Nyeti za siri zinapochafukwa

Nyeti za siri zinapochafukwa

giphy.gif

😛😛😛😛😛😛😛 sawa bwanaaaa!
 
Trump aliugua sana....

Boris Johnson aliugua sana...

Ni wazee kuliko yeye ila wote walipona kwa kuwekewa plasma za wagonjwa wa Covid waliopona. Nitashangaa kama hawana hii therapy na madawa mengine hapa nyumbani kwa ajili yao wakubwa. Nitashangaa sana kama tegemeo kubwa ni Bupiji na Covidol pekee; na nyungu, malimao na tangawizi tu.

Naomba ziwe tetesi tu. Kama za Ole Sabaya. Au Bilal...

Ila tumekuwa nchi ya hovyo sana. Hata sijui tumefikaje hapa. May God help us ALL !!!
Ukiulizwa unaongea kuhusu nini utasemaje
Yaani ukiulizwa useme nini kimetokea mpaka usema hivi utajibu nini
 
Mji mzito sana huu

Sir buyer hakuimbiwa parapanda, sasa limezukwa jipya.

Nyeti lazima ziwe za siri, hata zikichafukwa hazianikwi upenuni, labda zioze na kutoa uvundo mkali, lakini bado unaweza kuziswafi na tindikali kisha ukazihifadhi kwenye jokofu lililogandama kipupwe cha nyuzi baridi centigrade hasi 100.

Mji mzito sana huu. Kuna tafauti ndogo sana kati ya hasidi na hashua, japo kinyume chake kina kima cha kipenyo
Kama pembe la moo halifichiki, basi usijifanye kwio mbuni kufutika medulla ardhini ili kujikinga na hadhira isikutie machoni.

Mji mzito kwelikweli

Nyeti za siri zimeshaanza kudoda, kila mtu anatamba na kikingio chake. Hivi kudoda na kuvuja vinashabihiana ama kibantu kina maingiliano? Kwasababu tundu na tobo vinafanana lakini havishabihiani.

Je, uwazi nao ni tundu au ni tobo? Ama ni kipenyo?

Kipenyo penye uwazi, mwanya? Hupenyeza panapopenyeka na waja hupenyezeana. Wengine hupenyana
Bado tu utajinasibu na nyeti za siri?

Hivi hizi ni fununu ama ni tetesi au ni minong'ono?

Penye fununu hufunuliwa, penye minong'ono hunong'onwa, penye tetesi je? Panatestiwaa.

Nyatunyatu huleta kimuhemuhe kama kilivyo kisebubu japo hiki ni kiroho papo. Sio kiroho paaa, hiyo itakuwa blinking news! Habari za kumweka mweka

Mma yana hulka moja; hayazuiliki. Unaweza kuyakinga lakini si kuyazuia lazima yatatafuta upenyo yapenye. Na hata kama utayakinga yana kima chake. Yakizidi kima yatapasua na kuvunja kingo, na madhara yatakuwa kwa wengine wengi.

Hebu tufanyeni kikowa na kulimaliza hili lisifutikwe mchagoni, ndimi hazitatulia na midomo haitapumbaa....! na ndimi zisipotulia mafikara yataundiwa uhalisia kisha midomo itaropoka ropo!

Wakulaumiwa atakuwa nani?

Lisemwalo lipo kama halipo haliwezi kusemwa asilani.
Hii misemo kuntu. Fungua "medulla oblongata" uone kilichojificha ndani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom