Maofisa wengine mikoani wanakua miungu kwa kujiwezesha kimapato hadi wanadharau utawala. Naibu waziri ni kiongozi inabidi kumtii sio kupimana nae nguvu.OFISA Mifugo Manispaa ya Shinyanga, Dk. Velan Mwalukwa, ametiwa mbaroni kwa kumtolea lugha chafu Mbunge wa Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, na Ajira.
Ofisa mifugo mbaroni kumkashifu Naibu Waziri Katambi
OFISA Mifugo Manispaa ya Shinyanga, Velan Mwalukwa, ametiwa mbaroni kwa kumtolea lugha chafu Mbunge wa Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, na Ajira.www.ippmedia.com
Cha kujiuliza ni Bwana Katambi kamuita huyu Mzee mbele ya kadamnasi kumuhoji kama Nani na kwa mamlaka gani?,
Mkutano ulikuwa ni wa wa Serikali au Mkutano wa Kisiasa wa mbunge?
Kama wa kiserikali Je Naibu waziri (Tena asiye na dhamana na mada husika) akihisi kutoheshimiwa anaweza kuagiza Askari kumkamata raia?
Kama wa Mbunge, je mbunge anaweza kumuita na kumuhoji Mtumishi kwa tuhuma tu, na wasipoelewana kuagiza askari wamkamate?
Kwa nini asipeleke malalamiko kwa Mamlaka ya kinidhamu ya Daktari huyo?
View attachment 1859868View attachment 1859876
Bwana Mwalukwa ni huyu hapa pia:
Namtazama CV yake huyu Daktari nabaki kujiuliza huyu Mzee kwa taaluma yake na uzoefu wake miaka kadhaa serikalini ndo ambaye hajui heshima kwa viongozi au amekuwa provoked. Kwa tabia za Katambi za kupenda kuminyana nina mashaka na hii ishu.
MBUZI 47 WAMEDAIWA KUFA KWA KULA MAJANI YENYE SUMU KUTOKA MACHUNGANI ENEO LA JESHI
Mbuzi 47 wenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni mbili mali ya bwana Sleyo Rashidi mkazi wa mjini Shinyanga, wamedaiwa kufa kwa kula ...shinyanganews.blogspot.com
KANGE LUGOLA AKIFUNGA KIWANDA CHA PUNDA SHINYANGA
Naibu waziri wanchi ofisi ya makamu wa Rais Muungano na Mazingira Kange Lugola, amekifunga kiwanda cha kuchinja Punda cha Fang Hua kilich...shinyanganews.blogspot.com
Maofisa wengine mikoani wanakua miungu kwa kujiwezesha kimapato hadi wanadharau utawala. Naibu waziri ni kiongozi inabidi kumtii sio kupimana nae nguvu.
Dharau gani ameonesha hapo, au wewe hujui bwana mifugo na katambi ni yupi na yupi?Ndugu zangu sikilizeni video,
Huyo bwana mifugo anadharau za wazi sana halafu nijeuri.
Nendeni YouTube mtaelewa
AaOFISA Mifugo Manispaa ya Shinyanga, Velan Mwalukwa, ametiwa mbaroni kwa kumtolea lugha chafu Mbunge wa Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, na Ajira.
Mwalukwa, ametiwa Mbaroni jana wakati wa mkutano wa Mbunge Katambi, Kata ya Ibinzamata alipoitwa kujibu tuhuma zinazo mkabili, za kudaiwa kuhozi ardhi ya Mwananchi Zacharia Tingwa mkazi wa kata hiyo, na kutoa lugha zisizo za staha kwa mbunge huyo.
Kabla ya kuanza kujibu tuhuma hizo, Mwalukwa alianza kumtolea lugha chafu na za kumkejeli mbunge huyo, hali ambayo ili mkasilisha Katambi na kuagiza awekwe chini ya ulinzi kwa utovu wa nidhamu, na kisha baadae akachukuliwa na Polisi.
Aidha Katambi akizungumzia tukio hilo, alisema amesikitishwa na mtumishi huyo wa umma, kumdharau Mbunge tena Naibu Waziri mbele ya wananchi, na hivyo kuamua kumchukulia hatua, ili liwe fundisho kwa wengine.
"Huyu mtu anaonekana ana dharau na jeuri, mimi ana nifanyia hivi je Mwananchi wa kawaida, na hasa huyu ambaye ana mgogoro naye, si ndiyo balaa kabisa, hebu ngoja tumtia adabu ili tuone jeuri yake ipo wapi," alisema Katambi.
"Suala hili la Mgogoro baina yake na huyu Mwananchi, nitalivalia njuga Tena bahati nzuri na Mimi ni Mwanasheria, na sita pendelea upande wowote ule, mwenye haki na hilo eneo atapata haki yake," aliongeza.
Katika hatua nyingine Katambi, aliwahidi wananchi wa Ibinzamata kuwa ataendelea kutatua changamoto ambazo zinawakabili, ikiwamo Sekta ya Afya, Elimu, ujenzi wa Barabara, pamoja na kushughulia malipo ya Wastaafu kutoka chama cha ushirika mkoani Shinyanga SHIRECU.
Awali Mwanchi huyo Zacharia Tingwa, akitoa malalamiko yake ya kudhurumiwa ardhi, alidai kuwa eneo hilo ni lake, lakini Ofisa huyo Mifugo amekuwa akitumia Pesa ili amnyang'anye na kufikia hatua ya kuweka familia yake yote rumande na kumtolea vitisho.