P-Funk naye aishukia Clouds FM

P-Funk naye aishukia Clouds FM

[h=3]"SITAKI KUSIKIA NYIMBO ZA NGWEA ZIKIPIGWA CLOUDS FM.\..WAO NDO WALIOMFANYA AANZE KUVUTA BANGI ILI KUONDOA MAWAZO"...P FUNK[/h]


Muda mfupi uliopita djchoka amepokea simu kutoka kwa Producer mkongwe hapa bongo anayejulikana kwa jina la P ---- Majani na kumuuomba aipokee msg hii hapa chini na kuwaomba watanzania walijue hili na baadae atatoa barua rasmi.

Inaonekana hii redio hawana public interest, punde tu watakuwa kama TBC-redio na Tv. Miaka 5 ni mingi sana kwao kupoteza wasikilizaji na kurudi down to the grasses.

Clouds inaonekana kuwa ni watu wasiojali saana matakwa ya wasikilizaji wao, wangekuwa na akili nzuru, wamiliki wake wangetenga ubinafsi wao na uendeshaji wa redio yao. Wakumbuke kuwa wasikilizaji ndio first and most important clients- ndio wamiliki wenye hisa nyingi kwa maana ya kuwa wasikilizaji wanapokuwa wengi ndipo matangazo ya biashara yanakuwa mengi.

Clouds FM wachunge sana Magic FM is a threat to them.
 
Jana kwenye uzi wa kifo cha Ngwea nilisema Claus ndio wanaochangia wasanii wetu kujiingiza kwenye kazi haramu hadi kupelekwa vifo vyao.

maana wakisema wajitenge nao, wanabaniwa njia zote za kutoka kimuziki.

mjinga mmoja akinijibu mbovu.

Leo tena Majani anawalalamikia haohao.

tusipoangalia wasanii wetu watavuma mwishoni wanaishia kuwa ombaomba.!!
 
Ukistaajabu ya MUSA utayaona ya PFUNK, Asitafute umaaruf kwenye Misiba, Kama Ngwear alivuta mibangi na Madawa kwa sababu ya Frustration kwa Clouds, yeye nani amemfrustrate kuwa Muumini mzuri kwenye tasnia hiyo ya Vilevi! Dah. P Funk nae anapigania haki za Wasanii? Kama tukimpa Bastola ili auwe wezi wakubwa wa kazi za wasanii , akiwa Muadilifu anapaswa kujipiga bomba kwanza yeye mwenyewe!
 
hv hawa mawingu ni wanyonyaji wasanii ona wasanii wanavyokufa masikini huku wakiwa na majina makubwa
 
Jamani wasanii watambue life styles zao ndio adui yao mkuu, Je kama wasanii wanachukua hatua gan wenzao wakijiingiza kwenye ulevi wa pombe na madawa ya kulevya? Wakiisha ishiwa wanaanza tafuta sababu
 
waacheni walalamike wenyewe wasanii, kwanini mashabiki ndo mwayaongea hayo?? ina maana ninyi ndo mnajua sana ama???? matusi makubwa mnatukana kwny social networks mbalimbali, ina maana jide ndo aliyewaambia mtukane ama nini??? amkeni vjana, ninyi mnatukana wenzenu wana enjoy maisha, wakati huo muda unaotumia kutukana ungekuwa ushafanya mambo mengi tu

Mashabiki ndio wanasababisha uwepo wa wasanii, bila shabiki hakuna msanii.

Ni ruksa shabiki kumtetea msanii anayemuona akionewa na wanyonyaji wa kazi anazozishabikia kupitia msanii husika.

Hongera sana P.Funk
Hongera sana Prof. Ludigo
Hongera sana Lady Jay Dee
Hongera Sugu na VINEGA kwa ujumla.

Huuu ndo mwisho wa Clouds.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Clouds ishaniboa kabisa mie nipo E.A Radio na Lady Jay D kasitisha Tamasha Lake.
 
Ukistaajabu ya MUSA utayaona ya PFUNK, Asitafute umaaruf kwenye Misiba, Kama Ngwear alivuta mibangi na Madawa kwa sababu ya Frustration kwa Clouds, yeye nani amemfrustrate kuwa Muumini mzuri kwenye tasnia hiyo ya Vilevi! Dah. P Funk nae anapigania haki za Wasanii? Kama tukimpa Bastola ili auwe wezi wakubwa wa kazi za wasanii , akiwa Muadilifu anapaswa kujipiga bomba kwanza yeye mwenyewe!

wewe Pfunky autafute umaarufu sasa hivi kwa lipi
he was famous since back then........,he is right clouds wanafiki sana
 
just wondering why he never said so, when the man was still alive.......................................
 
Clouds ishaniboa kabisa mie nipo E.A Radio na Lady Jay D kasitisha Tamasha Lake.

hilo tamasha waliliandama saana,sasa sijui wale wengine walioahirisha
nao watakuja kuset date sawa ya hizo tarehe......,
king kong tuko pamoja EA
 
Last edited by a moderator:
'wamepanda.........wameshuka...........wanatetemeka.............sjui nini nini nini sjui itafahamika tu kama leo zamu yao kesho itakula kwao...............sio mimi jamani amesema NAYMA WA MITEGO huyo ndo aliyesema aisee'
 
Tatizo clouds wanadhani redio yao pekee ndio inaweza kuwatoa wasanii. SASA wanaanza kupotezwa na radio nyingine kama magic fm na east african radio na radio one. Walianza vizuri lakini naona vichwa vimeshajaa maji kwahiyo wasipojirekebisha haraka watapotezwa kabisa na radio nyinginezo na wasanii watawadharau. Siku zote mteja ndio mfalme na kwa radio yenu wasanii na wasikilizaji ndio wafalme. Wacheni kujifanya nyie ndie ma super power katika music industry hapa TZ. Msifikirie maslahi yenu na kupendwa kutukuzwa na kusujudiwa. ANGALIENI NDIO MNAPOTEZWA HIVYO
 
just wondering why he never said so, when the man was still alive.......................................


Hapo sasa, yeye alilitambua hilo afu akanyamaza leo Ngwea hatunae anakuja na kuropoka hovyo itasaidia nini wakati tayari kijana ameshapotea..... Kama clouds ni wanyonyaji sawa ila p funk nae mnafiki tu manake angekuwa wa maana sana kama angemwonyesha Ngwea njia sahihi wakati wa uhai wake..... Kukataza nyimbo kupigwa leo ni bure tu manake wala hatafufuka tena wamwache marehemu apumzike kwa amani!
 
Mbona ngoma za ngweair zilizotengenezwa bongo records bado zinagongwa clouds. Nmesikia kimya kimya muda si mrefu.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Ukistaajabu ya MUSA utayaona ya PFUNK, Asitafute umaaruf kwenye Misiba, Kama Ngwear alivuta mibangi na Madawa kwa sababu ya Frustration kwa Clouds, yeye nani amemfrustrate kuwa Muumini mzuri kwenye tasnia hiyo ya Vilevi! Dah. P Funk nae anapigania haki za Wasanii? Kama tukimpa Bastola ili auwe wezi wakubwa wa kazi za wasanii , akiwa Muadilifu anapaswa kujipiga bomba kwanza yeye mwenyewe!
Copyright ndo swala la msingi analosimamia P.Funk,

Nampongeza sana P.Funk na Bongo Records kwa ujumla kwa kuonyesha kuwa wanaweza kuwa dira ya kumsulubu mnyonyaji wa kazi za sanaa ya tz tena hili limeionyesha ukomavu kwani ni legally na ninahakika Kusaga na ruge wanaumia sana juu ya hili.

Kudos P.Funk,
Kudos Ludigo.


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
just wondering why he never said so, when the man was still alive.......................................

Kwasababu clouds fm wanajidai kumjali ngwea baada ya kifo while enzi za uhai wake walikua hawapigi nyimbo zake.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Ukistaajabu ya MUSA utayaona ya PFUNK, Asitafute umaaruf kwenye Misiba, Kama Ngwear alivuta mibangi na Madawa kwa sababu ya Frustration kwa Clouds, yeye nani amemfrustrate kuwa Muumini mzuri kwenye tasnia hiyo ya Vilevi! Dah. P Funk nae anapigania haki za Wasanii? Kama tukimpa Bastola ili auwe wezi wakubwa wa kazi za wasanii , akiwa Muadilifu anapaswa kujipiga bomba kwanza yeye mwenyewe!

majani amewasaidia sana akina ngwair, dark master, mabovu nk hata kuwarecordia bure.
 
Back
Top Bottom