Pengo amtolea uvivu Kikwete

Pengo amtolea uvivu Kikwete

NDUGU WAKALA WA PENGO AMA PENGO MWENYEWE KWA KIFICHO...TUMSIFU YESU KRISTU WA NAZARETH. Ungekuwa unaongea kwa upole uliotukuka kama ulivyofanya hapa tungekuwa pamoja na tusingetiliana mashaka wala kukashifiana...maana iwapo lengo ni kulinda na kujenga nchi, malumbano hayafai.

Nilichokulaumu ni kumdhalilisha kiongozi mkuu wa nchi hata kama ana mapungufu si busara kwa Taifa na hata kwa mataifa ya nje. Mimi nina imani kuwa uko kwenye nafasi nzuri kabisa kama Mkuu wa Kanisa lenye waumini wengi watanzania...kuzungumza na Rais ukamshauri uso kwa uso juu ya mambo ambayo umeyatoa hadharani.

Yeye hakukuita kwa kuwa mlengwa hukuwa wewe ktk saga la madawa. Hakuwa ana undermine kanisa kwa uislamu wake...bali alizungunza kama Kiongozi wa nchi mwenye dhamana ya watanzania wote. Wewe na yeye ni watu wazima tena Viongozi...mnapolumbana through media isn't fair kwetu sisi watoto wenu.

Ukimwona pengine si wa imani yako..basi ungepitia hata kwa PM pengine ambapo protokali lazima ingezingatiwa. Jitahidi kama Kiongozi Mkuu wa kidini usiiteteleshe serikali ambayo ipo madarakani kisheria na hujazuiwa kuikosoa ama kuishauri muda wote. Najua jinsi imani ya dini ilivyo na nguvu na kiongozi kama wewe ukiitumia kama shield au spear utaigawa nchi mjomba.....mtu mzima akikosea mwite faragha...sema naye..ni binadamu yule anaelewa...

Ukitumia imani kulumbana naye itakuwa kama Bin Laden Osama kutumia dini kama kivuli lkn finally ameuwawa na anaowaita infidels. Mumi nadhani kama JK angekuwa ana utawala wa kiimla...hata jamii forums isingekuwepo na kungekuwa na msako mkali dhidi ya wabaya wake just like Libya...etc. TUFIKE MAHALI TUJENGE KISIWA CHA AMANI JAMANI TUACHE TOFAUTI ZA KIDINI NA KISIASA.

IN WAR THERE IS NO WINNER...ALL ARE LOOSERS...alisema British Premier Chamberlain in WW2 akiwatahadharisha waingereza juu ya athari za kupigana na Hitler. Alujiuzulu kwa shinikizo na akarithiwa na Winston Churchill aluyeingia kwa kutangaza "There is nothing to offer except blood....sweat and tears" Ilikuwa patashika nguo kuungua.

Sasa twaweza furahi Rais akijiuzuru lakini je unaye mtu unayependekeza awe badala yake? Na je unadhani mtu huyo unayempendekeza anakubalika na majeshi yote ya ulinzi na usalama na wananchi? Yasije yakawa ya Kabila or JF Kennedy or A. Lincolin or unawajua bwana. Ushabiki wa kiimani ya dini na kuyasahau hayo itakuja tokea mambo ya Ariel Sharon btn Likurd na Kaduma yake...or ya Bingu wa Mutharika na chama chake.

Tumpe pumzi Rais ya kuongoza nchi huku tukimshauri kupitia majukwaa kama hivi ili nini afanye juu ya kipi tutakacho. Kumtukana Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vyote vya ulinzi na usalama na ambaye ni Rais kidemokrasia anayeachia demokrasia ya habari nchini....KWANGU MIMI NI UHAINI. NA INGELIKUWA MMENICHAGUA MIMI NDO RAIS...HAKI YA MAMA YANGU MZANAKI...UNAOKOTWA UNA MSUMARI WA INCH SITA UTOSINI..POTELEA KWA MBALI ILI NCHI ITAWALIKE BILA USWAHILI.

Kardinali kama kiongozi wa kidini, kaona kwamba ana uwezo wa kuingia Ikulu na kuteta na Kikwete, lakini baba hateti kwake katika kurekebisha mambo.

Wengi tunaona hili kama tatizo la Kikwete. Lakini Kikwete ni nani jamani? Si Mtanzania mwenzetu yule? Hizo tabia za kuteta teta, vineno nusu nusu, vijembe vijembe bila sababu siku hizi inaota sugu. Sasa basi, katika kumsema Kikwete, kuna ujumbe kwa wengi sana. Tuwe wakweli, tuwe wawazi, tuwe direct. Hizi habari za mafumbo fumbo hazifai, especially kwa mtu mwenye dhamana ya heshima kama rais.

Kwa hivyo ile ilikuwa broadcast maalum kwa Kikwete, lakini ujumbe utanufaisha wabongo wote wenye tabia kama hizo.
 
Nimesema angemnyoshea kidole na Mkapa "Kwanza".. kwa sababu Mkapa anahusika kwa madudu mengine mengi tuliyonayo sasa na binafsi naamini anastahili kujibu. Ningependa mtu kame Pengo amlaumu Kikwete kwa kutomchukulia hatua Mkapa! Haya ya udini na waachie wengine wanaobishania hayo.

Huwezi kupata kila unachopenda.

Ona hapa Kardinali anamuwajibisha raisi awe makini katika kauli tu watu washataka kuanzisha rabsha. Liberation Theology aside, huwezi kutaka Pengo ndio achukue jukumu la kusimamia kidete kila jambo.

Kwanza Pengo mwenyewe anaongea kwa kutumia Vatican script. Na Mkapa ingawa sakramenti yake Johhnie Walker Black Label na Kanisa lake Palm Beach Hotel lakini miaka yake kumi alijibalaguza pale St. Immaculatta. Kwa hiyo si bure.
 
Mwanakijiji,jana kwenye mada ya zitto uliomba zijadiliwe hoja na si mtu! Leo hoja unaweka pembeni unamjadili pengo! Lakin pia mbona pengo ametoa matamko mengi Rais achukue hatua kwa mafisadi wote! Tena kwa ukali mimi binafsi nimeshuhudia.hajawahi kumuombea msamaha mkapa jamani! Hata MM una fall on the same trap!Unaacha hoja unajadili mtu!
 
waliomshikia bango kwa sauti kubwa kabisa mkapa ni wakristo wenzake akina slaa,ulimwengu,mwanakijiji n.k mbona pengo amekuwa kila mara hachoki kuzungumzia ufisadi!
 
imechukua muda kutafakari kabla pengo hajatoa tamko,umepita muda kuona hatua kwa walioshukiwa hakuna!hili la kwenda kwenye tukio lilokusanya maaskofu nchi nzima na kutoa shutuma nzito bila kuweka wazi ulitaka akae kimya?
 
Mwanakijiji,jana kwenye mada ya zitto uliomba zijadiliwe hoja na si mtu! Leo hoja unaweka pembeni unamjadili pengo! Lakin pia mbona pengo ametoa matamko mengi Rais achukue hatua kwa mafisadi wote! Tena kwa ukali mimi binafsi nimeshuhudia.hajawahi kumuombea msamaha mkapa jamani! Hata MM una fall on the same trap!Unaacha hoja unajadili mtu!

Ni kweli lakini sijasema lolote kama Pendo ni mtu aina gan au sijasema namuwazia nini yeye binafsi. Nilichosema ni kuwa Pengo kama ameamua kujenga hoja dhidi ya watawala aende mbele kabisa.

Kwa sababu bado tuna issues za Mkapa ambazo ziko unresolved na hakuna mtu anayetaka kuzigusa issue hizo na ninaamini yeye kama ambavyo anachukulia wito huu nina uhakika anaweza kulileta hili la Mkapa vile vile.

Wengine wana luxury ya kuchagua nini wakomalie lakini katika hili tuna tatizo katika utawala na Kikwete ni sehemu ya tatizo hilo. So lets deal with the whole shabang!
 
****** hatumii busara na ndo maana anaongea pumba.hatujawah kuwa na rais mwenye welewa mdogo kama wa sasa.ngoje nov 1 2015 atajua pa kwenda.ila kwa kuwa mtoto wa zygon maneno yake ki zygon zygon
 
Kiranga,
Kaka hiki anachofanya Kardinali Pengo hakikuanza leo wala jana. Hii ni "Liberation Theology", kanisa linapowapigania watu masikini kama sehemu ya mafundisho ya Yesu Kristo. Kaangalie hata Papa John Paul aliingia katika siasa za Poland kumsaidia Lech Walesa kuwaondoa Wakomunisti, kuna maaskofu mpaka wameuawa huko kipande cha Latin America kwa kuwasemea mbovu ma dikteta wa kijeshi. Kwa hiyo ni vile tu siasa zetu hazijakomaa ndiyo maaana tunaona kitu kigeni. Lakini huko kipande cha Costa Rica na Nicaragua Askofu kumbwatia Commandante si kitu cha ajabu wala nini.
Mkuu kila case ina sababu zake na Historia. Kanisa limeweza kujiingiza ktk siasa kwa sababu za kiimani hili haliwezi kupotea..Makanisa yameingilia sana siasa sehemu ambazo Ukristu au haki ya watu kuabudu ilikuwa wananyimwa hivyo mikusanyiko ya kidini ilichukuliwa kama ni mikusanyiko ya Upinzani. Makanisa yaliwasaidia tawala zozote zile ili mradi tu swala la kiimani lipewe nafasi na ilitokea kwa nia njema ingawa sii lazima kisiasa ilikuwa kutetea wanyonge..Kwetu Afrika hao Makaburu na wakoloni walitumia makanisa kututawala na huko Ulaya kanisa lilitawala baadhi ya nchi za kusini kwa bara hilo, hivyo hakuna njia moja..Hata jitihadia za Uhuru wa nchi za kiafrika zilipigwa vita na baadhi ya makanisa huku mengine yaliyo karibu na weusi yakiwasaidia.

Lakini, huu sii ubishi wala sehemu ya mjadala wetu isipokuwa tunazungumzia Pengo kumtolea Uvivu JK. Mimi sioni kabisa sababu zaidi ya kutafuta ugonvi wa kidini...Ni maneno ya kawaida kabisa ambayo hayana ulazima wa kutaja majina ya wahusika. na nimeuliza mara mia kidogo hapa.. JK akitaja majina ya wafanya biashara za unga huyo Pengo atafanya nini?.. Yaani unamtaka rais ataje majina ya wauza unga kwa sababu kazungumzia kwa kukanya tabia ya viongozi wa dini kujihushisha na biashara za Unga?..Mimikila siku nawakanya watoto wangu kuhusiana na madawa ya kulevya, nawakanya kujiepusha na makundi ya baadhi ya watoto wenzao na haina maana nawatuhumu wao kuwa wabaya...

Kiranga JK ni rais hana sababu ya kutaja majina isipokluwa vyombo vya kuapmabana na madawa ya kulevya ndio wanaweza kumuomba majina hayo kwa sababu wanataka kuyanyia kazi. Pengo hajui majina hayo yako wapi, hajui kwa nini serikali inayaweka hata kama.... hii si kazi ya kanisa hivyo yeye kama kiongozi wa dini angeweza kabisa kumvuta JK pembeni na kupata maelekezo zaidi kuliko kukurupuka ktk jukwaa la kidini na kuanza kumshambulia JK sii kwa sababu nyingine ila ile inayowagusa kanisa.

halafu mnataka JK awe muazi ktk Kuwataja wahalifu?.. mkuu wangu kusema kweli hata kashfa ya Lowassa mimi simlaumu JK hata Kidogo. Yeye kama rais alikubali mashtaka yapelekwe bungeni na Lowassa akatimuliwa Uwaziri mkuu kisha sisi tukashindwa kumfungulia mashtaka tukitaka JK ndiye achukue jukumu hilo.. WHY JK wakati yeye kisha mvua kinga zote kilichjotakiwa ni sisi kumtengenezea kesi? lTunavyozungumza sasa hivi hakuna hata kesi moja iliwahi kupelekwa dhidi ya Lowassa na hata Bunge limezuia kuzungumzia maswala ya Richmond au Dowans..

Sisi wenyewe tumeshindwa hata kumfunga Chenge kwa mauaji, Karamagi na wengine wote tunategemea JK achuke jukumu zaidi la kuwafungulia mashtaka as if katiba inamtaka yeye tu ndiye afanye hivyo. Na leo hii Lowassa anakuja na utetezi mkubwa sana dhidi ya JK. tena Wadanganyika wamejipanga nyuma yake kuanzisha hadi maandamano huo Marekani..

hawa wote mimi nawaambia walifahamu mapema kwamba JK hatufai na wao kwa inda na tamaa zao walimchagua kwa nguvu zote arudi maradakani. Na hata kubarikiwa namisikiti na makanisa leo wanataka kuja hapa na kutuambia nini udhaifu wa JK... Mkuu wangu rais ni Leader, na kiongozi ni mtu anayeweza kuongoza watu ktk maadili mema kama alivyo Kardinal Pengo. Sii kazi ya Pengo kuwakamata au kuwataja hadharani Mapadre au wafuasi wa dini wahalifu au kutoa list yao..Tena basi yeye anazungumza kwamba kiongozi asiyeweza kutaja majina ya wahalifu ni dhaifu mbona kanisa linawakataza kutaja majina ya wahalifu walioungama.. Je naye tuseme ni dhaifu! - sidhani.

Mkuu wangu sio kazi ya JK kukamata wauza unga, na wala sii kazi ya Pengo kufuatilia wauza unga isipokuwa ukimsoma vizuri Kardinal Pengo utagundua ana beef na JK na mimi najua vizuri sana kwamba Uchaguzi wa 2010 - Pengo mwenyewe alimwabia JK ukitaka kura za wakristu njoo unione..Ni maneno ambayo watu wa karibu na JK wanayajua na yamezungumzwa sana mjini... Tumpe heshima yake kama kiongozi wa dini lakini tusipende sana kutetea kila kitu kwa sababu tu ya wadhifa wake.
 
Kiranga,
Mkuu kila case ina sababu zake na Historia. Kanisa limeweza kujiingiza ktk siasa kwa sababu za kiimani hili haliwezi kupotea..Makanisa yameingilia sana siasa sehemu ambazo Ukristu au haki ya watu kuabudu ilikuwa wananyimwa hivyo mikusanyiko ya kidini ilichukuliwa kama ni mikusanyiko ya Upinzani. Makanisa yaliwasaidia tawala zozote zile ili mradi tu swala la kiimani lipewe nafasi na ilitokea kwa nia njema ingawa sii lazima kisiasa ilikuwa kutetea wanyonge..Kwetu Afrika hao Makaburu na wakoloni walitumia makanisa kututawala na huko Ulaya kanisa lilitawala baadhi ya nchi za kusini kwa bara hilo, hivyo hakuna njia moja..Hata jitihadia za Uhuru wa nchi za kiafrika zilipigwa vita na baadhi ya makanisa huku mengine yaliyo karibu na weusi yakiwasaidia.

Lakini, huu sii ubishi wala sehemu ya mjadala wetu isipokuwa tunazungumzia Pengo kumtolea Uvivu JK. Mimi sioni kabisa sababu zaidi ya kutafuta ugonvi wa kidini...Ni maneno ya kawaida kabisa ambayo hayana ulazima wa kutaja majina ya wahusika. na nimeuliza mara mia kidogo hapa.. JK akitaja majina ya wafanya biashara za unga huyo Pengo atafanya nini?.. Yaani unamtaka rais ataje majina ya wauza unga kwa sababu kazungumzia kwa kukanya tabia ya viongozi wa dini kujihushisha na biashara za Unga?..Mimikila siku nawakanya watoto wangu kuhusiana na madawa ya kulevya, nawakanya kujiepusha na makundi ya baadhi ya watoto wenzao na haina maana nawatuhumu wao kuwa wabaya...

Kiranga JK ni rais hana sababu ya kutaja majina isipokluwa vyombo vya kuapmabana na madawa ya kulevya ndio wanaweza kumuomba majina hayo kwa sababu wanataka kuyanyia kazi. Pengo hajui majina hayo yako wapi, hajui kwa nini serikali inayaweka hata kama.... hii si kazi ya kanisa hivyo yeye kama kiongozi wa dini angeweza kabisa kumvuta JK pembeni na kupata maelekezo zaidi kuliko kukurupuka ktk jukwaa la kidini na kuanza kumshambulia JK sii kwa sababu nyingine ila ile inayowagusa kanisa.

halafu mnataka JK awe muazi ktk Kuwataja wahalifu?.. mkuu wangu kusema kweli hata kashfa ya Lowassa mimi simlaumu JK hata Kidogo. Yeye kama rais alikubali mashtaka yapelekwe bungeni na Lowassa akatimuliwa Uwaziri mkuu kisha sisi tukashindwa kumfungulia mashtaka tukitaka JK ndiye achukue jukumu hilo.. WHY JK wakati yeye kisha mvua kinga zote kilichjotakiwa ni sisi kumtengenezea kesi? lTunavyozungumza sasa hivi hakuna hata kesi moja iliwahi kupelekwa dhidi ya Lowassa na hata Bunge limezuia kuzungumzia maswala ya Richmond au Dowans..

Sisi wenyewe tumeshindwa hata kumfunga Chenge kwa mauaji, Karamagi na wengine wote tunategemea JK achuke jukumu zaidi la kuwafungulia mashtaka as if katiba inamtaka yeye tu ndiye afanye hivyo. Na leo hii Lowassa anakuja na utetezi mkubwa sana dhidi ya JK. tena Wadanganyika wamejipanga nyuma yake kuanzisha hadi maandamano huo Marekani..

hawa wote mimi nawaambia walifahamu mapema kwamba JK hatufai na wao kwa inda na tamaa zao walimchagua kwa nguvu zote arudi maradakani. Na hata kubarikiwa namisikiti na makanisa leo wanataka kuja hapa na kutuambia nini udhaifu wa JK... Mkuu wangu rais ni Leader, na kiongozi ni mtu anayeweza kuongoza watu ktk maadili mema kama alivyo Kardinal Pengo. Sii kazi ya Pengo kuwakamata au kuwataja hadharani Mapadre au wafuasi wa dini wahalifu au kutoa list yao..Tena basi yeye anazungumza kwamba kiongozi asiyeweza kutaja majina ya wahalifu ni dhaifu mbona kanisa linawakataza kutaja majina ya wahalifu walioungama.. Je naye tuseme ni dhaifu! - sidhani.

Mkuu wangu sio kazi ya JK kukamata wauza unga, na wala sii kazi ya Pengo kufuatilia wauza unga isipokuwa ukimsoma vizuri Kardinal Pengo utagundua ana beef na JK na mimi najua vizuri sana kwamba Uchaguzi wa 2010 - Pengo mwenyewe alimwabia JK ukitaka kura za wakristu njoo unione..Ni maneno ambayo watu wa karibu na JK wanayajua na yamezungumzwa sana mjini... Tumpe heshima yake kama kiongozi wa dini lakini tusipende sana kutetea kila kitu kwa sababu tu ya wadhifa wake.

Hapo JK kachemsha, Scarface anakwambia "If you wannna shoot, shoot, don't talk"

Kama JK ana uchungu na nchi, afanye kamatakamata, atie watu ndani, wahukumiwe mahakamani kwa haki, halafu baada ya hapo anaweza kuchonga anavyotaka fulani Askofu muuza madawa tumemfunga, hatutaki mchezo.

Yeye anabakia kuchekacheka huku watu wanakufa kwa janga. Stories nyiiingi. Ndiyo maana watu wanamuona mzushi tu.
 
Pengo amnyoshee kidole Mkapa kwanza; then sisi wengine tutamchukulia serious.

Mzee Mwanakijiji sasa, utakuwa umeanza kuzeeka vya kutosha sasa......hivi ni Pengo aliyeanza kuongea, au sijakuelewa na hii post yako ulikuwa unamjibu mtu mwingine?

Hivi inawezekana kweli shutuma atoe JK halafu aanze kumnyooshea kidole Mkapa, bila shaka wewe huyu huyu ungekuwa wa kwanza kusema Pengo anamuogopa JK kwa kuwa kwa sasa yupo madarakani na kuzidi kushangaa inakuwaje shutume atoe JK, halafu yeye amshambulie Mkapa, kweli pamoja na unawezoweza kuita hekima katika michango napata jibu kuwa watanzania tupo kwa ajiri ya malumbano na kulalamika tu
 
NDUGU WAKALA WA PENGO AMA PENGO MWENYEWE KWA KIFICHO...TUMSIFU YESU KRISTU WA NAZARETH. Ungekuwa unaongea kwa upole uliotukuka kama ulivyofanya hapa tungekuwa pamoja na tusingetiliana mashaka wala kukashifiana...maana iwapo lengo ni kulinda na kujenga nchi, malumbano hayafai.

Nilichokulaumu ni kumdhalilisha kiongozi mkuu wa nchi hata kama ana mapungufu si busara kwa Taifa na hata kwa mataifa ya nje. Mimi nina imani kuwa uko kwenye nafasi nzuri kabisa kama Mkuu wa Kanisa lenye waumini wengi watanzania...kuzungumza na Rais ukamshauri uso kwa uso juu ya mambo ambayo umeyatoa hadharani.

Yeye hakukuita kwa kuwa mlengwa hukuwa wewe ktk saga la madawa. Hakuwa ana undermine kanisa kwa uislamu wake...bali alizungunza kama Kiongozi wa nchi mwenye dhamana ya watanzania wote. Wewe na yeye ni watu wazima tena Viongozi...mnapolumbana through media isn't fair kwetu sisi watoto wenu.

Ukimwona pengine si wa imani yako..basi ungepitia hata kwa PM pengine ambapo protokali lazima ingezingatiwa. Jitahidi kama Kiongozi Mkuu wa kidini usiiteteleshe serikali ambayo ipo madarakani kisheria na hujazuiwa kuikosoa ama kuishauri muda wote. Najua jinsi imani ya dini ilivyo na nguvu na kiongozi kama wewe ukiitumia kama shield au spear utaigawa nchi mjomba.....mtu mzima akikosea mwite faragha...sema naye..ni binadamu yule anaelewa...

Ukitumia imani kulumbana naye itakuwa kama Bin Laden Osama kutumia dini kama kivuli lkn finally ameuwawa na anaowaita infidels. Mumi nadhani kama JK angekuwa ana utawala wa kiimla...hata jamii forums isingekuwepo na kungekuwa na msako mkali dhidi ya wabaya wake just like Libya...etc.

TUFIKE MAHALI TUJENGE KISIWA CHA AMANI JAMANI TUACHE TOFAUTI ZA KIDINI NA KISIASA. IN WAR THERE IS NO WINNER...ALL ARE LOOSERS...alisema British Premier Chamberlain in WW2 akiwatahadharisha waingereza juu ya athari za kupigana na Hitler. Alujiuzulu kwa shinikizo na akarithiwa na Winston Churchill aluyeingia kwa kutangaza "There is nothing to offer except blood....sweat and tears" Ilikuwa patashika nguo kuungua.

Sasa twaweza furahi Rais akijiuzuru lakini je unaye mtu unayependekeza awe badala yake? Na je unadhani mtu huyo unayempendekeza anakubalika na majeshi yote ya ulinzi na usalama na wananchi? Yasije yakawa ya Kabila or JF Kennedy or A. Lincolin or unawajua bwana. Ushabiki wa kiimani ya dini na kuyasahau hayo itakuja tokea mambo ya Ariel Sharon btn Likurd na Kaduma yake...or ya Bingu wa Mutharika na chama chake.

Tumpe pumzi Rais ya kuongoza nchi huku tukimshauri kupitia majukwaa kama hivi ili nini afanye juu ya kipi tutakacho. Kumtukana Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vyote vya ulinzi na usalama na ambaye ni Rais kidemokrasia anayeachia demokrasia ya habari nchini....KWANGU MIMI NI UHUNI.

NA INGELIKUWA MMENICHAGUA MIMI NDO RAIS...HAKI YA MAMA YANGU MZANAKI...UNAOKOTWA UNA MSUMARI WA INCH SITA UTOSINI..POTELEA KWA MBALI ILI NCHI ITAWALIKE BILA USWAHILI.
Kama mtu anakushambulia ni ruhusa kujilinda....ni lazima tuwe wa wazi kwa maslahi ya taifa, vinginevyo tunkiendekeza tafsiri zisizo sahihi tutaishia kuwa wajinga kwa kudhani tumeelwa kumbe sivyo, elewa kuwa rais hakutukunwa bali amejibiwa kama katika jibu lile mtu anaweza kutafsiri kuna matusi ndani yake, basi ujue hali hiyo ina reflect kauli ya msingi iliyotolewa na anayejibiwa.
 
ʞontɹact Sniper;2367109 said:
Mzee Mwanakijiji sasa, utakuwa umeanza kuzeeka vya kutosha sasa......hivi ni Pengo aliyeanza kuongea, au sijakuelewa na hii post yako ulikuwa unamjibu mtu mwingine?
Hivi inawezekana kweli shutuma atoe JK halafu aanze kumnyooshea kidole Mkapa, bila shaka wewe huyu huyu ungekuwa wa kwanza kusema Pengo anamuogopa JK kwa kuwa kwa sasa yupo madarakani na kuzidi kushangaa inakuwaje shutume atoe JK, halafu yeye amshambulie Mkapa, kweli pamoja na unawezoweza kuita hekima katika michango napata jibu kuwa watanzania tupo kwa ajiri ya malumbano na kulalamika tu

Ujamuelewa vizuri Mzee Mwanakijiji. anakuambia Pengo angemnyooshea mkono kwanza Mkapa kwa UFISADI alioufanya wakati wa kipindi chake cha utawala wake.
Kauza Migodi yote kwa wageni, Kauza nyumba zote za serikali, kabinafsisha kila kitu na Mgodi wa Kiwila akajiuzia Pengo anamuangalia tu kashindwa kumnyooshea kidole Mkapa! Watazania kwa kupenda kulalamika kama wewe unavyolalamika
 
Kiranga,
Mkuu kila case ina sababu zake na Historia. Kanisa limeweza kujiingiza ktk siasa kwa sababu za kiimani hili haliwezi kupotea..Makanisa yameingilia sana siasa sehemu ambazo Ukristu au haki ya watu kuabudu ilikuwa wananyimwa hivyo mikusanyiko ya kidini ilichukuliwa kama ni mikusanyiko ya Upinzani. Makanisa yaliwasaidia tawala zozote zile ili mradi tu swala la kiimani lipewe nafasi na ilitokea kwa nia njema ingawa sii lazima kisiasa ilikuwa kutetea wanyonge..Kwetu Afrika hao Makaburu na wakoloni walitumia makanisa kututawala na huko Ulaya kanisa lilitawala baadhi ya nchi za kusini kwa bara hilo, hivyo hakuna njia moja..Hata jitihadia za Uhuru wa nchi za kiafrika zilipigwa vita na baadhi ya makanisa huku mengine yaliyo karibu na weusi yakiwasaidia.

Lakini, huu sii ubishi wala sehemu ya mjadala wetu isipokuwa tunazungumzia Pengo kumtolea Uvivu JK. Mimi sioni kabisa sababu zaidi ya kutafuta ugonvi wa kidini...Ni maneno ya kawaida kabisa ambayo hayana ulazima wa kutaja majina ya wahusika. na nimeuliza mara mia kidogo hapa.. JK akitaja majina ya wafanya biashara za unga huyo Pengo atafanya nini?.. Yaani unamtaka rais ataje majina ya wauza unga kwa sababu kazungumzia kwa kukanya tabia ya viongozi wa dini kujihushisha na biashara za Unga?..Mimikila siku nawakanya watoto wangu kuhusiana na madawa ya kulevya, nawakanya kujiepusha na makundi ya baadhi ya watoto wenzao na haina maana nawatuhumu wao kuwa wabaya...

Kiranga JK ni rais hana sababu ya kutaja majina isipokluwa vyombo vya kuapmabana na madawa ya kulevya ndio wanaweza kumuomba majina hayo kwa sababu wanataka kuyanyia kazi. Pengo hajui majina hayo yako wapi, hajui kwa nini serikali inayaweka hata kama.... hii si kazi ya kanisa hivyo yeye kama kiongozi wa dini angeweza kabisa kumvuta JK pembeni na kupata maelekezo zaidi kuliko kukurupuka ktk jukwaa la kidini na kuanza kumshambulia JK sii kwa sababu nyingine ila ile inayowagusa kanisa.

halafu mnataka JK awe muazi ktk Kuwataja wahalifu?.. mkuu wangu kusema kweli hata kashfa ya Lowassa mimi simlaumu JK hata Kidogo. Yeye kama rais alikubali mashtaka yapelekwe bungeni na Lowassa akatimuliwa Uwaziri mkuu kisha sisi tukashindwa kumfungulia mashtaka tukitaka JK ndiye achukue jukumu hilo.. WHY JK wakati yeye kisha mvua kinga zote kilichjotakiwa ni sisi kumtengenezea kesi? lTunavyozungumza sasa hivi hakuna hata kesi moja iliwahi kupelekwa dhidi ya Lowassa na hata Bunge limezuia kuzungumzia maswala ya Richmond au Dowans..

Sisi wenyewe tumeshindwa hata kumfunga Chenge kwa mauaji, Karamagi na wengine wote tunategemea JK achuke jukumu zaidi la kuwafungulia mashtaka as if katiba inamtaka yeye tu ndiye afanye hivyo. Na leo hii Lowassa anakuja na utetezi mkubwa sana dhidi ya JK. tena Wadanganyika wamejipanga nyuma yake kuanzisha hadi maandamano huo Marekani..

hawa wote mimi nawaambia walifahamu mapema kwamba JK hatufai na wao kwa inda na tamaa zao walimchagua kwa nguvu zote arudi maradakani. Na hata kubarikiwa namisikiti na makanisa leo wanataka kuja hapa na kutuambia nini udhaifu wa JK... Mkuu wangu rais ni Leader, na kiongozi ni mtu anayeweza kuongoza watu ktk maadili mema kama alivyo Kardinal Pengo. Sii kazi ya Pengo kuwakamata au kuwataja hadharani Mapadre au wafuasi wa dini wahalifu au kutoa list yao..Tena basi yeye anazungumza kwamba kiongozi asiyeweza kutaja majina ya wahalifu ni dhaifu mbona kanisa linawakataza kutaja majina ya wahalifu walioungama.. Je naye tuseme ni dhaifu! - sidhani.

Mkuu wangu sio kazi ya JK kukamata wauza unga, na wala sii kazi ya Pengo kufuatilia wauza unga isipokuwa ukimsoma vizuri Kardinal Pengo utagundua ana beef na JK na mimi najua vizuri sana kwamba Uchaguzi wa 2010 - Pengo mwenyewe alimwabia JK ukitaka kura za wakristu njoo unione..Ni maneno ambayo watu wa karibu na JK wanayajua na yamezungumzwa sana mjini... Tumpe heshima yake kama kiongozi wa dini lakini tusipende sana kutetea kila kitu kwa sababu tu ya wadhifa wake.
Sioni kwanini kikuume na kukukwaza kisi hicho mkuu.....Pengo ametumia jakwaa lake, kumbuka Pengo anaongoza waumini ambao ni wanasiasa, wengine ni wanausalama, wanafunzi waalimu n. Sasa kama kauli inatolewa kwa ujumla ule ni hatari sana kwa watu kujenga imani na viongozi wao wa dini. Ndiyo maana kanisa likajiweka wazi zaidi kwa kumtaka rais kuwataja watu hao na ikibidi iwachukulia hatu.

Mimi nilichokitafsiri tangu mwanzo katika kauli za maaskofu si kujitetea kuwa hayo mambo hayafanyiki, bali wahusika watajwe lilijiweka wazi na wala halikutoa kauli za kujijengea uzio wasikaguliwe na serikali.

Kiongozi akitembelea kanda ya kati na magharibi mwa nchi yetu ataongelea mambo ya ukame, na kuwaahidi kujenga miuondo mbinu ya barabara, shughuli za maendeleo na kuangalia namna ya kuendesha shughuli za kilimo maeneo hayo, kwa kuwa maeneo hayo yana mahitaji ya aina hiyo, akienda Mbeya lazima kauli itabadilika japo wote ni watanzania.

Hivyo kwa kusema maaskofu wanajihusisha na biashara za madawa ya kulevya katika jukwaa la wakristo tena kumuapisha Askofu, bila kuwataja majina inaleta mkanganyiko, au alimlenga aliyekuwa anaapishwa hivyo ni kama alikuwa anajiuliza uadilifu na umakini wa kanisa kimalezi na kiimani uko wapi hadi kumuapisha muuza madawa ya kulevy? Ndiyo maana kanisa linahitaji msaada wake kwa kuwa muwazi zaidi kwani atakuwa amewasaidia sana.

Na ndiyo maana ya kauli ile ukichukulia hakutumia kauli ya kuwanyooshea baadhi na kuwatenga wengine bali ya kuwajumuisha wote. Kwa hiyo ina maana baada ya uchunguzi na kubaini maaskofu (kwa sababu kauli rais ilisema Maaskofu wanajihusisha, afadhali hata angetumia neno viongozi wa dini), kwa baada ya kubaini kuna maaskofu wakaamua kutumia ujumla ili kuuvuruga ukristo, hivi unadhani ukifanikiwa kuuvuruga ukristo au uislamu jamii hii inaweza ikasilimika kweli? Hivi pamoja na pande mbili hizi za dini kupeana shutuma hatuaoni mazuri yaliyofanywa na dini hizi?

Sidhani kama jamii yetu ina upofu wa macho na kiimani kwa kiasi hicho?
 
Ukiogopa kusema kweli kwa sababu unaogopa watu watakavyokutafsiri utakuwa huwezi kusema chochote maishani mwako, maana kila mtu anaweza kukutafisiri anavyotaka.



Kaka hiki anachofanya Kardinali Pengo hakikuanza leo wala jana. Hii ni "Liberation Theology", kanisa linapowapigania watu masikini kama sehemu ya mafundisho ya Yesu Kristo. Kaangalie hata Papa John Paul aliingia katika siasa za Poland kumsaidia Lech Walesa kuwaondoa Wakomunisti, kuna maaskofu mpaka wameuawa huko kipande cha Latin America kwa kuwasemea mbovu ma dikteta wa kijeshi. Kwa hiyo ni vile tu siasa zetu hazijakomaa ndiyo maaana tunaona kitu kigeni. Lakini huko kipande cha Costa Rica na Nicaragua Askofu kumbwatia Commandante si kitu cha ajabu wala nini.

Hebu angalia kipande hiki hapa wanaongelea hii "Liberation Theology" Liberation theology - Wikipedia, the free encyclopedia



Kwa nini unafikiri Kardinali anafikiri kanisa lake limesemwa wakati Kikwete kashasema si kanisa lake? Tatizo hapa ni ukweli kwamba Kikwete hawi muwazi, na kama kiongozi wa nchi kutokuwa muwazi ni noma. Sasa kasema si makanisa makubwa, ni madogo, madogo yako mangapi? Kashawapaka matope viongozi wa makanisa madogo wote tu.



Sasa Kardinali akimpaka rais kwa kuachia viongozi wa dini kufanya hivyo na kupiga soga badala ya kuchukua hatua utamshangaa?



Sasa kwa nini rais asihimize mkondo wa sheria ufuatwe na kuja kutoa taarifa kwa wananchi kuna viongozi hawa na hawa wa dini walijihusisha katika biashara haramu, serikali yangu haitaki mchezo? Kikwete ni joker, hilo ndilo tatizo, kasema anawajua wala rushwa bandarini, sasa kafanya nini mpaka leo?

Kwa nini hajasema kuna mabalozi wanatumia vyeo vyao kuuza silaha kwa waasi wa Congo? Kwa nini kamtoa yule balozi wa Tanzania Burundi kimyakimya? Si anajua kusema sana yeye?

Unafiki tu!


Kama hawawezi elewa maana hawastahili kuambiwa maana, wanadhani sisi hapa tunatetea dini au viongozi wa dini, hawajui kuwa tunahimiza uwajibakaji thabiti katika kauli na matendo......hatuhitaji mtu joker, kama ulivyosema kuhusu yule balozi, pia yeye akiwateua hatujawahi msikia akitoa kauli ya kuwatahadharisha mabalozi wengine kuhusiana na vitendo vile.

Kama Pengo angesema mbona kuna mabalozi wamefanya A, B na C hapo tungesema Pengo au Viongozi wa dini hawataki kuguswa, lakini walichofanya viongozi wa dini ni kumpa ruhusa ya kutaja hao watuhumiwa, nashangaa watetezi wa rais wanavyojaribu kutumia references na hoja mbali mbali kupoteza maana....any way hii ndiyo tanzania yetu, inabidi tujikubali na kujipenda tulivyo kwani ujinga ndiyo maumbile yetu
 
ʞontɹact Sniper;2367109 said:
Mzee Mwanakijiji sasa, utakuwa umeanza kuzeeka vya kutosha sasa......hivi ni Pengo aliyeanza kuongea, au sijakuelewa na hii post yako ulikuwa unamjibu mtu mwingine?
Hivi inawezekana kweli shutuma atoe JK halafu aanze kumnyooshea kidole Mkapa, bila shaka wewe huyu huyu ungekuwa wa kwanza kusema Pengo anamuogopa JK kwa kuwa kwa sasa yupo madarakani na kuzidi kushangaa inakuwaje shutume atoe JK, halafu yeye amshambulie Mkapa, kweli pamoja na unawezoweza kuita hekima katika michango napata jibu kuwa watanzania tupo kwa ajiri ya malumbano na kulalamika tu

Hata mimi hapa Mwanakijiji amenishangaza sana This is the least we expect from him on a serious issue like this one! Pengo anachosema ni very objective, kama unajua uoza why not speak! Wewe ndio Rais, unawajua wauza unga, sasa unaficha nini? Call a spade a spade, not a big spoon!
 
Hivi ikithibitika kuwa tuhuma zilizotolewa sio za kweli JK atafanya nini? ataomba radhi?
 
Hivi ikithibitika kuwa tuhuma zilizotolewa sio za kweli JK atafanya nini? ataomba radhi?
Aombe radhi kwani yeye amebishana Rais kuhusu hizo shutuma?

na kama kuna kuomba radhi hapo wa kuombwa radhi ni jamii, Rais yeye kwa upande wake atahitajika kujifunza kuwa muwazi badala ya kutoa kauli za mafumbo zinazogonganisha watu na kutishia kusambaratisha jamii.

Kwa kufanya hivyo ndiyo tutapata maana ya taifa na kuimarika
 
Hata mimi hapa Mwanakijiji amenishangaza sana This is the least we expect from him on a serious issue like this one! Pengo anachosema ni very objective, kama unajua uoza why not speak! Wewe ndio Rais, unawajua wauza unga, sasa unaficha nini? Call a spade a spade, not a big spoon!

Kwa mtu anayesema pengo ammyooshee kidole mkapa nadhani atakuwa hamtendei haki pengo! Mbona pengo na maaskofu wengine wako mstari wa mbele kuhimiza uwajibikaji serikalini, matumizi ya rasirimali zetu kwa manufaa ya wtz wote n.k..! Halafu hata kauli ya pinda aliyeitoa bungeni na yenyewe haina busara...maana imewajumlisha viongozi wote wa makanisa madogomadogo bila kuwa specific!
 
Kama unamwalika mtu kwenye sherehe ambaye unajua kwamba anawezakusema lolote pasipo kuliweka wazi au kufikiria athari yake, kisha unaanza kulalama tumwone mjinga ni yupi????

Nadhani wakati umefika wa viongozi wa dini kumpatia Mungu heshima kuliko kuhitaji sana uwepo wa viongozi wa kiserikali ambao mwisho wa siku wanasahau lililowapeleka katika shughuli walizo alikwa na kuishia kuchafua hali ya hewa ya makusudio ya sherehe husika!

Viongozi wa kanisa wajikague na kujua kama wanamtaka Mungu kuwepo katika sherehe husika au viongozi maarufu ambao hata umuhimu wa matukio ya kanisa au dhima ya shughuli za kanisa, kama kusimikwa kwa maaskofu..
 
Back
Top Bottom