Waasisi wetu walipokuwa wanapigania uhuru wa taifa hili, lengo na maono yao yalikuwa kutengeneza taifa lenye utukufu, lenye kutawala mataifa mengine …," alisema Kardinali Pengo na kuongeza:
Maelezo hayo ni upotovu, hatukua n NIA YA KUMTAWALA YEYOTE YULE. Sisi si wakoloni au KATOLIKI (kwa vile katoliki ni jadi kwa kuwatawala wengine na ni madhumuni makubwa ya kanisa hilo). Sina la kuongeza.
"Haiwezekani mtu mkubwa tu, wala siyo mdogo kuja katika eneo la Kanisa la Katoliki, kukiwa kumejaa Maaskofu kutoka karibu nchi nzima, unasema maneno haya halafu unasema, siyo nyie ni viongozi wa makanisa madogomadogo," alilalamika Kardinali Pengo. Alifikiri anaogopwa, eti kwa vile kajaza maaskofu toka nchi nzima ndio Raisi angefyata mkia. Weeeeee ANAJIDANGANYA, atasemwa tu, tena Rais akialikwa tena atarudia maneno hayo hayo, ni uamuzi wake Pengo ajichimbie shimo au afanye kama wale viongozi wa katoliki kule Rwanda, asaidie mauaji ya wananchi au aanzishe vita maana mwenye nia ya kutawala wengine hutumia silaha. Sasa hivi watanzania hatujali, asitutishe tishe. Na Rais kashamjibu 'ASIDHANI KUWA VIONGOZI WA KATOLIKI NI MALAIKA' Haya tunasubiri toka kwa Pengo!
Aliongeza kwamba: "Kama ndivyo hivyo kwa nini sasa uje kuyasema maneno hayo katika eneo la Kanisa Katoliki."
Akasisitiza: "Mapadri, watawa; naomba tujiangalie kama sisi tunaguswa na hii kauli, kama haitugusi tumshukuru Mungu, lakini ni vyema hawa watu wakatajwa. Hapo atajaza mwenyewe, kama amesoma na kuelimika jibu atalipata yeye si mtoto mdogo. Na kwa kumsaidia Rais kasema Wao si Malaika. Kwani kanisa hili lilipokuwa likilawiti watoto wadogo, Maaskofu walikuwa hawajui. Kanisa hili linahitaji kila mara lipate msaada wa kuwanyoshea vidole wahalifu wao toka nje ya kanisa. Tutaendelea kutoa msaada huo na kuwasaidia wengi.
"Rais ataje majina ni kina nani wanahusika na ndani ya saa 48 awe ameyataja la sivyo itakuwa ni aibu zaidi kwake na Serikali," alisema Makamu Mwenyekiti wa CCT, Askofu Dk Valentino Mokiwa. Hakuna cha saa 24 wala 48, hatajwi mtu. Hizi ni shughuli za kiintelijensia. Hii ilikuwa ni tahadhari, ajue ni nini kitalikuta kanisa lake. Idara husika itaposhughulikia individuals, watakuja kuwasalimia rumande , mahakamani au jela. Akuuaye hakuonyeshi kisu, na ukikiona kisu basi ujue umepona. Ngoja nimfundishe Pengo katika hili, Hata kama nakujua unauza madawa ya kulevya, ikiwa ushahidi wangu sijaukusanya vizuri basi mahakamani utanishinda. Kama waliokushuhudia hawataki kutoa ushahidi, ndugu yangu utashinda kilaini. Na hakuna sheria inayomlazimisha mtu akatoe ushahidi. Hivyo hapa inabidi kujipanga vizuri sana. Haya ndio mambo yanatokea sana huko Latin Amerika, shahidi anakataa kwenda mahakamani kushuhudia.
Fuatilia kitabu changu kitakuwa hewani hivi karibuni " The catholic church and political future of Tanzania"