Kwa kweli kaka yangu ninakuaminia sana kwa kufanya uchambuzi. Hata hivyo ukimya wako kuhusu kufanya uchambuzi na utabiri wa nini itakuwa athari kisiasa kuhusu uamuzi wowote utakaohusisha kesi ya Mbowe.
Kwa mfano kwa sasa tunasubiri iwapo Mahakama itaamua Mbowe na wenzake wana kesi ya kujibu na ikafikia hadi hatua ya utetezi athari zake zitakuwa ni zipi?
Baadaye wanajitetea na mwishowe utetezi wao unakuwa hauna mashiko then wanafungwa, hapo athari za kisiasa katika nchi hii na Mbowe mwenyewe zinakuwaje kwa uamzui huo?
Au inatokea wanajitetea na Mahakama inaona hawana hatia hapo pia kisiasa Mbowe na siasa za nchi kwa ujumla inakuwaje?
Au inawezekana pia DPP akaingia "nolle" ya ghafla ghafla ghafla tu hapo athari kisiasa kwa Mbowe na nchi kwa ujumla inakuwaje?
Kwangu mimi hakuna ubishi kabisa kuwa kesi hii ni ya kisiasa! Kila MTanzania anayefuatilia siasa zetu kwa umakini analijua hilo - na utabiri wangu iwapo Mbowe na wenzake watafungwa basi ninaamini siasa za nchi hii zitakuwa zimenoga zaidi kwani kwa muda wote Mbowe atakaokuwa gerezani watu wanakuwa wakiongelea yeye tu.
Watazidi kuchambua uamuzi uliomfunga na proceedings hizi zinazoendelea na pia watazidi kuilaumu Serikali inayoongoza kwa unyanyasaji, uonevu na mtazamo hasi kwa upinzani. Serikali haitakuwa na Amani na watoa maamuzi hayo pia hawatakuwa na Amani maisha yao yote.
Watu wataondoa hofu watajihisi kuwa Mtawala akiamua kukufunga hata kama huna makosa anakufunga tu! Akifungwa Mbowe itakuwa ni chachu ya kuimarisha zaidi upinzani wa nchi hii.
Iktokea Mbowe kaachiwa katika hatua ya "nolle" kabla ya kufikia hatua ya wao kuwa na kesi ya kujibu basi Jamhuri itakuwa imepunguza aibu ambazo itaenda kupata kwani inaonesha hatua ya utetezi inaweza ikaibua mauzo mengi kwa upande wa washtaki katika kesi hii.
Kwangu mimi kwa Jamhuri ni bora wasivuke hatua ya kuwa hawa mabwana wana kesi ya kujibu kwani aibu haitakuwa kubwa sana na hata kisiasa awamu ya sita itaonekana kama yenyewe ndiyo imeamua kufikia muafaka na upinzani.
Hayo ni mawazo yangu - Je, ndugu yangu Paskali Mayala wewe unalichambuaje suala hili?
Kwa mfano kwa sasa tunasubiri iwapo Mahakama itaamua Mbowe na wenzake wana kesi ya kujibu na ikafikia hadi hatua ya utetezi athari zake zitakuwa ni zipi?
Baadaye wanajitetea na mwishowe utetezi wao unakuwa hauna mashiko then wanafungwa, hapo athari za kisiasa katika nchi hii na Mbowe mwenyewe zinakuwaje kwa uamzui huo?
Au inatokea wanajitetea na Mahakama inaona hawana hatia hapo pia kisiasa Mbowe na siasa za nchi kwa ujumla inakuwaje?
Au inawezekana pia DPP akaingia "nolle" ya ghafla ghafla ghafla tu hapo athari kisiasa kwa Mbowe na nchi kwa ujumla inakuwaje?
Kwangu mimi hakuna ubishi kabisa kuwa kesi hii ni ya kisiasa! Kila MTanzania anayefuatilia siasa zetu kwa umakini analijua hilo - na utabiri wangu iwapo Mbowe na wenzake watafungwa basi ninaamini siasa za nchi hii zitakuwa zimenoga zaidi kwani kwa muda wote Mbowe atakaokuwa gerezani watu wanakuwa wakiongelea yeye tu.
Watazidi kuchambua uamuzi uliomfunga na proceedings hizi zinazoendelea na pia watazidi kuilaumu Serikali inayoongoza kwa unyanyasaji, uonevu na mtazamo hasi kwa upinzani. Serikali haitakuwa na Amani na watoa maamuzi hayo pia hawatakuwa na Amani maisha yao yote.
Watu wataondoa hofu watajihisi kuwa Mtawala akiamua kukufunga hata kama huna makosa anakufunga tu! Akifungwa Mbowe itakuwa ni chachu ya kuimarisha zaidi upinzani wa nchi hii.
Iktokea Mbowe kaachiwa katika hatua ya "nolle" kabla ya kufikia hatua ya wao kuwa na kesi ya kujibu basi Jamhuri itakuwa imepunguza aibu ambazo itaenda kupata kwani inaonesha hatua ya utetezi inaweza ikaibua mauzo mengi kwa upande wa washtaki katika kesi hii.
Kwangu mimi kwa Jamhuri ni bora wasivuke hatua ya kuwa hawa mabwana wana kesi ya kujibu kwani aibu haitakuwa kubwa sana na hata kisiasa awamu ya sita itaonekana kama yenyewe ndiyo imeamua kufikia muafaka na upinzani.
Hayo ni mawazo yangu - Je, ndugu yangu Paskali Mayala wewe unalichambuaje suala hili?