Pesa isiwe kipimo cha Utu, familia na taifa litaangamia

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,891
PESA ISIWE KIPIMO CHA UTU; FAMILIA NA TAIFA LITAANGAMIA.

Anaandika, Robert Heriel
Kuhani

Nataka watu waelewe kuwa Maisha hayana maana yoyote Kama hautajali utu wako na utu WA watu wengine.
Tafsiri sahihi ya Upendo ni kujijali utu wako na utu wa wanaokuzunguka.

Koo kubwa zote zenye nguvu zilijengwa katika misingi ya utu na kujaliana wao Kwa wao. Mataifa Makubwa yote unayoyaona yamejengwa katika msingi wa umoja, upendo na kujali utu WA binadamu.

Ukitaka familia na Ukoo utakaouanzisha uwe na nguvu basi lazima uujenge katika misingi na kanuni ya kujali utu, kupendana wao Kwa wao na kuheshimiana.

Ni hatari mtu kufanya kazi Kwa ajili ya pesa.
Ni hatari mtu kuwania uongozi Kwa ajili ya pesa.
Nasisitiza ni hatari Sana.
Hakuna taifa linalojengwa Kwa namna hiyo.

Ni hatari Mwanamke kutaka kuolewa na wewe Kwa sababu unapesa.
Ni hatari mwanaume kutaka kukuoa Kwa sababu unapesa.

Ukifika Maeneo ya makazini mwa watu ni rahisi kuelewa hatari ya watu waliojiingiza katika Kazi hizo Kwa sababu ya pesa au mishahara.

Ni hatari kuwa na wanaJeshi ambao wapo Kwa sababu ya pesa/mishahara. Ni hatari.

Ninaelewa nini ninakisema, ninaushahidi usio na Shaka katika Maeneo mbalimbali niliyoweza kufika nikajionea Kwa macho yangu.
Mahospitalini, mashuleni, viwandani n.k huko kote ni hatari kuwakuta watu waendekeza Pesa.

Hata Watu wanaouza nchi Kwa mikataba mibovu ni Kwa sababu ya kuendekeza Pesa.
Sio ajabu wenye uroho wa pesa hawaoni shida kutumia pesa za umma vibaya na kujilimbikizia Mali pasipo kujali utu wa wananchi masikini.

Pesa isiwe kipimo cha UTU.
Pesa iwe sehemu ya kuimarisha utu wa watu na sio kiwe kipimo cha UTU.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Ni better uwaambie ndugu zako hili swala...kwa sisi tunajali utu since day one
 
Dah kwa hili umechelewa sana....kuna watu hupotelea ughaibuni na wengine hufia hukohuko.....kwa kigezo cha kuogopa kurudi nyumbani na haliyakuwa hana kila kitu
 
kichwa cha habari kimenifanya niseme, "HONGERA KWAKO KWA KUONA MOJA YA POINT MUHIMU SANA INAYOIDIDIMIZA AFRICA"

Ulaya na USA waliujenga huu msingi wa kuheshimu utu hasa kupendana wao kwa wao na kujijali miongoni mwao, hii basic style of life ilipita kushoto kwa Mwafrica na matokeo yake kwenye kila kichwa cha MWAFRICA, PESA NDIO KIPAUMBELE NAMBA MOJA, iwe kuua, kuonea, kusimanga, unafiki, wizi, uzandiki nk ili tu apate pesa.

Slogani hii imeifanya Africa kuwa masikini kwa famili chache kuwa wabinafsi, kuifisadi Africa na kuwa madalali kuifisadi Africa ili wapate PESA kuendesha maisha na kujijengea himaya zao huku wakikandamiza utu wa kila mtu.
 
kichwa cha habari kimenifanya niseme, "HONGERA KWAKO KWA KUONA MOJA YA POINT MUHIMU SANA INAYOIDIDIMIZA AFRICA"

Ulaya na USA waliujenga huu msingi wa kuheshimu utu hasa kupendana wao kwa wao na kujijali miongoni mwao, hii basic style of life ilipita kushoto kwa Mwafrica na matokeo yake kwenye kila kichwa cha MWAFRICA, PESA NDIO KIPAUMBELE NAMBA MOJA, iwe kuua, kuonea, kusimanga, unafiki, wizi, uzandiki nk ili tu apate pesa.

Slogani hii imeifanya Africa kuwa masikini kwa famili chache kuwa wabinafsi, kuifisadi Africa na kuwa madalali kuifisadi Africa ili wapate PESA kuendesha maisha na kujijengea himaya zao huku wakikandamiza utu wa kila mtu.

Na hapo ndio maana sio ajabu mtu akaisaliti nchi yake Kwa Sababu ya pesa.
 
Nafikiri mfumo wa maisha sasa ya binaadam yanalazimisha watu waipe fedha kipaumbele zaidi ya utu, maana huwezi kupata huduma yoyote pasipo kitu fedha hivyo usipokuwa nayo maana yake hutahudumiwa, hivi leo kuna baadhi ya Mahospital ukiingia mapokezi kuna fedha kiasi inatakiwa utoe kabla ya mgonjwa hajamfikia daktari kama tahadhari, Jiulize sasa kama huna hiyo hela maana yake daktari hutamuona siku hiyo.
 
Nafikiri mfumo wa maisha sasa ya binaadam yanalazimisha watu waipe fedha kipaumbele zaidi ya utu, maana huwezi kupata huduma yoyote pasipo kitu fedha hivyo usipokuwa nayo maana yake hutahudumiwa, hivi leo kuna baadhi ya Mahospital ukiingia mapokezi kuna fedha kiasi inatakiwa utoe kabla ya mgonjwa hajamfikia daktari kama tahadhari, Jiulize sasa kama huna hiyo hela maana yake daktari hutamuona siku hiyo.

Huo ni uhuni na utapeli uliohalalishwa kisheria
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom