Palamagamba Kabudi, Unaivuruga Nchi....!

Palamagamba Kabudi, Unaivuruga Nchi....!

Tusimlaumu kabudi. Tulikosea wenyewe 25/10/2015.
haya ni matokeo ya kura zetu.
Kabudi yuko sahihi.
Mkikosa kumpata kiongozi mkuu aliye sahihi, mtarajie kuwapata wasaidizi wake wasio sahihi.
 
OK labda nikuulize kulikuwa na umuhimu wowote wa yeye kusema HATOWAPIGIA MAGOTI WAZUNGU KUWAOMBA MSAADA.
kwani kuna mashindano kati yetu na wazungu?
Nani anayeteseka kati yetu na wao?
Hayo yanafanywa na watu waliokosa hekima lakini wanaamini wana akili wakati hawana.
 
Hizo sera hazina nafasi katika awamu hii, tulimchagua wengi (the majority) na tunamuunga mkono, wakati wa uchaguzi ukiwadia chagueni kibaraka wenu wa wazungu mnayemtaka na tutaheshimu maamuzi yenu maadamu mtakuwa wengi.

Ingekuwa mnaheshimu kura za wananchi leo hii mngekuwa mkono nje zamani sana, na huenda ccm leo hii ingekuwa kama KANU ya Kenya.
 
Kabisa.. ni jinai kumsema vibaya muzungu
Kwa nini umseme mzungu wakati hakuna sababu ya kumsema? Ni pale mtu aliyepungukiwa anapofikiri atakamilika kwa kuonesha ubabe dhidi ya aliyefanikiwa.
 
Komenti ziwe fupifupi tu kuhusu huyu jamaa aliyeiingiza chaka nchi dhidi ya MUTEMBEI
Hatuna waziri anaitwa Kalamagamba kosa la kwanza

Hoja yako haina mashiko na umeandika hayo kwasababu Avatar yako inathibitisha ulichokiandika na maneno ya Palamagamba Aidan Mwaluko Kabudi!!!

Acha umagharibi katika kufikiri !!

Nikuambie tu machache kuhusu Unakokupenda huko ...nchi ya Kongo DRC inaweza ku supply HEP Barani Africa kwa 22 asilimia ,,ina vyama vya siasa vinakaribia 200 na ushehe na ndio miongoni mwa nchi ktk Afrika zinazojiita Democratic lakn kiuhalisia hakuna demokrasia ....huu n wimbo ambao wazungu wameuleta tunauimba hadi leo mbaya zaidi hata watoto wadogo wameanza kuuimba yani uhuru uhuru uhru uhuru uhuru na kusahau mambo ya msingi,,,, si kwenye kutenda ,kufikiri kuabudu na hata kwenye utamaduni ndio maana leo kote uendako tunaangalia movie za kigeni na wewe kuutukuza umagharibi kwa kuona kujiita hvyo ni kuwa civilized !! Afrika hakuna cha kujivunia sasa bali ni kupigana majungu tu na kubezana sisi kwa sisi kwa kutumia sindano za hawa jamaa ....pata muda ujifunze ya Libya na maisha yao hivi leo.....Hakuna kitu kibaya iwe katika haki za binadamu ama kidemokrasia kwa Afrika kulaumiwa!!! Yote haya walitengeneza wao kwetu na sasa sisi tulioathiriwa sasa tumesaahau kw kisa tu wamekuja kivingine !!

Amka!
 
Wewe unataka tuwe nini, Kimashariki/KiChina?

Kiafrika kikoje?

Mtu unapokuwa na elimu yako, ukashindwa kuitumia elimu hiyo ipasavyo, ukabaki kuwa na nyimbo za wewe kuchotwa akili na 'wamagharibi' kwa kila kitu, maana yake ni kuwa elimu uliyopata haikusaidii chochote.

Huwezi kuja hapa na kusema mabaya yote tunaletewa na 'wamagharibi.' Kama unaelewa maana ya 'Demokrasia huwezi kuja hapa na kusema hiyo ni ya 'magharibi', kwa hiyo ni mbaya! Ni kwamba hujui demokrasia ni nini.

Unapotaka dikteta ndie awe wa kuamua kila jambo linalowagusa wananchi, hiyo wewe ndio unaona ni uafrika wetu kwa hiyo tuusifu?
Hujaelewa hoja yangu bali umejibu kiushabiki!!

Demokrasia kwa taarifa yako tu ilianza kwa Wagiriki (Athens) miaka ya 300BC na kipindi hiko haikwa demokrasia yenu hii iliyokujwa kuchukuliwa na Wamarekani!! Ilikuwa demokrasia ya kweli!! Huwezi ukashangilia demokrasia ya kijinga ya kuwa na utitiri wa vyama vya siasa wakat nchi mwanzilishi vyama vya siasa wao ni viwili tu!!

Bado mawazo yako yapo kule kule ...uliyoandika ni matokeoa ya nilichokisema na kamwe kwa mentality yako hutakuja kutumia muda wako kujiandaa kuelewa!!! Wacha tuzidi kulalamika demokrasia wenzetu ambao ndio wanawashawishi mpigane kwa njia ya kudai uhuru wanawatengenezea siraha halafu wanajidai ni wanademokrisia!!! Hivi ushawasikia wanaleta propaganda zao kwa nchi kama China??

Endeleeni kubishana demokrasia sjui hata shuleni mlijifunza nn .mnaongea utafikiri demokrasia hiyo kwao ipo!!! Yanayotokea Ulaya kama BREXIT ingekuwa Afrika sashv ingeluwa haikariki......lakn kwa kukosa maarifa kwetu badala ya kufocus mambo ya msingi tunaelekea sasa mwaka wa Tano tangu serikali hii iingie madarakani tunaimba wimbo uleule ..nothing new rather than talking nonsense!!!
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] huyu ndo anasema hapigi magoti??
images-3.jpg
 
Mzungu yeye mambo yake anayaendesha kisomi.
Sababu za wao kukata misaada Tanzania wamezitoa na zina eleweka.
Na hakuna hata sehemu moja katika barua zao WAMEANDIKA WANATAKA WAPIGIWE MAGOTI.
sasa kabudi mambo ya kupigiana MAGOTI kayatoa wapi?
anatakiwa kujenga hoja sio kupanik.
Wazungu sio chadema wale.
na umapotaka kutunishiana nao misuli kama hivyo wewe ndo utaumia.
wamekata misaada basi maisha yaendelee VIJEMBE VYA NANI?
Hakuwa anaongea na wazungu alikuwa anaogea na Wabunge wa Tanzania. Wabunge wa upinzani ambao toka siku ya kwanza ya kuwasilisha bajeti yake wanamzodoa. Amewambia jinsi alivyoenda "Jiniva" na kuvunja vunja umbeya wa barua zao walizokuwa wanatuma kupendekeza tunyimwe misaada sababu "Serikali inakiuka haki za binadamu". Anawambia vinoko vijana wa leo wasiojua dunia ilikotoka kuwa nchi za magharibi ndizo wakiukaji wakubwa wa haki za binadamu sio Tanzania. Wanatakiwa wajue Uhuru wowote ktk haki za binadamu UNAMIPAKA na kawaeleza hao wanaowasujudia na wamemuelewa😃😃. Na wakiendelea na kelele zao zitajibiwa kwa nguvu ileile wanayotumia wao 😆😆
 
..na wanaotukopesha siyo mabeberu?

..kabudi alipaswa kuwasilisha hoja zake kisomi na kidiplomasia, siyo kwa kufoka na kupiga makelele namna ile.
Mara nyingi Kabudi majibu yake huwa off point. Huwa hajibu hoja.
 
Mikopo si tunakopesheka

Utazilipaje hizo ulizokopa kama revenue inabaki hivyo hivyo lakini matumizi yanaongezeka? Kumbuka miradi yote ya jiwe haina short-term returns which means inaongeza matumizi tu kwa sasa wakati haiingizi mapato.
 
Kabudi achunge mdomo wake ipo siku ataiingiza nchi kwenye matatizo
Aiingize nchi kwenye matatizo mara ngapi/lini?

Mbona tuko matatizoni muda mrefu tu.

Hili maganda ni tatizo kubwa, huyu hana tofauti na Bashite ktk kila kitu.

Hawa ndiyo wateule Wa Rais sasa fikiria huyo Rais yukoje
 
lakini unajua kuwa dunia sasa ni kijiji.
yote yanayofanyika huku hao wafadhili wanayaona sio mpaka upinzani waandike barua.
Hakuwa anaongea na wazungu alikuwa anaogea na Wabunge wa Tanzania. Wabunge wa upinzani ambao toka siku ya kwanza ya kuwasilisha bajeti yake wanamzodoa. Amewambia jinsi alivyoenda "Jiniva" na kuvunja vunja umbeya wa barua zao walizokuwa wanatuma kupendekeza tunyimwe misaada sababu "Serikali inakiuka haki za binadamu". Anawambia vinoko vijana wa leo wasiojua dunia ilikotoka kuwa nchi za magharibi ndizo wakiukaji wakubwa wa haki za binadamu sio Tanzania. Wanatakiwa wajue Uhuru wowote ktk haki za binadamu UNAMIPAKA na kawaeleza hao wanaowasujudia na wamemuelewa[emoji2][emoji2]. Na wakiendelea na kelele zao zitajibiwa kwa nguvu ileile wanayotumia wao [emoji38][emoji38]
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] huyu ndo anasema hapigi magoti?? View attachment 1113594
Unafiki ni kitu kibaya sana, Marehemu Ruge aliwahi kutamka "ogopa teknolojia". Picha inadhihirisha jinsi WaTz wanavyodanganywa na utawala huu na ingekuwa kwa wenzetu Wakenya wanaojitambua Viongozi wa aina hii tungeshawasahau maana wao hawataki use.. enge na unafiki wa aina hii
 
Back
Top Bottom