Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Hata TV, mafridge yalikuwepo duniani wakati Nyerere yupo madarakani; lakini WTZ hawakuruhusiwa kuwa navyo. Wanajeshi WTZ walipoivamia Uganda walishangaa kuona Waganda wana TV, fridge, lakini bongo kulikuwa hakuna kitu.

Bado tunaendelea kukumbuka ule unga "Yanga" kwa sababu ya Ujamaa.

Bado tunaendelea kukumbuka ile foleni mafuta.

Ebu, acha ubishi wa Simba na Yanga.

Hadi hii leo tunapanga foleni kununua mafuta ya petrol na diesel, chini ya utawala "mahiri" wa kikwete. Ama wewe hauko Tanzania ukajionea mwenyewe kwa macho yako jinsi tunavyokimbia huku na huko na vidumu kutafuta mafuta?

Mtu anayeamini kwamba tv ilikuwa ni kipaumbele cha watanzania kuliko chuo kikuu, inabidi achunguzwe uraia wake. Kwa mtanzania anayetumia akili yake kisawa sawa, hawezi kuwa na mawazo muflisi kama hayo.
 
Kwa akili yako unaona tv ndio kitu cha kipaumbele kwa watanzania? leo hii karibia kila mtu ana tv mbona bado watanzania wengi wako hoi bin taabani kimaisha. Hizo tv mbona zimeshindwa kuwapatia watu japo mlo wa siku moja, au hujui kwamba kwa sasa Tanzania ni nchi ya tatu duniani kwa umatonya pamoja na rasilimali zote tulizonazo na "uongozi mahiri" tulionao?

Kipaumbele cha mwalimu ilikuwa ni elimu ndio maana aliamua kujenga chuo kikuuu ili watanzania wapate elimu. Zanzibar walikuwa na tv, tena ya rangi tangu miaka ya mwanzoni mwa 1900s, mbona hakuna chochote walichonacho kuliko sisi?

Kama si Nyerere Zanzibar ingekua mbali...
 
Ritz,
Barabara za Mwanza wakati wa Nyerere zilikuwa namba moja Tanzania nzima. Nimeishi Mwanza na naweza sema mkazi...Ni baada ya kuondoka Nyerere barabara za Mwanza zilikufa kabisa kama viwanda vyetu..Hata ile barabara nzuri ya Nyerere road ilikuwa mashimo matupu. UHuru, Kenyatta, Rufiji yaani inasikitisha kabisa zilikuwa kama vichochoro.. Barabara hizo kama zilikuja tengenezwa basi ni wakati wa Mkapa maana nilikwenda Mwanza kutembelea familia yangu mwaka 2000..Watu walikuwa wakipitia Kenya kufika Mwanza toka wakati huo hadi majuzi tu... The only easyway ilikuwa kuruka na ATC..

Na mradi wa kutengeneza barabara ya Mwanza Dar ulianza toka mwaka 1982 na nadhani mradi ulikawia kutokana na ukosefu wa fedha lakini mpango wa barabara hiyo na nIle ya Musoma ilikuwepo toka enzi ya Mwalimu ambaye nakumbuka vizuri sana ktk miradi yake mikubwa ilikuwa Barabara ya Dar -Arusha, Dar - Mbeya, Dar - Mwanza na kisha kuunganisha mikoa yote lakini ndio hakuweza kufanikiwa kumaliza yote na ndio ikafa kabisa maana tulingia ktk mikakati ya IMF ktk uwekezaji, ubinafsishaji na kadhalika - Miundombinu ikapigwa full stop!

Jambo moja tu lazima tukubali. Ni kwamba barabara zake mwalimu 'Baba wa Taifa' zimedumu na imara, sidhani kama kuna barabara imara kama ya Pugu road, Morogoro road toka mjini kwenda Magomeni na mjini kwenda Salender bridge kwa sababu zilijenga toka chini kuhakikisha mifereji ya kutosha kuvuta maji ya mvua na usafi...

Nimeona leo utabiri wa hewa wakisema mtakuwa na mvua ya week nzima mikoa ya nyanda za juu, kati na Pwani sasa hiki ndio kipimo kizuri cha sifa mnazowamimia kina Mwinyi na JK... mimi natazama tu Luninga mtanipa habari maana mvua hizi hazitakwisha kesho.. tusubiri majibu.
 
Matthew 23:9

English Standard Version (ESV)


[SUP]9[/SUP] And call no man your father on earth, for you have one Father, who is in heaven.

Matayo 23:9

Swahili New Testament (SNT)

[SUP]9[/SUP]Na msimwite mtu ye yote hapa duniani `baba' kwa maana mnaye Baba mmoja, naye yuko mbinguni.

FF uliyoandika ina maana unayaamini. Huko nyuma uliandika kuwa unamwita baba aliyekuzaa tuu. Hata hivyo umeweka nukuu inayokukataza kumwita mtu yeyote baba isipokuwa aliye mbinguni. Sasa kwa nini ulisema unamwita baba aliyekuzaa wakati hiyo nukuu yako inakukataza? Lakini pia hapa unaweka nukuu nyingine kuonyesha kukubali kuwa yupo mwingine unayeweza kumwita baba. Hata hivyo ulitakiwa kufahamu vema mazingira ya mafundisho ya Jesus katika nukuu yako na maana ya mafundisho hayo. Lakini pia angalia kwenye biblia, jina baba limetumika mara nyingi kumwelezea Ibrahimu kama baba wa imani. Rejea Roman 4: 1 what shall we say then that Abraham our father... 12...but who also walk in the steps of that faith of our father Abrahim. Pia rejea Roman 4:11. Maneno Nyerere baba wa Taifa huwezi kuyakwepa. Pia umeshaelezwa mara nyingi kuwa waislamu wenzio wa Pakstan wanatunia jina hilo baba wa taifa.
 
Pamoja na yote hayo, leo wanaona umuhimu wa Mwalimu na ujamaa, wanamtambua kama baba wa taifa la tanzania, na wanaiga mengi ya mwalimu, tazama link hii hapa chini:

Daily News | Raila Odinga emulates Mwalimu-education for all East Africans



Mkuu nimesoma article yako ndeefu ila kuna kitu umekosea sana , mekuwa too judgemental na umeelemea upande mmoja, hizi hoja za Nyerere kukosolewa kwa bahati mbaya zanakuja kipindi hiki kukiwa na mwamko wa modern world

Ila from now on jifunze kuwa kuna makundi manne yanayomkosoa Nyerere

1. Kuna intelectuals/ wasio intelectuals ambao wanamkosoa Nyerere bila hidden agenda wako wazi kusema wapi alikosea na wapi alipatia

2. Kuna kundi la pili ambao wanamkosoa Nyerere kwa sababu wao wameshindwa kufanya wajibu wao kama viongozi na excuse zinakuwa na Nyerere naye alikosea.

3. wako wanaomkosa Nyerere kwa sababu za kidini, it just happen and we can not help them and difficult to know them!

4. wako ambao wanamkosoa Nyerere kwa sababu waliathirika na siasa za Nyerere (vifo kipindi cha vijiji vya ujamaa, kutaifisha mali za watu binafsi n.k), hawa hata ufanye vipi maadamu wamebeba visasi na uchungu.....hutaweza kuwa convince unless you kill them.


Kwa sisi ambao tunamheshimu Nyerere ila tunamkosoa kwa mabaya aliyoyafanya unatuweka kwenye article hii??

maana article inaonyesha ulikuwa unapiga kijembe fulani na ukafanya assignment yako vizuri sana kwa hao watu wa ufahamu kama huu wako.


Ku-review article yako at a glance na kuwa upeo mkubwa kidogo ni kuwa

1. Nyerere hajawahi kuleta uhuru Tanzania, Tanzania haijawahi kuwa huru kwa namna yeyote ile, achilia mbali bendera na wimbo wa taifa wa kudesa. tunatumia lugha isiyo yetu, tuna mitaala ya elimu ya kizungu, judiciary system siyo ya kiafrika, na mavazi na kila kifanyikacho sasa tangu zama zile siyo za ki-afrika. maamuzi ya mataifa ya nje kutuamulia bei za mali ghafi zetu tangu enzi hizo...hakupelekei kusema tuna uhuru

2. Hujasema Nyerere alikosea wapi na lini, Nchi ya Tanzania imekuwa 'huru' kwa maana ya uhuru unaousema wewe kutoka mwaka 1961-1967 kipindi hicho kulikuwa na vyama vingi, na uchumi ulikuwa mzuri, baadaye vyama vya siasa vyote vikafutwa….kikabaki TANU/CCM why?? Any reason behind? Greedy!

3. Maana ya baba wa Taifa ni absurd, ila terminology kama founding fathers kwa nchi yetu ni more appropriate hata Nyerere mwenyewe angeipendekeza. Founding fathers sound better than father of nation. Founding fathers means some people were key to our 'uhuru' kama neno uhuru unachukulia uhuru huu ni uhuru!


4. Nyerere alifeli kwenye Logic ya siasa za ujamaa au ubepari


Siasa ya ujamaa inalazimisha lazima kiongozi awe dikteta ili kuwa -equalize binadamu wote na kuwafanya wote waende kwa tune ya viongozi! Nyerere kama msomi aliyebobea alikuwa anajua hili...more than you do!!! ndiyo maana aka-blend ujamaa wa china, castro, india n.k na kuja na ujamaa wa kitanzania ambao una misingi ile ile ya ujamaa wa mahali popote pale...Nyerere alikuwa na dilemma mbili.....

1. atekeleze siasa za ujamaa kama dikteta........na asipokuwa dikteta basi ujamaa husingefanikiwa!!! au akubali kuendelea na ujamaa ambao alijua uta-fail kwa sababu hakuwa dikteta!! au alikuwa dikteta na ujamaa ulifeli kwa sababu hakuwa dikteta kweli kweli!!

2. Au atekeleze ujamaa kwa kutumia wengine ili yeye akijificha kama malaika, tunaona kawawa na sokoine walivyofanyika chambo na wabaya katika kutekeleza majukumu ya ujamaa….he knows!!


Sasa katika vyote viwili, Nyerere alichemsha kwa sababu in either case logically hakuamini, hakukusudia, wala hakufikisha hata nusu ya mawazo yake...maana angekuwa dikteta kweli ( which I like) kwa siasa za kijamaa na udikteta tungekuwa mbali!! Alichukua siasa ambayo for sure alijua hawezi kutekeleza, hakuwa na clear plan…na…na……na ya kuwa ALIWAAMNI SANA WATANZANIA HAWA KUWA KWA NGUVU YA MAULANA WOTE WATATEKELEZA SIASA ZA UJAMAA NA KUJITEGEMA PASI KUSUKUMWA!!! This is great failure of all time….unajua tabia ya binadamu ni ubinafsi yet unaamini HAWATAKUWA WABINAFSI KWA SABABU UNAAMINI HIVYO..AU KWA SABABU AMESEMA NA KUAMUA!!! Believe it or not, he failed HERE HERE……….

Nyerere alitaka u-chief wa muda mfupi na alipoona mambo yanamharibikia anaachia ngazi, ili hali anajua anatakiwa na alikwepa kubeba lawama kwa muda huo na akakubali makosa baadae.


5. Nyerere kuthibitisha kuwa hakueleweka anataka nini na hakuelewesha wengine, hakuna mfusasi wa Nyerere, si katika uongozi si katika falsafa zake...ila tumebaki sisi tunaopenda mno hotuba zake na vitabu vyake ambavyo havijsaidia chochote kwenye modern Tanzania

6. Katiba ilimfanya Nyerere kuwa mfalme na leo we are crying over the same isssue, kuteau jaji mkuu, mkuu wa majeshi,DPP, CAG, mkuu wa takukuru,m mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi.....does this makes sense??

Nyerere ndiye aliyesema zidumu fikra zake, na kutufanyisha uchaguzi wa kivuli na mtu!!! does this makes sense

haya nayaeleza ujue impact ya Nyerere kwenye modern Tanzania ni kubwa, NYERERE alikuwa muadilifu...kwa uadilifu wake alitegemea with the same KATIBA, atakuja rais mwingine muadilifu??? kama yeye?? ona madudu ya mwinyi, mkapa na kikwete ikulu? they are free to flee any charges because of the same katiba!! yet he is our father?

sifa ya kiongozi ni kutengeneza kiongozi mwingine kama yeye , kama kikwete alikuwa chipukizi wa TANU, leo hii muhubiri mkubwa wa ubepari yeye, mkapa na viongozi wengin then can something very terble kwenye uongozi wa Nyerere na hamtaki kusema!

Nyerere alikuwa hashauriki, haambiliki, na walimziria nchi.......you can have good idea but you can miss the plan.....Nyerere alijua kila kitu! we are result of Nyerere.....mtu fulani anasema mbona aliondoka siku nyingi?? RAHA YA KUWA NA RAIS MWENYE SIFA YA UFALME UMELETA MARAIS WAFALME WA KWELI! we have
Kikwete na Ridhwan..these are result of Nyerere.

Here you are from no where you can write and say anything..IMPACT ya Nyerere iko wazi hata sasa na asante hata mnaompenda mnampenda hata sasa...tena humu mitandaoni, hatusikii Nyerereism hata ndani ya chama ali-chokiasisi!!! sembuse vyama vingine

Chadema wanataka serikali tatu! wanataka Tanganyika na hiyo ni call ya kutaka ukombozi wa Tanganyika ambapo bila matwaka ya wengi...leo Tanganyika haipo na bila aibu watoto walewale wa Nyerere wanafanya kama baba yao angekuwepo...wanasema Tanzania ina miaka hamsini ina kutumia bilioni 64!

Mchambuzi baba hawa hawaambii wanawe kuwa yeye ni baba!!! mwiko kabisa, siwezi kumwita mtoto wangu na kumwambia mimi ni baba yako....ubaba unajipigania, unajisimami...ubaba unajitegemeza na kamwe hauwi na mashaka mashaka

Niliishwahi kuwaambia wenzko kama wewe ambao kwa lolote lile mnaona anayemkosoa Nyerere ni m'baya na hafai...NILIWAAMBIA MAMENO YAFUATAYO..NYERERE SIYO MTUME WALA SIYO DINI, japo hata mitume na dini zao wanakosolewa na wengine kuuawa

Nyerere, kazi zake nzuri zitasimama na ubaya wako utasimama na kusemwa...HUNA HUWEZO NA WALA HADHI YA KUWA MTETEZI WA NYERERE...NYERERE HATETEWI KIRAHISI RAHISI...HADHI ALIYOIFIKIA NYERERE ATAJITETEA YEYE MWENYEWE TU! HATA VIZAZI VYA TANO NA MIA MOJA...NYERERE HAFI YUPO ANAISHI NA KWA SABABU HIYO ATASEMWA TU KWA MABAYA NA MAZURI iwe kwenye facebook au twitter, iwe kwenye dadalada au majumbani...iwe vilabuni na kila kona ambako huwezi kusikia wala kuona Nyerere anatajwa kwa mazuri na mabaya! kusema wewe ni mtetezi wa Nyerere ni kujitakia presha za maini na moyo! huwezi! wenzio tumeshindwa...logic hazipangiki..tumebaki kumpenda kwa ksuoma kazi zake na ku-tu inspire...thats alll , his era has gone, his manipulation is still lives....his failure is visible...his legacy to love his people will continue forever..This makes all issues regarding Nyerere was so complex and can not be explained easily.......

lugha ya kiswahili, umoja wa kitaifa vitamlinda Nyerere siku zote zijazo...ila technically alikosea vitu vingi mpaka aibu, aliburuza wengi bila huruma, aliua wengi kimya kimya, alidumaza ubongo wa watanzania bila huruma.......hata leo waona...waona weye mwenyewe! watetezi wa kweli wa Nyerere huwa nikisema haya huwa wanajibu...''kweli alikosea ila alikuwa na sababu nzuri''...he failed but he has good intention...at least this makes sense....( however we believe so).....Jana tulikuwa na debate wengine wakasema kwa saikolojia ya Nyerere na damu yake kuwa chief kulimtosha sana...(ALIPENDA KUNYENYEKEWA KULIKO MALI) kama mpare kuwa na ng'ombe lakini hauzi hata kama anakufa kwa kukosa dawa....sijui unasemaje!
 
Ritz,
Barabara za Mwanza wakati wa Nyerere zilikuwa namba moja Tanzania nzima. Nimeishi Mwanza na naweza sema mkazi...Ni baada ya kuondoka Nyerere barabara za Mwanza zilikufa kabisa kama viwanda vyetu..Hata ile barabara nzuri ya Nyerere road ilikuwa mashimo matupu. Huru, Rufiji yaani inasikitisha kabisa zilikuwa kama vichochoro.. Barabara hizo kama zilikuja tengenezwa basi ni wakati wa Mkapa maana nilikwenda Mwanza kutembelea familia yangu mwaka 2000..Watu walikuwa wakipitia Kenya kufika Mwanza toka wakati huo hadi majuzi tu... The only easyway ilikuwa kuruka na ATC..

Na mradi wa kutengeneza barabara ya Mwanza Dar ulianza toka mwaka 1982 na nadhani mradi ulikawia kutokana na ukosefu wa fedha lakini mpango wa barabara hiyo na nIle ya Musoma ilikuwepo toka enzi ya Mwalimu ambaye nakumbuka vizuri sana ktk miradi yake mikubwa ilikuwa Barabara ya Dar -Arusha, Dar - Mbeya, Dar - Mwanza na kisha kuunganisha mikoa yote lakini ndio hakuweza kufanikiwa kumaliza yote na ndio ikafa kabisa maana tulingia ktk mikakati ya IMF ktk uwekezaji, ubinafsishaji na kadhalika - Miundombinu ikapigwa full stop!

Jambo moja tu lazima tukubali. Ni kwamba barabara zake mwalimu 'Baba wa Taifa' zimedumu na imara, sidhani kama kuna barabara imara kama ya Pugu road, Morogoro road toka mjini kwenda Magomeni na mjini kwenda Salender bridge kwa sababu zilijenga toka chini kuhakikisha mifereji ya kutosha kuvuta maji ya mvua na usafi...

Nimeona leo utabiri wa hewa wakisema mtakuwa na mvua ya week nzima mikoa ya nyanda za juu, kati na Pwani sasa hiki ndio kipimo kizuri cha sifa mnazowamimia kina Mwinyi na JK... mimi natazama tu Luninga mtanipa habari maana mvua hizi hazitakwisha kesho.. tusubiri majibu.

Mkandara.
Bahati nzuri hata mimi nimesoma Mwanza...Lake Secondary, napajua vizuri..

Barabara zilikuwepo zijengengwa na wakoloni kama barabara ya Uhuru, Nyerere, Lumumba, Libert, Bantu..

Barabara nyingine zilikuwa vumbi tupu kama Kenyata, Makongoro, kampuni ya Astad ya Italy ndio imejenga barabara zote za mji wa Mwanza, kipindi cha Mkapa..

Kutoka Mwanza kwenda Dar kupitia Nairobi ukianza safari kutoka Mwanza Mjini mpaka Nyangunge ni mashimo matupu..

Kupitia njia ya kati Mwanza, Shinyanga, Manyoni Singida mashimo matupu..

Unaweza kutukumbusha ni barabara gani Mwanza zilijengwa na Nyerere?
 
Mkandara.
Bahati nzuri hata mimi nimesoma Mwanza...Lake Secondary, napajua vizuri..

Barabara zilikuwepo zijengengwa na wakoloni kama barabara ya Uhuru, Nyerere, Lumumba, Libert, Bantu..

Barabara nyingine zilikuwa vumbi tupu kama Kenyata, Makongoro, kampuni ya Astad ya Italy ndio imejenga barabara zote za mji wa Mwanza, kipindi cha Mkapa..

Kutoka Mwanza kwenda Dar kupitia Nairobi ukianza safari kutoka Mwanza Mjini mpaka Nyangunge ni mashimo matupu..

Kupitia njia ya kati Mwanza, Shinyanga, Manyoni Singida mashimo matupu..

Unaweza kutukumbusha ni barabara gani Mwanza zilijengwa na Nyerere?
Aaaah kumbe tumesoma shule moja? basi nami nimeingia hapo mwaka 1970..duh ama kweli dunia ndogo!

Hakuna barabara yoyote Tanzania ktk miji yake ilijengwa na rais yeyote. Miji ilikwisha pangwa barabara zilikwisha wekwa kumbuka tunazungumzia miaka 23 baada ya Uhuru, hakuna rais duniani aloanzisha barabara za mji mpya within 23 yrs ya Uhuru wake. Swala la mijini ni ukarabati wa barabara hizo na Barabara zote ulizosema zilikuwa ktk hali nzuri wakati wa Nyerere. Kenyatta road ilikuwa ya Lami na mashimo na ikaishia kuharibika vibaya zaidi wakati wa Mwinyi. Hakuna ambalo Mwinyi alilifanya kwa mji wa Mwanza.

Nachotaka kusema hapa ni kwamba ujenzi wa barabara kuu ulianza mwaka 1980. Hizi zote tunaziona leo zimejengeka zilikuwa ktk mpango wa Nyerere toka wakati ule na hawa Astad mbona walikuwepo toka mwaka 1982?..wao Lonho na Kajima ndio walikuwa na tender kubwa za utengenezaji barabara za Tanzania.

Samahani napata habari kwamba watu wamekufa Tz kwa mafuriko na hali ni mbaya sana mjini - haya ya kweli ama?
 
Hivi hoja yako kimsingi ni nini, uongozi kiuchumi chini ya Mwalimu Vis-a-Vis Kiongozi Unayempenda Wewe OR Uchumi chini ya Ujamaa vis-a-vis Free Market?

1961-1966 - Free Market (miaka 5); [Nyerere]
1967-1985 - Command/Planned Economy (miaka 18); [Nyerere]
1986 - 2011 - Free Market (Miaka 25); [Mwinyi, Mkapa, Kikwete]

Miaka 30 chini ya Soko huru Vs Miaka 18 chini ya Ujamaa.

Unaweza kuwa muwazi kidogo nini haswa unalenga?

Mchambuzi maaelezo ya FF hubadilika kama kinyonga bila kujua kuwa anajipinga mwenyewe. Mwanzoni alisema baba ni la kikatoliki. Akakumbushwa kuwa kwenye familia tunawaita watu baba. Akabadilika, akasema ni baba tu wa kumzaa ndiye anastahili kuitwa baba. Hapa akakumbushwa jinsi Wapakstani wanavyomwita baba, baba yao wa taifa Jinna. Kiufupi, FF anahoja inayoonyesha ubaguzi wa kidini. Kuwa watu wa dini tofauti hawatakiwi kuchangamana katika jamii. Hata akasema wakristo na hasa wakatoliki hawatumii jina Rais ambalo alisema asili yake ni neno ni kiarabu. Nikamwambia yeye ni mpotoshaji. Nikamkumbusha kuwa Ruwaichi ni rais wa TEC yaani baraza la maaskofu wakatoliki Tanzania. Mawazo yote ni ya kibaguzi ila anasahau kuwa Tanzania watu wake tumechangamana, kuoana na kushirikiana watu wa imani tofauti.
 
Aaaah kumbe tumesoma shule moja? basi nami nimeingia hapo mwaka 1970..duh ama kweli dunia ndogo!

Hakuna barabara yoyote Tanzania ktk miji yake ilijengwa na rais yeyote. Miji ilikwisha pangwa barabara zilikwisha wekwa kumbuka tunazungumzia miaka 23 baada ya Uhuru, hakuna rais duniani aloanzisha barabara za mji mpya within 23 yrs ya Uhuru wake. Swala la mijini ni ukarabati wa barabara hizo na Barabara zote ulizosema zilikuwa ktk hali nzuri wakati wa Nyerere. Kenyatta road ilikuwa ya Lami na mashimo na ikaishia kuharibika vibaya zaidi wakati wa Mwinyi. Hakuna ambalo Mwinyi alilifanya kwa mji wa Mwanza.

Nachotaka kusema hapa ni kwamba ujenzi wa barabara kuu ulianza mwaka 1980. Hizi zote tunaziona leo zimejengeka zilikuwa ktk mpango wa Nyerere toka wakati ule na hawa Astad mbona walikuwepo toka mwaka 1982?..wao Lonho na Kajima ndio walikuwa na tender kubwa za utengenezaji barabara za Tanzania.

Samahani napata habari kwamba watu wamekufa Tz kwa mafuriko na hali ni mbaya sana mjini - haya ya kweli ama?

Ni kweli watu wamepoteza maisha sehemu kubwa waliopatwa na janga ili wale waliojenga mabondeni...maeneo ya Kigogo, Jangwani, Tabata Segerea, Bonde la Mkwajuni lote limejaa maji..

Daraja la Jangwani limefungwa hakuna mawasiliano kati ya Magomeni na Kariakoo..

Ni hayo tu mkuu niliyoyaona..

Turudi kwenye mada ya Nyerere...ebu msome vizuri Waberoya kuhusu swaiba wako Nyerere!
 
Ni kweli watu wamepoteza maisha sehemu kubwa waliopatwa na janga ili wale waliojenga mabondeni...maeneo ya Kigogo, Jangwani, Tabata Segerea, Bonde la Mkwajuni lote limejaa maji..

Daraja la Jangwani limefungwa hakuna mawasiliano kati ya Magomeni na Kariakoo..

Ni hayo tu mkuu niliyoyaona..

Turudi kwenye mada ya Nyerere...ebu msome vizuri Waberoya kuhusu swaiba wako Nyerere!
Nimemsoma Waberoya na naheshimu mawazo yake lakini tatizo ni pale anapojaribu kusoma na kuwasemea mawazo ya wengine. Na hakuna Utawala ulioshinda duniani kwa sababu hakuna kipimo bora cha Uongozi bora hata hao Pharaoh, Julius Kaizali, Washington, Alexander the Great, Abraham Lincoln, Clinton na wengine wote walikuwa na mapungufu mengi tu ya uongozi wao..Failure inakuja pale taifa linapoanguka kabisa na Nyerere hakufikia ktk hali hiyo maana hawa wote unaowaona toka Mwinyi hadi JK ni matunda yake Nyerere na bado utawala unaendeleza fikra za mwalimu, hivyo tunaweza kuukosoa uongozi wake lakini Nyerere haku fail.. in fact amefanikiwa kuliko viongozi wengi sana.

Swala la kuuleta Uhuru ni la mtazamo, kuna ukweli mkubwa wa kwamba waasisi wa Uhuru wetu wapo wengi sana lakini kuna hoja ya Tanzania kama Taifa na uongozi wake kutokana na chama alichokiunda Nyerere. Hakuna mtu hapa anayebisha na hata yeye Waberoya kasema wazi kuhoji utawala wa Chama kimoja na Ujamaa. Lakini ameshindwa kuelewa kwamba pasipo hivyo (chama kimoja) CCM leo isingekuwa na nguvu walokuwa nayo hivi sasa..Muungano wa Tanzania nyerere played huge part pengine leo tusingekuwa Tanzania ..na UJAMAA hauwezi kuitwa failure kwa sababu sisi wote pamoja na tamaa zetu, ubinafsi wetu tunaamini kwamba sisi ni JAMII MOJA - na Ujamaa ni Itikadi, ni maagizo bora ya Ubinadamu ktk maisha na utawala. Sasa ajabu mtu kuamini undugu wetu lakini hutaki litumike neno linalohusu undugu huu kama msingi wa Utaifa wenu.

Basi tusingekuwa na dini zetu maana Mungu mwenyewe anajua sisi binadamu tuna tamaa natunafanya maasi kila siku kwa nini tuwe na dini ktk hali ambayo itashindikana?..Hivyo Waberoya alichokisema hapo juu ni kutofahamu msisitizo wa Ujamaa kama msingi wa maisha ambayo tunatakiwa kuishi hata kama tuna matatizo na mapungufu yetu ya kibinadamu.

It's like questioning why we buid Prison wakati tunajua kwamba crime ni moja ya tabia za binadamu kwa nini tusikazane kuwapa hawa criminals kila wakitakacho tukidhania kwa kuwapa hivyo wataacha. Hii ndio philosophy ya Ubepari yaani tushindane kwa tamaa zetu na kila mmoja wetu atapata akitakacho akiwezeshwa, bila kujua kwamba Ubinafsi ni zaidi ya kushare kwa lolote lile. Leo hii tunawaona matajiri wakitaka kutajirika zaidi na zaidi na hata wakiendelea kuiba wakati walizonazo zinaweza lisha wao na familia yao kwa karne..

Na hakika lazima mkumbuke kitu kimoja tu.. Kwamba huwezi kuwa MJAMAA bila kuwa DIKTETA kwa sababu vita kubwa ya Ujamaa ni UFISADI.. Na huwezi kuwa Bepari bila kuwa FISADI maana utajiri unatokana na tamaa uya faida na hakuna kipimo cha haki ktk kupata faida...Hivyo kumlaumu Nyerere kwa kuwa Dikteta wakati huwezi kuwa mjamaa bila kuwa Dikteta ni kushindwa kuelewa principals za vitu hivi..Nyerere alikuwa Dikteta na hilo halina Ubishi isipokuwa maadam dikteta leo ni utawala mbaya kutokana na jinsi tulivyofundishwa na tunaukumbatia Ubepari bila kujua sisi ni maskini na hatuna mtaji - Haiwezekani pia.

Hivyo tunarudi ktk Kutawaliwa tena na kweli aloyasema kwamba hatuna UHURU yana maana kwa sababu Nyerere hakuweza kutufikisha pale tunapoweza kujitawala. Leo hii tunachokifanya ni kugawana umaskini matajiri wakitulisha kama kikombe cha sadaka pale msikiti wa Ijumaa...
 
Ni sahihi kabisa, hakuna uchumi utakaojengeka, popote duniani bila ya kutumia infrastructure muhimu kabisa ambayo ni Reli.

Kwa Tanzania, in the 1960s, Worldbank walikataa kutukopesha pesa kujenga TAZARA ili ku protect interest za US; walitumia vigezo kwamba the terrain hapo katikati morogoro, iringa, kwenda Mbeya imekaa vibaya na haitawezekana kupitisha reli huko; Nyerere akasema okay, akawafuata wachina, wakaijenga in 10 yrs na kwa mkopo nafuu kabisa, na walivyopasua milima ile na kuweka tunnels, nyingine ambazo run for many kilometers chini kwa chini, project ile imebakia kuwa moja ya maajabu makubwa sana katika bara hili la Afrika; wenye nafasi siku moja wajipandie treni ya tazara kwenye Mbeya mjionee maajabu yale;

WorldBank walikataa TAZARA isijengwe ili to protect kiwanda cha Firestone cha matairi ya gari kule kenya which was a major supplier wa matairi ya kwa malori ya mizigo, mabasi, etc east Africa. Pia walijua kuna suala la ukombozi kusini mwa Afrika, jambo ambalo administration za nyakati zile zilikuwa zinaunga mkono makaburu (as you may recall, Mandela mpaka 8 years ago or so alikuwa bado yupo kwenye list of terrorists...)

Leo hii reli ya kati inakufa hivi hivi tu kwa sababu ya maslahi binafsi ya watu kadhaa.

Kuna taarifa pia kwamba hata mradi wa umeme wa makaa ya mawe wa mchuchuma – liganga, umekuwa unasumbua to take off on a serious note kwa sababu ya worldbank – hawa wakubwa wana stake kubwa sana through IFC kwenye mradi wa gesi wa songo songo, na payback period haijafika bado, so having umeme wa makaa ya mawe ni competition, wakati uhalisia wa mambo ni kwamba, competition is good for end users, au sio? Sasa kama hawa worldbank ndio vinara wa free market, mbona wanaji contradict hapa…..

Mchambuzi,
Wengi wanaongelea wasichokijua, major shareholder wa World Bank ni United States Gov; kwa hiyo unapojadili WB lazima uangalie kwa undani zaidi; unajadili kitu gani; hivi vyombo WB na IMF ni vikwazo vikubwa kwa maendeleo ya nchi masikini; Mwl. Nyerere siku zote alikuwa akizishauri nchi za dunia ya 3 kujihadhari na ukoloni mamboleo, unakumbuka speech aliyoitoa Mwl. Nyerere Cancun Mexico kwenye mkutano wa nchi tajiri na masikini? Yeye aliwauliza mambo 2 "Ni nani kati yenu asiyejua London, Paris na NY imejengwa kwa mitaji kutoka Afrika? "Mnapodai mmesamehe madeni nchi za Africa ukweli ni mnarudisha kila ambacho mlikichukua" . Miradi mingi inayodhaminiwa na WB na IMF inaangalia zaidi maslahi ya nchi za magharibi. Na ndio sababu kila inapofanyika mikutano ya WB na IMF yanafanyika maandamano ya kuvipinga si kwasababu vinatoa mikopo kwa nchi masikini bali riba na sera zao hazisaidii kutatua matatizo yetu; nchi nyingi zilikubali masharti ya WB na IMF wapolazimisha Structural Adjustment Program (SAP) hakuna hata nchi moja iliyofanikiwa zaidi walididimia kwenye madeni. Hivi mtu akikukopa na akashindwa kukulipa kasho akija kukopa utampa au utamwambia huna? Pamoja na kushindwa kulipa madeni ya WB na IMF wapo tayari kutukopesha siku zote; ukweli ni tunajikopesha pesa zetu wenyewe kutoka na riba tunayotozwa,


Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Mkuu nimesoma article yako ndeefu ila kuna kitu umekosea sana , mekuwa too judgemental na umeelemea upande mmoja, hizi hoja za Nyerere kukosolewa kwa bahati mbaya zanakuja kipindi hiki kukiwa na mwamko wa modern world.

Waberoya:

Nashukuru kwa mchango wako mzuri. Nianze kwa kukiri kwamba ni kweli, makala yangu ilikuwa ndefu sana, kitu ambacho nilishaiombea msamaha hapo awali.

Baada ya kusema hayo, ningependa nianze kwa kukumbushia tu kwamba makala yangu haikuwa inalenga kumpigia Nyerere debe awe nominated kuwa BABA WA TAIFA; Makala yangu haifananii na hekaheka za kumpigia mtu debe ili apate heshima au cheo ambacho bado hana au bado hajatuzwa bado, mfano kama tunavyoona juhudi mbali mbali za makundi mbali mbali za kupigia debe watu fulani fulani kwamba ndio wanafaa kuwa wagombea wa nafasi ya uRais (CCM) uchaguzi wa mwaka 2015. Kama ulisoma kwa makini, makala yangu imezaliwa katika mazingira ambayo tayari kuna mtu anayetambulika kama BABA WA TAIFA, ambae ni Mwalimu Nyerere, heshima ambayo imeshakuwa conferred, at least customarily, na inatumika ndani ya chombo cha kutunga sheria – BUNGE, katika mijadala mbali mbali, na na pia katika kutunga sheria nyingine mbalimbali za kuipa nguvu heshima hiyo kwa Mwalimu, mfano rejea hoja yangu juu ya Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ACT ya mwaka 2005. Kwahiyo naomba tuwe on par level hapa – kwamba makala yangu haikuwa kampeni for Mwalimu apate heshima, bali, recognition on heshima iliyopo, na kwanini mimi binafsi naona alistahili, na kwanini bado anastahili heshima hiyo kwa vigezo nilivyovieleza.

Baadae nikashauri kwamba malumbano juu ya Heshima kwa Mwalimu, hayawe tupeleka popote zaidi ya kupotezeana muda katika mazingira haya magumu aambapo miaka 50 baada ya uhuru, mwanakijiji bado ana hali ileile ya zamani, if not worse. Tuna kazi muhimu zaidi ya kujenga taifa letu katika mazingira hayo hayo unayoyasema ya MODERNITY, na mjadala juu ya Nyerere na ubaba wa taifa, una manufaa pale tu kama tutakuwa tunalenga zaidi kuchota hekima yake iliyompelekea kupata heshima hiyo, ili tuitumie kujanga taifa hili. Nikatoa mawazo kwamba ni vyema zaidi tujitahidi kushirikiana na viongozi wetu wa sasa na wa baadae ili na sisi Tanzania tupate our Abraham Lincolns, Thomas Jeffersons, Joachim Chissanos, na hata ikiwezekana, Nobel Laureates na Good Governance Awards recipients (from Mohamed Ibrahim Foundation), na haijalishi kama viongozi hao watatokea CCM, CHADEMA, CUF, vyama vingine 14 vilivyopo, au hata Mgombea binafsi, kama katiba itaruhusu.

Kuhusu makosa ya Mwalimu Kiutendaji, nakubaliana na wewe, yapo mengi sana kwani it is obvious, just like in any newly independent country AT THAT PERIOD, Under Mwalimu, THERE WERE SOME THINGS THAT WENT RIGHT but also THERE WERE SOME THINGS THAT WENT WRONG. Lakini lazima tukubaliane kwamba katika nchi nyingine, hali zilikuwa mbaya sana, coups, vita vya wenyewe kwa wenyewe, wizi wa kupindukia wa mali za taifa na wanasiasa, political assassinations ambazo zina ushahidi wa wazi, mauaji ya halaiki – kidini, kikabila, kwa makusudi kabisa, n.k.. Kwa Tanzania kwa kweli things were very calm in comparison. Otherwise, nimewahi kuyataja mapungufu ya Mwalimu from time to time, na nipo tayari kuendelea kuyajadili. Lakini as already mentioned, hiyo haikuwa focus ya makala yangu.

Baada ya kusema hayo yote, makosa ya kiongozi katika utendaji/sera, in my humble opinion, sio kigezo to disqualify heshima yake kama BABA WA TAIFA. Vinginevyo, I agree kuna mambo mengi hayakwenda sawa chini ya Mwalimu kiutendaji na kimtazamo, and I am ready to debate that lakini as long as lengo letu liwe to determine how we should move forward na kurekesbisha mambo kadhaa, hususan yale ndani ya Azimio la Arusha, pamoja na mawazo mengine mapya yenye lengo la kuwainua ndugu zetu milioni zaidi ya 30 huko vijijini. Otherwise kama focus ya mjadala juu ya Mwalimu itaishia kuwa nani kashinda au kushindwa kwa hoja, haitatujenga au kutusaidia kupelekea nchi yetu mbele, especially kupunguza umaskini vijijini na sehemu za mijini.

Kuhusu Nyerere kwamba hakuleta uhuru kwa sababu ambazo umeziweka bayana kama vile hoja yako kwamba tuliendeleza mfumo wa kigeni, utamaduni, lugha n.k, now this is where it gets very interesting. It can be a very stimulating debate intellectually, kwani kama unaleta hiyo variable kwenye equation ya uhuru kama moja ya disqualifications za ubaba wa taifa, ina maana hata kina Samora Machell ambae nchi yake lugha kuu ni Kireno, Kenyatta ambae taifa lake linatawaliwa na lugha ya Kiswahili na kiingereza, na wengine wengi, wote hawa kwa hoja yako UBABA WAO WA TAIFA ni wa mashaka. Lakini angalau wakati tunajiandaa na mjadala huo, tumpe Mwalimu credit basi ya kutuunganisha na lugha moja ya Kiswahili, lugha ambayo tayari ilikuwa spoken widely, hivyo akaona ni njia rahisi kutuunganisha katika ujenzi wa taifa kupitia lugha ambayo wengi wali relate nayo kama siyo ya kigeni kwa kuletewa bali ya kigeni kutokana na interactions na jamii za kiarabu, kireno, Kiswahili, miaka mingi sana kabla ya uhuru.

Pia tumpe Mwalimu angalau credit kwa kuanzisha vyuo vya sanaa na utamaduni, kuwa na maafisa utamaduni wa mikoa na wilaya nchi nzima kukuza utamaduni wetu, na mambo kama hayo. Kwa taarifa niliyonayo, mambo mengi ya sanaa yametupwa, hata Jumba la Sanaa Dar-es-salaam linabadilishwa na kuwa moja ya maeneo ya uwekezaji wa magorofa marefu ya vioo ambayo mtanzania ambae alikuwa na uwezo wa kuingia miaka ya nyuma, hata kama ni fukara mwenye mwili ulioodhofika kwa njaa, na mavazi ya kimaskini, jingo lile pale jipya mtu huyo hatothubutu tena kusogea kwani ataweza itwa mwizi.

Lakini inanisikitisha sana kwamba, anything ambacho mnakiona aliharibu, anapewa lawama yeye kama Nyerere, lakini anything ambacho mnakubali alifanya vizuri, mnasema lazima kiwe shared na wengine katika mazingira ya founding fathers. Ndugu zangu, mnasimama wapi???

All that said, mjadala kuhusu father of the nation versus founding fathers, ni mjadala mzuri, and as you rightly said, kila mtu yupo huru kuwa na mtazamo anaodhania ni sahihi kwake, akiwa kama sehemu ya taifa hili. Lakini, as I said kwenye my original post, mpaka tufikie huko, tumpe Mwalimu heshima yake ambayo tayari anayo ndani na nje ya nchi kama BABA WA TAIFA. Ni heshima aliyonayo tayari na hawezi pokonywa; kama mjadala ni kwamba wapo wengine wanaostahili, that is debatable, lakini haina maana kwamba heshima hiyo basi Mwalimu apokonywe. Hilo haliwezekani, na nina uhakika mkubwa tu kwamba hatutafika huko.

Pia naomba uelewe kwamba mimi sijalenga rais au kiongozi yoyote specifically aliyemfuatia Mwalimu after 1985, ninachokifanya ni kuongelea wote kwa ujumla wao, focus ikiwa utawala chini ya soko huria VS Ujamaa under Mwalimu. Ukiona nataja kiongozi huyu au yule hapa na pale, ni katika kujibu tu hoja kadhaa au kuomba ufafanuzi, vinginevyo kutaja viongozi fulani, watoto wao, na familia zao, mimi lengo langu sio hilo, lengo langu katika mijadala ya namna hiyo huwa ni Ujamaa (Nyerere) VS Soko Huru (Mwinyi, Mkapa, Kikwete);

Baada ya kusema hayo, ningependa kusikia juu ya mtazamo wako: Kwa Tanzania, ni vigezo gani vingekuwa sahihi kwa Nyerere kuitwa FATHER OF THE NATION na ni Vigezo gani ni sahihi kwa sasa kutumia Neno FOUNDING FATHERS?
Ni matumainu yangu kwamba nimegusia maeneo yote muhimu ambayo yanahitaji majibu yangu ya haraka, mengine tutaendelea kujadili kadri tunavyopata nafasi.
 
Mchambuzi,
Wengi wanaongelea wasichokijua, major shareholder wa World Bank ni United States Gov; kwa hiyo unapojadili WB lazima uangalie kwa undani zaidi; unajadili kitu gani; hivi vyombo WB na IMF ni vikwazo vikubwa kwa maendeleo ya nchi masikini; Mwl. Nyerere siku zote alikuwa akizishauri nchi za dunia ya 3 kujihadhari na ukoloni mamboleo, unakumbuka speech aliyoitoa Mwl. Nyerere Cancun Mexico kwenye mkutano wa nchi tajiri na masikini? Yeye aliwauliza mambo 2 "Ni nani kati yenu asiyejua London, Paris na NY imejengwa kwa mitaji kutoka Afrika? "Mnapodai mmesamehe madeni nchi za Africa ukweli ni mnarudisha kila ambacho mlikichukua" . Miradi mingi inayodhaminiwa na WB na IMF inaangalia zaidi maslahi ya nchi za magharibi. Na ndio sababu kila inapofanyika mikutano ya WB na IMF yanafanyika maandamano ya kuvipinga si kwasababu vinatoa mikopo kwa nchi masikini bali riba na sera zao hazisaidii kutatua matatizo yetu; nchi nyingi zilikubali masharti ya WB na IMF wapolazimisha Structural Adjustment Program (SAP) hakuna hata nchi moja iliyofanikiwa zaidi walididimia kwenye madeni. Hivi mtu akikukopa na akashindwa kukulipa kasho akija kukopa utampa au utamwambia huna? Pamoja na kushindwa kulipa madeni ya WB na IMF wapo tayari kutukopesha siku zote; ukweli ni tunajikopesha pesa zetu wenyewe kutoka na riba tunayotozwa,


Chama
Gongo la Mboto DSM

Chama,

Nimependa sana hoja yako. Viongozi wa after 1985 ambao ndio wameleta SAPs, wanastahili kuwaomba msamaha watanzania kwa kuleta sera ambazo zimezaa informal sector, shillingi kuporomoka, wawekezaji migodini ambao hawalipi kodi na sana sana kumaliza maisha ya ndugu zetu kule kwa kumwaga kemikali kwenye vyanzo vya maji, wageni kuvuna samaki wote lake victoria na kuachia watanzania mapanki, vijana kukosa ajira na kuzuzura ovyo ambapo sasa ndio wanasema ni timing bomb, yote haya ni matokeo ya kuruhusu soko huria kiholela; WorldBank na IMF waliona tatizo hilo, lakini ofcourse hawakuomba msamaha na badala yake kuanza kurudisha mambo kadhaa ya mwalimu kama elimu (ndio tunaona shule za kata), mradi mkubwa wa maji ziwa victoria mwaka jana, na huduma nyingine kadhaa za kijamii ambazo 1986 hadi miaka ya 1990s, walizuia kabisa serikali isijiingize; kuna wakati worldbank wakati wa Mwalimu, waliiambia serikali yetu kwamba University education is a luxury, focus on primary education; wamekuja badilika baadae, ndio tunaona UDOM n.k;

Inasikitisha kwamba wanaombeza Mwalimu hawaoni matatizo yaliyokuja na soko huru, wao focus yao ni yale yale ya ujamaa ambayo lengo lake lilikuwa kuwaboreshea maisha yao; soko huru, lengo sio kuboreseshe watanzania maisha yao, ikitokea hivyo, ni kwa bahati mbaya; nimeshalifafanua hilo huko nyuma;
 
Waberoya:

Nashukuru kwa mchango wako mzuri. Nianze kwa kukiri kwamba ni kweli, makala yangu ilikuwa ndefu sana, kitu ambacho nilishaiombea msamaha hapo awali.

Baada ya kusema hayo, ningependa nianze kwa kukumbushia tu kwamba makala yangu haikuwa inalenga kumpigia Nyerere debe awe nominated kuwa BABA WA TAIFA; Makala yangu haifananii na hekaheka za kumpigia mtu debe ili apate heshima au cheo ambacho bado hana au bado hajatuzwa bado, mfano kama tunavyoona juhudi mbali mbali za makundi mbali mbali za kupigia debe watu fulani fulani kwamba ndio wanafaa kuwa wagombea wa nafasi ya uRais (CCM) uchaguzi wa mwaka 2015. Kama ulisoma kwa makini, makala yangu imezaliwa katika mazingira ambayo tayari kuna mtu anayetambulika kama BABA WA TAIFA, ambae ni Mwalimu Nyerere, heshima ambayo imeshakuwa conferred, at least customarily, na inatumika ndani ya chombo cha kutunga sheria  BUNGE, katika mijadala mbali mbali, na na pia katika kutunga sheria nyingine mbalimbali za kuipa nguvu heshima hiyo kwa Mwalimu, mfano rejea hoja yangu juu ya Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ACT ya mwaka 2005. Kwahiyo naomba tuwe on par level hapa  kwamba makala yangu haikuwa kampeni for Mwalimu apate heshima, bali, recognition on heshima iliyopo, na kwanini mimi binafsi naona alistahili, na kwanini bado anastahili heshima hiyo kwa vigezo nilivyovieleza.

Baadae nikashauri kwamba malumbano juu ya Heshima kwa Mwalimu, hayawe tupeleka popote zaidi ya kupotezeana muda katika mazingira haya magumu aambapo miaka 50 baada ya uhuru, mwanakijiji bado ana hali ileile ya zamani, if not worse. Tuna kazi muhimu zaidi ya kujenga taifa letu katika mazingira hayo hayo unayoyasema ya MODERNITY, na mjadala juu ya Nyerere na ubaba wa taifa, una manufaa pale tu kama tutakuwa tunalenga zaidi kuchota hekima yake iliyompelekea kupata heshima hiyo, ili tuitumie kujanga taifa hili. Nikatoa mawazo kwamba ni vyema zaidi tujitahidi kushirikiana na viongozi wetu wa sasa na wa baadae ili na sisi Tanzania tupate our Abraham Lincolns, Thomas Jeffersons, Joachim Chissanos, na hata ikiwezekana, Nobel Laureates na Good Governance Awards recipients (from Mohamed Ibrahim Foundation), na haijalishi kama viongozi hao watatokea CCM, CHADEMA, CUF, vyama vingine 14 vilivyopo, au hata Mgombea binafsi, kama katiba itaruhusu.

Kuhusu makosa ya Mwalimu Kiutendaji, nakubaliana na wewe, yapo mengi sana kwani it is obvious, just like in any newly independent country AT THAT PERIOD, Under Mwalimu, THERE WERE SOME THINGS THAT WENT RIGHT but also THERE WERE SOME THINGS THAT WENT WRONG. Lakini lazima tukubaliane kwamba katika nchi nyingine, hali zilikuwa mbaya sana, coups, vita vya wenyewe kwa wenyewe, wizi wa kupindukia wa mali za taifa na wanasiasa, political assassinations ambazo zina ushahidi wa wazi, mauaji ya halaiki  kidini, kikabila, kwa makusudi kabisa, n.k.. Kwa Tanzania kwa kweli things were very calm in comparison. Otherwise, nimewahi kuyataja mapungufu ya Mwalimu from time to time, na nipo tayari kuendelea kuyajadili. Lakini as already mentioned, hiyo haikuwa focus ya makala yangu.

Baada ya kusema hayo yote, makosa ya kiongozi katika utendaji/sera, in my humble opinion, sio kigezo to disqualify heshima yake kama BABA WA TAIFA. Vinginevyo, I agree kuna mambo mengi hayakwenda sawa chini ya Mwalimu kiutendaji na kimtazamo, and I am ready to debate that lakini as long as lengo letu liwe to determine how we should move forward na kurekesbisha mambo kadhaa, hususan yale ndani ya Azimio la Arusha, pamoja na mawazo mengine mapya yenye lengo la kuwainua ndugu zetu milioni zaidi ya 30 huko vijijini. Otherwise kama focus ya mjadala juu ya Mwalimu itaishia kuwa nani kashinda au kushindwa kwa hoja, haitatujenga au kutusaidia kupelekea nchi yetu mbele, especially kupunguza umaskini vijijini na sehemu za mijini.

Kuhusu Nyerere kwamba hakuleta uhuru kwa sababu ambazo umeziweka bayana kama vile hoja yako kwamba tuliendeleza mfumo wa kigeni, utamaduni, lugha n.k, now this is where it gets very interesting. It can be a very stimulating debate intellectually, kwani kama unaleta hiyo variable kwenye equation ya uhuru kama moja ya disqualifications za ubaba wa taifa, ina maana hata kina Samora Machell ambae nchi yake lugha kuu ni Kireno, Kenyatta ambae taifa lake linatawaliwa na lugha ya Kiswahili na kiingereza, na wengine wengi, wote hawa kwa hoja yako UBABA WAO WA TAIFA ni wa mashaka. Lakini angalau wakati tunajiandaa na mjadala huo, tumpe Mwalimu credit basi ya kutuunganisha na lugha moja ya Kiswahili, lugha ambayo tayari ilikuwa spoken widely, hivyo akaona ni njia rahisi kutuunganisha katika ujenzi wa taifa kupitia lugha ambayo wengi wali relate nayo kama siyo ya kigeni kwa kuletewa bali ya kigeni kutokana na interactions na jamii za kiarabu, kireno, Kiswahili, miaka mingi sana kabla ya uhuru.

Pia tumpe Mwalimu angalau credit kwa kuanzisha vyuo vya sanaa na utamaduni, kuwa na maafisa utamaduni wa mikoa na wilaya nchi nzima kukuza utamaduni wetu, na mambo kama hayo. Kwa taarifa niliyonayo, mambo mengi ya sanaa yametupwa, hata Jumba la Sanaa Dar-es-salaam linabadilishwa na kuwa moja ya maeneo ya uwekezaji wa magorofa marefu ya vioo ambayo mtanzania ambae alikuwa na uwezo wa kuingia miaka ya nyuma, hata kama ni fukara mwenye mwili ulioodhofika kwa njaa, na mavazi ya kimaskini, jingo lile pale jipya mtu huyo hatothubutu tena kusogea kwani ataweza itwa mwizi.

Lakini inanisikitisha sana kwamba, anything ambacho mnakiona aliharibu, anapewa lawama yeye kama Nyerere, lakini anything ambacho mnakubali alifanya vizuri, mnasema lazima kiwe shared na wengine katika mazingira ya founding fathers. Ndugu zangu, mnasimama wapi???

All that said, mjadala kuhusu father of the nation versus founding fathers, ni mjadala mzuri, and as you rightly said, kila mtu yupo huru kuwa na mtazamo anaodhania ni sahihi kwake, akiwa kama sehemu ya taifa hili. Lakini, as I said kwenye my original post, mpaka tufikie huko, tumpe Mwalimu heshima yake ambayo tayari anayo ndani na nje ya nchi kama BABA WA TAIFA. Ni heshima aliyonayo tayari na hawezi pokonywa; kama mjadala ni kwamba wapo wengine wanaostahili, that is debatable, lakini haina maana kwamba heshima hiyo basi Mwalimu apokonywe. Hilo haliwezekani, na nina uhakika mkubwa tu kwamba hatutafika huko.

Pia naomba uelewe kwamba mimi sijalenga rais au kiongozi yoyote specifically aliyemfuatia Mwalimu after 1985, ninachokifanya ni kuongelea wote kwa ujumla wao, focus ikiwa utawala chini ya soko huria VS Ujamaa under Mwalimu. Ukiona nataja kiongozi huyu au yule hapa na pale, ni katika kujibu tu hoja kadhaa au kuomba ufafanuzi, vinginevyo kutaja viongozi fulani, watoto wao, na familia zao, mimi lengo langu sio hilo, lengo langu katika mijadala ya namna hiyo huwa ni Ujamaa (Nyerere) VS Soko Huru (Mwinyi, Mkapa, Kikwete);

Baada ya kusema hayo, ningependa kusikia juu ya mtazamo wako: Kwa Tanzania, ni vigezo gani vingekuwa sahihi kwa Nyerere kuitwa FATHER OF THE NATION na ni Vigezo gani ni sahihi kwa sasa kutumia Neno FOUNDING FATHERS?
Ni matumainu yangu kwamba nimegusia maeneo yote muhimu ambayo yanahitaji majibu yangu ya haraka, mengine tutaendelea kujadili kadri tunavyopata nafasi.
The way ninavyokuelewa ungekuwa Lecturer wangu ningelamba banda! Wewe kichwa mkuu!
 
Mchambuzi,
Unajua mimi huwashangaa sana watu wanaobeza Ujamaa hali wao wenyewe katika maisha yao ni Wajamaa. Na ktk Ujamaa wao wanakubali kabisa kwamba baba zao ni dikteta na wao kama wazazi ni madikteta vile vile. Ndio maisha ya kila Mtanzania mzazi ana sauti kubwa ndani ya familia na kuna sababu ya kuwa hivyo. Sasa kwa nini mzazi asimwache huru mtoto atafute riziki zake maadam kisha zaliwa na atakuwa na maisha yake aachiwe tu atafute maisha!...

Hata wanyama hawafanyi hivyo kuna kipindi cha mzazi kumwachia mwanaye hizi propaganda za nchi za Magharibi ambao kwa miaka zaidi ya 50 wamekuwa vitani hata baada ya Uhuru na wakiishi kwa amri za majeshi leo wanataka kutuambia sisi jinsi ya Kujitawala!. Hawa wazungu walilazimishwa kwenda vitani walilazimishwa kushiriki ktk ujenzi na hata kufanya kazi viwandani kutumikia majeshi yao na hakika mageuzi ya nchi hizi yalitokana na necessity za wakati wao ambao ulikuwa ni vita.

Hivyo Ujamaa ulikuwa na lengo zuri tu, sisi tulipopata Uhuru, asilimia 98 ya wananchi wake walikuwa maskini, middle class yenyewe walikuwa maskini vile vile maana hawakufika hata asilimia 5 na hawakuwa na uwezo wa hata kuendesha maisha yao wenyewe iwe elimu ama afya. Sasa hii nchi sii kama mtoto? na mtoto alitakiwa kulindwa kukuzwa na kufikia mahala anapoweza kujitegemea ndipo unampa uhuru wa kutafuta maisha yake mwenyewe lakini hatukutazama Uhuru wetu kwa jicho hilo bali kwamba sasa mkoloni kaondoka ni wakati wa kugawana utajiri na mamlaka walioacha. Ugonvi mkubwa baina ya Nyerere na viongozi wengi hasa hawa wanaomchukia ilikuwa mgawanyo wa kile mkoloni alichokiacha. Tazama nyumba zote walizokuwa nazo viongozi wetu ni zile za wakoloni.. kati ya mwaka 1961 hadi 1967 viongozi hawa hawa waliotuletea Uhuru ndio walikuwa wa kwanza kwenda kushika nyumba hizo maana hawa waliishi Kariakoo Ilala na Magomeni ghafla wote wamehamia Uzunguni..

Kwa hiyo wasiweke roho juu, Ujamaa ulikuja kwa nia njema kabisa lakini hauweza kufanikiwa kwa sababu sisi wenyewe hakukuwa tayari, tulitegemea kugawana utajiri waloacha mkoloni na haikuwa hivyo. Halafu basi ajabu ya Firaun tumeingia katika Ubepari watu wanawaita Chadema ni chama cha Kibepari?. Heee! itakuwaje dira ya Taifa iwe ya kibepari lakini tunabeza Chadema kama chama cha kibepari?... kwani nchi bado ipo ktk Ujamaa?... watakwambia hapana na hawataki kuusikia kabisa..

Hivyo kuna kushindwa watu kuelewa kwamba tupo ktk Ubepari na kwa kila baya na zuri linalofanyika leo linatokana na Ubepari lakini haina maana tunashindwa kwa sababu ya Ubepari isipokuwa itikadi zetu wenyewe ndizo hazina sera bora zaidi ktk kufikia malengo hayo ndani ya Ubepari lakini Ubepari ni tayari tumeubeba na sidhani kuna chama kinalaani Ubepari - a Socialist party - Hakuna!..Tumeshindwa hata kabla hatujaanza!
 
Mkuu Mchambuzi, nitaanza kwa kukupa pongezi nyingi kwa jitihada zako za kujaribu kuwaelimisha watu ambao kwa kiwango chochote kile naamini hawako tayari kujielimisha. Kuna watu wanakurupuka na kudandia hii hoja bila hata ya kuwa na ustaarabu wa kufuatilia mtiririko wa hoja mbali mbali ambazo tayari zimetolewa.

Ishu hapa si kumpigia debe Mwalimu aitwe Baba wa Taifa, la hasha, tayari anatambulika kama Baba wa Taifa la Tanzania ndani na nje ya nchi yetu. Ishu ni kuwa kuna kampeni maalum chafu za kumbeza Baba wa Taifa, kumkejeli na sasa imefikia kumtukana na bahati mbaya ni kuwa anayedhihakiwa hayupo na hawezi kujitetea.

Swali ambalo wengine wetu tunajiuliza ni kwa nini haya yanatendeka wakati huu ambapo nchi inaelekea kukwama kwa kuwa na viongozi legelege wengi wao wakiwa wezi na walafi. Taifa linaelekea kukwama kwa kukosa uongozi adilifu unaoheshimu na kufuata misingi ya utawala bora pamoja na kujali na kulinda haki za raia wake.

Hebu fikiria, pamoja na uhuru wa maoni kwa nchi kubwa kama Marekani, hii leo hawezi kutokea mtu au kikundi cha watu na kuanza kumdhihaki George Washington kama Father of the Nation. Mathalan, hawezi akatokea Mmarekani na kudai kutomtambua hivyo au kutaka picha yake iondolewe kwenye "basic currency unit yao, dollar."

Fikiria atokee mtu huko Pakistan na kuanza kudai kuwa Mohammad Ali Jinnah si Baba-e-Qaum wao, bila shaka huyo atapondwa mawe hadi afe. Huwezi ukamkejeli A. K. Fazlul Haq kuwa hafai kuitwa Banglar Baagh wa Bangladesh halafu ukaendela kutanua mitaani kama hukufungwa na kuchomwa moto hadharani.

Hapo juu nimetoa mifano kwa kuangalia two extremes katika mifumo lakini hapa Tanzania wanaanza kujitokeza watu kama FaizaFoxy wanamtukana Baba wa Taifa and they get away with it, why ? Jibu ni rahisi sana, hatuna uongozi ! Utawala uliopo unafikiri utakwepa majukumu yake ya Uongozi kwa kumtupia lawama Mwalimu.

Namwambia Kikwete kwamba hapa amenoa na kama kweli maji kayavulia nguo basi ajitose aonje makali yake na aache kabisa kuvitumia vikaragosi vyake. Aseme wazi kuwa kashindwa kuongoza kwa sababu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere halafu awe tayari kujibu kwa nini pamoja na hilo aliutaka huo Uongozi wa nchi in the first place.
 
Mr. Right
Samahani kama nitakuwa nimedandia; kinachosababisha nchi nyingi za Africa kuwa uduni wa bei za bidhaa zao za kilimo kwenye world market si demand and supply hiyo inaweza kuchangia kwa kiasi kidogo ukweli ni nchi za magharibi ambao wao ndio wanunuzi wakubwa wa bidhaa zetu wao ndio wapangaji wa bei; kumbuka wazalishaji wa bidhaa za kilimo hawana cartel kama walivyo wazalishaji wa mafuta; kinachosikitisha zaidi hata wanacholipa hakiendani na gharama za uzalishaji; nchi nyingi za Africa zinalazimika kukubali bei wanayopangiwa kwa sababu hawana cha kufanya.

Chama
Gongo la Mboto DSM

Hiyo issue inatokana na competitive advantage, wenzetu wana efficiency ktk commercial agriculture. Wenzetu wemeinvest technology ktk agriculture, today nchi za West zinatumia GM food, na new advance technology in fertilizer, sasa unategemea Africa wateweza kucompete na West?

Ndiyo maana kuna policy sasa hivi TZ ya kuuza ardhi ili investors waje kuleta hiyo technology in agriculture. Is that a good strategy?

Ujamaa wa Nyerere haukufikiria hii competition. Ndiyo maana Nyerere alikiri kufeli kwa Ujamaa wake.
 
Nyerere alikuwa anataka Taifa lijitegemee, halafu Mkandara na wengineo wanasema Wazungu wanataka kununua bidhaa zetu kwa bei ya chini. Sasa mbona mnajicontradict wenyewe. Kwa nini mnataka kuuza mazao yetu ya Ujamaa kwa West? hao wenye Free Market na advance Technology? Nyerere alikuwa anataka WTZ tujitegemee halafu anataka mazao yetu tuuze kwa nchi za West!! Je Nyerere hakujua hilo? Hapo ndipo ujue kwamba Mwalimu Nyerere hakujua anachokifanya.

Nyerere alijua Mkulima wa Jembe ataweza kucompete na nchi za West zenye Free Market with advance technology? Inaonekana ALISHINDWA kufikiri kwamba kuna Competitive Advantage.


Nyerere alikuwa MZUNGUMZAJI MZURI SANA!! lakini Utendaji wake ni ZERO.
 
Back
Top Bottom