Palamagamba Kabudi, Unaivuruga Nchi....!

Palamagamba Kabudi, Unaivuruga Nchi....!

..Unazungumzia AFDB yenye makao makuu Abidjan, Ivory Coast?

..kuna mabeberu wana hisa ktk benki hiyo.

..pia mahitaji yetu ya mikopo kwa ajili ya miradi ya maendeleo ni makubwa na hayawezi kutoshelezwa na AFDB peke yao.

..muelekeo tuliochukua utatuletea ugumu ktk kupata misaada na mikopo ya masharti nafuu.

..Tukichukua mikopo mingi ya masharti magumu tunaweza kufika mahali ncho ikaelemewa na mzigo wa madeni. Nadhani unakumbuka matatizo ya ulipaji madeni tuliyokuwa nayo wakati wa utawala wa Mzee Mkapa.

..marafiki zetu and our development partners, wanatushauri, hawatulazimishi, tulinde haki za binadamu, tudumishe utawala wa sheria na katiba, tujenge demokrasia ya kweli, tukomeshe vitendo vya kikatili, etc etc.

..mengi wanayotushauri ni mambo ambayo tunaweza kuyatekeleza. Hakuna haja ya kuliumiza taifa[ walio wengi] kwa kiburi cha watu wachache.

..Ushauri wangu ni Raisi Magufuli afanyie kazi dondoo ambazo haziwaridhishi marafiki zetu na wadau wetu wa maendeleo. Akifanya hivyo ataiweka nchi ktk nafasi ya kufanya mambo makubwa zaidi ya kimaendeleo.

Ushauri mzuri, lakini wao wanachotafuta ni sifa.
Wakisikika na hao wanaowavimbisha vichwa kwa vigelelegele maneno kama anayoyasema Kabuti "hatutapiga magoti" kwao inakuwa faraja kubwa.

Inashangaza kidogo, kwa sababu mwanzo nilidhani ni utani tu, walipoanza kelele za "Mabeberu, Wasaliti," n.k., kwa sababu maana ya maneno kama haya enzi hizi kwa kweli yamepitwa na wakati sana.

Enzi za Mwalimu Nyerere maneno kama 'unyonyaji', mabeberu yalikuwa na maana, na tulijifunza maana hizo tukazielewa.
Sasa kuendelea na mbinu zile zile za kuita watu majina wakati huu kwa kweli hakufai.

Hii haina maana kwamba hakuna wapigaji/wanyonyaji. Lakini kama unajiandaa mwenyewe ili unyonywe pamoja na kujua kuwa kunyonywa kupo, halafu ukizinduka uanze kupiga kelele zile zile za zamani za kuita watu kijumlajumla majina- 'mabeberu' kana kwamba umegundua mvinyo mpya haipendezi.. Kwa hiyo sisi tunalianzisha upya, la Magharibi na Mashariki; vita baridi mpya inaanzia Tanzania?

Vita ya mabwenyenye na watwana ilishapiganwa miaka mingi. Leo hii ukitaka tena kujiweka kwenye utwana hiyo ni hiari yako hakuna anayekukataza. Lakini unapojifanya umezinduka na kuanza kupiga kelele zilizopigwa zamani, watu watakuona kama mwenda wazimu fulani.

Kama umegundua mahali umegongwa, shughulika na hao hao wanaokugonga. Usianze kujifanya unapambana na mfumo na kuhusisha kila mtu. Wazungu wote kwa sababu ya uzungu wao hawawezi kuwa 'mabeberu'.

Kwa ujinga mwingi sasa nchi nzima inaimba 'Mabeberu'. Huu sio ukichaa? Nilidhani ni utani; kumbe hali hiyo ndiyo inayowaletea sifa na wanafurahi wanapoona wajinga wakishangilia upuuzi huo.

Profesa mzima anakwenda kuongea Bungeni "kuwapigia magoti" watu, na wakati huo huo analilia wawekezaji waje kwa wingi kuwekeza nchini. Anawekea mkazo "hatutawapigia magoti", ili wajinga waone kuwa nchi inamsimamo - lakini wajinga wasichojua viongozi hawa ndio wapiga magoti wakubwa; ombaomba wa kutupwa kwa njia mbalimbali wasizotaka wajinga wao wasizitambue kama ndio 'kupiga magoti' kwenyewe huko.
 
Waziri wa Mambo ya nje ni mtu muhimu sana katika taifa. Ni mwanadiplomasia mkuu ukimuondoa Rais. Leo tnaye Palamagamba Kabudi, namba moja kuwaimbia Mabeberu Singeli.

Ni huyu Kabudi aliyekuja na sheria za hovyo zinazotufanya sasa hivi kuonekana vituko kimataifa. Ndiye Kabudi aliyesababisha wawekezaji wengi kuondoka Tanzania akiwa Waziri wa Sheria.

Huyu Kabudi anayeimba nyimbo za kuwakandia mabeberu ndiye aliyekuwa namba moja kuzunguka nchi za Ulaya kupiga magoti tusiwekewe vikwazo. Inakuwaje anawahadaa watanzania huku anaivuruga nchi?

Bila shaka, Kabudi ndio beberu namba Tanzania.

Ebu twambie ni muwekezaji yupi aliyekimbia kuwekeza, fwatilia kwa makini mapato tunayopata kwa sasa baada ya sheria mpya za madini, kwanini Watanzania tu nawapenda watu wanatuibia? Nadhani tumtende haki Kabudi kwenye eneo hili la sheria za madini kasimamia vizuri Sana.
 
Ni kweli tunakopesheka sasa uwezo wetu ni lets say ktk mia sisi tuna uwezo wa kupata hamsini, halafu hii hamsini ww unasema tunakopa good, mwaka huu tunakopa then mwakani inatakiwa tulipe mkopo wa mwaka huu plus interest na pia tukope tena hamsini! Which means uwezo wetu wa kukopa na kulipa haviendani lazima tukapitishe bakuli kwa mabeberu kutusaidia

Ni kweli tunakopesheka! Sasa hapo ndipo wanapokuja hao wa kutukopea mabeberu imf, world bank, africa bank, chinese etc pia hapo ndo kuna mabeberu wa misaada! Ni kama mimi sina uwezo wa kujiendesha kibishara naenda kukopa crdb inayomilikiwa na mabeberu huku nikisema bora beberu ww kuliko beberu nmb!

Halafu baadaye naenda kupiga mzinga huku nimebeba magazeti yote ya nchi nampelekea balozi ( sijui alikuwa wa marekani yule mama nimesahau) kuna pic kabudi anamuonyesha balozi jinsi nchi ilivyo huru kihabari, hii iliyotokea pale gazeti la citizen lilipofungiwa!

Budget ya msimu huu tulikuwa na mapungufu ya 12 trillion! Tumekopewa tisa trillion na ma bank ya kibeberu na tukasaidiwa trillion 3 na mabeberu.
Tunakoelekea...
BEBERU ATABAKA MBUZI KAMA SI KUMTIA MIMBA!!!!
Naota tu...
 
Ebu twambie ni muwekezaji yupi aliyekimbia kuwekeza, fwatilia kwa makini mapato tunayopata kwa sasa baada ya sheria mpya za madini, kwanini Watanzania tu nawapenda watu wanatuibia? Nadhani tumtende haki Kabudi kwenye eneo hili la sheria za madini kasimamia vizuri Sana.
Sana tu Mkuu kama alivyosimamia la koroshow. ..
 
Waziri wa Mambo ya nje ni mtu muhimu sana katika taifa. Ni mwanadiplomasia mkuu ukimuondoa Rais. Leo tnaye Palamagamba Kabudi, namba moja kuwaimbia Mabeberu Singeli.

Ni huyu Kabudi aliyekuja na sheria za hovyo zinazotufanya sasa hivi kuonekana vituko kimataifa. Ndiye Kabudi aliyesababisha wawekezaji wengi kuondoka Tanzania akiwa Waziri wa Sheria.

Huyu Kabudi anayeimba nyimbo za kuwakandia mabeberu ndiye aliyekuwa namba moja kuzunguka nchi za Ulaya kupiga magoti tusiwekewe vikwazo. Inakuwaje anawahadaa watanzania huku anaivuruga nchi?

Bila shaka, Kabudi ndio beberu namba Tanzania.
Kala maganda hadi akabugi
 
Sana tu Mkuu kama alivyosimamia la koroshow. ..

Korosho ni issue ndogo Sana mikataba yake ni muda kununua na kulipa, Mambo makubwa ndiyo tuyajadili kama watu huru, kitendo cha kusimamia kubadili sheria za madini ni msingi Sana, tuache siasa na chuki binafsi ukweli ubaki ukweli, kwenye korosho tumepoteza nini? Hawajanunua basi, hata kama ni hasara hatuwezi kutomtendea haki Kabudi kwa namna anavyofanya mazuri yenye faida endelevu.
 
Korosho ni issue ndogo Sana mikataba yake ni muda kununua na kulipa, Mambo makubwa ndiyo tuyajadili kama watu huru, kitendo cha kusimamia kubadili sheria za madini ni msingi Sana, tuache siasa na chuki binafsi ukweli ubaki ukweli, kwenye korosho tumepoteza nini? Hawajanunua basi, hata kama ni hasara hatuwezi kutomtendea haki Kabudi kwa namna anavyofanya mazuri yenye faida endelevu.
Ni issue ndogo kwa sababu wewe hujailima wala hu miongoni mwa wasiolipwa... ni issue ndogo kwa sababu "njaa ile" haikugusi wala haijawagusa jamaa zako...
Mikataba iwekwe wazi ili kila kitu na faida vijulikane...
Hakuna mikataba mizuri ifanyikayo na kufichwa chini ya meza...
Sheria ya takwimu....
 
Ni issue ndogo kwa sababu wewe hujailima wala hu miongoni mwa wasiolipwa... ni issue ndogo kwa sababu "njaa ile" haikugusi wala haijawagusa jamaa zako...
Mikataba iwekwe wazi ili kila kitu na faida vijulikane...
Hakuna mikataba mizuri ifanyikayo na kufichwa chini ya meza...
Sheria
 
Ni issue ndogo kwa sababu wewe hujailima wala hu miongoni mwa wasiolipwa... ni issue ndogo kwa sababu "njaa ile" haikugusi wala haijawagusa jamaa zako...
Mikataba iwekwe wazi ili kila kitu na faida vijulikane...
Hakuna mikataba mizuri ifanyikayo na kufichwa chini ya meza...
Sheria, Siyo kila mtu atatunga sheria, ndiyo maana kwote duniania palipo Taifa hakuna hadithi tunayoaminishwa kuweka wazi, nenda Marekani kama utaona wanaweka wazi kila kitu, huenda huko kwenye kununua korosho Sawa
 
Kuna msaada usio na masharti?
Hauna msaada usio na masharti. Mwelevu kabla ya kupokea msaada anaangalia hayo masharti yana maslahi gani kwake. Kabudi ametukumbusha maamuzi magumu yaliyowahi kuchukuliwa na Tanzania. Kurudisha Fedha za misaada kwa waliotaka kutumia masharti ya mikopo kama silaha ya kutupangia nini tufanye.
 
lakini unajua kuwa dunia sasa ni kijiji.
yote yanayofanyika huku hao wafadhili wanayaona sio mpaka upinzani waandike barua.
Wapinzani wa kwetu hawajui hilo, waliandika na kujisifu mitandaoni kuwa tumeandika😁😁
 
Ujuha na ongo mtupu,hakuna wakati wowote Tanzania imewahi kurudisha msaada.
Kukataa msaada nako mnaita ni maamuzi magumu!
Ni masharti gani yasio na maslahi kwetu ambayo tumepewa mpaka sasa?Hakuna.
Iwe kurudisha watoto waliopata mimba shuleni,kuheshimu haki za wakosoaji, uchaguzi huru,nk
Hauna msaada usio na masharti. Mwelevu kabla ya kupokea msaada anaangalia hayo masharti yana maslahi gani kwake. Kabudi ametukumbusha maamuzi magumu yaliyowahi kuchukuliwa na Tanzania. Kurudisha Fedha za misaada kwa waliotaka kutumia masharti ya mikopo kama silaha ya kutupangia nini tufanye.
 
Mazuri yapi yenye faida endelevu amefanya? Taja matatu tu.
Korosho ni issue ndogo Sana mikataba yake ni muda kununua na kulipa, Mambo makubwa ndiyo tuyajadili kama watu huru, kitendo cha kusimamia kubadili sheria za madini ni msingi Sana, tuache siasa na chuki binafsi ukweli ubaki ukweli, kwenye korosho tumepoteza nini? Hawajanunua basi, hata kama ni hasara hatuwezi kutomtendea haki Kabudi kwa namna anavyofanya mazuri yenye faida endelevu.
 
Waziri wa Mambo ya nje ni mtu muhimu sana katika taifa. Ni mwanadiplomasia mkuu ukimuondoa Rais. Leo tnaye Palamagamba Kabudi, namba moja kuwaimbia Mabeberu Singeli.

Ni huyu Kabudi aliyekuja na sheria za hovyo zinazotufanya sasa hivi kuonekana vituko kimataifa. Ndiye Kabudi aliyesababisha wawekezaji wengi kuondoka Tanzania akiwa Waziri wa Sheria.

Huyu Kabudi anayeimba nyimbo za kuwakandia mabeberu ndiye aliyekuwa namba moja kuzunguka nchi za Ulaya kupiga magoti tusiwekewe vikwazo. Inakuwaje anawahadaa watanzania huku anaivuruga nchi?

Bila shaka, Kabudi ndio beberu namba Tanzania.
Kama ksbudi
 
Prof wa ajabu sana!!! Huongea kama kuna mashindano ya kutoa macho au sauti kumbe ni hoja tu!
 
Hujaelewa hoja yangu bali umejibu kiushabiki!!

Demokrasia kwa taarifa yako tu ilianza kwa Wagiriki (Athens) miaka ya 300BC na kipindi hiko haikwa demokrasia yenu hii iliyokujwa kuchukuliwa na Wamarekani!! Ilikuwa demokrasia ya kweli!! Huwezi ukashangilia demokrasia ya kijinga ya kuwa na utitiri wa vyama vya siasa wakat nchi mwanzilishi vyama vya siasa wao ni viwili tu!!

Bado mawazo yako yapo kule kule ...uliyoandika ni matokeoa ya nilichokisema na kamwe kwa mentality yako hutakuja kutumia muda wako kujiandaa kuelewa!!! Wacha tuzidi kulalamika demokrasia wenzetu ambao ndio wanawashawishi mpigane kwa njia ya kudai uhuru wanawatengenezea siraha halafu wanajidai ni wanademokrisia!!! Hivi ushawasikia wanaleta propaganda zao kwa nchi kama China??

Endeleeni kubishana demokrasia sjui hata shuleni mlijifunza nn .mnaongea utafikiri demokrasia hiyo kwao ipo!!! Yanayotokea Ulaya kama BREXIT ingekuwa Afrika sashv ingeluwa haikariki......lakn kwa kukosa maarifa kwetu badala ya kufocus mambo ya msingi tunaelekea sasa mwaka wa Tano tangu serikali hii iingie madarakani tunaimba wimbo uleule ..nothing new rather than talking nonsense!!!
Kwanza, dhana nzima ya Demokrasia ilianzishwa na Wagiriki miaka 500BC na sio miatatu. Pili wamarekani wana zaidi ya vyama vya siasa 30 na sio viwili tu. Hivyo viwili ndio vyenye ushawishi mkubwa na ni mahasimu wa siku nyingi sana.

Tukiacha hayo, hakuna anayetulazimisha kufanya yaliyo kinyume na tuliyojipangia kwenye Katiba yetu. Huwezi ukasema unailinda Katiba inayoruhusu uhuru wa maoni, uhuru wa kujumuika, uhuru wa vyama vya siasa, haki sawa kwa wote, ulinzi kwa kila mwanachi ndani na nje ya mipaka ya nchi kwa kukandamiza haki hizo hizo. Kuna mtu anadiriki kumtishia mtanzania mbele ya kadamnasi, tena kwa kujiamini kuwa "akipotezwa" mtanzania mmoja kati ya watanzania milioni 55 hakuna atakaye jali. Huyu mtu bado yuko uraiani.

Tunatia saini mikataba na "mabeberu" tena kwa mbwembwe nyingi mbele ya waandishi wa habari bila kuwaambia watanzania masharti ya mikataba hiyo. Tunaishia kutaja kiasi cha fedha na zitakavyotumika. Siku tukikiuka masharti tukiambiwa, tunawakimbilia watanzania kuwaambia mabeberu ni wabaya.

Huu unafiki wa kisiasa ndio unaotudidimiza. Tabia ya kuweka mpira kwapani katikati ya mechi kisa ulikurupuka kuingia kwenye mechi ilhali ligi huiwezi.

Kwa ufupi Demokrasia ni kama aina ya gari. Kuna aina mbalimbali za uongozi kama ilivyo aina mbalimbali za magari. Unapoamua kuchagua brand ya Demokrasia, unachagua gari gani unataka kutokana na uwezo wako na matumizi yako. Kama matumizi yakibadilika baadae na uwezo ukabadilika uko huru kubadilisha. Lakini huwezi kuilazimisha IST kuwa kama Toyota 200GT, halafu ikishindwa unamlaumu mwenye kiwanda. Kama tunaona aina ya Demokrasia tuliyonayo ni ya kibeberu, tubadilishe katiba na sheria zetu na siyo uongo wa kuapa kulinda kitu tusichoamini wala kuthamini!
 
Mkuu umenena sana japo naweza nisiwe ktk muktadha wa mlengwa wako!!! Lakn cha msingi ni kujiuliza kwann kila kitu ni msaada??? Tulikosea wapi na tunakosea wapi???? Kila kitu ni nje why??? Je hii misaada tunayopewa je tunaitazaman kwa kina ktk Do-s and Dont-s zake????
Kwasababu tumeshindwa kuwekeza kwenye afya za akili za watanzania na kuimarisha mifumo ya utawala na uchumi. Tumedumaza elimu yetu na kuimarisha watawala na wachumia tumbo wachache.
Mwaka 1945 asilimia kubwa ya Berlin na miji mingine ya Ulaya iliathirika sana na vita kuu ya pili ya dunia. Marekani ilitoa misaada chini ya mpango wa Marshall (Marshall Plan) ndani ya miaka 20 hawakuhitaji tena misaada na leo Ujerumani ni kati ya mataifa tajiri na yenye nguvu duniani. Wao waliwezaje na sisi tunashindwa nini?
 
Korosho ni issue ndogo Sana mikataba yake ni muda kununua na kulipa, Mambo makubwa ndiyo tuyajadili kama watu huru, kitendo cha kusimamia kubadili sheria za madini ni msingi Sana, tuache siasa na chuki binafsi ukweli ubaki ukweli, kwenye korosho tumepoteza nini? Hawajanunua basi, hata kama ni hasara hatuwezi kutomtendea haki Kabudi kwa namna anavyofanya mazuri yenye faida endelevu.
Korosho ni issue ndogo?!! Zao linalotuletea hadi asilimia 15 ya mapato ya kigeni?! Unajua katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, Tanzania ndio iliyoongoza kwa mauzo ya zao la korosho?!!
Ningewaona viongozi wetu wamefanya jambo la maana kama wangeendeleza miundo mbinu na ujuzi wa watanzania kuongozea thamani zao la korosho ili tusiuze kama mali ghafi tu.
Maisha ya watu yanategemea zao hili, uchumi wa nchi unategemea zao hili.
 
Mkuu umenena sana japo naweza nisiwe ktk muktadha wa mlengwa wako!!! Lakn cha msingi ni kujiuliza kwann kila kitu ni msaada??? Tulikosea wapi na tunakosea wapi???? Kila kitu ni nje why??? Je hii misaada tunayopewa je tunaitazaman kwa kina ktk Do-s and Dont-s zake????


Ww jamaa hivi unayoandika unasadiki?
Kama serikali hii haitaki misaada, imefanya jitihada zipi za kuonesha kua nchi sasa inajitosheleza na misaada haihitajiki?
 
Back
Top Bottom