenye vitambi na kiburi, huwezi uza gari kupitia wao.

Wakati wa JPM likajitokeza neno VYUMA vimekaza. Mwanzoni mwa utawala wa JPM miradi binafsi na iashara zilidoda, hili hata mimi lilinikumba lakini kuna wakati mambo yalininyookea hatari.

Awamu hii ya mama, tulitegemea mambo yanyooke zaidi kwani kwa kauli kuwa anaifungua nchi tulitegemea neema zaidi.

Mambo yamekuwa kinyume sana. Biashara nyingi zimeyumba, mfano kariakoo hali sio nzuri kabisa.

Makampuni mengi binafsi yako hoi.

Shule binafsi wanalia.

Wananchi huku chini uraiani hali ni tete kuliko maelezo.

Je huko uliko hali ikoje?
 
Ndiyo maana Chadema ni mazwazwa mnapinga hadi ujenzi wa bwawa la umeme ambao ni kwa ajili yenu wenyewe.

Kucha kuombaomba tu walichofanyia kazi wanaume wenzenu,
. Lema na Lisu Familia zao wanalishwa na wazungu.
we jamaa mbona unakuwa too much extremelly na chadema, kwani hapa tunajadili vyama vya siasa? Jenga hoja achana na chadema, chadema ni kama ccm na act tu,
 
Nimejaribu kila mbinu, hela haionekani. Naanza kujiuliza nimekosea wapi? Why now? Lakini pia kila ninaemuuliza anasema sio wewe tu hali imekuwa mbaya. But why? What has happened?
Kuna tatizo, tunahitaji wataalam wa uchumi watueleze kuna nini.

1. Je kodi inakusanywa lakini hiyo pesa hairudi mtaani kiasi cha pesa kupotea mtaani?

2. Serikali haitoi ajira ya kutosha?

3. Miradi mikubwa zinapewa kampuni za kigeni tu?

4. Mafisadi wanaficha pesa nje?

Sijui mkuu
 
Mkapa alijenga nchi vizuri ikawa kwenye direction sahihi, akaja Kikwete na kuivuruga vuruga, kiasi kuwa Magufuli alipojaribu kuinyoosha tena ikawa tatizo kubwa, na mama huyu ndiye imekuwa taabu kabisa. Uongozi wa nchi huhitaji uthabiti na maono imara, siyo blah blah za kujaza pesa kwenye mzunguko ili kufurahisha watu.
 
Mkapa alijenga nchi vizuri ikawa kwenye direction sahihi, akaja Kikwete na kuivuruga vuruga, kiasi kuwa Magufuli alipojaribu kuinyoosha tena ikawa tatizo kubwa, na mama huyu ndiye imekuwa taabu kabisa. Uongozi wa nchi huhitaji uthabiti na maono imara, siyo blah blah za kujaza pesa kwenye mzunguko ili kufurahisha watu.
Gwajima aliongea vizuri sana alipoingia bungeni kuwa hii tabia kila rais akiingia anaanza lwake hatufiki.

Kwangu mimi JK ndiye alikuwa muharibifu zaidi na magenge yake.

JPM alikuwa na nia njema sana ya kuijenga nchi...isipokuwa ubabe na kutosikiliza wataalamu wa uchumi.

But...Magufuli alianza kutufanya tuanze kutumia akili zaidi.

Sasa tuko zama za uchawa mtupu na hatujui uelekeo
 
Mimi namuelewa sana. Uzuri mimi nilikuwa na target kubwa kwenye biashara yangu. Hela nyingi nilikuwa na re-invest back into business so capital kubwa kiasi naweza ku-absorb hii situation kwa muda ila vinginevyo ningefunga biashara. Mauzo kudondoka 60% na gharama za uendeshaji zinakuwa si kitu kidogo.
Ni hatari sana mkuu
 
Back
Top Bottom