Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Ndiyo maana nimekuambia kwamba upo OFF topic. Mkandara alikuwa anazungumzia issue ya mwaka 1980 na wewe unaleta takwimu za mwaka 2011!!

Nimempa sababu zinazosababisha price ni Supply na Demand, yeye akawa ananiambia mambo ya wanunuzi kwamba walitaka kununua kwa bei ndogo. Sasa mnunuzi atataka kununua bei ndogo bila kuona Supply kubwa?

Ukiwa na bidhaa ikizidi excess of supply basi ujue mnunuzi lazima atataka kukupangia bei. Kwa sababu anajua atapata sehemu nyengine. Ndiyo maana nikamjibu changing in price ni kati ya Supply na Demand.

Mr. Right
Samahani kama nitakuwa nimedandia; kinachosababisha nchi nyingi za Africa kuwa uduni wa bei za bidhaa zao za kilimo kwenye world market si demand and supply hiyo inaweza kuchangia kwa kiasi kidogo ukweli ni nchi za magharibi ambao wao ndio wanunuzi wakubwa wa bidhaa zetu wao ndio wapangaji wa bei; kumbuka wazalishaji wa bidhaa za kilimo hawana cartel kama walivyo wazalishaji wa mafuta; kinachosikitisha zaidi hata wanacholipa hakiendani na gharama za uzalishaji; nchi nyingi za Africa zinalazimika kukubali bei wanayopangiwa kwa sababu hawana cha kufanya.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Barabara zote, tena zilikuwa zinapitika bila lami, kiangazi au masika. Zilikuwepo kabla ya Nyerere.

Nyerere hakuleta barabara mpya wakati wake zaidi ya vichochoro vya Sinza, Manzese na Buguruni. Na hata hivyo vilikuiwa havipitiki kabla ya yeye kuondoka.
Ile barabara ya Mwanza-Musoma ilijengwa mwaka gani vile? Baadhi yetu humu lawama kwa Mwalimu ni ili tujifunze zaidi. Kwa kuwa enzi za Mwalimu hapakuwa na Tv na vyombo vingi vya habari kama ilivyo sasa, mengi aliyoyafanya hayafahamiki kwa watu kama Faiza ambao kwa mila na desturi za Pwani na DINI yao walijifungia ndani muda mwingi tu na walipotoka walielekea Uarabuni ambako masharti kwa wanawake ni magumu zaidi. Natumaini mmefunguka si haba!
 
Bw, Mkubwa... Hakuna mtz aliyezaliwa kumchukia Nyerere, kama kukosolewa kwakwe ,kwako wewe ni sawa na chuki ,hiyo juu yako na kasumba zako. Nyerere anavuna alicho panda (lima). Wapo waliopoteza ndugu zao wakati wa Udikteta wake na kamwe hawatakaa kimya . Mnae muuabudu fanyeni hivyo kwa maslahi yenu binafsi.

kwa ujinga wao....ili waonekane eti wazalendo.....na kujipendekeza wka watu fulani fulani

Nyerere mharibifu sana, leo hii tunataka katiba aliyeiweka mbaya ni nyerere...bahati mbaya waliofuata wote walipenda unyerere huo huo na tunawaona wabaya kwa sababu ya kutofautiana tabia na nyerere halisi!
 
Kinachosikitisha zaidi ni kuwa kama malengo ya awali ya kusaidia landlock countries hayapo, kwanini Tanzania istumie kipande cha Dar hadi Mbeya kwa usafiri wa abiria na mizigo.

Treni ndio usafiri unaochukua bidhaa nyingi kwa wakati mmoja na kwa bei rahisi sana. Inasikitisha mahindi yanaoza Sumbawanga halafu kuna mtu anakufa njaa Monduli. Yaani reli ipo hata maarifa ya kuweka injini na mabehewa hayapo.
Nakumbuka Tazara ilivyokuwa ukombozi kwetu kule Mang'ula, Mlimba, Ifakara, Kisaki n.k. Sisi wa Mtimbira na Kidogobasi tukikumbuka tunabubujikwa na machozi.
Uwepo wa reli ungesaidia kuongeza muda wa maisha ya bara bara za lami.

Nchi zote zilizoendelea, marekani, Uingereza, Canada, Japan watu wanatumia reli. Margareth Thatcher alipoanza kuiongelea reli kuhusu ubinafsishaji waingereza wakamwambia ampishe mwingine number 10 Down street.

Huyo Nyerere anayeitwa kila majina ya uovu, akiondoka ikulu reli zilikuwa na mabehewa na injini. Nakumbuka wakati huo ukisikia Injini ya Mcanada (Bombardier) basi uelewe behewa 40 zimefunga, Mwanza, Tabora, Kigoma n.k zinahamia Dar.
Waliofuata wakawaalika matapeli wakang'oa reli kama vyuma chakavu. Hawa ndio tunaaminishwa wamejenga reli na kuweka lami. Hii imani kama si upuuzi ni nini. Ni hawa ndio tunaambiwa wameleta Internet huku nchi ikirudi miaka 20 nyuma. Kuna wenzetu wanaamini Pipi na Big za Pakistan ni maendeleo! poor friends.


Ni sahihi kabisa, hakuna uchumi utakaojengeka, popote duniani bila ya kutumia infrastructure muhimu kabisa ambayo ni Reli.

Kwa Tanzania, in the 1960s, Worldbank walikataa kutukopesha pesa kujenga TAZARA ili ku protect interest za US; walitumia vigezo kwamba the terrain hapo katikati morogoro, iringa, kwenda Mbeya imekaa vibaya na haitawezekana kupitisha reli huko; Nyerere akasema okay, akawafuata wachina, wakaijenga in 10 yrs na kwa mkopo nafuu kabisa, na walivyopasua milima ile na kuweka tunnels, nyingine ambazo run for many kilometers chini kwa chini, project ile imebakia kuwa moja ya maajabu makubwa sana katika bara hili la Afrika; wenye nafasi siku moja wajipandie treni ya tazara kwenye Mbeya mjionee maajabu yale;

WorldBank walikataa TAZARA isijengwe ili to protect kiwanda cha Firestone cha matairi ya gari kule kenya which was a major supplier wa matairi ya kwa malori ya mizigo, mabasi, etc east Africa. Pia walijua kuna suala la ukombozi kusini mwa Afrika, jambo ambalo administration za nyakati zile zilikuwa zinaunga mkono makaburu (as you may recall, Mandela mpaka 8 years ago or so alikuwa bado yupo kwenye list of terrorists...)

Leo hii reli ya kati inakufa hivi hivi tu kwa sababu ya maslahi binafsi ya watu kadhaa.

Kuna taarifa pia kwamba hata mradi wa umeme wa makaa ya mawe wa mchuchuma – liganga, umekuwa unasumbua to take off on a serious note kwa sababu ya worldbank – hawa wakubwa wana stake kubwa sana through IFC kwenye mradi wa gesi wa songo songo, na payback period haijafika bado, so having umeme wa makaa ya mawe ni competition, wakati uhalisia wa mambo ni kwamba, competition is good for end users, au sio? Sasa kama hawa worldbank ndio vinara wa free market, mbona wanaji contradict hapa…..
 
Dada Faiza na Wenzako katika Hoja,

Juhudi zenu to minimize Nyerere's prominence kwa vizazi vijavyo ibakie kuwa kama ya Kina Kinjeketile na Chifu Mkwawa, hazitawezekana. At least not when some of us are still breathing.
 
Kwa kuongezea Makambako-Songea

Chama
Gongo la Mboto DSM

Tena hii pamoja na hali ngumu ya uchumi wakati ule late 1970s, Nyerere aliendelea na ujenzi wake, na kukamilika around the time he was stepping down;
 
Dada Faiza na Wenzako katika Hoja,

Juhudi zenu to minimize Nyerere's prominence kwa vizazi vijavyo ibakie kuwa kama ya Kina Kinjeketile na Chifu Mkwawa, hazitawezekana. At least not when some of us are still breathing.
Katika jamii ya wenzetu Waislaam hasa misikiti ya hapa Dar wamefaulu kwa kiasi fulani. Umesikia bila shaka yale maandamano ya kupinga MoU ya makanisa na serikali. Agenda yake ni pana zaidi. Na haya hayaonekani kama ni uchochezi isipokuwa makala ya Mwigamba kwenye Tanzania Daima.
 
Ile barabara ya Mwanza-Musoma ilijengwa mwaka gani vile? Baadhi yetu humu lawama kwa Mwalimu ni ili tujifunze zaidi. Kwa kuwa enzi za Mwalimu hapakuwa na Tv na vyombo vingi vya habari kama ilivyo sasa, mengi aliyoyafanya hayafahamiki kwa watu kama Faiza ambao kwa mila na desturi za Pwani na DINI yao walijifungia ndani muda mwingi tu na walipotoka walielekea Uarabuni ambako masharti kwa wanawake ni magumu zaidi. Natumaini mmefunguka si haba!

Unapotosha kusema barabara ya Mwanza- Musoma, sema Magu- Musoma..

Kutoka Mwanza Mjini mpaka Nyanguge ilikuwa mashimo matupu wakati wa Nyerere..

Imejengwa wakati wa Mwinyi pamoja na barabara zote za Mwanza mjini..
 
Unapotosha kusema barabara ya Mwanza- Musoma, sema Magu- Musoma..

Kutoka Mwanza Mjini mpaka Nyanguge ilikuwa mashimo matupu wakati wa Nyerere..

Imejengwa wakati wa Mwinyi pamoja na barabara zote za Mwanza mjini..

Hoja yako ni barabara kujengwa au barabara kuwekewa lami? ni vizuri tukatofautisha hayo kwani kipimo cha infrastructural development (barabara hususan) ni paved roads (lami na zisizo lami), na uchumi ukiruhusu, ndipo lami huwekwa;

Vinginevyo katika maisha yangu ya utotoni na utu uzima, sijawahi sikia kuna mradi mpya wa barabara ambao ume involve clearance ya mapori, vichuguu n.k ili kujenga barabara mpya itakayoleta mawasiliano na upande mwingine; what i have witnessed ni mwendelezo wa barabara zile zile alizoacha mwalimu ambazo baada ya yeye, zimekuwa zinaweka lami; ingawa kuna nyingine aliziwekea lami lakini ikaja kuisha baadae;

Mbaya zaidi, barabara za sasa zile kubwa ni muendelezo ule ule wa kikoloni wa dendritic pattern ya barabara (yani umbo la uma/fork ya mezani) whereby, barabara zinatoka maeneo mbali mbali kuja kujiunga na mto mkubwa wa barabara kuelekeza DSM kuwakimbizia wakubwa wa nje dhahabu na mazao ya kilimo; tusisahau kwamba ni WorldBank ndio walikuja na mkakati wa kuzijenga barabara hizi, sio tanzania tu bali kote wanapoingilia maamuzi ya bajeti za wenye nchi; nia yao ilikuwa ni kuongeza efficiency katika uchumi, na hilo lilianzia na mikakati yao ya ku reform tax administration ili kwanza tuweze kuji finance wenyewe badala ya kutegemea mikopo yao ambayo hailipiki; pili tuwe na hela za kuwalipa mikopo yao; na tatu, ili tuweze finance projects kama za barabara or any other sectors that are good kiuchumi for them and sponsors wao (G8, OECD...);

Otherwise, sijawahi sikia ujenzi wa barabara ya kiwango cha juu ambayo intention yake ni kuongeza efficiency ya commercial activities kati ya kijiji A na kijiji B;

Nasimama kusahihishwa;
 
Kenya ni ndugu zetu ambao, unlike Tanzania, wao waliendelea na soko huru baada ya uhuru miaka ya 1960s; Sisi tulikuja jiunga nao katika hilo baadae; despite all that, leo hii tupo nao katika kikapu kimoja cha nchi maskini kabisa duniani in terms of GDP growth outcome on literacy rates, educational outcomes, life expectancy, and over all quality of life; Nafasi hizi za kenya na tanzania kwa miaka mingi sana zimekuwa zinabakia hivyo hivyo, despite ya GDP growth za kustaajabisha;

Pamoja na yote hayo, leo wanaona umuhimu wa Mwalimu na ujamaa, wanamtambua kama baba wa taifa la tanzania, na wanaiga mengi ya mwalimu, tazama link hii hapa chini:


Daily News | Raila Odinga emulates Mwalimu-education for all East Africans
 
Dada Faiza na Wenzako katika hoja:

Ni vizuri pia mkaweka juhudi zenu au mkawashauri viongozi wenu wapendwa waliokuja baaada ya 1985 na wale watakaokuja miaka ya mbeleni, pia wajikite katika kuandika vitabu na articles mbalimbali juu ya mipango yao na nchi, vision, changamoto, n.k, ili kuachia vizazi vijavyo mambo ya kusoma, na waweze kuwaelewa viongozi wao waliopita in a critical way, hence kuendeleza legacy zao n.k; Vinginevyo porojo zetu hizi za JamiiForums, ukweli ni kwamba sote hatuna mkataba na mwenyezi mungu muumba wa yote, leo tupo, kesho hatupo, hoja na mijadala yetu itafikia tamati kishabiki zaidi;

Mwalimu Nyerere aliandika mengi sana kwa ajili ya Watanzania juu ya mambo mbali mbali; vile vile aliandikwa sana na wengine wa ndani na nje, kwa mabaya na mazuri; legacy yake ni matokeo ya hilo pia; Vinginevyo legacy haijengwi hivi hivi tu, Literature huchangia sana; na sote tunajua umuhimu wa "maandiko" katika hilo;
 
Unapotosha kusema barabara ya Mwanza- Musoma, sema Magu- Musoma..

Kutoka Mwanza Mjini mpaka Nyanguge ilikuwa mashimo matupu wakati wa Nyerere..

Imejengwa wakati wa Mwinyi pamoja na barabara zote za Mwanza mjini..
Bila shaka kulikuwa na lami kati ya Nyanguge na Mwanza mjini ambayo baadae iligeuka ikawa mashimo. Historia haiandikwi upya wala kurekebishwa.
 
Bila shaka kulikuwa na lami kati ya Nyanguge na Mwanza mjini ambayo baadae iligeuka ikawa mashimo. Historia haiandikwi upya wala kurekebishwa.

Mkuu, Lami ya Mwanza-Nyanguge aliwekwa na nani na mwaka gani?
 
Pamoja na kazi yoooote ya uchambuzi alofanya Mchambuzi haya ndio majibu.

Sasa naelewa kwa nini walimu wetu wakati mwingine wanatembeza bakora.........
Umeona eenh! kuna mijitu kichwa ngumu bila bakora haiendi. wewe huoni wazee wa Kiswahili bakora mikononi haziwatoki wanajua bila bakora hawataelewana!!
 
Hakuna lawama dhidi ya Nyerere, upo uzushi unaoundwa na kikundi cha watu wachache kama Takashi ambao hawana hoja, data wala ukweli. Wamejazwa hadi akili haziwezi kubaini kati ya kudanganya au kudanganywa.

Nimeweka maswali hapo juu hakuna anayejibu, bali tunaona watu wakibadili mada na kuleta udikteta, Zimbabwe, unit n.k.

Nikuulize wewe Takashi unayedhani huna chuki mdomoni lakini moyoni ni mweusi. Maswali ni haya:

1. Mwinyi, Mkapa, Kikwete wamejenga bara bara gani kwa pamoja kushinda Nyerere. Sio kuweka lami uelewe!

2. Watatu hao wamewekeza kiasi gani katika 'energy' kuliko Nyerere

3. Ni kitu gani kinafanyika sasa hivi ambacho hakina msingi alioweka Nyerere

Ukijibu maswali hayo nitajua upo kwa mjadala, usipojibu kaa kimya chuki itafaune nafasi yako.

Bw,Nguruvi3, mimi siko hapa kumfananisha Nyerere na waliofatia baada yake. Wote hao wana kasoro zao . Ninacho kipinga na nitaendelea kukipinga ni zile sifa na utukufu anaopewa Nyerere .Hakuwa matakatifi, wala innocent , he was as all dictators are...Kama alijenga bararbara kutoka tz hadi south Africa kwangu mimi haibadilishi kitu.

Hilo kundi lenu lenye kumuabudu Nyerere, tunajua mnafanya hivo kwa maslahi yenu binafsi. Hivi yule mzee angekua bado yupo madarakani , JF ingekuwepo? Hivi angeruhusu wa Tz wawe na mijadala ya wazi kuhusu masuala ya nchi yao? Aliwanyima hata TV kwa kuhofia wa Tz watafungua macho mapema.
 
Bw,Nguruvi3, mimi siko hapa kumfananisha Nyerere na waliofatia baada yake. Wote hao wana kasoro zao . Ninacho kipinga na nitaendelea kukipinga ni zile sifa na utukufu anaopewa Nyerere .Hakuwa matakatifi, wala innocent , he was as all dictator are...Kama alijenga bararbara kutoka tz hadi south Africa kwangu mimi haibadilishi kitu.

Hilo kundi lenu lenye kumuabudu Nyerere, tunajua mnafanya hivo kwa maslahi yenu binafsi. Hivi yule mzee angekua bado yupo madarakani , JF ingekuwepo? Hivi angeruhusu wa Tz wawe na mijadala ya wazi kuhusu masula ya nchi yao? Aliwanyima hata TV kwa kuhofia wa Tz watafungua macho mapema.

Kwa akili yako unaona tv ndio kitu cha kipaumbele kwa watanzania? leo hii karibia kila mtu ana tv mbona bado watanzania wengi wako hoi bin taabani kimaisha. Hizo tv mbona zimeshindwa kuwapatia watu japo mlo wa siku moja, au hujui kwamba kwa sasa Tanzania ni nchi ya tatu duniani kwa umatonya pamoja na rasilimali zote tulizonazo na "uongozi mahiri" tulionao?

Kipaumbele cha mwalimu ilikuwa ni elimu ndio maana aliamua kujenga chuo kikuuu ili watanzania wapate elimu. Zanzibar walikuwa na tv, tena ya rangi tangu miaka ya mwanzoni mwa 1900s, mbona hakuna chochote walichonacho kuliko sisi?
 
Back
Top Bottom