Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,638
- 697,929
Wazungu wanasema .. Shortcut is the longest way you were not going... Na Waswahel wanasema unaweza kuruka ndogo(haja) ukadhani umesalimika kumbe unaenda kukutana na kubwa
Na shida ya kubwa ni moja haichomi, haiumizi lakini ukiikanyaga lazima uchecheme kama aliyekanyaga mwiba ukamchoma akiwa peku ama ukiwa umevaa kiatu ama kobazi lisilo na soli imara!
Na shida ya kubwa ni moja ukishaikanyaga umeitibua uvundo wake wote
Utanuka wewe na wengine watakukwepa kutokana na harufu hiyo wasijue kutofautisha kama ni yako ama ni ya mwingine umeipitia tuu..!
Tunaaswa na wahenga tukiwa kwenye taharuki tusiwe watu wa kuchukua maamuzi ya haraka! Lakini kubwa kuliko yote kuepuka kuchukua maamuzi yanayotokana na ushauri wa kunguni na papasi
Chama kimeyakanyaga! Kinatoa uvundo mkali.. Wenye pua ambazo silika za kunusa bado zinafanya kazi wataanza kukikimbia
Sent using Jamii Forums mobile app
Na shida ya kubwa ni moja haichomi, haiumizi lakini ukiikanyaga lazima uchecheme kama aliyekanyaga mwiba ukamchoma akiwa peku ama ukiwa umevaa kiatu ama kobazi lisilo na soli imara!
Na shida ya kubwa ni moja ukishaikanyaga umeitibua uvundo wake wote
Utanuka wewe na wengine watakukwepa kutokana na harufu hiyo wasijue kutofautisha kama ni yako ama ni ya mwingine umeipitia tuu..!
Tunaaswa na wahenga tukiwa kwenye taharuki tusiwe watu wa kuchukua maamuzi ya haraka! Lakini kubwa kuliko yote kuepuka kuchukua maamuzi yanayotokana na ushauri wa kunguni na papasi
Chama kimeyakanyaga! Kinatoa uvundo mkali.. Wenye pua ambazo silika za kunusa bado zinafanya kazi wataanza kukikimbia
Sent using Jamii Forums mobile app