Orijino Komedi: Kwa faida ya nani?

Selous

JF-Expert Member
Jan 13, 2008
1,325
144
Shadrack Sagati
Daily News; Saturday,May 31, 2008 @00:05


Kundi la vichekesho la Ze Comedy limetangaza kuhamishia maonyesho yake katika runinga ya Taifa ya TBC1 kuanzia Julai. Wachekeshaji hao waliokuwa wakifanya shughuli zao East Africa

Television ‘Channel 5’ pia wamemtangaza Mfanyabiashara maarufu nchini ambaye pia ni mfadhili wa klabu ya Yanga, Yusuf Manji kuwa mlezi wao ambaye atakuwa na jukumu la kuwagharimia katika safari mbalimbali watakazozifanya kwa ajili ya maonyesho.

Mkurugenzi Msaidizi wa kundi hilo, Emmanuel Mgaya maarufu kama Masanja, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa kundi hilo limeingia mkataba wa mwaka mmoja na kituo hicho.

“Tunatangaza rasmi kuwa tayari tumesaini mkataba mnono na TBC1…kwa kweli ni mkataba wa heshima na unajitosheleza ndio maana tumeamua kufanya kazi na kituo hicho,” alisema Masanja jana.

Kitendo cha wachekeshaji hao kumtangaza Manji kama mlezi wao kinaweza kuzusha hisia mbalimbali miongoni mwa wapenzi wao hasa kutokana na uhasama wa kibiashara uliopo kati ya Manji na Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi.

Hata hivyo wasanii hao wameweka bayana kuwa wao ndio waliomwomba Manji awe mlezi wao na suala hilo halihusiani na chuki za kibiashara zilipo kati ya mlezi huyo na Mengi ambaye ndiye mmiliki wa Channel 5 kupitia Kampuni ya IPP.

Masanja alisema wamemteua Manji kuwa mlezi wa kundi lao kutokana na kuamini kuwa busara na umri wake atawalea vyema kama ambavyo amekuwa anafanya kwa klabu ya Yanga ambayo tangu atangaze kuifadhili imekuwa yenye mafanikio.

“Tumeona mafanikio yake akiwa na Yanga kwa hiyo tunaamini kuwa sisi kundi la watu saba hatashindwa kutulea,” alisema Masanja na kuongeza kwa kuanzia wiki ijayo wataenda Afrika Kusini kwa ajili ya mafunzo zaidi ya sanaa za uchekeshaji na safari hiyo itagharimiwa na mlezi huyo.

Naye muongozaji wa kundi hilo, Sekion David, Seki akizungumzia mkataba wake na TBC1 alisema kuna mambo mengi ambayo yameongezeka katika mkataba wao na kituo hicho. Mojawapo ni kuwekewa bima ya kutibiwa wao na familia zao wakati wote watakuwa ndani ya mkataba huo.

“Unajua Ukimpiga teke Chura umemwongezea safari,” alisema Seki ambaye kwa maelezo yake alisisitiza kuwa kulikuwa na uhuru mkubwa katika kuandaa mkataba huo “Tulikuwa huru na mambo tuliyokubaliana ni ya msingi.”

The Comedy ilisitisha kuonyesha vichekesho vyake katika Channel 5 baada ya mkataba wao kumalizika. Kundi hilo limesema tangu wasitishe maonyesho wamekuwa wakipigiwa simu nyingi na kutumiwa barua pepe zinazowataka warejee kwenye uwanja wa sanaa.
 
Jamani hapa ni siasa au akili ndogo au niseme nini? Kimsingi kwangu hili kundi halina maana tena
 
Jamani Si Wanaangalia Maslahi Au??????????kuna Mtu Anaetaka Kushibisha Wafiwa Huku Maiti Aijulikani Inaperlekwa Kijijini Lini!!!!hongereni Wakubwa Kama Kweli Nkataba Ni Nnono Kuliko Eatv....najiuliza Tu Kama Wameweza Kununuliwaa Kirahisi Kwa Sababu Ya Hela Je Wataweza Kuendelea Kuikemea Serikali Ya Chama Cha Majambazi Wakati Mmiliki Wa Television Ndie Jambazi Huyohuyo Jamani Tutafika Kweli Mh..angalien Maslahi Na Maisha Ya Watanzania Pia......
 
hilo la kwenda sauzi kuongeza ujuzi mie kwa kweli nawapongeza its a great step ahead kwa maisha yao ya kisanii...but how cud they do it bila kutafuta mlezii??
ila la kutoa kwa mengi kuingia kwa manji...mwee letswait wakianza maigizo yao mayb tutashuhudia more evil things za dat other side ya mheshimiwa
 
Duh! Mwanakijiji alisema kule klhnews kumbe kweli. tunataka kuona matendo ya kifisadi yakionyeshwa kama ilivyo kuwa kule EATV vinginevyo nanyi mtakuwa mmeingia katika mtandao wa kifisadi na mtakosa heshma katika jamii tena katika umri mdogo mlionao, itakuwa aibu kubwa.
 
Jamani hapa kinacho angaliwa ni masirahi na wao wameona hilo ndo maana TBC1 wamefika dau kubwa....lakini naona watu wanaona kama wamecheza dili chafu na Manji wao wandai wamemwomba awe mlezi wao na yeye kakubali sasa nn watu mnashobokea??mbona Yanga anamwaga mihela na hamsemi kule analea mafisadi..
Tunataka watu wenye mioyo ya kuendeleza vipaji kama hawa wafadhiri...wafadhiri wengine uchwala tu wanaangalia masirahi yao binafsi.
 
Kila mtu nadhani anajaribu kutafuta maisha bora ama kuyaona maisha yake katika mwanga bora, nawapongeza ze comedi katika hili ni jambo la busara sana na naamini itawa ni hatua ya maendeleo kwao na kwa sanaa ya uchekeshaji katika Runinga Tanzania.

Lakini suala la kuangalia hapa ni je hawa ze komedi wamenunulika ama wameingia mkataba mpya. Dira na Mwelekeo wa yale mazuri na mabaya kidogo waliyofanya walipokuwa pale EATV wataendeleza wakiwa katika Television Station inayomilikiwa na Mafisadi. Hilo ni jaribio kuu ambalo ndugu zet uwa Ze Komedi watatakiwa walivuke na kututhibitishia watanzania kwamba wao ni wakweli wenye mioyo ya Kimapinduzi!
 
Hapo ni nguvu ya UZALENDO vs MIFEDHA mwamuzi akiwa SIRIKALI. Kudadadeki, mshindi lazima ajulikane mapemaa!!!.
 
guys lets wait n see kasi watakayoturudia nayo hewani...if wakiwa hawaongelei masuala ya kuponda serikali kwenye ma burekiiiiing nyuuuuziii yao basi tutajua fika walifanywa mnada elsewise ni jus one of the moves towards kutafuta maisha bora kwa kila mmoja wao jamani hiyo ni fani yao n wanajaribu kujenga maisha yao
 
Manji ajitosa Ze Comedy

Shadrack Sagati
Daily News; Saturday,May 31, 2008 @00:05


Kundi la vichekesho la Ze Comedy limetangaza kuhamishia maonyesho yake katika runinga ya Taifa ya TBC1 kuanzia Julai. Wachekeshaji hao waliokuwa wakifanya shughuli zao East Africa

Television ‘Channel 5’ pia wamemtangaza Mfanyabiashara maarufu nchini ambaye pia ni mfadhili wa klabu ya Yanga, Yusuf Manji kuwa mlezi wao ambaye atakuwa na jukumu la kuwagharimia katika safari mbalimbali watakazozifanya kwa ajili ya maonyesho.

Mkurugenzi Msaidizi wa kundi hilo, Emmanuel Mgaya maarufu kama Masanja, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa kundi hilo limeingia mkataba wa mwaka mmoja na kituo hicho.

“Tunatangaza rasmi kuwa tayari tumesaini mkataba mnono na TBC1…kwa kweli ni mkataba wa heshima na unajitosheleza ndio maana tumeamua kufanya kazi na kituo hicho,” alisema Masanja jana.

Kitendo cha wachekeshaji hao kumtangaza Manji kama mlezi wao kinaweza kuzusha hisia mbalimbali miongoni mwa wapenzi wao hasa kutokana na uhasama wa kibiashara uliopo kati ya Manji na Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi.

Hata hivyo wasanii hao wameweka bayana kuwa wao ndio waliomwomba Manji awe mlezi wao na suala hilo halihusiani na chuki za kibiashara zilipo kati ya mlezi huyo na Mengi ambaye ndiye mmiliki wa Channel 5 kupitia Kampuni ya IPP.

Masanja alisema wamemteua Manji kuwa mlezi wa kundi lao kutokana na kuamini kuwa busara na umri wake atawalea vyema kama ambavyo amekuwa anafanya kwa klabu ya Yanga ambayo tangu atangaze kuifadhili imekuwa yenye mafanikio.

“Tumeona mafanikio yake akiwa na Yanga kwa hiyo tunaamini kuwa sisi kundi la watu saba hatashindwa kutulea,” alisema Masanja na kuongeza kwa kuanzia wiki ijayo wataenda Afrika Kusini kwa ajili ya mafunzo zaidi ya sanaa za uchekeshaji na safari hiyo itagharimiwa na mlezi huyo.

Naye muongozaji wa kundi hilo, Sekion David, Seki akizungumzia mkataba wake na TBC1 alisema kuna mambo mengi ambayo yameongezeka katika mkataba wao na kituo hicho. Mojawapo ni kuwekewa bima ya kutibiwa wao na familia zao wakati wote watakuwa ndani ya mkataba huo.

“Unajua Ukimpiga teke Chura umemwongezea safari,” alisema Seki ambaye kwa maelezo yake alisisitiza kuwa kulikuwa na uhuru mkubwa katika kuandaa mkataba huo “Tulikuwa huru na mambo tuliyokubaliana ni ya msingi.”

The Comedy ilisitisha kuonyesha vichekesho vyake katika Channel 5 baada ya mkataba wao kumalizika. Kundi hilo limesema tangu wasitishe maonyesho wamekuwa wakipigiwa simu nyingi na kutumiwa barua pepe zinazowataka warejee kwenye uwanja wa sanaa.
 
Ya kweli haya? Au Manji kawapa hiyo mistari waitamke hadharani? Huo mkataba waliosaini na TBC hauwezi kugharamia safari wanazotaka kuzifanya? Kundi la wachekeshaji linatakiwa liwe huru ili kuweza kumuingiza yeyote yule katika vichekesho vyao bila kuwa na wasi wasi. Hichi kitendo cha kumkubali Manji kama mlezi wao kinaashiria kwamba Ze comedy hawatamgusa Manji.
 
Manji ni adui namba moja wa Mengi ambae alikuwa mmiliki wa EATV naona Manji katake advantage hapo.Lakini Mengi mnyonyaji sana kwa watumishi wake!
 
hawa vijana njaa inawasumbua, lakini hawamjui manji, atawatumia kutafuta umaarufu, akishaupata anawaacha njia panda, kama alivyowaacha yanga wakati ule. waha waajemi hawana jema na watu wetu, kwao watu wetu ni madaraja ya kuwavusha kutimiza malengo yao. after all nani angewahamu akina ze comedy kama siyo EATV?
 
Ya kweli haya? Au Manji kawapa hiyo mistari waitamke hadharani? Huo mkataba waliosaini na TBC hauwezi kugharamia safari wanazotaka kuzifanya? Kundi la wachekeshaji linatakiwa liwe huru ili kuweza kumuingiza yeyote yule katika vichekesho vyao bila kuwa na wasi wasi. Hichi kitendo cha kumkubali Manji kama mlezi wao kinaashiria kwamba Ze comedy hawatamgusa Manji.

Jamani eee hawa wenzetu walikuwa wanahitaji mtu wa kuwawezesha, sasa amejitokeza mmoja. Kwanini tunaanza kuangalia what negatives tunaweza kupata katika mafanikio ya watu.
Manji ni mwananchi aliyejitokeza kuwafadhili hawa, tunapaswa kumshukuru kwa kuwawezesha watu wanaoipa burudani jamii.
Kwani wewe unatarajia ze comedy watengeneze vichekesho vya kumhusu kila mtanzania??? how much time will that take. So why should it be touching if Manji will be left aside?
 
hawa vijana njaa inawasumbua, lakini hawamjui manji, atawatumia kutafuta umaarufu, akishaupata anawaacha njia panda, kama alivyowaacha yanga wakati ule. waha waajemi hawana jema na watu wetu, kwao watu wetu ni madaraja ya kuwavusha kutimiza malengo yao. after all nani angewahamu akina ze comedy kama siyo EATV?

That is reciprocal relationship, wao wanapata mlezi na Manji anapata umaarufu au kingine anachohitaji kwenye huo uhusiano.Au ulitegemea Manji asinufaike na ulezi wake kwa ze comedy?

Na ukweli ni kwamba ukiona uhusiano uliokuwa na manufaa kwako hauna tena manufaa hayo, basi hakuna haja ya kubakia na uhusiano huo.

Ze comedy wana akili timamu na wanajua wanachofanya, wameona wanaweza kukipata toka kwa Manji - waacheni waendelee na waombeeeni mafanikio!
 
Jamani eee hawa wenzetu walikuwa wanahitaji mtu wa kuwawezesha, sasa amejitokeza mmoja. Kwanini tunaanza kuangalia what negatives tunaweza kupata katika mafanikio ya watu.
Manji ni mwananchi aliyejitokeza kuwafadhili hawa, tunapaswa kumshukuru kwa kuwawezesha watu wanaoipa burudani jamii.
Kwani wewe unatarajia ze comedy watengeneze vichekesho vya kumhusu kila mtanzania??? how much time will that take. So why should it be touching if Manji will be left aside?

Manji ni fisadi na kuna tuhuma mbali mbali zinazoonyesha amehusika katika kuwapa mapesa viongozi wa juu wa CCM yeye pamoja na Jeetu Patel na yule Subash. Na hata katika kutafuta mgombea wa CCM mwaka 2005 alikuwa mstari wa mbele kugawa mabilioni ya shilingi katika kinyang'anyiro kile.
 
Manji ni fisadi na kuna tuhuma mbali mbali zinazoonyesha amehusika katika kuwapa mapesa viongozi wa juu wa CCM yeye pamoja na Jeetu Patel na yule Subash. Na hata katika kutafuta mgombea wa CCM mwaka 2005 alikuwa mstari wa mbele kugawa mabilioni ya shilingi katika kinyang'anyiro kile.

Ze comedy ni kikundi cha burudani! Tujaribu kuweka siasa pembeni wakati mwingine.
 
Siku zote nilikua naamini kwamba ili hawa jamaa waendelee kufanya kazi zao katika mazingira huru ingekuwa ni vizuri wakaendelea kuwa na mkataba na kituo binafsi cha television, tusitegemee tena kuona blunders za viongozi wa serekali na CCM zikiigizwa na hawa jamaa huko TBC. You cant take the mickey out of your employers.
 
Siku zote nilikua naamini kwamba ili hawa jamaa waendelee kufanya kazi zao katika mazingira huru ingekuwa ni vizuri wakaendelea kuwa na mkataba na kituo binafsi cha television, tusitegemee tena kuona blunders za viongozi wa serekali na CCM zikiigizwa na hawa jamaa huko TBC. You cant take the mickey out of your employers.

Thank you KKN! Unajua watu hawalioni hili. US kuna kipindi cha kuchekesha Satuday Night Live ambacho kiko huru na kinaweza kikaandaa vichekesho vya yeyote yule toka Republican au Democratic bila kuwa na wasi wasi wowote. Kwa sababu wachekeshaji hao wako huru katika kuamua waandae vichekesho vya aina gani.

Sasa hawa Ze comedy kwa kujihusisha na Manji basi wameshapoteza uhuru waliokuwa nao. Manji akiwaambia kwamba sitaki muandae vichekesho vya fulani na fulani basi hawatakuwa na ubavu wa kufurukuta na kufanya vinginevyo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom