Mkuu wangu kama kweli ungekuwa huna udini usingeandika hivi hata iwe kwa kutolea mfano tu, kwa kufanya hivi unachochea moto zaidi badala ya wewe pia kujadili mada yenyewe..Sijawa huko na sitaruhusu kujirahisisha kujadili udini, hapa nilikuwa najaribu tu kumwambia tunaja mengi na historia kuliko wanavyofahamu ila hatuko tayari kwani tukifanya hivyo wenye moyo mchache wa kujadili ukweli watakimbilia majambia.
Ndio maana nasisitiza tujadili hoja iliyoletwa hapa na kama hoja ya dini aanzishe anayetaka thread yake na kama mod ataruhusu ndipo tuijadili. Kwa hapa tunajadili Cardinal pengo anapoonya maovu na udhaifu wa serikali kwa manufaa ya watanzania wote.
Tunaoonja makali ya maisha ni sote, na tukiendekeza ushabiki kwa misingi ambayo wengine wanaendekeza hapa tutaishia umaskini wa kutupwa na kuona tatizo ni yule unayemwona mbele yako badala ya kuelewa ukweli wa nini viongozi wetu wafunguke mioyo na akili zao kuona, kusikia na kufanya tunayowaambia, maana kujitetea kwa viongozi na kutafuta visingizio vya hapa na pale si hoja ya kuondoa matatizo yaliyopo.
Katika Udini huo huo tunaoupiga vita umemjibu huyo jamaa hivi:-
Kaanzishe thread ya kujadili udini, hapa tunajadili thread ya Kikwete mbele ya maaskofu katoliko wote Tanzania kwamba viongozi wa dini ni wauza unga. Kaambiwa ataje majina ya wauza unga hadi leo kimya. Hii ya kujadili udini si mahali pake maana nikikuambia Mtume muhamad alifukuwa dini ya ukristo na kwenda kinyume cha maadili ndipo akaenda kuanzisha uislamu utaenda kutafuta jambia kunikata kichwa, Hahahaha wajameni tujadili yanayojilia tusiingize udini hapa si mahali pake.