Fahamu tu jambo moja CDM tuna watu nyeti kila mahali.CDM ni Taasisi kubwa sana.CDM ina intelejensia yake ambayo kila kinachofanywa sirini tunakijua kupitia mfumo wetu wa usalama.
Ndiyo maana tunajua na tunasema bila kupepesa jicho kwamba ACT ni Tawi la CCM ambalo limeanzishwa mahsusi kupambana na CDM na nguvu ya Ukawa kwa ujumla.
Ndiyo maana hata wafuasi mkipiga porojo hapa namna gani mnapoteza tu muda.Tunawafahamu viongozi wa hiki Chama mpaka pesa wanayoitumia wanapata wapi.
Tulishafunga ukurasa kwamba hiki chama cha ACT hakina tofauti yoyote na CCM.Na tutatembea kila kona ya nchi kuwaambia Watanzania Ukweli kwamba wakiogope hiki chama kama Ukoma.
Sasa wewe mwanachama wa CDM uliyefunga ukurasa wa ACT, unafanya nini humu kwenye mada ya Zitto, ambaye ni Kiongozi wa ACT, anayehubiri sera za ACT?huoni huu ni undumilakuwili?
Wewe umekuwa nani kuwaambia watanzania kitu gani wakiogope na kitu gani wasikiogope?kwa nini usiwaachie wao hiyo kazi ya kujua kipi ni kizuri na kipi ni kibaya kwao? Hujui kuwa trait za kuwa-manipulate watu kuwalazimisha wakipende au kukichukia kitu flani zinatoka kwenye elements za udikteta?
Eneza sera za CDM, mimi binafsi naamini ni nzuri sana, na zinatosha kushawishi watanzania wengi kujiunga na CDM au kuwa nyuma yao. Lakini siamini kuwa CDM litakuwa Chaguao Pekee la watanzania. kwani hata kwenye nchi zisizo na matatizo kama TZ wananchi wao bado wanapenda vyama tofauti vya siasa.
kama ACT ni chama bomu, hakuna atakayewafuata, kama CCM haitakiwi, kura zitaonesha hilo. Unachokionesha wewe, ni kuwa ili Tanzania Demokrasia iwepo, basi CDM iachiwe iwe chama pekee cha upinzani,REALLY? ndio siasa za wapi hizi? CDM haitakiwi kupinga ujaji wa vyama vyengine vya upinzani,inatakiwa kusapoti hali hii. kwani kuna maeneo CDM haina ushawishi, vyama vya upinzani vilivyobaki vinashinda maeneo hayo na kurudisha ushawishi kwenye upinzani. Miaka nenda rudi mmeshindwa kuwa na ushawishi Zanzibar, CUF wamefanikiwa hadi kuunda serikali, sijawasikia wakisema CDM wako zanzibar kuwapunguzia kura zao hata siku moja, wanamini wana ushawishi na watashinda.
CUF inaonekana ni chama thabiti na chenye mtazamo chanya kushinda CDM kwenye demokrasia kuliko nyie.
Solace pekee iliyobaki ni kuwa wewe ni mshabiki tu, na unachoamini sio wanachoamini viongozi wako, kama wanaamini kwenye ujima wa aina hii, basi political doomsday yao inakaribia.