Pendekezo: SLAA amrithi SUMARI Arumeru!

Pendekezo: SLAA amrithi SUMARI Arumeru!

msisahau kuwa cuf nao walikua na mtaji igunga kilichowapata hawatakaa waahau na nyie cdm lazima mtambue ya kwamba uchaguzi huu wa arumeru unaweza kuwaletea matokeo kama ya cuf Igunga
Hiyo ilikuwa ni CUF na hii ni CHADEMA, halitupati lolote hatuogopi vitisho CDM songa mbele tuu!!!!!

 
Kauli ya Dr Slaa iheshimiwe kazi yake kubwa ni kuwapika vijana hivyo mgombea 2010 aendelee na mikakati ya kuchukua jimbo
 
Suala sio chadema mimi kwangu taifa kwanza vyama baadae ndio mana nilikua wa kwanza kupendekeza slaa arudi bungeni kuimarisha makali ya bunge ili serikali isilale usingizi but haina maana naipenda chadema lakini namuhitaji slaa bungeni kwa maslahi ya taifa tuelewane hapa..
Mkuu wacha ujanja kwa sababu kama hupendi CHEDEMA sasa una nia gani, ungependa taifa lako usingeshabikia maghamba ambao ni wezi wanafilisi taifa!!!!

 
sALAM sana wana JF,Hakika naamini maoni yatolewayo hapa yanapitiwa na waratibu wa CHADEMA.Kwa kweli CHADEMA inakubalika sana na hili halina ubishi.Kimsingi Dr akimua kugombea Jimbo la Arumeru atapata ushindani mkubwa sana na pia matokeo au mchakato mzima unaweza ukapoteza wasifu wake kutokana na mazingira pamoja na watu wenye hulka tofauti.Wengi watamthamini mzawa zaidi kuliko atakavyoweza kufanya Dr. Mie pia ningependa agombee na aingie bungeni ili atoe changamoto kama awali, ila kwa heshima aliyoshajijengea ni vyema akawashukuru wote wanaomsihi agombee na kuwashawishi juu ya uwezo wa atakayeteuliwa na chama kuipeperusha bendera kama CHADEMA. Wote tunampenda Dr ila kwa Meru awachie Wameru ili kuepuka msigano na kumarisha chama kwa kina zaidi.
 
Dr. Slaa vp mbona kimya wakati kuna jimbo tupu la Arumeru? Si unaweza kugombea? Nenda kachukue jimbo uingie mjengoni ukawatetemeshe kama kawaida yako. Sisi tupo nyuma yako mpambanaji wetu.
 
Suala sio chadema mimi kwangu taifa kwanza vyama baadae ndio mana nilikua wa kwanza kupendekeza slaa arudi bungeni kuimarisha makali ya bunge ili serikali isilale usingizi but haina maana naipenda chadema lakini namuhitaji slaa bungeni kwa maslahi ya taifa tuelewane hapa..

Ushauri mzuri mkuu na ni nzuri kuona kua una nia njema na taifa lako,lakini kwa Dr kurudi bungeni hapana,hata huku alipo anaiamsha serikali na watanzania pia!nassari nae ni mpambanaji mzuri na ataleta chachu bungeni,kama nia yako ni ya dhati,basi naomba umuunge mkono nassari na kumuacha dr akiendelea na majukumu yake!
 
mimi naona Dr aendelee kukifanyia kazi chama kama katibu mkuu, na awaelimishe watu wa Arumeru kuwa kama wanampenda basi wampe kura mgombea atakaye chaguliwa na Chadema, ila aongeze usimamizi juu ya wabunge wake, maana dr. hawezi kuwa mbunge kwenye kila jimbo maana ni karibu majimbo yote wanamuhitaji sasa atakuwa mbunge wa majimbo mangapi?
 
Wana chadema,

Kuanzia waliomtuma na Kim Kardash mwenyewe wanajua fika kazi anayoifanya Dr. Slaa kwa sasa ya kuratibu mipango yote ya kuimarisha chama kwa ajili ya ushindi wa 2015 hivyo kwa vichwa vyao vya nazi wanadhani CDM na Dr. Slaa watahadaika. Joshua anarudi tena na jimbo linanyakuliwa na nguvu ya umma.

Dr. ameshavuka hatua ya uwakilishi wa jimbo na sasa tunajiandaa kumpeleka magogoni akiwa Rais.
 
Siungi mkono hata kidogo wazo la Dr Slaa kugembea ubunge Arumeru Mashariki. Kama taifa ambalo liko kwenye njia panda baada ya miaka 50 ya majaribio tunahitaji mtu wa aina ya Dr Slaa awe na muda wa kujenga fikra mbadala nje ya bunge la Anna Makinda!
Mfumo wa sasa naona ni mzuri, Lissu bunge la Makinda na Dr Slaa kwenye bunge la wananchi - uraiani. Kwa kifupi naamini faida za Dr Slaa kuwa nje ya bunge (kwa sasa) ni kubwa kuliko kuwa ndani ya bunge huko Dodoma. Hata hivyo kutokana na siasa za ki-ukoo huko Arumeru itakuwa kazi ngumu sana kwa Dr Slaa.
 
Nakubaliana na nyie wakuu wote,
Dr. yuko juu ya kiti zaidi ya kiti cha ubunge,
ingependeza awaachie vijana yeye aendelee
kukitangaza chama nchini hapa na nje ya nchi.
CHAGUA CHADEMA CHAGUA MAENDELEO.
 
hawa wametumwa dr keshasema hagombei na hatoki huko sasa wao wanalazimisha nini? nia yao wanataka agombee ili wakamuibie kura na kujifanya hakubaliki ili kummaliza kisisasa hili tunalijua sana hawa ccm sio watu

Mbowe, kasema ruksa Dk Slaa kugombea Arumeru!
 
Hakuna kitu kama hicho bana..Mzee wangu .....Rais wangu acha kwenda arumeru kugombea nenda kapige kampeni tu.
 
na mimi nashauri tusitumie nyundo kuuwa inzi.

dr si size yake arumeru.
 
Ushauri mzuri mkuu na ni nzuri kuona kua una nia njema na taifa lako,lakini kwa Dr kurudi bungeni hapana,hata huku alipo anaiamsha serikali na watanzania pia!nassari nae ni mpambanaji mzuri na ataleta chachu bungeni,kama nia yako ni ya dhati,basi naomba umuunge mkono nassari na kumuacha dr akiendelea na majukumu yake!


problem ndugu yangu sio kuangalia upambanaji hapa tunaangalia pia nafasi ya dr slaa kama atagombea ni rahisi kuupata ushinde kwa kuwa kutokana an nafasi itabidi ifanyike kampeni ya kitaifa kumuwezesha kushinda,lengo ni kiti kile kiende upinzani,hakuna mgombea anaweza kuishinda ccm pale zaidi ya slaa,kama unabisha tukutane hapa baada ya matokeo ya uchaguzi ambao atasimamishwa huyo Nassari.

Nimeshauri chadema iachane na ndoto za urais kwanza,ijiimarishe bungeni,urais ni kiti kidogo sana,unaweza kuwa rais bila serikali,sasa chadema inaweza kuunda serikali lakini ikaicha ccm na urais bila serikali,amkeni wana chadema.
 
Hakuna kitu kama hicho bana..Mzee wangu .....Rais wangu acha kwenda arumeru kugombea nenda kapige kampeni tu.

Roho yangu itatulia siku nikimuona DR SLAA anaapishwa pale bungeni ambapowaoshwa vinywa sijui sura zenu hizi mtaziweka wapi..watu wa ajabu sana nyie mnapinga kiongozi wenu asiingie bungeni kuibana serikali?
 
Heshima kwenu wakuu..!

Kuelekea uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru Mashariki. Vyama mbalimbali ndo vishaanza mchakato wa kupata wagombea watakao peperusha bendera za vyama vyao.Binafsi naomba nijikite katika Chama cha Demokrasia na Maendeleo.

Mchakato ndani ya Chadema wa kumpata Mgombea wa Jimbo hilo unaendelea na Kupitia Vyombo vya habari na Mitandao ya Kijamii tumepata kusikia kuwa Watu mbalimbali wanashauri Dr Slaa agombee kit hicho kupitia Chadema.Binafsi sikubaliana na Mawazo ya watu hawa kutokana na Sababu zifuatazo..,

1. Dr Slaa ni Kiongozi Makini na Ameweza Kutikisa nchi katika Uchaguzi uliopita na hili kila mtu analifahamu na amekuwa mwiba mkari ndani ya Serikali.Hivyo kitendo cha kugombea katika jimbo la Arumeru Mashariki Itaoneka na itakuwa kama Viongozi wa CDM ni wenye uchu wa Madaraka.,

Pia Dr ameonyesha namudu hasa nafasi y ukatibu Mkuu akiwa nje ya Bunge..,kwani utaratibu wa kuikuza Chama miongoni mwa jamii umekuwa mkubwa na haya yote ni sababu ya mipango makini ya Dr Slaa.

2.Kijana Joshua Nasari yupo makini sana na ni Kamanda mpambanaji kiukweli..,hivyo itakuwa ni kumnyima nafasi yake kama kijana ya kuonyesha uwezo wake ndani ya Bunge.

3.Chadema imeonyesha uwezo mkubwa kupitia wabunge vijana ndani ya ukumbi wa Bunge na kuichachafya vilivyo Serikari na Wabunge wake wa CCM..,hivyo ni vizuri na si vibaya kwa Joshua Kuungana na VIjana wenzake kundeleza Mashambulizi dhidio ya CCM na Serikali yao.

Nimeandika machache kutokana na ufinyu wa Muda.,Nimalizie kwa Kusema ipohaja kwa Viongozi wa Chadema kujitokeza hadharani na kutoa msimamo wa Chama juu ya hili.

Naomba Kuwasilisha na Michango yenu ni muhimu katika hili..
 
Kama kuna wilaya ambayo UKABILA na UKOO ni kigezo namba moja katika kuchagua na kuchaguliwa ni hii ya ARUMERU. Msimdanganye Dr Slaa kwamba umaarufu wake unatosha kumpatia Ubunge jimbo hili. Halafu, mbona tayari anafanya kazi nzuri tu ya Ukatibu Mkuu wa CHADEMA jukwaa pana zaidi kuliko Ubunge wa Jimbo?
Tuliambiwa humu kuwa analipwa vizuri tu na chama chake kama Eto'o kule Urusi au Anelka kule China. Siasa za Arumeru ziacheni hivohivo kwani hata ULUTHERI ni kigezo muhimu sana.
 
Roho yangu itatulia siku nikimuona DR SLAA anaapishwa pale bungeni ambapowaoshwa vinywa sijui sura zenu hizi mtaziweka wapi..watu wa ajabu sana nyie mnapinga kiongozi wenu asiingie bungeni kuibana serikali?
Usitudanganye KK. Ipo siku mtamwambia Dr Slaa akagombee majimbo ya Pemba!
 
Back
Top Bottom