Nyuma yako (Riwaya ya S. Mollel)

Nyuma yako (Riwaya ya S. Mollel)

*NYUMA YAKO (MSIMU WA TATU) -- 28 & 29*

*Simulizi za series*


“Aaahmm … hapana. Sema tu sikukutaraji. Si unajua. It is more than a surprise.”

“Nilihisi utahitaji kuniona ama sivyo?”

Kelly akacheka kiuongo. Aliporudisha macho yake akamkuta Marshall akiwa anamtazama kwa macho ya mkazo. Kidogo akahofia.

“Yah! Sijakuona muda, Marshall. Tangu mahakamani.”

“Ni kweli. Naomba basi unipatie maji ya kunywa. Nimengoja uniulize lakini nimeona kimya.”

Kelly akatabasamu.

Alikuwa amekalia bunduki.

Ni kivipi angesimama?

ENDELEA

Basi akawaza na kuwazua ndani ya muda wake mchache na punde akavuta mto uliokuwepo karibu na kuzuga kuushikashika.

“Ungependelea maji gani Marshall, baridi ama moto?”

“Naomba ya baridi.”

“Yasiwe na ladha yoyote?”

“Hapana. Maji kama maji tu.”

Basi Kelly akanyanyuka upesi na kusogeza mto wake pale alipokuwa ameketi. Kisha akaendaze kufuata jokofu na kuthoa maji humo kuyamimina ndani ya glasi na kwenda nayo sebuleni kumpa Marshall.

“Niambie Marshall. Maisha yamekwendaje? Ni muda mrefu sasa na umepitia mengi hapa karibuni.”

**

“Una uhakika?” sauti iliuliza ndani ya simu.

“Ndio, nina uhakika. Kwa macho yangu nimemwona,” akasema mwanaume mnene aliyevalia shati limembana. Mwanaume huyo alikuwa ana pipi ya kijiti mdomoni, kofia kaigeuzia nyuma.

Tumbo lake lilikuwa kubwa kiasi kwamba shati halikuwa linamtosha. Jeans yake ilikuwa imepauka na viatu vyake havikuwa inaridhisha.

“... ameingia ndani ya jengo muda si mrefu. Kwa macho yangu kabisa nimemtambua. Ndiye yeye!”

“Sawa tunakuja!” sauti ikasema kimamlaka. Bwana huyo kabla hajakata simu, akauliza, “na vipi kuhusu pesa yangu?”

“Utapata pesa punde tutakampotia mkononi kwa kutumia taarifa yako.”

Baada ya hapo simu ikakata akibakia mwenye hamu. Alitoa pipi yake mdomoni akajaribu kupiga tena lakini hakupokelewa. Akalaani akiwa amekunja ndita.

Kwasababu za madai, akakaa kando kungoja wana usalama watakaokuja ili basi apate kuonana nao na kuwadai pesa yake.

**

Kelly alicheka akiwa ameziba kinywa chake. Alitengenezea nywele zake vema kisha akamtazama Marshall. “Nadhani utakuwa unatania.”

“Hapana,” Marshall akatikisa kichwa. “Nipo serious kabisa.”

Basi Kelly akalifinya tabasamu lake la uongo na kusema, “sijui unachokiongelea, Marshall. Kabisa.”

“Kwenu ni wapi Kelly?” Marshall akauliza. “Usiniambie New Zealand maana ni wongo.”

Kelly akamtazama kwanza Marshall. Kuna kitu alikuwa anakiwaza kichwani mwake.

“Kwanini waniuliza vivyo, Marshall? Unadhani nilikudanganya?”

“Sidhani bali ni kweli ulinidanganya.”

“Kwanini?”

“Sijajua kwasababu gani, Kelly. Labda uniambie lengo lako ni nini haswa? Kuna mtu alikutuma kunifuatilia tangu kule Hong Kong?”

Kelly akaduwaa. Akatabasamu kiuongo kabla hajatikisa kichwa chake na kutengenezea nywele zake kichwani.

“Nani amekutuma Kelly. Niambie kweli na sitafanya jambo. Nitakuachia huru uende zako.”

“Marshall, nimeshasema hapo awali. Sijui unachokiongea. Nilikutana na wewe Hongkong wote tukiwa kwenye utalii. Tumekutana tena Marekani sababu nimekuja kusoma. Hivyo vitu viwili ndo’ vimekufanya uunganishe matukio kiasi hicho?”

Marshall akazamisha mkono wake kwenye mfuko wa koti alafu akatoa picha aliyoirushia mezani. Kelly akadaka picha hiyo na kuitazama. Ilikuwa ya Keen!

Hapo mapigo yake ya moyo yakachumpa kabla ya kukimbia. Alihisi mambo mengi sasa. Kwa kufupisha, alijiona hayupo salama tena.

Akatoa macho yake kwenye picha na kumtazama Marshall, wakakutana macho kwa macho. Kuna kitu kilikuwa kinanenwa japo vinywa vilikuwa kimya.

Kelly akarejesha macho yake kwenye picha lakini sasa mawazo yake yakiwa mbali. Alikuwa anawaza namna ya kujikomboa ama kummaliza Marshall.

Kulikuwa kuna kaukimya ka ufu kwa muda kidogo.

Punde ukimya huo ukavunjwa na mlio wa king’ora cha polisi huko nje. Kila mtu alishtuka. Walitazamana na upesi kila mmoja akatoa silaha yake kumwonyeshea mwenzake. Tendo hilo lilichukua kama sekunde moja tu!

“Weka silaha chini!” Marshall akafoka, Kelly akabinua mdomo wake na kutikisa kichwa, “weka wewe silaha chini , Marshall,” akasema kwa sauti ya pole.

Wakiendelea kujibizana, wakasikia sauti za watu zikiwa zinajongea karibu, na zaidi zikiwa zinakwea ngazi.

Walitazamana kwa tahadhari na kidogo tu wakahisi watu wapo mlangoni.

Mwanaume mmoja aliyevalia sare za kikosi cha kupambana na majanga na maswahiba ya wepesi, alitazama wenzake wanne na kuwapatia ishara. Walikuwa wamebebelea bunduki na vifua vyao vimekingwa na ‘bulletproof’. mmoja kati yao alikuwa amebebelea gogo la chuma kwa ajili ya kuvunjia mlango.

Wakahesabu moja, mbili, tatu wakavunja mlango na kuzama ndani wakiwa wamenyooshea midomo yao ya bunduki sebuleni. Hawakuona kitu. Wakatoa macho kuangaza na punde yule mmoja wao, captain, akawaagiza wenzake watawanyike kusaka maeneo mbalimbali humo ndani.

Walisaka kwa kama dakika tatu, hawakupata kitu!

“Hamna kitu, cap!” alisema bwana mmoja. Captain akatazama dirisha na kugundua lilikuwa wazi. Akasonga na kulitazama, hapo kwenye kingo za dirisha akaona kukiwa kumebonyea.

Alipotazama kwenda juu, akaona bomba kubwa likielekea kwenye paa ya ghorofa, upesi akawaambia wenzake waelekee juu ya paa kwani mlengwa wao yupo huko.

Basi haraka kwa kutumia ngazi wakakwea na kukwea mpaka huko juu. Wakatazama wasione kitu.

“Atakuwa ameelekea wapi?”

Maghorofa yalikuwa mengi sana papo. Ukiyatazama kwa juu ni kana kwamba miti ndani ya misitu. Waliwaza itakuwa mlengwa karukia maghorofa na kupotelea kusikojulikana, lakini sasa kwenda upande upi?

“Cap, kuna suspect upande wa magharibi mtaa wa tatu. Wapo wawili wanakimbia!” sauti ilimeta kwenye kifaa cha mawasiliano cha Cap.

Basi upesi mabwana hao wakashuka tena toka walipo waende huko wanapoelekezwa.

Ilikuwa ni tukio la upesi sana. Hakukuwa na muda wa kupoteza. Walishuka ngazi wakiendelea kuwasiliana zaidi na zaidi.

Walipofika chini, bwana yule mnene aliyetoa taarifa akatokea na kusimama mbele yao,

“Subiri! Subiri!” alinyoosha mikono yake yote miwili. “Naombeni kwanza pesa yangu. Ni mimi ndiye niliwapa taarifa!”

Mabwana hao hawakutia neno, captain alimpiga kumbo zito akadondokea kando kama kiroba, kisha wakaendelea na safari yao kwenda huko walipokuwa wanaelekezwa.

Kulikuwa na magari mawili chini. Moja likafyatuka kuondoka kwa kasi sana. Kwa ndani lilikuwa na maafisa wawili. Wengine walikuwa wameshawahi kwenda eneo la tukio!

Mabwana hawa wanne wakiwa wanatumia miguu, wakakimbia sana, muda si mrefu wakawasili eneo la tukio na kukuta hapo magari mawili. Moja lilikuwa ni lile lililotoka mapema zaidi na jingine ndo’ lile lililofyatuka baada ya wao kushuka chini.

Walipotazama ndaniye, wakakuta watu wote wakiwa wamelala chini. Majeruhi wanaomimina damu lukuki!

“Shit!” captain akalaani akibonda gari.

“Tumempoteza mlengwa … tumempoteza mlengwa!” akanena kwenye kifaa chake cha mawasiliano kabla hajakitupa kunining’inia kifuani.

**

"So uko wapi? Akauliza Danielle. Uso wake ulikuwa umeparamiwa na hofu kiasi. Baada ya punde akanyanyuka upesi na kufuata gari yake.

Majira yalikuwa ni jioni ya mapema.

Alijikwea kwenye gari na kuelekea mahali anapopajua yeye kichwani. Aliendesha kwa kasi sana na baada ya kama dakika arobaini na tano akawa amefika kwenye eneo tulivu, hapo akaegesha gari na kuangaza.

Ilikuwa ni katikati ya jiji pia. Hakuwa anajua atakuwapo hapo kwa muda gani. Alitazama 'side mirrors' zake kuhakikisha usalama, punde akaona gari moja likijiegesha nyuma kwa mbali kidogo.

Hakulitilia maanani, magari kadhaa yalikuwapo hapo. Akaendelea kuangazaangaza akiwa anajiuliza. Punde akatumiwa ujumbe, "nakuja!"

Alipotoa macho yake kwenye simu akamwona mtu karibu na gari, punde mtu huyo akafungua mlango na kuzama ndani. Alikuwa ni Marshall!

Alikuwa anahema kwanguvu akiwa ameshikilia mkono wake wa kushoto chini kidogo ya kiwiko.

"Twende!"

Danielle akatia moto na gari likahepa.

"Tuwafuate!" Alisema mwanaume ndani ya gari. Gari lile ambalo lilipaki nyuma ya mbali ya la Danielle. Kumbe walikuwa wanamfuatilia mwanamke huyo.

"Hamna haja ya kuwafuata," akasema mwingine. "Tulichokuwa tunakitafuta, tumekipata."

Ndani ya gari hilo alikuwa ameketi bwana James na Smith. James alikuwa amekalia usukani huku mwenzake akikaa pembeni yake.

Bwana James alikuwa ameshikilia kamera ambayo anaipekua kutazama picha zake. Kwenye picha hizo Marshall alikuwa anaonekana akitazama chini akitembea mpaka alipozama kwenye gari.

James akatabasamu.

"Hatimaye. Marshall na Danielle!"

Kisha akacheka cheko kubwa na kumtazama Smith aliyekuwa amekaa kando.

"Sasa umenielewa sio?"

"Hakika!"

"Nilikuambia tuliza munkari. Ile ishu ilivyotangazwa, tumuwahi na tumtazame Danielle. Yeye atatupa ramani wapi twende."

Smith akasafisha koo. "Lakini tulikuwa tumeshamaliza kila kitu. Mbona tukawaacha waende?"

"Smith!" James akaita. "Mimi ndiye nimekupanga katika yote haya. Najua ninachokifanya. Trust the process. Hamna haja ya kutumia nguvu sana. Tutaharibu."

Kukawa kimya kidogo.

"Mbu akitua kwenye korodani, utaelewa si kila jambo lahitaji nguvu," akahitimisha James kabla hajawasha gari na kuondoka huku Smith akiwa hoi kwa kucheka.

Maneno ya James yalimkuna.


**

Saa mbili usiku ...


Marshall alibandua bandeji aliyokuwa nayo mwanzoni kisha akaiweka kando na kupachikwa nyingine na Danielle. Wote walikuwa wamekaa kwenye kiti kimoja ingali Jack akiwa amejitenga kidogo.

Yeye alikuwa ameketi kwenye kiti kingine uso wake ukiwa umemezwa na mawazo. Alikuwa anatazama chini muda wote.

Kichwani mwake alikuwa anatafakari mambo kadhaa, haswa kumhusu Kelly ambaye mbivu zake ametoka kuzifahamu muda si mwingi toka kwa Marshall.

"Nilikuwa mpumbavu sana," akasema kwa sauti ya chini. Kauli yake hiyo ikafanya wote wamtazame. "Niliruhusu mapenzi yakawa upofu. Nakiri kukosa, nisameheni."

"Usijali, Jack," Marshall akamsihi. "It's not a big deal. Kingetokea tu."

"Hapana!" Jack akakanusha. "Nilipaswa kuhusisha akili yangu kwenye hili."

"Nafahamu. Haukupata muda wa kutulia tangu uachane na Vio. Ulifanya maamuzi kwa upesi."

"Ni kweli. Moyo wangu ulihitaji kupoa kwa upesi, matokeo yake ukaumizwa zaidi!"

Kukawa kimya kidogo. Danielle alimalizia kumfunga Marshall bandeji mwanaume huyo akajiveka nguo yake vema kuficha kifua.

"Kelly si mwanamke wa kawaida," akasema Marshall. "Ni mwanamke mwerevu, mwepesi wa kufanya maamuzi. Lakini pia mwenye uwezo wa kupambana."

Aliposema hivyo akaweka kituo. Alikuwa anavuta kumbukumbu fulani.

"Nimeshindwa kumweka nguvuni. Polisi waliharibu kila kitu. Badala ya kufanya kilichonipeleka, nikabaki kufanya namna ya kutoroka salama.
Na pengine nilimshusha sana adui wangu. Sikutaraji."


**
 
*NYUMA YAKO (MSIMU WA TATU) -- 30 & 31*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

"Ni kweli. Moyo wangu ulihitaji kupoa kwa upesi, matokeo yake ukaumizwa zaidi!"

Kukawa kimya kidogo. Danielle alimalizia kumfunga Marshall bandeji mwanaume huyo akajiveka nguo yake vema kuficha kifua.

"Kelly si mwanamke wa kawaida," akasema Marshall. "Ni mwanamke mwerevu, mwepesi wa kufanya maamuzi. Lakini pia mwenye uwezo wa kupambana."

Aliposema hivyo akaweka kituo. Alikuwa anavuta kumbukumbu fulani.

"Nimeshindwa kumweka nguvuni. Polisi waliharibu kila kitu. Badala ya kufanya kilichonipeleka, nikabaki kufanya namna ya kutoroka salama.
Na pengine nilimshusha sana adui wangu. Sikutaraji."

ENDELEA

Lakini kwanini Kelly alikuwa anayafanya yote hayo? Kuwafuatilia wakina Marshall na washirika? Hawakupata majibu lakini waliamini kabisa kuwa mabwana hao ndio ambao walikuwa wanafanya yale mauaji na mashambulizi ambayo bwana Ian alikanusha kuhusika nayo.

Ikiwamo yale mauaji ya bwana O’neil na hata pia majaribio ya kumuua miss Danielle.

“Yatupasa kulianika hili gazetini?” akauliza Danielle.

“Hili la Kelly?” Marshall akauliza.

“Ndio. Ama unawaza nini?”

“Hatuna ushahidi lakini. Ni makisio tu ambayo bado hayajathibitishwa.”

“Kwahiyo tuachane nalo?”

Marshall akanyamaza kwanza kufikiri. “Pengine tukiandika kuhusu ule mlipuko pekee. Unajua hilo limekuwa ni jambo kubwa na mpaka sasa halijapatiwa majibu.”

“Ni kweli.”

Basi baada ya kujadili hilo wakapumzisha akili zao kwa kuteta mengine. Ilikuwa ni siku ndefu, hususani juma refu, haikuwa mbaya kama wangejipongeza hata kidogo.

Danielle akaendea jokofu na kutoa chupa kubwa mbili za whiskey, akaziweka mezani na kuongezea glasi tatu ndogo nene. Kila glasi akaijaza na kumpatia muhusika.

Na kusindikizia vinywaji vyao wakawasha na muziki kwa mbali. Basi taratibu wakiwa wanateta, taratibu wakawa wanakunywa. Kila muda ulivyokuwa unaenda watu wakazidi kuchangamka zaidi, haswa Marshall.

Hakuwa na kichwa cha pombe. Si mzoefu wa kutia kilevi mdomoni. Kichwa chake kilianza kuwa kizito na mdomo kuwa mwepesi.

Alikuwa anacheka kwa jambo dogo. Alikuwa amechangamka sana kiasi kwamba Jack na Danielle wakawa wanakonyezana kwa siri kumhusu mlengwa wao.

Ilifikia kipindi Marshall akashindwa kabisa kujibeba, akaketi akinywa na kunywa. Macho yake yakaanza kumlaghai kwa kumwona Danielle ni mrembo zaidi ya anavyoonekana. Alimkumbatia mwanamke huyo mara kwa mara na kumbusubusu akimtaka wacheze pamoja.

“Marshall, nini shida?” Danielle akauliza akimtazama mwanaume huyo machoni. Mwanamke huyo alikuwa amelegeza macho na kinywa. Alikuwa teketeke.

Mkono wa Marshall uliminya kiuno cha Danielle na kumsogeza karibu. Marshall akamtazama Danielle kwa kitambo kidogo kabla hajasema, “unataka kujua shida yangu?”

“Ndio, nataka kujua,” Danielle akasema akitabasamu kwa mbali. Ni kama vile alikuwa anamsanifu Marshall.

“Nataka nikukumbatie hivihivi siku nzima.”

“Kweli?”

“Ndio. Kwani kuna shida?”

“Hapana, hamna. Lakini naogopa.”

“Nini unaogopa?”

Danielle akamtazama Marshall machoni akiwa kimya kidogo.

“Naogopa maana hautaweza kuvumilia kwa muda.”

Marshall akatabasamu. Kidogo akacheka na kumminya Danielle kiunoni. Kabla hajasema kitu akamvuta mwanamke huyo na kumbusu shingoni kisha shavuni na kwenye lips.

“Naweza kuvumilia vinavyovumilika,” Marshall akanong’oneza. Sauti yake nzito ikasisimua mwili wa Danielle. Mwanamke huyo alihisi chuchu zake zimesimama na kuna kitu kimecheza ndani ya nguo yake ya ndani.

“Marshall,” Danielle alitokwa na sauti pasipo kutarajia. Mwili wake ulipigwa na mtetemeko fulani wa kupumbaza. Alimtazama Marshall kisha akatabasamu kwa mbali.

“Kwani utashindwa kuvumilia?”

Marshall akanyoosha mikono yake kudaka makalio ya Danielle, akayapapasa makalio hayo na kuyaminya. Alafu katika namna ya nguvu, akambeba mwanamke huyo.

Danielle alizungusha miguu yake kwenye kiuno cha Marshall, wakatazamana kimapenzi na taratibu wakaanza kusogeana wapate kukutanisha midomo. Kabla hawajatimiza adhma, Jack akasafisha koo.

“Jamani, sijaondoka. Bado nipo hapa.”

Marshall na Danielle wakatabasamu. Marshall akamshusha Danielle chini kisha kila mmoja akashika glasi yake na kuendelea kunywa. Wakanywa na kunywa zaidi kiasi kwamba hata Danielle akaanza kushinwa kujimudu.

Alijikuta mwili wake unapata joto na kujawa na hamu kila anapomtazama Marshall. Jack alipoona hali inazidi kuwa tete, akaaga aende zake chumbani huku akiwa amebebelea chupa kubwa ya kinywaji.

Ni yeye peke yake sasa ndo’ alikuwa anajitambua. Alitembea kwa kujiweza mpaka chumbano ambapo huko akajitupia kitandani na kutazama dari kwa mawazo.

Yeye alikuwa peke yake. Hakuna mtu wa kumpa kampani mbali wala karibu. Alijihisi uchungu. Alitikisa kichwa chake mara kwa mara akiwa anaminya na kubinua lips zake.

Akiwa katikati ya mawazo, akajikuta anakumbuka kuwa humo chumbani hakuwa mwenyewe. Hakuwa na sababu ya kuhuzunika.

Alitazama kando yake akaona chupa kubwa ya kinywaji. Akatabasamu. Akaivuta chupa hiyo na kuikumbatia kwanguvu.

“Nashukuru upo hapa.”

Akafungua chupa hiyo na kunywa kana kwamba mtu mwenye kiu kupita kiasi. Alikuwa anataka kujipumbaza. Alikuwa anataka akili yake ipotee kabisa kwenye ulimwengu usiofahamika. Ulimwengu ambao haumpatii msongo wa mawazo.

Huko sebuleni, Danielle alimbusu Marshall na kisha akamkumbatia kwanguvu. Macho yao yalikuwa yamelegea haswa, miili yao ilikuwa imepata joto.

Hawakukaa muda mrefu hapo wakabebana kwenda chumbani. Kama watu waliojawa na uchu, wakavuana nguo na kuzitupia huko! Walivuana kwa upesi kana kwamba wanawahi kuzima bomu.

Walipomaliza, wakanyonyana ndimi zao na kupapasana kwa fujo. Haikuchukua muda wakatimiza adhma zao na kulala usingizi mzito. Walikuja kuamka majira ya saa tatu asubuhi wakiwa hoi na wachovu.

Ni Marshall ndiye ambaye alimwamsha Danielle.

“Hey, muda wa kazini,” Marshall alisema kwa sauti ya chini. Danielle alifungua macho yake kivivu kisha akayafumba tena. Alikuwa anahisi kichwa kizito kama ndoo iliyojaa maji. Pia mwili ukiwa mchovu kupita kiasi.

“Danielle, amka. Hauendi kazini?” Marshall aliita tena, mara hii akiwa amekaza sauti. Danielle akanguruma tu kunung’una lakini asifunue macho. Kope zilikuwa nzito haswa. Kila alipokuwa anataka kuzifungua zilimshinda nguvu.

“Mimi siee --- n,” Danielle alisema kwa sauti ya puani.

“Kwanini huendi?” Macho ya Marshall yalikuwa mekundu haswa na legevu. Hata shingo yake haikuwa inaweza kubeba kichwa, ilielemewa.

Mwanaume huyo alipoona Danielle hajali anachokiongea basi akanyanyuka na kwenda zake bafuni. Huko akaoga na kurejea kitandani kumkuta Danielle. Bado mwanamke huyo alikuwa hajiwezi akikoroma.

Alijaribu tena kumwamsha lakini wapi, mwisho wa siku hata na yeye akalala. Walikuja kuamka majira ya saa saba mchana. Mara hii Danielle ndo akimwamsha Marshall.

“Amka ni mchana sasa.”

Chakula kilikuwa tayari mezani. Marshall alijisogeza kwenda huko akamkuta Jack. Wakala wakiwa kimya kidogo kana kwamba hakuna kilichotokea jana yake. Ni kama vile kila mtu alikuwa anamtegea mwenzake.

“Nimekuta missed call za James,” Danielle akavunja ukimya.

Marshall akamtazama, “Anasemaje?”

“Ametuma ujumbe,” Danielle akajibu na kuongeza, “Anasema ananihitaji tuonane. Ni kikao muhimu.”


**


*SEHEMU YA 31*


Marshall alimtazama Danielle pasipo kusema jambo. Alitafuna na alipomeza akajifuta mdomo wake na kusema, “hajakuambia maudhui ya kikao hicho?”

Danielle akabinua mdomo. “Lah! Hajaniambia. In fact, sijataka kumuuliza. Alin’tumia ujumbe baada ya kuona sijapokea simu zake.”

“Inabidi uwe makini, Danielle,” Jack akatia neno. Alikuwa anatafuna akiwa anamtazama mwanamke huyo. “hawa watu wa usalama, ni wa kuishi nao kwa umakini.”

“Najua. Najua ananitafuta sana lakini hawezi nipata,” Danielle akatia neno. Basi wakala mpaka kikomo, mwanamke huyo akanyanyuka na kwenda kujiandaa aende kazini.

Kitendo cha kunyanyuka hapo, Jack akamtazama Marshall kisha akatabasamu. Marshall hakusema jambo, akaendeleza kula kana kwamba hakumwona Jack.

Jack akatabasamu. Alikuwa anaendelea kumtazama Marshall.

“Oyah … oya Marshall,” Jack akaita kwa sauti ya chini. Alipoona Marshall haitiki, akamgusa mkono. “si nakuita ndugu.”

“Unataka nini?”

“Mbona hasira mzee?” Jack akauliza kisha akatabasamu na kulegeza macho, “Vipi jana mwanangu?”

“Sikumbuki!”

“Aaah ukumbuki wapi wewe!”

“Niambie basi mwanangu. Ilikuaje? Eeenh? … oyaaa … niambie basi mwanangu? … najua ilikuwa fresh kweli!”

“Sasa kama unajua hivyo kwanini unauliza?”

“Si nataka tu kuhakikisha kwa kinywa chako.”

“Mimi sina chochote cha kukuhakikishia.”

“Natak ---”

Danielle akafika sebuleni. Jack akaacha kuongea na kubaki akitafuna.

“Kwaherini, guys. Baadae!”

Mwanamke huyo akambusu Marshall kisha akaenda zake. Jack akamtazama tena Marshall na akashinda kujizuia kutabasamu.


**

Saa nane mchana …


“Nipo hapa ku make a deal na wewe,” alisema bwana James akimtazama Danielle machoni. Bwana huyo alikuwa amevalia suti yake maridadi rangi nyeusi. Alikuwa yu mwenyewe, bwana Smith akimuacha kwenye gari.

Ingawa Danielle hakuwa anajua ni nini bwana James alikuwa amefuata, lakini alijikuta akiwa kwenye lepe la mashaka. Alikuwa anahisi kuna kitu hakipo sawa. Alijikuta anawaza mambo kadhaa kichwani mwake akipembua na kuchambua wapi atakapokuwa amekosea.

“Unajua bwana Ian alikutwa akiwa amenyweshwa kiasi kikubwa cha kilevi, Sodium thiopental, hivyo nachelea kuamini kuwa bwana huyo atakuwa ametoa taarifa mahali. Taarifa ambayo nasi tunaitafuta kwa udi na uvumba.

Imekuwa ni ngumu, hataki kusema wala kushirikiana nasi. Lakini najua wewe utanisaidia kwenye hilo.”

Danielle akatikisa kichwa, kabla hajatia neno akaona bahasha ikitupwa mezani.

“Pengine ukiona hayo utabadilisha mawazo yako,” alisema bwana James.

Danielle akavuta bahasha na kuitazama kwa ndani. Mulikuwa na picha. Alipozitama picha hizo akajikuta akipoteza nguvu. Akitetemeka.

Alimwona Marshall pichani akiwa anajipaki kwenye gari lake. Jana tu, punde alipoenda kumchukua bwana huyo.

“Vipi hapo Danielle?” bwana James akauliza akitabasamu.

“Ni nini unataka, James?”

“Nimeshakuambia ninachotaka. Taarifa za bwana Ian.”

Danielle akanyamaza akimtazama bwana huyo.

“Deal?” James akauliza.

Baada ya muda kidogo James akatoka ndani ya ofisi hiyo kwenda kukutana na mwenzake ndani ya gari. Alipoketi akatabasamu. Alikuwa na furaha sana kwani hatimaye alikuwa amewaweka mtegoni watu waliokuwa wanamsumbua.

“Kwahiyo?” Smith akauliza.

“Nimeshaelewana naye, usijali,” bwana James akamtanabahi.

“Utawaacha huru? Inabidi wakamatwe!”

“Ah ah! Nilishakuambia hapo kabla. Tulia. Tulia. Najua cha kufanya.”

“Lak--”

“Smith, ukiendelea hivi nitajitoa muda si mrefu.”

Hiyo ikawa kauli ya mwisho ya bwana James kabla hajawasha gari na kutimka.


**


Saa kumi na moja jioni ...


Kilikuwa ni kikao cha siri. Hakukuwa na watu kabisa hapa isipokuwa wawili tu ambao ni Abdulaziz na Jamal. Manwana hao walikuwa wameketi kwenye chumba wakiwa wamekunja nne na kujinywea mvinyo mweupe.

Abdulaziz alikuwa amevalia kanzu nadhifu rangi ya maziwa ilhali Jamal yeye alikuwa amevalia sare zake za jeshi. Nguo nyeupe zenye vielelezo vingi vya vyeo. Lakini pia safi zinazong'aa.

Vidoleni mwa Jamal kulikuwa na pete mbili za dhahabu. Na saa iliyokuwa mkononi mwake ilikuwa ni ya Rolex, kubwa na ya aghali. Vilevile kwa Abdulaziz. Saa yake ilikuwa imedariziwa na dhahabu.

Kama tu ungelipata saa hii, basi shida zako ndogondogo zingekoma mara moja.

Uso wa Jamal ulikuwa mwembamba, pua ndefu na mdomo mwekundu. Mustachi wenye afya na kidevu kisafi kilichopruniwa ndevu.

Macho yake yalikuwa makubwa yenye kiiini kikubwa cheusi. Sauti yake ilikuwa nyembamba kali.

Maongezi haya hayakuwa yameanza hapa karibuni, lah! Yamedumu kwa kama lisaa. Huko nje walikuwa wamesimama wanajeshi imara wenye silaha zao.

"Kwahiyo unasemaje?" Abdulaziz akauliza. Jamal akashusha pumzi ndefu kisha akanywa fundo moja la mvinyo wake. Akasafisha koo na kusema, "nipe leo, nitakuletea kichwa chake usiku huu!"

"Uhakika?" Abdulaziz akauliza.

"Ndio. Nakuhakikishia," Jamal akasema kisha mabwana hawa wakapeana mikono ya makubaliano.

Waliteta mengi. Na huyo ambaye kichwa chake kilikuwa kinaenda kuvunwa alikuwa ni wa kwanza kati ya wengi wanaofuata.

Damu itamwagika.

Bwana Jamal akaenda zake ambapo ndani ya muda mchache, kama lisaa moja, akawa amekutana na wanaume wanne. Wanaume wa kazi. Wanaume hao akawapa maelekezo lakini pia na deadline.

Anataka kichwa cha mtu usiku huu.

**
 
*NYUMA YAKO (MSIMU WA TATU) -- 30 & 31*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

"Ni kweli. Moyo wangu ulihitaji kupoa kwa upesi, matokeo yake ukaumizwa zaidi!"

Kukawa kimya kidogo. Danielle alimalizia kumfunga Marshall bandeji mwanaume huyo akajiveka nguo yake vema kuficha kifua.

"Kelly si mwanamke wa kawaida," akasema Marshall. "Ni mwanamke mwerevu, mwepesi wa kufanya maamuzi. Lakini pia mwenye uwezo wa kupambana."

Aliposema hivyo akaweka kituo. Alikuwa anavuta kumbukumbu fulani.

"Nimeshindwa kumweka nguvuni. Polisi waliharibu kila kitu. Badala ya kufanya kilichonipeleka, nikabaki kufanya namna ya kutoroka salama.
Na pengine nilimshusha sana adui wangu. Sikutaraji."

ENDELEA

Lakini kwanini Kelly alikuwa anayafanya yote hayo? Kuwafuatilia wakina Marshall na washirika? Hawakupata majibu lakini waliamini kabisa kuwa mabwana hao ndio ambao walikuwa wanafanya yale mauaji na mashambulizi ambayo bwana Ian alikanusha kuhusika nayo.

Ikiwamo yale mauaji ya bwana O’neil na hata pia majaribio ya kumuua miss Danielle.

“Yatupasa kulianika hili gazetini?” akauliza Danielle.

“Hili la Kelly?” Marshall akauliza.

“Ndio. Ama unawaza nini?”

“Hatuna ushahidi lakini. Ni makisio tu ambayo bado hayajathibitishwa.”

“Kwahiyo tuachane nalo?”

Marshall akanyamaza kwanza kufikiri. “Pengine tukiandika kuhusu ule mlipuko pekee. Unajua hilo limekuwa ni jambo kubwa na mpaka sasa halijapatiwa majibu.”

“Ni kweli.”

Basi baada ya kujadili hilo wakapumzisha akili zao kwa kuteta mengine. Ilikuwa ni siku ndefu, hususani juma refu, haikuwa mbaya kama wangejipongeza hata kidogo.

Danielle akaendea jokofu na kutoa chupa kubwa mbili za whiskey, akaziweka mezani na kuongezea glasi tatu ndogo nene. Kila glasi akaijaza na kumpatia muhusika.

Na kusindikizia vinywaji vyao wakawasha na muziki kwa mbali. Basi taratibu wakiwa wanateta, taratibu wakawa wanakunywa. Kila muda ulivyokuwa unaenda watu wakazidi kuchangamka zaidi, haswa Marshall.

Hakuwa na kichwa cha pombe. Si mzoefu wa kutia kilevi mdomoni. Kichwa chake kilianza kuwa kizito na mdomo kuwa mwepesi.

Alikuwa anacheka kwa jambo dogo. Alikuwa amechangamka sana kiasi kwamba Jack na Danielle wakawa wanakonyezana kwa siri kumhusu mlengwa wao.

Ilifikia kipindi Marshall akashindwa kabisa kujibeba, akaketi akinywa na kunywa. Macho yake yakaanza kumlaghai kwa kumwona Danielle ni mrembo zaidi ya anavyoonekana. Alimkumbatia mwanamke huyo mara kwa mara na kumbusubusu akimtaka wacheze pamoja.

“Marshall, nini shida?” Danielle akauliza akimtazama mwanaume huyo machoni. Mwanamke huyo alikuwa amelegeza macho na kinywa. Alikuwa teketeke.

Mkono wa Marshall uliminya kiuno cha Danielle na kumsogeza karibu. Marshall akamtazama Danielle kwa kitambo kidogo kabla hajasema, “unataka kujua shida yangu?”

“Ndio, nataka kujua,” Danielle akasema akitabasamu kwa mbali. Ni kama vile alikuwa anamsanifu Marshall.

“Nataka nikukumbatie hivihivi siku nzima.”

“Kweli?”

“Ndio. Kwani kuna shida?”

“Hapana, hamna. Lakini naogopa.”

“Nini unaogopa?”

Danielle akamtazama Marshall machoni akiwa kimya kidogo.

“Naogopa maana hautaweza kuvumilia kwa muda.”

Marshall akatabasamu. Kidogo akacheka na kumminya Danielle kiunoni. Kabla hajasema kitu akamvuta mwanamke huyo na kumbusu shingoni kisha shavuni na kwenye lips.

“Naweza kuvumilia vinavyovumilika,” Marshall akanong’oneza. Sauti yake nzito ikasisimua mwili wa Danielle. Mwanamke huyo alihisi chuchu zake zimesimama na kuna kitu kimecheza ndani ya nguo yake ya ndani.

“Marshall,” Danielle alitokwa na sauti pasipo kutarajia. Mwili wake ulipigwa na mtetemeko fulani wa kupumbaza. Alimtazama Marshall kisha akatabasamu kwa mbali.

“Kwani utashindwa kuvumilia?”

Marshall akanyoosha mikono yake kudaka makalio ya Danielle, akayapapasa makalio hayo na kuyaminya. Alafu katika namna ya nguvu, akambeba mwanamke huyo.

Danielle alizungusha miguu yake kwenye kiuno cha Marshall, wakatazamana kimapenzi na taratibu wakaanza kusogeana wapate kukutanisha midomo. Kabla hawajatimiza adhma, Jack akasafisha koo.

“Jamani, sijaondoka. Bado nipo hapa.”

Marshall na Danielle wakatabasamu. Marshall akamshusha Danielle chini kisha kila mmoja akashika glasi yake na kuendelea kunywa. Wakanywa na kunywa zaidi kiasi kwamba hata Danielle akaanza kushinwa kujimudu.

Alijikuta mwili wake unapata joto na kujawa na hamu kila anapomtazama Marshall. Jack alipoona hali inazidi kuwa tete, akaaga aende zake chumbani huku akiwa amebebelea chupa kubwa ya kinywaji.

Ni yeye peke yake sasa ndo’ alikuwa anajitambua. Alitembea kwa kujiweza mpaka chumbano ambapo huko akajitupia kitandani na kutazama dari kwa mawazo.

Yeye alikuwa peke yake. Hakuna mtu wa kumpa kampani mbali wala karibu. Alijihisi uchungu. Alitikisa kichwa chake mara kwa mara akiwa anaminya na kubinua lips zake.

Akiwa katikati ya mawazo, akajikuta anakumbuka kuwa humo chumbani hakuwa mwenyewe. Hakuwa na sababu ya kuhuzunika.

Alitazama kando yake akaona chupa kubwa ya kinywaji. Akatabasamu. Akaivuta chupa hiyo na kuikumbatia kwanguvu.

“Nashukuru upo hapa.”

Akafungua chupa hiyo na kunywa kana kwamba mtu mwenye kiu kupita kiasi. Alikuwa anataka kujipumbaza. Alikuwa anataka akili yake ipotee kabisa kwenye ulimwengu usiofahamika. Ulimwengu ambao haumpatii msongo wa mawazo.

Huko sebuleni, Danielle alimbusu Marshall na kisha akamkumbatia kwanguvu. Macho yao yalikuwa yamelegea haswa, miili yao ilikuwa imepata joto.

Hawakukaa muda mrefu hapo wakabebana kwenda chumbani. Kama watu waliojawa na uchu, wakavuana nguo na kuzitupia huko! Walivuana kwa upesi kana kwamba wanawahi kuzima bomu.

Walipomaliza, wakanyonyana ndimi zao na kupapasana kwa fujo. Haikuchukua muda wakatimiza adhma zao na kulala usingizi mzito. Walikuja kuamka majira ya saa tatu asubuhi wakiwa hoi na wachovu.

Ni Marshall ndiye ambaye alimwamsha Danielle.

“Hey, muda wa kazini,” Marshall alisema kwa sauti ya chini. Danielle alifungua macho yake kivivu kisha akayafumba tena. Alikuwa anahisi kichwa kizito kama ndoo iliyojaa maji. Pia mwili ukiwa mchovu kupita kiasi.

“Danielle, amka. Hauendi kazini?” Marshall aliita tena, mara hii akiwa amekaza sauti. Danielle akanguruma tu kunung’una lakini asifunue macho. Kope zilikuwa nzito haswa. Kila alipokuwa anataka kuzifungua zilimshinda nguvu.

“Mimi siee --- n,” Danielle alisema kwa sauti ya puani.

“Kwanini huendi?” Macho ya Marshall yalikuwa mekundu haswa na legevu. Hata shingo yake haikuwa inaweza kubeba kichwa, ilielemewa.

Mwanaume huyo alipoona Danielle hajali anachokiongea basi akanyanyuka na kwenda zake bafuni. Huko akaoga na kurejea kitandani kumkuta Danielle. Bado mwanamke huyo alikuwa hajiwezi akikoroma.

Alijaribu tena kumwamsha lakini wapi, mwisho wa siku hata na yeye akalala. Walikuja kuamka majira ya saa saba mchana. Mara hii Danielle ndo akimwamsha Marshall.

“Amka ni mchana sasa.”

Chakula kilikuwa tayari mezani. Marshall alijisogeza kwenda huko akamkuta Jack. Wakala wakiwa kimya kidogo kana kwamba hakuna kilichotokea jana yake. Ni kama vile kila mtu alikuwa anamtegea mwenzake.

“Nimekuta missed call za James,” Danielle akavunja ukimya.

Marshall akamtazama, “Anasemaje?”

“Ametuma ujumbe,” Danielle akajibu na kuongeza, “Anasema ananihitaji tuonane. Ni kikao muhimu.”


**


*SEHEMU YA 31*


Marshall alimtazama Danielle pasipo kusema jambo. Alitafuna na alipomeza akajifuta mdomo wake na kusema, “hajakuambia maudhui ya kikao hicho?”

Danielle akabinua mdomo. “Lah! Hajaniambia. In fact, sijataka kumuuliza. Alin’tumia ujumbe baada ya kuona sijapokea simu zake.”

“Inabidi uwe makini, Danielle,” Jack akatia neno. Alikuwa anatafuna akiwa anamtazama mwanamke huyo. “hawa watu wa usalama, ni wa kuishi nao kwa umakini.”

“Najua. Najua ananitafuta sana lakini hawezi nipata,” Danielle akatia neno. Basi wakala mpaka kikomo, mwanamke huyo akanyanyuka na kwenda kujiandaa aende kazini.

Kitendo cha kunyanyuka hapo, Jack akamtazama Marshall kisha akatabasamu. Marshall hakusema jambo, akaendeleza kula kana kwamba hakumwona Jack.

Jack akatabasamu. Alikuwa anaendelea kumtazama Marshall.

“Oyah … oya Marshall,” Jack akaita kwa sauti ya chini. Alipoona Marshall haitiki, akamgusa mkono. “si nakuita ndugu.”

“Unataka nini?”

“Mbona hasira mzee?” Jack akauliza kisha akatabasamu na kulegeza macho, “Vipi jana mwanangu?”

“Sikumbuki!”

“Aaah ukumbuki wapi wewe!”

“Niambie basi mwanangu. Ilikuaje? Eeenh? … oyaaa … niambie basi mwanangu? … najua ilikuwa fresh kweli!”

“Sasa kama unajua hivyo kwanini unauliza?”

“Si nataka tu kuhakikisha kwa kinywa chako.”

“Mimi sina chochote cha kukuhakikishia.”

“Natak ---”

Danielle akafika sebuleni. Jack akaacha kuongea na kubaki akitafuna.

“Kwaherini, guys. Baadae!”

Mwanamke huyo akambusu Marshall kisha akaenda zake. Jack akamtazama tena Marshall na akashinda kujizuia kutabasamu.


**

Saa nane mchana …


“Nipo hapa ku make a deal na wewe,” alisema bwana James akimtazama Danielle machoni. Bwana huyo alikuwa amevalia suti yake maridadi rangi nyeusi. Alikuwa yu mwenyewe, bwana Smith akimuacha kwenye gari.

Ingawa Danielle hakuwa anajua ni nini bwana James alikuwa amefuata, lakini alijikuta akiwa kwenye lepe la mashaka. Alikuwa anahisi kuna kitu hakipo sawa. Alijikuta anawaza mambo kadhaa kichwani mwake akipembua na kuchambua wapi atakapokuwa amekosea.

“Unajua bwana Ian alikutwa akiwa amenyweshwa kiasi kikubwa cha kilevi, Sodium thiopental, hivyo nachelea kuamini kuwa bwana huyo atakuwa ametoa taarifa mahali. Taarifa ambayo nasi tunaitafuta kwa udi na uvumba.

Imekuwa ni ngumu, hataki kusema wala kushirikiana nasi. Lakini najua wewe utanisaidia kwenye hilo.”

Danielle akatikisa kichwa, kabla hajatia neno akaona bahasha ikitupwa mezani.

“Pengine ukiona hayo utabadilisha mawazo yako,” alisema bwana James.

Danielle akavuta bahasha na kuitazama kwa ndani. Mulikuwa na picha. Alipozitama picha hizo akajikuta akipoteza nguvu. Akitetemeka.

Alimwona Marshall pichani akiwa anajipaki kwenye gari lake. Jana tu, punde alipoenda kumchukua bwana huyo.

“Vipi hapo Danielle?” bwana James akauliza akitabasamu.

“Ni nini unataka, James?”

“Nimeshakuambia ninachotaka. Taarifa za bwana Ian.”

Danielle akanyamaza akimtazama bwana huyo.

“Deal?” James akauliza.

Baada ya muda kidogo James akatoka ndani ya ofisi hiyo kwenda kukutana na mwenzake ndani ya gari. Alipoketi akatabasamu. Alikuwa na furaha sana kwani hatimaye alikuwa amewaweka mtegoni watu waliokuwa wanamsumbua.

“Kwahiyo?” Smith akauliza.

“Nimeshaelewana naye, usijali,” bwana James akamtanabahi.

“Utawaacha huru? Inabidi wakamatwe!”

“Ah ah! Nilishakuambia hapo kabla. Tulia. Tulia. Najua cha kufanya.”

“Lak--”

“Smith, ukiendelea hivi nitajitoa muda si mrefu.”

Hiyo ikawa kauli ya mwisho ya bwana James kabla hajawasha gari na kutimka.


**


Saa kumi na moja jioni ...


Kilikuwa ni kikao cha siri. Hakukuwa na watu kabisa hapa isipokuwa wawili tu ambao ni Abdulaziz na Jamal. Manwana hao walikuwa wameketi kwenye chumba wakiwa wamekunja nne na kujinywea mvinyo mweupe.

Abdulaziz alikuwa amevalia kanzu nadhifu rangi ya maziwa ilhali Jamal yeye alikuwa amevalia sare zake za jeshi. Nguo nyeupe zenye vielelezo vingi vya vyeo. Lakini pia safi zinazong'aa.

Vidoleni mwa Jamal kulikuwa na pete mbili za dhahabu. Na saa iliyokuwa mkononi mwake ilikuwa ni ya Rolex, kubwa na ya aghali. Vilevile kwa Abdulaziz. Saa yake ilikuwa imedariziwa na dhahabu.

Kama tu ungelipata saa hii, basi shida zako ndogondogo zingekoma mara moja.

Uso wa Jamal ulikuwa mwembamba, pua ndefu na mdomo mwekundu. Mustachi wenye afya na kidevu kisafi kilichopruniwa ndevu.

Macho yake yalikuwa makubwa yenye kiiini kikubwa cheusi. Sauti yake ilikuwa nyembamba kali.

Maongezi haya hayakuwa yameanza hapa karibuni, lah! Yamedumu kwa kama lisaa. Huko nje walikuwa wamesimama wanajeshi imara wenye silaha zao.

"Kwahiyo unasemaje?" Abdulaziz akauliza. Jamal akashusha pumzi ndefu kisha akanywa fundo moja la mvinyo wake. Akasafisha koo na kusema, "nipe leo, nitakuletea kichwa chake usiku huu!"

"Uhakika?" Abdulaziz akauliza.

"Ndio. Nakuhakikishia," Jamal akasema kisha mabwana hawa wakapeana mikono ya makubaliano.

Waliteta mengi. Na huyo ambaye kichwa chake kilikuwa kinaenda kuvunwa alikuwa ni wa kwanza kati ya wengi wanaofuata.

Damu itamwagika.

Bwana Jamal akaenda zake ambapo ndani ya muda mchache, kama lisaa moja, akawa amekutana na wanaume wanne. Wanaume wa kazi. Wanaume hao akawapa maelekezo lakini pia na deadline.

Anataka kichwa cha mtu usiku huu.

**
Steve saruti
 
Ili kupata mwendelezo imezoeleka mpk tuombe na kunyenyekea tena kwa sauti kuu,haya na tuanze...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom