Ni katiba iliyopo ndio iliyosema matokeo ya urais hayatahojiwa popote baada ya kutangazwa!, sio NEC waliosema hivyo bali ni katiba!. Hata hoja kama rais wa JMT hatalipa kodi yoyote sio rais ni katiba!, au rais hatashitakiwa mahakamani ni katiba na sio rais!. Hata hivyo kwenye katiba pendekezwa, matokeo ya urais, yanahojiwa mahakamani.
Nimeelewa kwa nini baadhi ya wa TZ siyo analytical and for this trend it will be very difficult to develop this country.
Issue ya Zanzibar, waachie wenyewe!, sheria, taratibu na kanuni zipo, kama hazikufuatwa kuna taratibu za kupinga zipo, kama aliyoyafanya Jecha ni kinyume cha sheria, taratibu na kanuni, jee nani alilalamika rasmi?!, au kule kwenda hotelini kufanya press conference ndio kulalamika kwenyewe?!. Nani aliipinga rasmi ile haramu ya Jecha?!. Haramu iliachwa bila kukanushwa, inageuka halali!. Hivyo uchaguzi wa marudio ni halali!.
Paskali