Osama bin Laden killed!

Status
Not open for further replies.
Kama Osama anauawa kama panzi, je hao masalia yake?

Njia moja tu hao. Kwanza Osama kawasumbua Marekani sababu wamemfundisha wao mbinu zote. Hawa wengine ni ubwabwa tu. Kazi moja ila utashangaa kuna wapuuzi watataka kuandamana na kumwita shujaa! Subiri uone vituko
 
Pakistan hawakuambiwa kuhusu operation hadi baada ya tukio.

Haiwezekani operation kama hiyo ifanikiwe bila baadh ya watu waaaminifu ngazi ya juu pakistan kufahamu.

Pakistan ni nchi ina waislam wengi wenye msimamamo mkali. na serikali yao haiwez kukiri wazi mchango wake. but lazima rais au kiongozi wa Jeshi la pakistan alijua hiyo. Serikali ikiri wazi wazi itapoteza support kubwa. Kumbuka sio operation yaya kufanya kijijini na imewachukua dk 41 na wanasema just three ppl died.......
 
Kifo cha Osama hakimaanishi kifo cha Al-Qaida wala Ugaidi.Moto ndio kwanza umewashwa.Kwanza Osama kitambo tu alikuwa si kiongozi tena wa Al-Qaida,wapo akina Al-Zawahir na wengineo.Halafu,Osama kama hajafa hivi.........

Hujui historia, niambie ni vita gani iliyo kuwa endelevu duniani baada ya kiongozi mkuu kukamatwa ama kuuawa? Je ni Savimbi, Amini, Hitler, Mussolin, Milambo, Mkwawa, Kinjiketile, Noriega, Garang, Bakar na wengine wengi tu! Ukipiga mchungaji lazima kondoo watatawanyika tu!
 
Mi nadhani aitwe marehem hivyohivyo kwani c watz tutajuaje kwa hilo kama ni fek or not.
 
Inawezekana
 
Tarifa za kifo cha Osama,vita vya Lilbya na vimbunga kwa kweli vinanipa harufu ya kiama.
Nahisi Marekani imepata mafanikio katika teknolojia za kijeshi lakini imezidi kuchukiwa.Matukio yanayoendelea kwenye ulimwengu wa kiislamu hatimae utawaweka madarakani watu ambao hawako tayari kushirikiana na Marekani kwa lolote.
Habari za Osama zimekuzwa sana lakini zamani waislamu walikwishamsahau katika uwanja wa vita muda ambao tumeshuhudia ongezeko la vijana waliotolea hasira zao kwa wamarekani na Nato huko Afghanistan na Pakistan na ambao wala hawakuamrishwa na Osama.
Angalia Saudia ilivyofanya kwa kushirikiana na Baharain,unadhani mfalme Abdulla ataunga mkono Marekani kupiga Libya kwa kisingizio cha kulinda raia,kumbe na yeye kafanya vile vile alivyofanya Gadhafi.Kwa upande mwengine unadhani Ali Abdulla Saleh akiondoka itakuwa rahisi kumpata raisi kama yeye wa kushirikiana na Amerika na Nato.?.
 
Umeshaambiwa ni " Conspiracy" na ziko nyingi tu kama ifuatavyo:
Obama was not born in the US
2Pac didn't die
Elvis is alive
Sadam is alive
JFK is alive
Hitler is alive
9/11 didn't happen
Mandela and Tutu are Freemasons
Nyerere died of HIV
Mama Maria killed Nyerere
Karume is in Oman and alive
Sokoine was killed by Nyerere
JK ni mgonjwa
Loliondo ni mradi wa Lowassa

......and many more....so it's up to u to either believe or shut up! Kama Osama yupo basi ajitokeze ama atoe hivyo viji-tapes vyake kulee al Jazira
 
Tuone wapambe watakuja na staili gani ya kutetea ujinga!
 

Actually Wapakistani wanadai walishiriki, Wamarekani wanasema hawakuambiwa mpaka baada ya tukio so theory yako haileti maana yoyote.

Kama Pakistan inaogopa retaliation wasingedai wameshiriki.
 
Unajua ukimiliki vyombo ya habari unamiliki na akili za watu wasiopenda kufikiri, bbc news wamesema kapigwa risasi ya kifua, jioni ya leo CNN NEWS wamesema kapigwa risasi za macho. The Sun wamesema alikuwa kalala ndani kwake elikopta ikamshambulia, habari zingine zinasema kazikwa na watu wachache baharini, Marekani walisema wanamtaka Osama akiwa hai au amekufa, Osama kauwawa usiku halafu kazikwa asubuhi. Ahahahaha..
 

Acha utani innocent people watakuwaje ktk mazingira ya uhalifu? Watakubali vipi kuwa na muuaji? Je kasisi au sheikh akikutwa kwenye danguro anaweza kujitetea kuwa alikuwa anajaribu kuwahubiria wazinzi?
 
Na picha zikatengenezwa haraka haraka.

 
Last edited by a moderator:
Wamemuua, hawajampiga picha hata moja halafu wanasema eti wamemzika baharini.
Full changa la macho.
Nilikua naamin waafrika ndio waongeaji uzushi zaidi...kumbe na nchi kubwa wamo zaidi kwa u.z.u.s....
Wapo juu kwa technology iweje asipigwe picha aonekane vizuri????
Iweje picha alipouliwa ionekane kama kuna ukungu...na hapo walikuepo baadhi ya askari/watu wengine?
Hayo maajabu ya maajabu. Sijaamin kabisa...tena tuache ushabiki si kweli.
 
Hahahaha mliozoea kuhoji hahahahaha. Una digrii ya kuhoji? Hata ivo haibadili ukweli kuwa osama kafa

Kuhusu uwezekano wa kufa sipingi lakini mimi nahisi hakufa jana bali kitambo,na kama ni jana basi alikuwa hospitali mahututi.Kifo chake kama kweli kinatumika kwa maslahi ya kisiasa .Hili kwa Marekani wamefanya mara nyingi tangu kisa cha uongo cha kwenda mwezini.

Hospitali aliyokwenda Osama kutibiwa
 
You can't fool great thinkers Straatkasyambe, do you see how Mkasika has reveal your silly post? Don't Try It again!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…