BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,377
- 8,121
MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Omary Mwanga, maarufu Marioo, anayedaiwa zaidi ya Sh. milioni 500 kwa kuvunja mkataba, anatarajiwa kujitetea Mahakama Kuu Machi 18 na 19, mwaka huu.
Marioo na Meneja wake Sweetbert Mwinula wameshtakiwa katika Mahakama Kuu Masjala ya Wilaya ya Arusha mbele ya Jaji Joackim Tiganga, wakidaiwa jumla ya Sh. 550,000,000 kwa madai ya kuvunja mkataba wa kutumbuiza katika hafla ya Mr & Miss Vyuo Vikuu Kanda ya Kaskazini.
Mdai katika shauri hilo ni Kampuni ya Kismaty inayojihusisha na kuandaa matukio ya burudani mbalimbali nchini.
Mdai anayewakilishwa na Wakili John Lairumbe, anadai kuwa Septemba 23, 2021, aliingia mkataba na wadaiwa kutumbuiza siku ya mashindano hayo kwa gharama ya Sh. milioni 15.
NIPASHE