Pengine serikali ya CCM imechanganyikiwa

Pengine serikali ya CCM imechanganyikiwa

ile miaka mia moja ya manguli wa sheria za mkataba wa dipi weldi imepotelea Mbeya au USA?
JamiiForums-1147096054.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii inaitwa political surprising, wakati mikataba ya bandari inasainiwa wakati ilileta mkwaruro wa kutojulikana ukomo wake, tayari ukomo umewekwa. Ili kuchanganya watu wagawanyike kuchambua mambo, uteuzi wa makonda aliyezua gumzo awamu ile ukachomekewa paaaa kimkakati. Haya wale dp waende kule na wa makonda waje huku, that is devide and rule. Jambo moja hufunika jingine muda upite maisha yaendelee
 
Mkuu alihitajika mtu kama Makonda kufufua chama maana Chama kililoose popularity na wanachama walipungua kwa 30%
So lazma warudishe watu kama makonda kwenye system
Magufuli alipoingia tuliambiwa kabla yake watu walikuwa wanaogopa kuvaa nguo za CCM ila ameifufua. Haya na sasa tunaambiwa tena Makonda ndiyo anakuja kuifufua. Hizi ni dalili za kuwa CCM iko kwenye siku zake za mwisho. Najua kwa ufinyu wa akili zako unaweza usione hili lakini muda utaamua.
 
Ila yupo vizuri katika amsha amsha kupitia hilo domo lake.

Daudi yupo vizuri ktk kutumia 🔫 tu na polccm guard, mambo ya amsha amsha kwa domo lake hawezi, hivyo uenezi hawezi domo zege huyo.
Anaamsha amsha wajinga wajinga ambao wako wengi sana kwenye mitaa ya Tanzania. Ule ujinga wa kufanya mambo bila kutumia akili huyu ni bingwa. Leo atashika suala la wajane, kesho atashika suala la vibaka, keshokutwa atashika suala la tezi dume... yaani ujinga ambao hauna matokeo yoyote bali unazidisha tatizo na kutumia muda na fedha bila matokeo. Bahati mbaya ni kuwa huwezi kuwadanganya watu muda wote.. kuna siku itafika...
 
Magufuli alipoingia tuliambiwa kabla yake watu walikuwa wanaogopa kuvaa nguo za CCM ila ameifufua. Haya na sasa tunaambiwa tena Makonda ndiyo anakuja kuifufua. Hizi ni dalili za kuwa CCM iko kwenye siku zake za mwisho. Najua kwa ufinyu wa akili zako unaweza usione hili lakini muda utaamua.
Ilo najua mkuu na ndo maana makonda kawekwa ili kurudisha kidgo heshima..watu wamerudisha sana kadi...Zaidi ya kadi 20k zimerudishwa...
 
Anaamsha amsha wajinga wajinga ambao wako wengi sana kwenye mitaa ya Tanzania. Ule ujinga wa kufanya mambo bila kutumia akili huyu ni bingwa. Leo atashika suala la wajane, kesho atashika suala la vibaka, keshokutwa atashika suala la tezi dume... yaani ujinga ambao hauna matokeo yoyote bali unazidisha tatizo na kutumia muda na fedha bila matokeo. Bahati mbaya ni kuwa huwezi kuwadanganya watu muda wote.. kuna siku itafika...
Hayo ndiyo malengo ya CCM, ila wananchi wajinga wanazidi kupungua so ipo siku watakosa wa kumdanganya.
 
Wazungu wanasema .. Shortcut is the longest way you were not going... Na Waswahel wanasema unaweza kuruka ndogo(haja) ukadhani umesalimika kumbe unaenda kukutana na kubwa

Na shida ya kubwa ni moja haichomi, haiumizi lakini ukiikanyaga lazima uchecheme kama aliyekanyaga mwiba ukamchoma akiwa peku ama ukiwa umevaa kiatu ama kobazi lisilo na soli imara!

Na shida ya kubwa ni moja ukishaikanyaga umeitibua uvundo wake wote
Utanuka wewe na wengine watakukwepa kutokana na harufu hiyo wasijue kutofautisha kama ni yako ama ni ya mwingine umeipitia tuu..!

Tunaaswa na wahenga tukiwa kwenye taharuki tusiwe watu wa kuchukua maamuzi ya haraka! Lakini kubwa kuliko yote kuepuka kuchukua maamuzi yanayotokana na ushauri wa kunguni na papasi
Chama kimeyakanyaga! Kinatoa uvundo mkali.. Wenye pua ambazo silika za kunusa bado zinafanya kazi wataanza kukikimbiaView attachment 2789168View attachment 2789169

Sent using Jamii Forums mobile app
MENEMENE TEKERI NA PERESI.
 
Watajua hawajui

Sent using Jamii Forums mobile app
Hili sula la bandari mimi naona madhara yatasambaa na kusababisha mambo mengine mabaya zaidi. 1. Bandari itakuwa uchochoro wa kupitisha raslimali zetu kwa wingi sana 2. Waarabu hawatataka kabisa rais yoyote aongozi Tanzania bali watahakikisha rais fisadi wanayemtaka wao ataingia, hivyo watahakikishia suala la katiba linafanyika kulingana na matakwa yao.
 
Ilo najua mkuu na ndo maana makonda kawekwa ili kurudisha kidgo heshima..watu wamerudisha sana kadi...Zaidi ya kadi 20k zimerudishwa...
Sasa wewe kweli unaona Makonda ndiye kiongozi wa kurudisha heshima? Makonda anakwenda kuiporomosha zaidi. BTW kadi za vyama hazina uhusiano wowote na kuridhika kwa wananchi. Hata uwape kadi wananchi wote wa Tanzania bila kuboresha maisha ni bure.
 
Back
Top Bottom