Pendekezo: SLAA amrithi SUMARI Arumeru!

Pendekezo: SLAA amrithi SUMARI Arumeru!

Chama cha siasa kisipokuwa na ndoto ya URAIS hakipaswi kuendelea kuwepo. Hakifai. Wakigeuze kiwe NGO kama TAMWA ya Mama Nkya.
Dr Slaa tayari ana kazi kubwa na nzuri tu. Arumeru haijapungukiwa vichwa vya UBUNGE. Ubunge hauhitaji watu wa kukodi. Uliona Mrema hakumaliza kipindi chake cha Ubunge pale Temeke. Hakujali waliompigia kura. Aliondoka kihuni tu. Hawezi kufanya hivo kwao Vunjo.

kwa hiyo unataka kusema sugu nae ataondoka kihuni mbeya mjini kama mrema temeke sio?

Kuhusu urais usikunyime usingizi mzee,unaweza kuwa rais lakini bila serikali sasa sijui huo urais utakuwa na faida gani?ndio mana tunawaambie mfunguke mpanie kuichukua serikali sio urais,urais ni kitu kidogo sana,ambacho kitakujachenyewe mkiweza kuunda serikali.
 
Gazeti Tanzania Daima la jana (16/02/12) katika habari yake 'Dk. Slaa apewa mtihani mzito' likielezea mitazamo ya makundi mbalimbali lilimalizia hivi; 'Hata hivyo, Dk. Slaa alipotafutwa na gazeti hili awezeuzungumzia juu ya hatua hiyo, alisema kwa kifupi: "Siwezi kulizungumzia jambo hilo, maana nilikwishasema muda mrefu kuwa sitaki tena ubunge na isitoshe mimi si mwenyeji wa Arumeru" Alisisitiza kuwa kwa sasa ana kazi moja ya kukijenga chama chake cha Chadema ili kiweze kushika mizizi kwenye maeneo yote nchini.'

My take: wanaoendelea kutaka agombee hawamtakii Dk. Slaa na CDM mema.
 
kwa hiyo unataka kusema sugu nae ataondoka kihuni mbeya mjini kama mrema temeke sio?

Kuhusu urais usikunyime usingizi mzee,unaweza kuwa rais lakini bila serikali sasa sijui huo urais utakuwa na faida gani?ndio mana tunawaambie mfunguke mpanie kuichukua serikali sio urais,urais ni kitu kidogo sana,ambacho kitakujachenyewe mkiweza kuunda serikali.
KK,
Mr Sugu ni mwenyeji wa Mbeya! Lile jina Mbilinyi lisikufanye umpeleke Songea. Hauwezi kuwa Rais bila serikali. Unautenganishaje Urais na serikali? Uelewa wako wa mambo haya unatosha kweli! Arumeru ina vichwa vingi vizuri kuliko huyo Dr Slaa.
 
presidential material akagombee ubunge kisa kashndwa uraisi. Mbn wanataka kumuaibisha rais wetu Umesikia huyo amekuwa mrema? Pili ataonekana ana tamaa baba bak huko huko endelea kuwanyoosha.
 
Mimi napendekeza hii nafasi aliyonayo Dr. Slaa na hadhi aliyonayo,ukijumlisha na majukumu aliyonayo naonelea yeye akamsimamie kijana tuchukuwe jimbo hadhi na mamlaka aliyonayo Dr. ni makubwa kuliko huu ubunge, mwanche aandae chama kwa ajili ya kuendelezwa na vijana siku za baadaye wao wakiwa wastaafu nao waje kuwa nembo njema ya chama siku za usoni. Dr. nakutakia uimarishwaji mwema wa chama.Peoplesssssssssssss Power!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
KIM KARDASH

  • ulisha sikia katibu mkuu wa CCM ni mbunge - CDM ni chama tawala cha upinzani na katibu mkuu anazo kazi za kufanya
  • kazi ukiianzisha si rahisi kuimalizia mwenywe wapo wanao kuunga mkono wataimalizia kwa techniques mpya kama ikina Tundu Lissu, Godbless Lemma, Sugu etal
  • TFFA ina rais . Rais ni kiongozi wa watu na huwezi kuwazuia wanao mwita rais kumbuka yeye hajiiti kama Rais sijui kinacho kuuma nini
  • Basi huo msamiati usengekuwepo kama kura haziibiwi
  • hili ndilo lililo mwangusha Mpesya aliroka kuwa vijana wengi ni mashabiki tu na hawapigi kura na kwambia safari hii wapiga watakuwa hawa unao wadharau maadamu daftari liboreshwe utaona

SIIUNGI MKONO HOJA DR SLAA ASIGOMBEE UBUNGE

Nashukuru kwa msaada wako Duble Cris, nilikuwa najiuliza jinsi ya kumuelewesha hu Kim Kadash. Hoja yake ni dhaifu sana sana tu, mie nahofia anatumikia upande flani hivi wa kushoto. Tunamuomba sana dk Slaa asigombee ubunge ubunge Arumeru Mashariki sababu bado ana nafasi yake yake ndani ya mioyo yetu. YEYE NI RAIS AJAYE.
 
KK,
Mr Sugu ni mwenyeji wa Mbeya! Lile jina Mbilinyi lisikufanye umpeleke Songea. Hauwezi kuwa Rais bila serikali. Unautenganishaje Urais na serikali? Uelewa wako wa mambo haya unatosha kweli! Arumeru ina vichwa vingi vizuri kuliko huyo Dr Slaa.

Bwana mzee mbeya hawakuwa na hiyo huko nyuma,marehemu Bruno mpangala angekua hai ningekutuma ukamuulize,yeye kiasili alikua anatoka mkoa mmoja na kabila moja na sugu lakini alikua mwenyeji wa mbeya pia kama sugu,lilipokuja suala la ubunge akachukua fomu ya kugombea ubunge pale mbeya mjini(kumbuka alikua katibu mkuu wa ottu taifa)hivyo alikua ni mtu mwenye ushawishi lakini wanyakyusa wakasema hapana hata ccm wenzake hawakumpigia kura,wote wakampigia mnyakyusa mwenzao bwana Mwaisyeje aliesimama kwa tikiti ya NCCR mageuzi ya mrema,hiyo ndio mbeya nilioifahamu,lakini watu wanabadilika,alipokuja sugu kamshinda mzawa japo hakua mnyakyusa,alikua ni msafwa ambao kiasili kabisa ndio wenye mbeya yao,tena kukuonyesha kwamba nakijua zaidi ninachosema sugu alimshinda mwalimu wake wa literature pale mbeya secondary bwana Mpesya!

Narudi kwenye mada kama sugu kaweza kuivunja mizizi mizito ya ukabila pale mbeya ambapo hapakuwahi kutokea mbunge asie mzawa wa pale itakua slaa mwenye muscles za kutosha,slaa ni heavy weight politician miongoni mwa wagombea wote watakaosimamishwa arumeru,labda lowassa agombee ndio wanaweza kulingana kitu ambacho hakiwezi kutokea cuz lowassa tayari ni mbunge
 
Nashukuru kwa msaada wako Duble Cris, nilikuwa najiuliza jinsi ya kumuelewesha hu Kim Kadash. Hoja yake ni dhaifu sana sana tu, mie nahofia anatumikia upande flani hivi wa kushoto. Tunamuomba sana dk Slaa asigombee ubunge ubunge Arumeru Mashariki sababu bado ana nafasi yake yake ndani ya mioyo yetu. YEYE NI RAIS AJAYE.

kwa hiyo na mbowe nae aliezungumzia uwezekano wa slaa kugombea arumeru nae anatumika?anatumiwa na nani labda?anywayz bwana kuna siku mtanikumbuka lakini baada ya uchaguzi wa arumeru ambapo mbunge mpya ataapishwa.
 
Bwana mzee mbeya hawakuwa na hiyo huko nyuma,marehemu Bruno mpangala angekua hai ningekutuma ukamuulize,yeye kiasili alikua anatoka mkoa mmoja na kabila moja na sugu lakini alikua mwenyeji wa mbeya pia kama sugu,lilipokuja suala la ubunge akachukua fomu ya kugombea ubunge pale mbeya mjini(kumbuka alikua katibu mkuu wa ottu taifa)hivyo alikua ni mtu mwenye ushawishi lakini wanyakyusa wakasema hapana hata ccm wenzake hawakumpigia kura,wote wakampigia mnyakyusa mwenzao bwana Mwaisyeje aliesimama kwa tikiti ya NCCR mageuzi ya mrema,hiyo ndio mbeya nilioifahamu,lakini watu wanabadilika,alipokuja sugu kamshinda mzawa japo hakua mnyakyusa,alikua ni msafwa ambao kiasili kabisa ndio wenye mbeya yao,tena kukuonyesha kwamba nakijua zaidi ninachosema sugu alimshinda mwalimu wake wa literature pale mbeya secondary bwana Mpesya!

Narudi kwenye mada kama sugu kaweza kuivunja mizizi mizito ya ukabila pale mbeya ambapo hapakuwahi kutokea mbunge asie mzawa wa pale itakua slaa mwenye muscles za kutosha,slaa ni heavy weight politician miongoni mwa wagombea wote watakaosimamishwa arumeru,labda lowassa agombee ndio wanaweza kulingana kitu ambacho hakiwezi kutokea cuz lowassa tayari ni mbunge
Ndio maana nikakueleza sifa mama za kuupata Ubunge majimbo mengi nchi hii ukiondoa yale ya miji mikubwa kama Dar:
-Uwe mwenyeji wa Jimbo husika. Dr Slaa hana sifa hii kule Arumeru.
-Sifa yako mwenyewe. Mr Sugu alikuwa celebrity na CHADEMA ya Dr Slaa 2010 iliwakamata Wamachinga wengi wa mijini.
-DINI nayo inashika kasi siku hizi.
KK, Ubunge wa Dr Slaa kule AruMeru utaisaidia nini CHADEMA na NCHI yetu? Nyongeza ya RUZUKU?
 
siungi nkono hoja.Nassari apewe haki yake.Slaa ana kazi kubwa ya kuimarisha chadema nchi nzima akijiandaa kukamata dola 2015

kaka hiyo ni kweli kuna watu hawaitakii mema chadema wanataka wamchakachue thern 2015 waseme kama alishindwa ubunge Arumeru urais ataweza?

Daktari nakuomba usithubutu hao hawakutakii mema
 
ndio maana nikakueleza sifa mama za kuupata ubunge majimbo mengi nchi hii ukiondoa yale ya miji mikubwa kama dar:
-uwe mwenyeji wa jimbo husika. Dr slaa hana sifa hii kule arumeru.
-sifa yako mwenyewe. Mr sugu alikuwa celebrity na chadema ya dr slaa 2010 iliwakamata wamachinga wengi wa mijini.
-dini nayo inashika kasi siku hizi.
Kk, ubunge wa dr slaa kule arumeru utaisaidia nini chadema na nchi yetu? Nyongeza ya ruzuku?

kwa hiyo huoni umuhimu wa upinzani kuongeza viti bungeni sio?basi kazi ipo.sasa ndio nimekuelewa kwanini hunielewi ninaposema muhimu ni serikali sio urais.

Ok kwa kuwa mimi ni mwalimu kitaaluma ntakuingiza darasani kwanini nasema serikali ndio muhimu kuhusu urais,hapa ni suala la mahesabu tu,unajua kwamba chama chenye wabunge wengi ndio kinaunda serikali?pengine tuanzie hapo kwanza ndio tutaenda sawa..unalifahamu hilo?
 
Mi naomba nipingane na wewe. Nimshauri Dr. afokas kwenye mbio za urais na harakati nyingine za Chama. Kugombea jimbo hilo ataonesha ana uchu wa madaraka coz there others who can stand for that post. He better stays behind
 
kwa hiyo huoni umuhimu wa upinzani kuongeza viti bungeni sio?basi kazi ipo.sasa ndio nimekuelewa kwanini hunielewi ninaposema muhimu ni serikali sio urais.

Ok kwa kuwa mimi ni mwalimu kitaaluma ntakuingiza darasani kwanini nasema serikali ndio muhimu kuhusu urais,hapa ni suala la mahesabu tu,unajua kwamba chama chenye wabunge wengi ndio kinaunda serikali?pengine tuanzie hapo kwanza ndio tutaenda sawa..unalifahamu hilo?
Najua Mwalimu KK lakini sio kwa TANZANIA. Katiba yetu ya sasa haisemi hivo! Ila Rais atalazimika kumteua Waziri Mkuu kutoka chama chenye Wabunge wengi. Hawa wawili kwa kushauriana wataunda serikali.
 
Mi naomba nipingane na wewe. Nimshauri Dr. afokas kwenye mbio za urais na harakati nyingine za Chama. Kugombea jimbo hilo ataonesha ana uchu wa madaraka coz there others who can stand for that post. He better stays behind
kwahiyo urais hakuna vichwa huko chadema mwenye akili ya kuwa rais ni yeye tu?
 
Najua Mwalimu KK lakini sio kwa TANZANIA. Katiba yetu ya sasa haisemi hivo! Ila Rais atalazimika kumteua Waziri Mkuu kutoka chama chenye Wabunge wengi. Hawa wawili kwa kushauriana wataunda serikali.

Umesema vizuri sana,kwamba rais atachagua waziri mkuu toka chama chenye wabunge wengi,katiba haisemi rais atachagua waziri mkuu toka kwenye chake bali kile chenye wabunge wengi,wanaposema waziri mkuu ndio serikali yenyewe mzee,ndio mana waziri akijiuzulu kunakuwa hakuna serikali..na waziri mkuu iliawe waziri mkuu ni lazima athibitishwe na bunge,sasa kama chadema au chama chochote kitakua na wabunge wengi ni wazi kwamba kitamthibitisha waziri mkuu kinaemtaka jina likija bungeni,someni kwanza kabla ya kukurupuka,sasa nashangaa kila mtu huko chadema anawaza urais tu,mnaweza kuupata urais lakini msiunde serikali mkawa na rais kivuli tu,ndio mana tunawaambia muachane na ndoto za urais mjikite kwenye ubunge lengo likiwa ni kuunda serikali,waacheni ccm wabaki na urais nyie muwe na serikali,amkeni nyie watu!
 
Mkuu WildCard,

Nakubalina na hoja ya 100%.Dr W Slaa asitie pua Arumeru Mashariki,Ukatoliki wake,UIraq wake dhidi ya Umeru na Ulutheri utamweka pabaya.Tuache kujidanganya Tanzania ukabila upo tusifananishe Dar,Arusha,Mwanza na Mbeya.


Majimbo ya Dar ni "No man's land", kama hicho ni kiingereza sahihi. ARUMERU ni ngazi nyingine kabisa. Hata wilaya na majimbo yenyewe unaona majina yake. Tusifichane bwana. Nchi hii Ubunge na Udiwani vigezo hivi ni muhimu sana ukiondoa majimbo ya miji mikubwa ya Dar, Mwanza na Arusha. Narudia, vigezo vizito vya Ubunge wa Arumeru Mashariki ni:
-Uwe Mmeru wa koo kama Kaaya, Ndosi, Pallangyo...
-Uwe Mlutheri. Ukatoliki kama wa Dr Slaa ni kikwazo tosha.
-Lowasa anakufahamu?
Acheni Dr Slaa aendelee na kazi yake ya kukiimarisha chama chake. Hana wabunge waasi kama alookuwa nao Mrema mwaka 1995 kule NCCR-M.
 
Kumekuwa na shinikizo lenye uzito wa kilo nyingi kutoka kwa watanzania wakimtaka Dr.P.W.SLAA kuingia kwenye kinyang'anyiro cha ubunge jimboni ARUMERU.Ni ukweli usiopingika kuwa kwa mvuto wa kisiasa alionao dr.SLAA atalikomboa jimbo hilo kutoka kwenye utumwa wa CCM.Lakini kitendo cha dr SLAA kugombea ubunge binafsi nakiona kama anajishusha sana kwani ni sawa na kujidhalilisha kisiasa. Je dk SLAA atakubali kudhalilisha?,
 

Attachments

  • animated_soccer_ball01_12_t.gif
    animated_soccer_ball01_12_t.gif
    24.3 KB · Views: 159
Slaa sasa ni national figure hana haja ya kukimbilia bungeni kwa kuwa hoja yoyote anayotaka iende bungeni anaweza kuisukuma kupitia wabunge wa chama chake, yeye abaki kukiimarisha chama na kukiandaa kwa uchaguzi wa mkuu 2015. Ajikite zaidi kwenye masuala ya kitaifa hasa katiba mpya na vita dhidi ya ufisadi,. na pia atoe dira mbadala namna ya watanzania watakavoweza kujikwamua na umasikini,.yeye sio saizi ya ubunge tena he is the president to be!!
 
Upotoshaji jazz band...hivi kwani DR SLAA ndio kiongozi wa kwanza wa upinzani kujaribu bahati yake kugombea urais hapa nchini?mbona mnakuza sana mambo bila sababu za msingi?wote kina MBOWE ambao wamewahi kugombea urais ina maana mnakiri kwamba hawana hadhi kwa sasa wamefilisika kisiasa???naomba mnijibu hapa ili twende sawa otherwise acheni upotoshaji
 
Nafikiri umekwisha msikia aliyetangaza nia ya kugombea Jimbo hilo kwa tiketi ya CHADEMA.

SIDHANI kama Dr Slaa ni mroho wa madaraka kihivyo, kwa amsukume dogo kando aingie yeye. Hiyo ni tabia ya kina Mrema, A.L. et al.
 
Back
Top Bottom