Paul Makonda arejea nchini kimya kimya

Paul Makonda arejea nchini kimya kimya

ukisikia ukuda ndio huu..kwani unaposema karejea kimyakimya alivyoondoka alipiga matarumbeta?
Mleta mada yuko sahihi, wala usitoe povu. Kabla ya timbwili la vyeti vyake rafiki yako kila alichokuwa akifanya alikuwa anatupia picha mtandaoni, ikiwemo safari yake ya Marekani. Lakini alipowekwa kwenye kona kuhusiana na vyeti akaanza kupiga kimya...
 
WAGOSI WA KAYA - "Vinatia Uchungu"
--------------------------------------

(verse 1)
Msije mkaona watu wanapewa ridandasi,Eti mkafikiri walikuwa wazembe wa kazi. Hiyo ndiyo hali halisi hapa kwetu Tanzania. Kila mmoja kazini kwa nguvu zake amepania, kumtimua mwenzake abakie peke yake.
Mmesha mtimua mpeni madai yake, mnamzungusha hamjui mnampotezea muda wake, nyie mnadhani profesa Ludigo anatokea hapa town? Basi kwa taarifa yenu mwenzenu anatokea Lushotooo..

Mnamdanganya na Kiingereza chenu cha ugoko,Eti you know sijui, sometimes photocopy together, pailot standard sijui ma’ crossing check. Please Ludigo hebu come tomorrow, hiyo timiro timoro kuna siku n’tamminya mtu nimtoe uharo, hatielewani kiofisi mpaka tileteane kokolo.

Chonde chonde ndugu zangu mlio chuo kikuu, mkipata kazi msilete zarau na makuu, mtakuta vikongwe kazini tena wana wajukuu, wanaelimu ndogo bwana wanatembea kwa miguu.

Ole wako ufanye kazi pale miezi sita tu, halafu wakuone huyooo unaingizana na mark II, hawakawii kukwambia umeshaibia shirika, Bongo ukiwa na mark II watu wanaona umetajirika,utajiri gani huo fanyeni kazi acheni upumbavu.

Tinaomba Tanzania amani ijae makazini, pasipo na amani hapo ni uchawi na kutupiana majini, siikiza ndugu yangu nikuhadithie huu mkosi, Mama Josephine alituhadithia huu mkosi.

Bosi alimzimia halafu akamtongoza, yeye akakataa ndugu yangu akafukuzwa, hakuchukua raundi ridandasi lilimpata, sasa yuko Sahale huko na mwanae Josephine, wana kigenge chao wanauza bamia, nd’o hivyo tena Mungu anawasaidiaaa.

KIITIKIO

Wapo walofukuzwa kazi, wapo walo shushwa ngazi ah! vinatia uchungu ridandasi, hizi za majungu
x 3

(verse 2)
Khoo! I am very sorry, mimi nikiwa mzima maneno hayatoki mdomoni, lakini sasa nimekunywa naweka mambo hadharani, anayeniona mlevi anichukulie mlevi, anayenisikiliza hilo jambo liko wazi.

Hii inaonekana sana sehemu za kazi, This is too much utanipotezeaje kazi, kama ni kusoma mimi nimefika Makerere, tena kule kule alikosoma Nyerere.

Mimi sikuajiriwa kwa kufoji vyeti, wanaofanya hivyo ndiyo hao hao wanafiki, wanasababisha makazini hakukaliki, chai ya messenger vile vile hainyweki, waweza kunywa kumbe wamekuwekea kitu, unajua nini roho zao za kutu.

Wakiona unajenga wanasema eti mwizi, wanasababisha mpaka unafukuzwa kazi, hivi ni kwa nini mnakuwa wambea wambea?, au kwa sababu mnakosa hela ya bia.

Mimi nakunywa kutokana na biashara zangu, swezi kukaa kutegemea mshahara wangu, nashangaa kazini mnaniwekea majungu na vikwazo, nd’o maana nakunywa ili nipoze mawazo.

Khoo! sitapiki, naeleza ukweli na siyo unafiki, hata mkisema John Hoka analopoka poa tu, ujumbe wangu umefika.

KIITIKIO

(verse 3)
Ole wako wende kazini hufuati mambo yako, kila ukikaa ni unafiki kwa wenzako, ipo siku ukaambiwa lete cheti chako, utaanza hoo! bosi unajua, mimi nimesoma na degree za kuhonga honga mjini, lete cheti baba maneno mengi ya nini, kelele mtindo mmoja ka’soko la Ngamiani, sasa nd’o hapoo utapo tahayari.

Watu wenye tabia hii naomba mjihadhari, uongo mwingi, fix nyingi, kumbe vyeti hamna ,mna roho mbaya,nd’o mana kumbe maendeleo hamna, miji ofisi kibao imejaa ukabila, watu wajigawa mafungu sababu ya ukabila, Mtumeee! Allah akbar.

Kaombe kazi uone walivyo na dharau, kwanza watakuuliza je?, wajua Kingereza, kama so broken hapo utawaweza, ukiwajibu watakupeleka kwenye ukabila, huko ndugu yangu najua tu utateleza.

Zipo ridandasi za mashirika kuuzwa, lakini majungu nayo si ya kuyapuuza, fanyeni kazi jamani acheni majungu.

KIITIKIO...

NIMEWAMISI SANA HAWA WATU.
MASHAIRI YAO HADI KESHO YANASIKILIZIKA LOOOH JAAAMAAAANI.
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam mchapa kazi

Mchapa kazi na mbunifu.

Anayethubutu na asiyeogopa MTU kwa jina wala wadhifa wake

Mtetezi wa kizazi kinachopotea kwa madawa ya kulevya

Mbunifu wa ajira kwa vijana

Shujaa asiye tetereka

Mkuu wa Mkoa mwenye anayetaka mabadiliko

Mkuu wa Mkoa aliyetukanwa sana

Mkuu wa Mkoa asiyekataa tamaa

Mkuu wa mkoa atakayepiga vita mpaka mwisho madawa ya kulevya

Mkuu wa mkoa aliyetajwa sana kuliko wote toka Uhuru.

Mkuu wa mkoa wa kwanza kijana Dar

Mkuu wa mkoa asiyeangalia wala kujali unatoka chama gani anachotaka ni uwajibikaji tu.

Mkuu wa mkoa anayeaminika na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mkuu wa mkoa anayeandamwa hata na wabunge vita ya Madawa ya kulevya ktk mkoa wake

Mkuu wa Mkoa aliyeanzisha vita ya madawa ya kulevya Dar es salaam na sasa imeenea nchi mzima.

Mkuu wa mkoa aliyetoka familia masikini kabisa baba hajasoma kabisa na mama ni darasa la saba lakini amepata shahada moja na kuwatumikia wanainchi vile inavyopaswa.

Mkuu wa mkoa ambaye amesababisha baadhi ya watanzania kushikiwa akili na baadhi ya watu na hatimaye kuwafuata kila wasemalo na kuliamini.

Mpaka Leo 12 March 2017 hakuna aliyetuwekea ushahidi wa vyeti zaidi ya episode za Mch Gwajima tu.
Sielewi! Wa kuweka vyeti ni wanaomtuhumu au mtuhumiwa aweke vyeti ili awaaibishe wanaomtuhumu? Kimya kingi kina mshindo mkuu!
 
Wakuu habari za weekend nimepenyezewa habari kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambaye kwa sasa anatuhumiwa kughushi vyeti amerejea jioni ya leo akitokea Afrika ya Kusini.

Habari hizi zimethibitishwa na mpenyezaji kwani walikuwa wamepanda ndege moja kutokea huko kwa Madiba.

Dokezo zaidi linaonyesha Makonda atakuwa kwenye uzinduzi wa shughuli flani maeneo ya Kurasini!
Atuletee cheti chake tu vinginevyo safari hii ataenda hata makanisa kumi kwa siku kulia madhabauni
 
Wakuu habari za weekend nimepenyezewa habari kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambaye kwa sasa anatuhumiwa kughushi vyeti amerejea jioni ya leo akitokea Afrika ya Kusini.

Habari hizi zimethibitishwa na mpenyezaji kwani walikuwa wamepanda ndege moja kutokea huko kwa Madiba.

Dokezo zaidi linaonyesha Makonda atakuwa kwenye uzinduzi wa shughuli flani maeneo ya Kurasini!
Lekin SIZONJE toyari kwishafanza amuzi juu vake. Soon yu wili noo iti 😱 😛
 
Sielewi! Wa kuweka vyeti ni wanaomtuhumu au mtuhumiwa aweke vyeti ili awaaibishe wanaomtuhumu? Kimya kingi kina mshindo mkuu!
IMG_20170306_183652.JPG
 
Kuna watu mnawatafuta watu badala ya maisha yenu. Mbona mnahangaika sana na watu wakati yenu yamewashinda?
Mambo yepi? Kuonyesha cheti ndiyo kufuatilia mambo ya watu? Hivi kuna mtu anawaza kuajiriwa serikalini bila cheti? Acha utetezi wa kijinga hapa ni cheti tu kama alifikiri kwenda bondeni kutatufanya tumsahau hapa imekula kwake
 
Una vielelezo vya hizo tuhuma??
Mtuhumiwa hana hata ubavu wa kukanusha! Kielelezo ni ukimya wa Mtuhumiwa! Kanuni inayokubalika kimataifa ni kuwa "kuzinyamazia tuhuma ni kukubaliana nazo"
Haiwezekani utuhumiwe kiasi hicho na ukae kimya halafu utegemee watu wasiamini kuwa tuhuma ni za kweli.
Mamlaka za kufuatilia tuhuma za jinai zipo na zenyewe kwa ishu ya Daudi Bashite ziko kimya!
Ila uzuri nikuwa Mungu hatakaa kimya! Maana Mungu hurudisha madhara ya uovu juu ya kichwa cha mhusika! Vinginevyo afanye toba ya wazi maana uovu uko wazi!
 
Unafiki wa mzee Mwafwaaa tutauona sasa mdogo wake hamtumbui kwa nini
Hapo ndio nakuwa na wasiwasi na mahaba aliyonayo kwa huyu dogo. Huyu si alisema hata mkewe mumkamate mbona kwa huyu anapatwa na kigugumizi? Na hata si mwanae wa damu. Kunani??
 
Wakuu habari za weekend nimepenyezewa habari kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambaye kwa sasa anatuhumiwa kughushi vyeti amerejea jioni ya leo akitokea Afrika ya Kusini.

Habari hizi zimethibitishwa na mpenyezaji kwani walikuwa wamepanda ndege moja kutokea huko kwa Madiba.

Dokezo zaidi linaonyesha Makonda atakuwa kwenye uzinduzi wa shughuli flani maeneo ya Kurasini!
Eh! Si tuliambiwa yuko likizo ya miezi miwili!!!! Imeisha?
 
Back
Top Bottom