Over confidence ya wanaume wa kikurya inanivutia

Over confidence ya wanaume wa kikurya inanivutia

Wakuu nimekaa na wakurya sehemu mbalimbali, hawa watu wamenivutia kwa confidence waliyonayo. Sio waongeaji lakini wanajiamini sana wanapofanya jambo. Hawa jamaa kila nilipokuwa nao karibu nilishuhudia wadada wengi wakijipiga vikumbo kwa kuwatamani, hii ilinifanya nijione mdogo sana na kutaka kujua kwanini wako hivyo? kuna watu waliniambia hao jamaa wamezaliwa hivyo, wengine wanasema ni urefu wao maana wengi wao ni warefu. Wakuu naomba kujua kwanini hawa jamaa wako hivyo?
mabahiliiiiiiiiiii ishiiiiii
 
Duuh kuna kamsemo kua ''akileta shombo tunatia ndimu'' nadhani ndo kametumika hapa

Ahha habar ndo hiyo me nashangaa mtu kukereka na jambo ambalo halimhusu hata mguu halafu ukichek hatujuani humu zaid kutumia id fakes ndo hata sina kaz na mtu
 
La Kairo Hotel Mwanza ni mali ya mkurya mbunge Airo.

Matajili wa Mwanza ukiacha wenyewe Wasukuma ni Wakurya kama hao kina Chambiri na Gachuma.

Dili za mkoa wa Mwanza kwa kiasi kikubwa zimeshikwa na Wakurya na ndio maana hata Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje ni mkurya.

Mkoa wowote wenye border huwezi kusema watu hawana pesa, nenda Tarime au Shirati leo ukashuhudie bila kuwa na kalenda huwezi kujuwa leo ni jumangapi wala tarehe ngapi watu wanakula good time muda wote.

Mwisho Wakurya na mkoa mzima wa Mara kiujumla ni watu wamekwenda shule kiuhakika.

Si sahihi kwa mtu ambaye hajafika Moshi wala haijui Moshi aseme wachaga ni majambazi na Wamachame hawafai kuolewa wana tabia za kuuwa waume zao. Hizi ni kauli zinazoweza kutolewa na mtu mjinga tu na ambaye amekimbia shule.

Wakhatabahu.

Mkuu lakairo sio mkurya ni mjaluo anaitwa lameck airo, pia wenje ni mjaluo. Wakurya ni Chambili, Gachuma na Peter Zakaria mwenye mabasi.
 
La Kairo Hotel Mwanza ni mali ya mkurya mbunge Airo.

Matajili wa Mwanza ukiacha wenyewe Wasukuma ni Wakurya kama hao kina Chambiri na Gachuma.

Dili za mkoa wa Mwanza kwa kiasi kikubwa zimeshikwa na Wakurya na ndio maana hata Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje ni mkurya.

Mkoa wowote wenye border huwezi kusema watu hawana pesa, nenda Tarime au Shirati leo ukashuhudie bila kuwa na kalenda huwezi kujuwa leo ni jumangapi wala tarehe ngapi watu wanakula good time muda wote.

Mwisho Wakurya na mkoa mzima wa Mara kiujumla ni watu wamekwenda shule kiuhakika.

Si sahihi kwa mtu ambaye hajafika Moshi wala haijui Moshi aseme wachaga ni majambazi na Wamachame hawafai kuolewa wana tabia za kuuwa waume zao. Hizi ni kauli zinazoweza kutolewa na mtu mjinga tu na ambaye amekimbia shule.

Wakhatabahu.

Usahihisho kidogo mkuu; Lakairo inamilikiwa na Lameck Airo Mbunge wa Rorya, sio Mkurya ni Mjaluo kwao Utegi.

Mbunge wa Nyamagana sio mkurya, ni mjaluo kwao Shirati.

Mengine yote uko sahihi.
 
Shule yako juu ya wakurya ni ndogo mno. Kama unakula chips na upo Dar, uliza mayai au hao kuku wa nyama kwa kiasi kikubwa kinatoka wapi!!!!! Wanaojua watakwambia. Ama kuhusu utajiri na biashara inaelekea upo enzi za kijerumani za kina Odemba. Tembelea Musoma, Bunda, Tarime, Mwanza kisha fuatilia ni kabila lipi wanamiliki zaidi biashara.

Poleni kwa kuibiwa ngo'mbe (i assume wewe ni mjaluo). Lakini, kumbuka kwa miaka lukuki wamasai walikuwa wanakuja kuiba ngombe hadi maeneo yenu ya ujaluoni. Ni wakurya tuu tulio-put a stop kwa hawa wamasai. Sasa tozo kidogo la ujira wetu kwa kuwalindeni na mifugo yenu dhidi ya wamasai ndiyo "mna-mind" hivi?

We lazima umefaidika na wizi wa ngo'mbe za wajaluo ,,utetezi wa kipuuzi kabisa wamasai watatoka arusha kuja kuiba ng'ombe za wajaluo rorya? Matajiri wengi wa Tarime walitajirika kwa kupitia kuwaibia wajaluo ng'ombe na mpaka leo wakuria bado wanashuka ujaluo i kuiba ng'ombe, its a very very serious matter nyie wakuria mlioenda shule ndo mnatakiwa mtafute namna ya kuwaelimisha ndugu zenu kukomesha hii tabia mbaya ya wizi inayozidi kuleta chuki kati yenu na wajaluo lakini kinyume chake ndo nyie mnaongea mzaa mnaona kama sifa vile kuwaibia ndugu zenu ng'ombe.
 
We lazima umefaidika na wizi wa ngo'mbe za wajaluo ,,utetezi wa kipuuzi kabisa wamasai watatoka arusha kuja kuiba ng'ombe za wajaluo rorya? Matajiri wengi wa Tarime walitajirika kwa kupitia kuwaibia wajaluo ng'ombe na mpaka leo wakuria bado wanashuka ujaluo i kuiba ng'ombe, its a very very serious matter nyie wakuria mlioenda shule ndo mnatakiwa mtafute namna ya kuwaelimisha ndugu zenu kukomesha hii tabia mbaya ya wizi inayozidi kuleta chuki kati yenu na wajaluo lakini kinyume chake ndo nyie mnaongea mzaa mnaona kama sifa vile kuwaibia ndugu zenu ng'ombe.

Haya Jaduong The Spit, rai yako na itifaki yote imezingatiwa. Hebu tutulize roho kidogo wakati tunawaza jinsi ya ku-tackle wizi wa mifugo.

 
Last edited by a moderator:
Nimesoma michango kadhaa humu yenye machanganyiko wa mapenzi na uchumi, nitajitahidi ku-cover michache, Makabila mengi ya mkoa wa Mara isipokuwa wajaruo hutahiriwa nyumbani kwa kisu bila ganzi na huwa ni sherehe kubwa sana ya mila nikiwemo mimi miaka mingi kidogo iliyopita nilipigwa hicho kisu cha alfajiri! kusema wakurya hawatahiri ni kosa kubwa ambalo adhabu yake ni kughecha tu! Suala la makabila Wilaya ya Tarime na jimbo ya Rorya ni tata sana kuna makabila mengi hapo mengine yamechanyika na wajaruo kiasi cha kupotea kabisa usishangae kukuta mjaruo anaitwa Ghati au Matiku! Lameck Airo na Wenje ni wajaruo lakini kwa ujumla uchumi Ukanda wa Tarime hadi Mwanza kwa sasa unashikiliwa na wakurya, angalia wamiliki wa visima karibu vyote vya mafuta kwenye hiyo barabara, maduka, ng'ombe utaelewa vizuri juu ya hili, Suala la wizi wa ng'ombe ni tata na linatusumbua sana mkoani kwetu miaka ya nyuma wamasai wa Loliondo na viunga vyake walikuwa wanavuruga mkoa mzima kwa wizi wa ng'ombe, waIkoma walioko ukingoni waliathirika sana na hili tatizo at the same time waKurya hasa Wanyabasi na Wakira walikuwa wanaiba ng'ombe sana na hivyo waIkoma kubaki hoi kiuchumi ingawa sasa tatizo limepungua sana na linaelekea kuisha hopeful tutakuwa na amani mkoa wa mara. Makabila karibu yote ya Mara ni family oriented kwa hilo ni watu wenye upendo mkubwa sana kwa familia zao so haishangazi kuwa makabila mengi sasa yanatamani kuolewa mara ni full furaha na kujiachia,
 
Back
Top Bottom