Tunapozungumzia usalama wa taifa, maana yake ni kwamba tunazumgumzia roho ya nchi.
Ukiona taifa lolote lina watu maskini, wajinga, wasiojitambua, ujue kwamba hata intelligence ya nchi pia haijitambui na iko dhaifu kupindukia.
Ukitaka kufanikiwa kimaisha, waige waliofanikiwa, usiige maskini.
Rais wa Marekani,Donald Trump anaweza kutolewa madarakani wakati wowote na CIA, kwa kivuli cha Bunge, lengo ni maslahi mapana zaidi ya Marekani na siyo yeye Trump na genge lake la Republicans.
Wamarekani wanaipenda nchi yao, sisi hatuipendi Tanzania yetu bali tunapenda CCM na CHADEMA.
Ndo maana Rais wetu ni mungu mtu yeye huwa hakosei.
Naamini hata Nyerere hakuwa mzalendo wa kweli wa Tanzania yetu, kwa kauli yake hii mzee huyu nilimvua uzalendo,namnukuu.
"Kwa katiba hii Tanzania ikipata Rais Dikteta mtakiona cha moto ".
Mungu amrehemu mzee wetu huko alipo,alijua katiba ya Tanzania ni mbovu inayomfanya Rais awe Mungu mtu, Kwanini hakuibadili mapema akiwa madarakani badala yake akatoka na kuanza kulia lia Kama mimi My Son drink water ninavyolia sasa?
Tanzania ina watu mil 50,watu active wanaohangaika na maisha ni mil 15 walioajiriwa hawazidi laki 8,waliojiajiri sekta isiyo rasmi ni hawazidi laki mil 1.
Mil 35 iliyobaki, ni watoto, wazee mno, wagonjwa, wafungwa na idadi kubwa ya mil 30 ni ma jobless tupu.
Humo ndo kunazalishwa matapeli, wezi, vibaka, malaya wa kujiuza, wapiga mizinga, ombaomba na balaa zote.
Mossad retired agent.
"if we want to topple a government, the best group to collaborate with is the big number of the haves not, such people deeply hate their government and they are easily persuaded ".
Mwisho wa kumnukuu huyo jabali.
Je TISS mnalijua hilo?
Inaendelea...