Pascal Mayalla atoa dongo kwa UKAWA

Pascal Mayalla atoa dongo kwa UKAWA

tunataka maendeleo sio maandamano, mnyika miaka 5 anaandamana kila mara badala ya kuleta maendeleo kutahamaki uchaguzi huu na jimboni hakuna alichofanya akaamua kuhama jimbo

It's very strange! Maendeleo ya namna gani ndugu? Hivi CDM wanataka kufanya maandamano ya kupinga urais kweli? Au mnajifurahisha tu, kwa hiyo UKAWA wanavyobanwa bungeni hawaruhusiwi wala hoja zao zozote hazisikilizwi huku vitendo vya kejeli na hata matusi vyenye hatari kwa afya ya amani ya bunge/nchi vikishamiri na kupaliliwa na naibu spika.
Wafanye maendeleo kwa jinsi gani ndani ya ubaguzi wa wazi bungeni, hata watanzania tumenyimwa uhuru wa kufuatilia bunge liv!, na nina hakika 100% kuwa sio kwamba eti mnaipenda sana na kuamini serikali inavyoendeshwa zaidi ya kujali vyeo na malupulupu mnayopata kutoka serikali ya ccm
 
Huyo Mayala naye kama kiazi fulani hivi au kasahau tu. Hajui kuwa katika nchi hii matokeo ya uchaguzi wa urais hayahojiwi mahala popote pale katika JMT au watu wa NEC walisahau kumwambia hilo!!!!!!!!!!.
Mkuu Ruga, uchaguzi ni process na una stages mbalimbali, kukitokea hitilafu zozote, au irregularities kuna fomu maalum ya kujaza kuripoti mapungufu hayo, bila kujalisha ni uchaguzi wa rais, mbunge au diwani!. Jee kuna complant yoyote iliyowasilishwa rasmi, ili kujenga basis ya kutoyatambua matokeo?!.

Matokeo ya urais yakiishatangazwa asmi ndipo hayapingwi popote, lakini kama kuna mapungufu yoyote genuine, na taratibu za kuripoti mapungufu hayo, matokeo hayatatangazwa mpaka hoja zijibiwe!.

Tufike mahali tukubali, mgombea wetu alishindwa kihalali bila bao lolote la mkono!, uchaguzi umeisha sasa tu focus on 2020!.

Paskali
 
Mmmmmmm

Sasa unaandika mengine hata sijaongelea na ninaongelea sasa na baadae muweje ubishi mwingi na mie kama mwananchi nasema mnaniboa na hamnivutiiiii...hadi nimeshindwa kusoma yote uliyoandika...hadi kama nitapata muda sijui lini.
Nahisi hukumuelewa. Kwa kifupi mambo ya uchaguzi yamekwisha tuendelee kujenga nchi yetu!
 
Mkuu Ruga, uchaguzi ni process na una stages mbalimbali, kukitokea hitilafu zozote, au irregularities kuna fomu maalum ya kujaza kuripoti mapungufu hayo, bila kujalisha ni uchaguzi wa rais, mbunge au diwani!. Jee kuna complant yoyote iliyowasilishwa rasmi, ili kujenga basis ya kutoyatambua matokeo?!.

Matokeo ya urais yakiishatangazwa asmi ndipo hayapingwi popote, lakini kama kuna mapungufu yoyote genuine, na taratibu za kuripoti mapungufu hayo, matokeo hayatatangazwa mpaka hoja zijibiwe!.

Tufike mahali tukubali, mgombea wetu alishindwa kihalali bila bao lolote la mkono!, uchaguzi umeisha sasa tu focus on 2020!.

Paskali

Naomba uniwekee ni fomu namba ngapi ya NEC inayo jazwa kulalamikia matokeo au mwenendo wa uchaguzi wa urais. Kupeana elimu ndiyo faida kubwa ya jamvi hili.
 
Mkuu Ruga, uchaguzi ni process na una stages mbalimbali, kukitokea hitilafu zozote, au irregularities kuna fomu maalum ya kujaza kuripoti mapungufu hayo, bila kujalisha ni uchaguzi wa rais, mbunge au diwani!. Jee kuna complant yoyote iliyowasilishwa rasmi, ili kujenga basis ya kutoyatambua matokeo?!.

Matokeo ya urais yakiishatangazwa asmi ndipo hayapingwi popote, lakini kama kuna mapungufu yoyote genuine, na taratibu za kuripoti mapungufu hayo, matokeo hayatatangazwa mpaka hoja zijibiwe!.

Tufike mahali tukubali, mgombea wetu alishindwa kihalali bila bao lolote la mkono!, uchaguzi umeisha sasa tu focus on 2020!.

Paskali

Hivi Hon. Mayalla kama mwandishi nguli ulijaribu kuhoji NEC ni kwa nini ni mwiko kabisa kuhoji matokeo ya uchaguzi wa rais katika nchi hii, au kwa nini wao wakisema hata kama takwimu si sahihi hakuna kuoji, na kwa nini matokeo mengine yahojiwe ispokuwa ya urais tu?????
Ref Zanzibar where only one man determined the election fate as there was no even ZEC meeting to determine the level of fraud leading to nullification of entire process. Ukifika hapo jiulize what kind of process you are referring to??????????
 
Mkuu sikusema wajumbe wa jf, jf haina wajumbe!, nimesema baadhi ya members wa jf, wanaoshupalia mgombea wao kashinda ila kapigwa bao la mkono.

Uchaguzi wa 2015, kura za urais zimehesabiwa vituoni!, hivyo hao mawakala wao, wanazo fomu halisi za matokeo ya kweli walizosaini baada ya kuhesabu kura, na matokeo hayo ndio yaliyobandikwa kwenye vituo vya kupigia kura, na kutumwa NEC. Kama kuna wizi umefanyika, tallying yao ingeonyesha tofauti na tallying ya NEC!, nimeauliza walete fomu za motokeo za mawakala wao, tulinganishe!, kimya!, kazi kulalamika!.

Kwanza mimi sio mwanachama wa chama chochote cha siasa, na kampuni yangu inapokea tenda za matangazo, toka taasisi yoyote ya umma na binafsi, ambapo jukumu langu kuu ni to tell nothing but the truth.

Thanks.

Paskali

Paschal, Sina shaka na umakini wako katika kauli wala uhuru wako wa kisiasa; nilikuwa namzungumzia mleta mada aliyepindisha maneno yako kwa manufaa yake.

Lakini mtazamo wangu ni kwamba hakuna haja ya kuwashambulia watu wanaodai kupigwa bao la mkono (hata kama hatuwezi kuthibitisha). Historia yetu katika chaguzi kuu na matukio kadhaa yasiyo na mantiki ikiwa ni pamoja na yale ya Zanzibar na kauli ya kada maarufu wa chama kilekile kusisitiza ushindi ni lazima hata kwa bao la mkono, vinatosha kutoa upenyo wa mashaka. Wakasemee wapi zaidi ya JF jukwaa pana na lililojijengea umaarufu wa pekee (kama Hyde Park ya London)? Na sitegemei kauli zao zimpe taabu yeyote. Let them speak. JF inatoa nafuu kubwa ya kisaikolojia kwa wengi sana hasa wasomi wenye kero zao.

Pia ninavyofahamu, data zote kuhusu kura za uchaguzi wa rais ni eneo nyeti sana; ni NEC tu ndiyo inayohusika. Ndio maana tulipata habari ya watu/taasisi zilizojaribu kukusanya data hizo kupata misukosuko mikubwa toka vyombo vya dola. Waliwekwa ndani na vifaa vyao kusanywa. Sasa sijui hiyo jeuri ya kudai kulinganisha data/makabrasha waliyokusanya na data za NEC wangeitoa wapi? Wrong or right, let them vent it here. Kesho tunasahau na maisha yanaenda kama kawaida. Ndio uzuri wa nchi yetu.

Shukran.
 
Naomba uniwekee ni fomu namba ngapi ya NEC inayo jazwa kulalamikia matokeo au mwenendo wa uchaguzi wa urais. Kupeana elimu ndiyo faida kubwa ya jamvi hili.
Mkuu Ruga, mimi sio NEC kukutajia namber za form, ile pale kwenye banda lao, nimeonyeshwa fomu zote tatu za malalamiko ya udiwani, ubunge na urais na hakuna yeyote aliyejaza fomu kulalamika!.

Kwa lengo la kusaidiana kuelimishana, karibu pande hizi
Tume ya Taifa ya Uchaguzi: Mwanzo

Paskali
 
Hivi Hon. Mayalla kama mwandishi nguli ulijaribu kuhoji NEC ni kwa nini ni mwiko kabisa kuhoji matokeo ya uchaguzi wa rais katika nchi hii, au kwa nini wao wakisema hata kama takwimu si sahihi hakuna kuoji, na kwa nini matokeo mengine yahojiwe ispokuwa ya urais tu?????
Ref Zanzibar where only one man determined the election fate as there was no even ZEC meeting to determine the level of fraud leading to nullification of entire process. Ukifika hapo jiulize what kind of process you are referring to??????????
Ni katiba iliyopo ndio iliyosema matokeo ya urais hayatahojiwa popote baada ya kutangazwa!, sio NEC waliosema hivyo bali ni katiba!. Hata hoja kama rais wa JMT hatalipa kodi yoyote sio rais ni katiba!, au rais hatashitakiwa mahakamani ni katiba na sio rais!. Hata hivyo kwenye katiba pendekezwa, matokeo ya urais, yanahojiwa mahakamani.

Issue ya Zanzibar, waachie wenyewe!, sheria, taratibu na kanuni zipo, kama hazikufuatwa kuna taratibu za kupinga zipo, kama aliyoyafanya Jecha ni kinyume cha sheria, taratibu na kanuni, jee nani alilalamika rasmi?!, au kule kwenda hotelini kufanya press conference ndio kulalamika kwenyewe?!. Nani aliipinga rasmi ile haramu ya Jecha?!. Haramu iliachwa bila kukanushwa, inageuka halali!. Hivyo uchaguzi wa marudio ni halali!.

Paskali
 
Ni katiba iliyopo ndio iliyosema matokeo ya urais hayatahojiwa popote baada ya kutangazwa!, sio NEC waliosema hivyo bali ni katiba!. Hata hoja kama rais wa JMT hatalipa kodi yoyote sio rais ni katiba!, au rais hatashitakiwa mahakamani ni katiba na sio rais!. Hata hivyo kwenye katiba pendekezwa, matokeo ya urais, yanahojiwa mahakamani.

Issue ya Zanzibar, waachie wenyewe!, sheria, taratibu na kanuni zipo, kama hazikufuatwa kuna taratibu za kupinga zipo, kama aliyoyafanya Jecha ni kinyume cha sheria, taratibu na kanuni, jee nani alilalamika rasmi?!, au kule kwenda hotelini kufanya press conference ndio kulalamika kwenyewe?!. Nani aliipinga rasmi ile haramu ya Jecha?!. Haramu iliachwa bila kukanushwa, inageuka halali!. Hivyo uchaguzi wa marudio ni halali!.

Paskali
dah mkuu umemjibu vizuri sana...asipoelewa hapo aende Dodoma kuzuia mkutano wa ccm
 
He he heeeeeeee! Sijacheka kitambo, anyway sukari imeanza kupatikana acha nicheke tena.

Nijuavyo mimi, SABA SABA ni INTERNATIONAL TRADE FAIR...haya NEC nao wana biashara ipi?

Mwaka huu hadi makaburi yatapigiwa promo. Ndio maana Mzee alikabidhi 12bn faida ya mwaka wa fedha uliopita.
nafikiri hujaelewa maana ya biashara, wakati mwingine sio kila penye biashara lazima nawe ufanye biashara. Nafikiri NEC walienda sabasaba baada ya kuona uchaguzi wa mwaka jana ulikuwa na malalamiko mengi, so wakaona sehemu pekee ya kuelezea wanaolalamika ni sabasaba maana pana umati mkubwa wa watu..lakin mbona hujashangaa kuliona jeshi la polisi(PT)sabasaba achana na uwepo wa jkt maana wanakampuni ya uzalishaji mali suma jkt watajitetea kuhusu hilo?
 
Back
Top Bottom