Open Letter: Rais Samia, TRA isiyo na Support yako, ni Kifo cha Taifa

Tuelewe spirit ya Rais kuhusu kodi ni kuwa wigo wa kodi upanuliwe na wawe wabunifu. Lakini pia falsafa ya Rais ni kuwa ukusanyaji wa kodi ufanyike kwa weledi na ufasaha bila kubambakiza kodi na kuwanyanyasa wafanya biashara ambao baadhi wamekimbia nchi na kufanya uchumi kusinyaa. Hivyo, watu wasipotoshe nia njema ya Rais.

Kitendo cha kuchukua mali au fedha za mfamya biashara benki ni kinyume na lengo zuri la ongeza mtaji, ongeza biahara na ongeza kodi (OMOBOK) ILi kuleta maendeleo ya dhati.

Rais yuko sahihi walipa kodi wabadilishe "mindset" zao kuhusu kodi na biashara. Wafanya biashara ni partners wao. Wabadilishe mbinu km ambavyo ukaguzi wa mahesabu walipo kuja na njia mbinu mpya.

Watoke kwenye enforcement ya kuharasss(reactive) kwenda kwenye proactive. Hii ni pamoja na kuelemisha na kujenga mitizamo chanya na endelevu ya kulipa kodi kuliko sasa. Itafika mahala kodi za nguvu zitakwama kabisa zaidi ya kuendekeza kazi. Kamishna Mkuu wa TRA ana kazi kubwa ya kubadilisha mitizamo na mbinu za utendaji wa watu wake,mifumo ya ufuatiliaji na ushirikishwaji wa jamii badala ya kukaa ofisni na kucheza na makaratasi bila kuzingatia uhalisia wa biashara vinginevyo hakuna mwekezaji atayekuja. TRA msaidie mama acheni kutumia mbinu zilezile katka mazingira mapya.

Rais Hayati Mgafuli aliwahi pia kulionya hili la kunyanyasa wafanya biashara na kupelekea Kichere kamishna mkuu wa wakati ule kumwondoa madarakani.

Kuhusu kusemea hadhara masuala ya kodi badala ya vikao vya ndani, Rais hafundishwi namna ya kusema so fa masuala ya kisera na maelekezo hutolewa hadhara ili kuweka uwazi.

Kimsingi zingatieni maelekezo ya Rais vinginevyo tunahitaji -total transformation sekta ya kodi. Hata hivyo-Wito -wafanya biashara walipe kodi
Labda nikuulize swali mkuu,umetumia njia zote za kiungwana ili mfanyibiashara alipe kodi na halipi,what do you do,a straight answer please.

Unajua,nilitegemea Rais asisitizie juu ya umuhimu wa wafanyibiashara kulipa kodi kama sheria inavyowataka kufanya.Then nilitegemea aseme kwamba kwa mfanyi biashara yeyote ambaye hatapenda kulipa kodi kwa hiari,sheria itachukua mkondo wake,kwa kuwa zipo sheria.

Mkuu huwezi kumbembeleza mfanyibiashara asiyetaka kulipa kodi kwa hiari.Ukimbembeleza hata lipa.Lazima sheria zimbane ili alipe.
 
Watu waliomshauri kuhusu hili swala wana nia ya kumkwamisha..na hakika atakwama kama hatarudi nyuma.
mnapenda mapato yasiyotokana na uhalisia.Mapato yanayotokana na faini au mapatano na DPP hayalipeleki taifa mbali na hayaonesha uhalisia wa uchumi tulio nao.Mapato halisi na endelevu ni yale yanayotokan na shughuli za kiuchumi,biashara,maduhuli,utalii,matumizi binafsi ya watu.
 
Miaka mitano ya Magufuli atujaona IMF wala WB kuja kukutana na wizara ya fedha kisa wasiwasi wa nchi kuweza kulipa madeni yake kutokana na makusanyo madogo ya kodi kama ilivyozoeleka zama za JK. If anything walikuwa hawana shida kumkopesha.

Huko baadae mambo yakienda mrama wasitafute mchawi mwingine Magufuli sijui alikopa sana, la hasha matatizo haya wakubali tu huko mbele wameyatengeneza wao.
Kwa hiyo tangu mliopanza kukusanya kodi kwa njia kandamizi deni la taifa limeshuka kwa % ngapi?
 
Wewe si lolote zaidi ya mpigania legacy, wewe ni genge tu wala TRA hawawezi kuandika utopolo uliouandika hapo. Ulikuwa unaona raha sana watu kufunga biashara na kuwa masikini kama wewe ,unaposikia hali ya hewa nzuri inakuja upande wao ndipo sasa roho yako mbaya inakuuma.

Mama Samia hakutoa maelekezo ya kuacha kulipa kodi,, kama TRA hawakusanyi kodi huo ni udhaifu wao na wanapaswa kuwajibishwa.

Ila nakufahamu msimamo wako umekaa upande wa kutetea ule ukatili uliokuwa unakulisha wewe na familia yako.
Uovu wenu wa kunyanyasa watu umekwisha,, nenda katubu umrudie Muumba wako.
Ww utakuwa likwepa kodi
 
Mhe Rais, naomba utumie dakika chache kusoma barua hii wewe mwenyewe, na kama hautapata muda naomba wasaidizi wako wakusaidie kuusoma na kukufikikishia.

Naandika haya kama Raia aliye na wasiwasi baada ya kutafakari kwa kina juu ya "TONE" yako uliyokwishaitoa hadharani kuhusu taasisi hii nyeti inayokusanya mapato ya nchi.

Pia ni baada ya kukaa na baadhi ya maafisa kodi ambao wanakiri kwamba toka kauli yako kazi yao imekuwa ngumu kupindukia ni kama wamewekwa benchi !!

Mhe. Rais, kwa sasa kuna mambo makuu mawili yanayotokea ambayo sidhani kama umeshayajua.

i) Wafanyabiashara wameacha kutoa risiti za EFD na ukiwadai wanasema kabisa WASISUMBULIWE maana Rais wao ameshatoa maelekezo hayo. Wapo HOLIDAY!!.

Hata TRA wenyewe wamecancel mazoezi ya ku-enforce utoaji risiti. Maana wanajua wakienda watabagazwa!

Swali kubwa hapa, Je, Kodi gani itakusanywa na nchi bila watu kutoa risiti? Unawezaje kutrack mauzo ya mlipa kodi bila kutoa risiti ya EFD?

ii) Wafanyabiashara hawapeleki tena malipo ya kodi kwa kama kasi ya awali, kila mmoja ameset mind ya kupinga kodi maana anaona kama kile alichokadiriwa si sahihi baada ya kauli ya Rais.

Wataalam wenyewe wanasema impact yake itaonekana katika taarifa za mapato mwezi huu na ijayo!.

Mhe Rais, katika taasisi zote chini yako zinazohitaji Top Level Presidential Support ya moja kwa moja ni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Bila TRA yenye support ya Rais, Taifa linakufa, na hakika litashindwa kufikia malengo yake.

Ni sawa na katika taasisi za kawaida, kitengo ambacho kinaleta mapato kwa taasisi, ndicho Mkurugenzi Mkuu hukitolea macho na kukipa support yote inayohitajika ili aweze kufikia malengo yake kibiashara.

Mhe Rais, sitaki kurejea katika maagizo yako ya nyuma kuhusu namna TRA wanavyofanya kazi ambayo uliyatoa hadharani, ila ningekuwa mmoja wa washauri wako ningeshauri usiongee sentensi zile hadharani bali uongee moja kwa moja na Viongozi na Wafanyakazi wa TRA indoors.

Kwa nini??. Kwa sababu nature ya mfanyabiashara ni kulalamika na kuficha mapato yake halisi. Hakuna mfanyabiashara hata mmoja aliye genuine ya kipato chake, Popote duniani. Hakuna!

Mhe. Rais, unaweza kukuta mfanyabiashara anafanya biashara yenye mauzo ya Billioni 2 anadeclare faida ya milioni 4, Seriously?

Katika mazingira hayo unahitaji Taasisi yenye nguvu na mamlaka ili iweze kutafuta wapi mtu huyu alipodanganya ili Serikali iweze kukusanya kodi yake. Otherwise, utachukua hio hio Milioni 4 alafu maisha yanaendelea wakati kwa hakika labda mtu huyo alipaswa kulipa milioni 50.

Mwisho:
Natambua kupitia maneno ya Makamu wako, Mhe. Mpango, umeweka malengo ya Trillion 2 kwa Mwezi, lakini ukweli ni kwamba hata kama sheria zitabadilika na baadhi ya kodi kupungua lazima kuna nyingine zitapanda ili kufikia lengo la Trillion 2. Sasa nani atatumika kuenforce ukusanyaji huo? Je ni hao hao TRA? Je wataweza ku-enforce huo ukusanyaji bila support yako? Au kuna watu wanaku-sabotage ili ushindwe kufikia malengo hayo?.

Naomba kuhitimisha kwa kukushukuru kwa muda wako.

Wako,
Raia aliye na wasiwasi.
15 April, 2021



Nyongeza muhimu kutoka kwa baadhi ya wadau
Hata aliyeandika uzi huu ni mtumishi wa TRA asie na weledi au mnufaika wa rushwa katika task force
 
Biashara ni hesabu ya kilichoingia, kilichopo dukani /stoo na kinachouzwa.
Hesabu ipo wazi mtu asipotoa stakabadhi ya manunuzi,TRA wataangalia stock na nini mtu huyo aliagiza ili waoanishe na kodi.
TRA kwa sasa wajikite na stock za wafanyabiashara na nini wanaagiza kina thamani gani /kinauzwaje ikiwezekana kutoa bei elekezi kwa wananchi.
Mali bila daftari hupotea bila Habari, Muheshimiwa Raisi wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi
 
Kodi za dhuluma hazina baraka! Unaweza nunua ndege kwa kodi za dhuluma na hayo mandege yasiruke na kuleta hasara au ukatumia kodi za dhuluma kujenga bwawa la umeme na mito ikakauka na bwawa likaishiwa maji ikawa Ni hasara ya ajabu...
 
Kwa hiyo tangu mliopanza kukusanya kodi kwa njia kandamizi deni la taifa limeshuka kwa % ngapi?
Swala sio deni kushuka au kupanda ni kuaminika na wakopaji unaweza lipa madeni yako. Sio unakopa hata kama deni lako dogo, halafu kila siku unachelewesha malipo, hakuna mtu atakupa hela yake kirahisi.

IMF Magufuli alipoanza walikuwa wagumu kutoa hela yao, ikabidi Dr Mpango kwenda NY kukutana na ‘Paris Club’ kutafuta mikopo yao. Ni kupitia kukua kwa makusanyo ya ndani IMF wenyewe wakarudi kujipendekeza kuikopesha Tanzania.
 
Mali bila daftari hupotea bila Habari, Muheshimiwa Raisi wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi
Na Jambo la kujifunza nchi ziliizoendelea kodi zinakusanywa in a very professional way na hakuna intimidation zinazodiscourage investment, mama yupo 100% perfect kwenye hili kurestore investors confidence, business community ni partners katika development sio maadui, ukiwaua mayai endelevu utapata wapi?, kuna fursa kibao za kodi wajaexplore wanakamua waliopo mpaka damu, unaenda kumdai mtu ana lodge 1.2 bn means ameingiza gross profit 12 bn annually, logically is it possible? Mimi ningetamani wafanyabiashara waliofanikiwa wangekua kwenye TRA BOARD of Directors
 
H
Biashara ni hesabu ya kilichoingia, kilichopo dukani /stoo na kinachouzwa.
Hesabu ipo wazi mtu asipotoa stakabadhi ya manunuzi,TRA wataangalia stock na nini mtu huyo aliagiza ili waoanishe na kodi.
TRA kwa sasa wajikite na stock za wafanyabiashara na nini wanaagiza kina thamani gani /kinauzwaje ikiwezekana kutoa bei elekezi kwa wananchi.
hesabu za kodi haziendi kwa mfumo wa namna hii mkuu.
 
Ww utakuwa likwepa kodi
Nalipa kodi yote vizuri bila kuchelewesha.
Hilo ondoa shaka, na hata TRA nilifanikiwa angalau walanikadiria vizuri hata enzi zile za mateso hivyo kwa upande wangu nalipa vizuri bila matatizo.
Lakini kuna majirani zangu hapa wanabaki kusema mbona huyu hamjamfanyia ivyo?? Kwakweli bado wanaumia.
 
Na Jambo la kujifunza nchi ziliizoendelea kodi zinakusanywa in a very professional way na hakuna intimidation zinazodiscourage investment, mama yupo 100% perfect kwenye hili kurestore investors confidence, business community ni partners katika development sio maadui, ukiwaua mayai endelevu utapata wapi?, kuna fursa kibao za kodi wajaexplore wanakamua waliopo mpaka damu, unaenda kumdai mtu ana lodge 1.2 bn means ameingiza gross profit 12 bn annually, logically is it possible? Mimi ningetamani wafanyabiashara waliofanikiwa wangekua kwenye TRA BOARD of Directors
Nchi zilizoendelea ndio Kuna Kodi kubwa kuliko kawaida na tena ndio nguvu unatumika Sana. Unakumbuka kilichomkuta Messi na Ronaldo mahakamani?
Huku Africa kwenye Kodi bado Sana, watu wanaonewa huruma sana
 
Tax base ya TRA ni ndogo sana,
Nchi hii watu wengi wapo vijijini lakini ukweli ni kwamba vijijini zipo biashara nyingi tu ambazo hazijasaliwa na TRA,

TRA wanapaswa wasikae maofisini waende vijijini wakasajili watu,waige mfano wa makampuni ya simu,

TRA wanapopewa target ya makusanyo ya 2trln wanachojua wao ni kuwapandishia watu kodi badala ya kuongeza wigo wa wa kodi.

Halafu ukweli ni kwamba nguvu waliopewa TRA awamu ya tano wamejineemesha Sana kwa rushwa kubwakubwa utawala huu hawa jamaa wametajirika sana kwa rushwa ,

Ninamashaka muandishi wa makala hii ni mfanyakazi wa TRA anaetetea tumbo lake.

NOTE
Ikifika mahali ukaona mfanyabiashara anafikia maamuzi yakuhamisha biashara zake nje ya nchi anaikimbia nchi yake haya sio maamuzi rahisi sana lazima TRA itakua na tatizo lazima wajirekebishe.
 
Najua ni mtumishi wa TRA,lakini ni kweli kwamba huwezi kumbembeleza mfanyibiashara asiyetaka kulipa kodi.Uta-coerse to some point,lakini akikataa ni lazima alazimishwe na sheria kufanya hivyo.
Nilishawashauri TRA mambo mengi kama mzalendo ili wasipoteze kodi, mfano kodi ya matangazo ya biashara ilipohamishwa kutoka local Government, trucks za Coca-Cola, TBL na Bakhresa to mention few walipandua mabango yote baada ya TRS kugoma kuwa flexible kupokea fixed annual rates, matokeo yake wakakosa kabisa, second niliwahi kuwashauri kupendekeza sheria ya kuruhusu wenye Magari yenye namba za zamani kuhuwisha kwenda namba mpya, mfano A kwenda D huku ukudelete old number kwenye mfumo kwa ada say 500,000 Tshs, wangepata pesa nyingi tena widely nk nk
 
Nchi zilizoendelea ndio Kuna Kodi kubwa kuliko kawaida na tena ndio nguvu unatumika Sana. Unakumbuka kilichomkuta Messi na Ronaldo mahakamani?
Huku Africa kwenye Kodi bado Sana, watu wanaonewa huruma sana
Mimi nimeishi Netherlands 5 years na nimekua nikilipa PAYE Kule TRA inaitwa Belasting Dienst, na nimetembelea 9 countries across Europe, hata police customer care ni kama upo 5 Star Hotel, tatizo la waajiriwa wengi wa Idara za Serikali ni lack of exposure na kukazania GPA
 
Back
Top Bottom